< 1 Wafalme 5 >

1 Hiramu mfalme wa Tiro aliwatuma watumishi wake kwa Sulemani kwa kuwa alisikia kuwa walikuwa wamemtawaza kuwa mfalme mahali pa baba yake, kwani Hiramu alimpenda Daudi.
Also Hiram, kyng of Tire, sente hise seruauntis to Salomon; for he herde that thei hadden anoyntide hym kyng for his fadir; for Hiram was frend of Dauid in al time.
2 Sulemani akatuma ujumbe kwa Hiramu, akisema,
Sotheli also Salomon sente to Hiram,
3 “Unajua kuwa Daudi baba yangu hakujenga nyumba kwa jina la BWANA, Mungu wake kwa sababu ya vile vita vilivyomzunguka, kwa kuwa wakati wa uhai wake BWANA alikuwa akiweka maadui wake chini ya nyayo za miguu yake.
and seide, Thou knowist the wille of Dauid, my fadir, and for he miyte not bilde an hows to the name of his God, for batels neiyynge bi cumpas, til the Lord yaf hem vndur the step of hise feet.
4 Lakini sasa BWANA amenipa mimi pumziko toka pande zote. Hakuna maadui wala majanga.
Now forsothe my Lord God yaf reste to me bi cumpas, and noon aduersarie is, nethir yuel asailyng;
5 Kwa hiyo ninakusudia kujenga hekalu kwa jina la BWANA, Mungu wangu, kama BWANA alivyosema kwa Daudi baba yangu, akisema, 'Mwanao ambaye nitamweka kwenye kiti chako cha enzi mahali pako, ndiye atakayenijengea hekalu kwa jina langu.'
wherfor Y thenke to buylde a temple to the name of my Lord God, as God spak to Dauid, my fadir, and seide, Thi sone, whom Y schal yyue to thee for thee on thi trone, he schal bilde an hows to my name.
6 Kwa hiyo sasa amuru wakate mierezi kutoka Lebanoni kwa ajili yangu. Watumishi wangu wataungana na watumishi wako, nami nitakulipa kwa ajili ya watumishi wako ili kwamba upate malipo mazuri kwa kila kitu utakchokubali kukifanya. Kwa kuwa unajua kuwa hakuna mtu mioingoni mwetu anayejua kukata miti kama Wasidoni.”
Therfor comaunde thou, that thi seruauntis hewe doun to me cedris of the Liban; and my seruauntis be with thi seruauntis; sotheli Y schal yyue to thee the meede of thi seruauntis, what euere meede thou schalt axe; for thou woost, that in my puple is not a man that kan hewe trees, as Sidonyes kunnen.
7 Hiramu aliposikia maneno ya Sulemani, akafurahi sana akasema, “BWANA na abarikiwe leo, ambaye amempa Daudi mwana wa hekiima juu ya kundi hili kubwa.”
Therfor whanne Hiram hadde herde the wordis of Salomon, he was ful glad, and seide, Blessid be the Lord God to dai, that yaf to Dauid a sone moost wijs on this puple ful myche.
8 Hiramu akatuma neno kwa Sulemani, akisema, “Nimeupata ujumbe ule ulionitumia. Nitatoa miti yote ya mierezi na miti ya miberoshi ambayo unahitaji.
And Hiram sente to Salomon, and seide, Y haue herde what euer thingis thou sentist to me; Y schal do al thi wille, in trees of cedres, and of beechis.
9 Watumishi wangu wataileta miti kutoka Lebanoni hadi baharini, nami nitaiendesha baharini mpaka mahali utakaponielekeza. Nitaigawa pale, nawe utaichukua. Utafanya kile ninachohitaji kwa kuwapa chakula watumishi wangu.”
My seruauntis schulen putte doun tho trees fro the Liban to the see, and Y schal araye tho trees in schippis in the see, `til to the place which thou schalt signyfie to me; and Y schal dresse tho there, that thou take tho; and thou schalt yyue necessaries to me, that mete be youun to myn hows.
10 Kwa hiyo Hiramu akampa Sulemani miti yote ya mierezi na miti ya miberoshi ambayo alihitaji.
Therfor Hiram yaf to Salomon `trees of cedres, and `trees of beechis, bi al his wille;
11 Sulemani akampa Hiramu kori ishirini elfu za ngano kwa ajili ya chakula cha watumishi wake na kori ishirii za mafuta safi. Sulemani akavitoa hivi kwa Hiramu mwaka baad ya mwaka.
forsothe Salomon yaf to Hiram twenti thousynde chorus of wheete, in to meete to his hows, and twenti chorus of pureste oile; Salomon yaf these thingis to Hiram bi alle yeeris.
12 BWANA akampa Sulemani hekima, kama alivyokuwa amemwahidi. Kulikuwa na amani kati ya Hiramu na Sulemani na wote wawili wakafanya agano.
Also the Lord yaf wisdom to Salomon, as he spak to hym; and pees was bitwixe Hiram and Salomon, and bothe smytiden boond of pees.
13 Mfalme Sulemani akaandaa wafanya kazi kutoka Israeli yote. Idadi ya watenda kazi walioandaliwa ilikuwa wanaume elfu thelathini.
And kyng Salomon chees werk men of al Israel; and the summe was thretti thousynde of men.
14 Aliwatuma kwenda Lebanoni, aliwatuma kwa zamu ya watu elfu kumi kila mwezi. Kwa mwezi mmoja walienda Lebanoni na miezi miwili walikaa nyumbani. Adoniramu ndiye aliyekuwa msimamizi wa watenda kazi.
And `Salomon sente hem in to the Liban, ten thousynde bi ech monethe bi whilis, so that in twei monethis bi whilis thei weren in her howsis; and Adonyram was on sich a summe.
15 Sulemani alikuwa na watu elfu sabini waliokuwa wabeba mizigo na watu elfu themanini wa kukata mawe milimani,
Therfor seuenti thousynde of hem, that baren burthuns, weren to Salomon, and foure score thousynde of masouns in the hil, with out the souereyns,
16 zaidi ya hao, walikuwepo maakida 3, 300 ambao pia waliokuwa wakiisimamia hiyo kazi.
that weren maistris of alle werkis, bi the noumbre of thre thousynde and thre hundrid, comaundynge to the puple, and to hem that maden werk.
17 Kwa amri ya mfalme walileta mawe makubwa ya thamani kwa ajili ya kulaza kwenye msingi wa hekalu.
And the kyng comaundide, that thei schulden take greete stonys, `and preciouse stonys, in to the foundement of the temple, and that thei schulden make tho square;
18 Kwa hiyo wajenzi wa Sulemani na wajenzi wa Hiramu na Wagebaliti walifanya kazi ya kukata na kuandaa mbao kwa ajili ya ujenzi wa hekalu.
whiche stoonys the masouns of Salomon, and the masouns of Hyram, hewiden. Forsothe Biblies maden redi trees and stonus, to the hows to be bildid.

< 1 Wafalme 5 >