< 1 Wafalme 5 >
1 Hiramu mfalme wa Tiro aliwatuma watumishi wake kwa Sulemani kwa kuwa alisikia kuwa walikuwa wamemtawaza kuwa mfalme mahali pa baba yake, kwani Hiramu alimpenda Daudi.
Et Hiram, roi de Tyr, envoya ses serviteurs vers Salomon, car il avait entendu qu’on l’avait oint pour roi à la place de son père; car Hiram avait toujours aimé David.
2 Sulemani akatuma ujumbe kwa Hiramu, akisema,
Et Salomon envoya vers Hiram, disant:
3 “Unajua kuwa Daudi baba yangu hakujenga nyumba kwa jina la BWANA, Mungu wake kwa sababu ya vile vita vilivyomzunguka, kwa kuwa wakati wa uhai wake BWANA alikuwa akiweka maadui wake chini ya nyayo za miguu yake.
Tu sais, quant à David, mon père, qu’il ne put bâtir une maison pour le nom de l’Éternel, son Dieu, à cause de la guerre dont [ses ennemis] l’entourèrent jusqu’à ce que l’Éternel les mit sous la plante de ses pieds.
4 Lakini sasa BWANA amenipa mimi pumziko toka pande zote. Hakuna maadui wala majanga.
Mais maintenant l’Éternel, mon Dieu, m’a donné de la tranquillité de tous les côtés; il n’y a ni adversaire ni événement fâcheux.
5 Kwa hiyo ninakusudia kujenga hekalu kwa jina la BWANA, Mungu wangu, kama BWANA alivyosema kwa Daudi baba yangu, akisema, 'Mwanao ambaye nitamweka kwenye kiti chako cha enzi mahali pako, ndiye atakayenijengea hekalu kwa jina langu.'
Et voici, j’ai résolu de bâtir une maison pour le nom de l’Éternel, mon Dieu, ainsi que l’Éternel a parlé à David, mon père, disant: Ton fils, que je mettrai à ta place sur ton trône, lui, bâtira une maison à mon nom.
6 Kwa hiyo sasa amuru wakate mierezi kutoka Lebanoni kwa ajili yangu. Watumishi wangu wataungana na watumishi wako, nami nitakulipa kwa ajili ya watumishi wako ili kwamba upate malipo mazuri kwa kila kitu utakchokubali kukifanya. Kwa kuwa unajua kuwa hakuna mtu mioingoni mwetu anayejua kukata miti kama Wasidoni.”
Et maintenant, commande qu’on me coupe des cèdres dans le Liban; et mes serviteurs seront avec tes serviteurs, et je te donnerai les gages de tes serviteurs selon tout ce que tu [me] diras; car tu sais qu’il n’y a personne parmi nous qui s’entende à couper le bois comme les Sidoniens.
7 Hiramu aliposikia maneno ya Sulemani, akafurahi sana akasema, “BWANA na abarikiwe leo, ambaye amempa Daudi mwana wa hekiima juu ya kundi hili kubwa.”
Et il arriva, quand Hiram entendit les paroles de Salomon, qu’il s’en réjouit beaucoup; et il dit: Béni soit aujourd’hui l’Éternel, qui a donné à David un fils sage, sur ce grand peuple!
8 Hiramu akatuma neno kwa Sulemani, akisema, “Nimeupata ujumbe ule ulionitumia. Nitatoa miti yote ya mierezi na miti ya miberoshi ambayo unahitaji.
Et Hiram envoya à Salomon, disant: J’ai entendu ce que tu m’as envoyé [dire]; je ferai tout ce que tu désires, à l’égard des bois de cèdre et des bois de cyprès.
9 Watumishi wangu wataileta miti kutoka Lebanoni hadi baharini, nami nitaiendesha baharini mpaka mahali utakaponielekeza. Nitaigawa pale, nawe utaichukua. Utafanya kile ninachohitaji kwa kuwapa chakula watumishi wangu.”
Mes serviteurs les descendront du Liban à la mer, et je les mettrai en radeaux sur la mer [pour les faire passer] jusqu’au lieu que tu m’enverras [dire]; et je les ferai délier là, et tu les enlèveras. Et toi, tu accompliras mon désir, en donnant du pain à ma maison.
10 Kwa hiyo Hiramu akampa Sulemani miti yote ya mierezi na miti ya miberoshi ambayo alihitaji.
Et Hiram donna à Salomon des bois de cèdre, et des bois de cyprès, tout ce qu’il désirait;
11 Sulemani akampa Hiramu kori ishirini elfu za ngano kwa ajili ya chakula cha watumishi wake na kori ishirii za mafuta safi. Sulemani akavitoa hivi kwa Hiramu mwaka baad ya mwaka.
et Salomon donna à Hiram 20 000 cors de froment pour nourrir sa maison, et 20 cors d’huile fine. C’est là ce que Salomon donna à Hiram chaque année.
12 BWANA akampa Sulemani hekima, kama alivyokuwa amemwahidi. Kulikuwa na amani kati ya Hiramu na Sulemani na wote wawili wakafanya agano.
Et l’Éternel donna de la sagesse à Salomon, comme il le lui avait dit. Et il y eut paix entre Hiram et Salomon, et ils firent alliance eux deux.
13 Mfalme Sulemani akaandaa wafanya kazi kutoka Israeli yote. Idadi ya watenda kazi walioandaliwa ilikuwa wanaume elfu thelathini.
Et le roi Salomon fit une levée sur tout Israël, et la levée fut de 30 000 hommes.
14 Aliwatuma kwenda Lebanoni, aliwatuma kwa zamu ya watu elfu kumi kila mwezi. Kwa mwezi mmoja walienda Lebanoni na miezi miwili walikaa nyumbani. Adoniramu ndiye aliyekuwa msimamizi wa watenda kazi.
Et il les envoya au Liban, 10 000 par mois, par relais: ils étaient un mois au Liban, deux mois à la maison; et Adoniram était [préposé] sur la levée.
15 Sulemani alikuwa na watu elfu sabini waliokuwa wabeba mizigo na watu elfu themanini wa kukata mawe milimani,
Et Salomon avait 70 000 [hommes] qui portaient des fardeaux, et 80 000 qui taillaient [la pierre] sur la montagne,
16 zaidi ya hao, walikuwepo maakida 3, 300 ambao pia waliokuwa wakiisimamia hiyo kazi.
outre les chefs, les intendants de Salomon, qui étaient [préposés] sur l’œuvre, 3 300, qui avaient autorité sur le peuple qui travaillait à l’œuvre.
17 Kwa amri ya mfalme walileta mawe makubwa ya thamani kwa ajili ya kulaza kwenye msingi wa hekalu.
Et le roi commanda, et on transporta de grandes pierres, des pierres de prix, pour faire les fondements de la maison, des pierres de taille.
18 Kwa hiyo wajenzi wa Sulemani na wajenzi wa Hiramu na Wagebaliti walifanya kazi ya kukata na kuandaa mbao kwa ajili ya ujenzi wa hekalu.
Et les ouvriers de Salomon et les ouvriers de Hiram, et les Guibliens, taillèrent et préparèrent le bois et les pierres pour bâtir la maison.