< 1 Wafalme 5 >

1 Hiramu mfalme wa Tiro aliwatuma watumishi wake kwa Sulemani kwa kuwa alisikia kuwa walikuwa wamemtawaza kuwa mfalme mahali pa baba yake, kwani Hiramu alimpenda Daudi.
And Hiram King of Tyrus sent his seruants vnto Salomon, (for he had heard, that they had anoynted him King in the roume of his father) because Hiram had euer loued Dauid.
2 Sulemani akatuma ujumbe kwa Hiramu, akisema,
Also Salomon sent to Hiram, saying,
3 “Unajua kuwa Daudi baba yangu hakujenga nyumba kwa jina la BWANA, Mungu wake kwa sababu ya vile vita vilivyomzunguka, kwa kuwa wakati wa uhai wake BWANA alikuwa akiweka maadui wake chini ya nyayo za miguu yake.
Thou knowest that Dauid my father could not build an house vnto the Name of the Lord his God, for the warres which were about him on euery side, vntill the Lord had put them vnder the soles of his feete.
4 Lakini sasa BWANA amenipa mimi pumziko toka pande zote. Hakuna maadui wala majanga.
But now the Lord my God hath giuen me rest on euery side, so that there is neither aduersarie, nor euill to resist.
5 Kwa hiyo ninakusudia kujenga hekalu kwa jina la BWANA, Mungu wangu, kama BWANA alivyosema kwa Daudi baba yangu, akisema, 'Mwanao ambaye nitamweka kwenye kiti chako cha enzi mahali pako, ndiye atakayenijengea hekalu kwa jina langu.'
And beholde, I purpose to build an house vnto ye Name of the Lord my God, as the Lord spake vnto Dauid my father, saying, Thy sonne, whom I wil set vpon thy throne for thee, he shall build an house vnto my Name.
6 Kwa hiyo sasa amuru wakate mierezi kutoka Lebanoni kwa ajili yangu. Watumishi wangu wataungana na watumishi wako, nami nitakulipa kwa ajili ya watumishi wako ili kwamba upate malipo mazuri kwa kila kitu utakchokubali kukifanya. Kwa kuwa unajua kuwa hakuna mtu mioingoni mwetu anayejua kukata miti kama Wasidoni.”
Now therefore commaund, that they hewe me cedar trees out of Lebanon, and my seruants shall be with thy seruants, and vnto thee will I giue the hire for thy seruants, according to all that thou shalt appoynt: for thou knowest that there are none among vs, that can hewe timber like vnto the Sidonians.
7 Hiramu aliposikia maneno ya Sulemani, akafurahi sana akasema, “BWANA na abarikiwe leo, ambaye amempa Daudi mwana wa hekiima juu ya kundi hili kubwa.”
And when Hiram heard the wordes of Salomon, he reioyced greatly, and sayde, Blessed be the Lord this day, which hath giuen vnto Dauid a wise sonne ouer this mightie people.
8 Hiramu akatuma neno kwa Sulemani, akisema, “Nimeupata ujumbe ule ulionitumia. Nitatoa miti yote ya mierezi na miti ya miberoshi ambayo unahitaji.
And Hiram sent to Salomon, saying, I haue considered the things, for the which thou sentest vnto me, and will accomplish all thy desire, concerning the cedar trees and firre trees.
9 Watumishi wangu wataileta miti kutoka Lebanoni hadi baharini, nami nitaiendesha baharini mpaka mahali utakaponielekeza. Nitaigawa pale, nawe utaichukua. Utafanya kile ninachohitaji kwa kuwapa chakula watumishi wangu.”
My seruants shall bring them downe from Lebanon to the sea: and I will conuey them by sea in raftes vnto the place that thou shalt shew me, and wil cause them to be discharged there, and thou shalt receiue them: nowe thou shalt doe mee a pleasure to minister foode for my familie.
10 Kwa hiyo Hiramu akampa Sulemani miti yote ya mierezi na miti ya miberoshi ambayo alihitaji.
So Hiram gaue Salomon cedar trees and firre trees, euen his full desire.
11 Sulemani akampa Hiramu kori ishirini elfu za ngano kwa ajili ya chakula cha watumishi wake na kori ishirii za mafuta safi. Sulemani akavitoa hivi kwa Hiramu mwaka baad ya mwaka.
And Salomon gaue Hiram twentie thousand measures of wheate for foode to his householde, and twentie measures of beaten oyle. Thus much gaue Salomon to Hiram yere by yere.
12 BWANA akampa Sulemani hekima, kama alivyokuwa amemwahidi. Kulikuwa na amani kati ya Hiramu na Sulemani na wote wawili wakafanya agano.
And the Lord gaue Salomon wisedome as he promised him. And there was peace betweene Hiram and Salomon, and they two made a couenant.
13 Mfalme Sulemani akaandaa wafanya kazi kutoka Israeli yote. Idadi ya watenda kazi walioandaliwa ilikuwa wanaume elfu thelathini.
And King Salomon raised a summe out of all Israel, and the summe was thirtie thousand men:
14 Aliwatuma kwenda Lebanoni, aliwatuma kwa zamu ya watu elfu kumi kila mwezi. Kwa mwezi mmoja walienda Lebanoni na miezi miwili walikaa nyumbani. Adoniramu ndiye aliyekuwa msimamizi wa watenda kazi.
Whome he sent to Lebanon, ten thousand a moneth by course: they were a moneth in Lebanon, and two moneths at home. And Adoniram was ouer the summe.
15 Sulemani alikuwa na watu elfu sabini waliokuwa wabeba mizigo na watu elfu themanini wa kukata mawe milimani,
And Salomon had seuentie thousand that bare burdens, and fourescore thousand masons in the mountaine,
16 zaidi ya hao, walikuwepo maakida 3, 300 ambao pia waliokuwa wakiisimamia hiyo kazi.
Besides the princes, whome Salomon appoynted ouer the worke, euen three thousande and three hundreth, which ruled the people that wrought in the worke.
17 Kwa amri ya mfalme walileta mawe makubwa ya thamani kwa ajili ya kulaza kwenye msingi wa hekalu.
And the King commanded them, and they brought great stones and costly stones to make the foundation of the house, euen hewed stones.
18 Kwa hiyo wajenzi wa Sulemani na wajenzi wa Hiramu na Wagebaliti walifanya kazi ya kukata na kuandaa mbao kwa ajili ya ujenzi wa hekalu.
And Salomons workemen, and the workemen of Hiram, and the masons hewed and prepared timber and stones for the buylding of the house.

< 1 Wafalme 5 >