< 1 Wafalme 5 >
1 Hiramu mfalme wa Tiro aliwatuma watumishi wake kwa Sulemani kwa kuwa alisikia kuwa walikuwa wamemtawaza kuwa mfalme mahali pa baba yake, kwani Hiramu alimpenda Daudi.
and to send: depart Hiram king Tyre [obj] servant/slave his to(wards) Solomon for to hear: hear for [obj] him to anoint to/for king underneath: instead father his for to love: lover to be Hiram to/for David all [the] day: always
2 Sulemani akatuma ujumbe kwa Hiramu, akisema,
and to send: depart Solomon to(wards) Hiram to/for to say
3 “Unajua kuwa Daudi baba yangu hakujenga nyumba kwa jina la BWANA, Mungu wake kwa sababu ya vile vita vilivyomzunguka, kwa kuwa wakati wa uhai wake BWANA alikuwa akiweka maadui wake chini ya nyayo za miguu yake.
you(m. s.) to know [obj] David father my for not be able to/for to build house: home to/for name LORD God his from face: because [the] battle which to turn: surround him till to give: put LORD [obj] them underneath: under palm: sole (foot my *Q(K)*)
4 Lakini sasa BWANA amenipa mimi pumziko toka pande zote. Hakuna maadui wala majanga.
and now to rest LORD God my to/for me from around: side nothing Satan and nothing chance bad: evil
5 Kwa hiyo ninakusudia kujenga hekalu kwa jina la BWANA, Mungu wangu, kama BWANA alivyosema kwa Daudi baba yangu, akisema, 'Mwanao ambaye nitamweka kwenye kiti chako cha enzi mahali pako, ndiye atakayenijengea hekalu kwa jina langu.'
and look! I to say to/for to build house: home to/for name LORD God my like/as as which to speak: speak LORD to(wards) David father my to/for to say son: child your which to give: put underneath: instead you upon throne your he/she/it to build [the] house: home to/for name my
6 Kwa hiyo sasa amuru wakate mierezi kutoka Lebanoni kwa ajili yangu. Watumishi wangu wataungana na watumishi wako, nami nitakulipa kwa ajili ya watumishi wako ili kwamba upate malipo mazuri kwa kila kitu utakchokubali kukifanya. Kwa kuwa unajua kuwa hakuna mtu mioingoni mwetu anayejua kukata miti kama Wasidoni.”
and now to command and to cut: cut to/for me cedar from [the] Lebanon and servant/slave my to be with servant/slave your and wages servant/slave your to give: pay to/for you like/as all which to say for you(m. s.) to know for nothing in/on/with us man: anyone to know to/for to cut: cut tree: wood like/as Sidonian
7 Hiramu aliposikia maneno ya Sulemani, akafurahi sana akasema, “BWANA na abarikiwe leo, ambaye amempa Daudi mwana wa hekiima juu ya kundi hili kubwa.”
and to be like/as to hear: hear Hiram [obj] word Solomon and to rejoice much and to say to bless LORD [the] day: today which to give: give to/for David son: child wise upon [the] people [the] many [the] this
8 Hiramu akatuma neno kwa Sulemani, akisema, “Nimeupata ujumbe ule ulionitumia. Nitatoa miti yote ya mierezi na miti ya miberoshi ambayo unahitaji.
and to send: depart Hiram to(wards) Solomon to/for to say to hear: hear [obj] which to send: depart to(wards) me I to make: do [obj] all pleasure your in/on/with tree: wood cedar and in/on/with tree: wood cypress
9 Watumishi wangu wataileta miti kutoka Lebanoni hadi baharini, nami nitaiendesha baharini mpaka mahali utakaponielekeza. Nitaigawa pale, nawe utaichukua. Utafanya kile ninachohitaji kwa kuwapa chakula watumishi wangu.”
servant/slave my to go down from [the] Lebanon sea [to] and I to set: make them raft in/on/with sea till [the] place which to send: depart to(wards) me and to shatter them there and you(m. s.) to lift: raise and you(m. s.) to make: do [obj] pleasure my to/for to give: give food house: household my
10 Kwa hiyo Hiramu akampa Sulemani miti yote ya mierezi na miti ya miberoshi ambayo alihitaji.
and to be Hiram to give: give to/for Solomon tree: wood cedar and tree: wood cypress all pleasure his
11 Sulemani akampa Hiramu kori ishirini elfu za ngano kwa ajili ya chakula cha watumishi wake na kori ishirii za mafuta safi. Sulemani akavitoa hivi kwa Hiramu mwaka baad ya mwaka.
and Solomon to give: give to/for Hiram twenty thousand kor wheat food to/for house: household his and twenty kor oil beaten thus to give: give Solomon to/for Hiram year in/on/with year
12 BWANA akampa Sulemani hekima, kama alivyokuwa amemwahidi. Kulikuwa na amani kati ya Hiramu na Sulemani na wote wawili wakafanya agano.
and LORD to give: give wisdom to/for Solomon like/as as which to speak: promise to/for him and to be peace between Hiram and between Solomon and to cut: make(covenant) covenant two their
13 Mfalme Sulemani akaandaa wafanya kazi kutoka Israeli yote. Idadi ya watenda kazi walioandaliwa ilikuwa wanaume elfu thelathini.
and to ascend: establish [the] king Solomon taskworker from all Israel and to be [the] taskworker thirty thousand man
14 Aliwatuma kwenda Lebanoni, aliwatuma kwa zamu ya watu elfu kumi kila mwezi. Kwa mwezi mmoja walienda Lebanoni na miezi miwili walikaa nyumbani. Adoniramu ndiye aliyekuwa msimamizi wa watenda kazi.
and to send: depart them Lebanon [to] ten thousand in/on/with month change month to be in/on/with Lebanon two month in/on/with house: home his and Adoniram upon [the] taskworker
15 Sulemani alikuwa na watu elfu sabini waliokuwa wabeba mizigo na watu elfu themanini wa kukata mawe milimani,
and to be to/for Solomon seventy thousand to lift: bearing(armour) burden and eighty thousand to hew in/on/with mountain: hill country
16 zaidi ya hao, walikuwepo maakida 3, 300 ambao pia waliokuwa wakiisimamia hiyo kazi.
to/for alone from ruler [the] to stand to/for Solomon which upon [the] work three thousand and three hundred [the] to rule in/on/with people [the] to make: do in/on/with work
17 Kwa amri ya mfalme walileta mawe makubwa ya thamani kwa ajili ya kulaza kwenye msingi wa hekalu.
and to command [the] king and to set out stone great: large stone precious to/for to found [the] house: home stone cutting
18 Kwa hiyo wajenzi wa Sulemani na wajenzi wa Hiramu na Wagebaliti walifanya kazi ya kukata na kuandaa mbao kwa ajili ya ujenzi wa hekalu.
and to hew to build Solomon and to build Hiram and [the] Gebalite and to establish: prepare [the] tree: wood and [the] stone to/for to build [the] house: home