< 1 Wafalme 4 >

1 Mfalme Sulemani alikuwa mfalme wa Israeli.
Og Kong Salomo var Konge over al Israel.
2 Hawa ndio waliokuwa wakuu wake: Azaria mwana wa Sadoki alikuwa kuhani.
Og disse vare de fornemste Befalingsmænd, som han havde: Asarja, Zadoks Søn, var Ypperstepræst;
3 Elihorefu na Ahiya mwana wa Shisha, walikuwa makatibu. Yehoshafati mwana wa Ahilui alikuwa mwandishi.
Elihoref og Ahia, Sisas Sønner, vare Skrivere; Josafat, Ahiluds Søn, var Historieskriver;
4 Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa mkuu wa jeshi. Sadoki na Abiatahari walikuwa makuhani.
og Benaja, Jojadas Søn, var over Hæren; og Zadok og Abjathar vare Præster;
5 Azaria mwana wa Natahani ndiye aliyekuwa juu ya hawa maakida. Zabudi mwana wa Nathani alikuwa kuhani na rafiki wa mfalme.
og Asarja, Nathans Søn, var over Befalingsmændene; og Sabud, Nathans Søn, Præsten, var Kongens Ven;
6 Ahishari alikuwa mkuu wa nyumba. Adoniramu mwana wa Abda alikuwa mkuu wa watenda kazi.
og Ahisar var Hovmester; Adoniram, Abdas Søn, var Rentemester.
7 Sulemani alikuwa na maakida kumi na wawili juu ya Israeli yote, ambao walitoa chakula kwa mfalme na watu wake wote. Kila mtu alikuwa na zamu ya kuhudumia kwa mwezi mmoja katka mwaka.
Og Salomo havde tolv Befalingsmænd over al Israel, og de forsynede Kongen og hans Hus; enhver havde en Maaned om Aaret at forsyne ham udi.
8 Majina yao yalikuwa ndiyo haya: Beni Huri, Kutoka milima ya Efraimu;
Og disse vare deres Navne: Hurs Søn paa Efraims Bjerg;
9 Beni Dekeri wa Makazi, Shaalibimu, Bethi Shemeshi, na Elonbethi Hanaan;
Dekers Søn i Makaz og i Saalbim og i Beth-Semes og Elon og Beth-Hanan;
10 Beni Hesed, wa Arubothi (kutoka kwake alipatikana Sokohi na nchi yote ya Hefa);
Heseds Søn i Aruboth, han havde Soko og hele Landet Hefer;
11 Ben Abinadabu, wa wilaya yote ya Dori (alikuwa na Tafathi binti wa mfalme ambaye alikuwa mke wake);
Abinadabs Søn havde hele Egnen Dor, han havde Tafath, Salomos Datter, til Hustru;
12 Baana mwana wa Ahiludi, wa Taanaki na Megido, na Beth Shani iliyo upande mwingine wa Zarethani chini ya Yezreel, Kutoak Bethi Shani mpaka Abeli Mehola iliyo upande mwingine wa Jokimeamu;
Baena, Ahiluds Søn, havde Thaanak og Megiddo og hele Beth-Sean, som er ved Zarthan neden for Jisreel fra Beth-Sean indtil Abel-Mehola, indtil paa hin Side Jokmeam;
13 Ben Geberi, ya Ramothi Gileadi (kutoka kwake tunapata miji ya Yairi mwana wa Manase, ambayo iko Gileadi, na mkoa wa Arigobu ulikuwa wake, ambao uko Bashani, miji sitini yenye maboma na yenye nguzo za malango ya shaba);
Gebers Søn var i Ramoth i Gilead; han havde Jairs, Manasse Søns, Byer, som ere i Gilead, han havde Argobs Egn, som er i Basan, tresindstyve store Stæder med Mure og med Kobberstænger;
14 Ahinadabu mwana wa Ido, wa Mahanaimu;
Ahinadab, Iddos Søn, var i Mahanaim;
15 Ahimaazi, wa Naftali (ambaye pia alimwoa Basimathi binti wa Sulemani kuwa mke wake);
Ahimaaz var i Nafthali, han tog og Basmath, Salomos Datter, til Hustru;
16 Baana mwana wa Hushai, ya Asherina Bealothi;
Baena, Husais Søn, var i Aser og i Aloth;
17 Yehoshafati mwana wa Paruha, kwa Isakari;
Josafat, Faruas Søn, var i Isaskar;
18 Shimei mwana wa Ela, wa Benjamini;
Simei, Elas Søn, var i Benjamin;
19 na Geberi mwana wa Uri, katika nchi ya Gileadi, ambayo ni nchi ya Sihoni mfalme wa Waamori na Ogi mfalme wa Bashani, na yeye ndiye akida pekee aliyekuwa katika nchi hiyo.
Geber, Uris Søn, var i Gileads Land, i Sihons, den amoritiske Konges, og i Ogs, Kongen af Basans, Land, og det var kun een Befalingsmand, som var i dette Land.
20 Yuda na Israeli walikuwa wengi kama mchanga wa baharini. Nao walikuwa wakila na kunywa na kufurahi.
Juda og Israel vare mange som Sand, der er ved Havet i Mangfoldighed; de aade og drak og vare glade.
21 Suleimani alitawala utawala wote kutoka mtoni hadi kwenye nchi ya Wafilisti na hadi kwenye mpaka wa Misri. Wote walileta kodi na walimtumikia Sulemani katika siku za maisha yake yote.
Og Salomo var en Herre over alle Rigerne fra Floden til Filisternes Land og indtil Ægyptens Landemærke; de bragte ham Skænk og tjente Salomo alle hans Livsdage.
22 Mahitaji ya Sulemani kwa siku moja yalikuwa ni Kori thelathini za unga mzuri na kori unga wa ngano,
Og den Mad, der gik med for Salomo til hver Dag, var tredive Kor fint Mel og tresindstyve Kor Hvedemel;
23 makisai kumi walionona, na fahari ishirini wa malisho, na kondoo mia moja, nje ya ayala, paa, na kulungu na kuku walionona.
ti fede Øksne og tyve Græsøksne og hundrede Faar, foruden Hjorte og Raadyr og Bøfler og alle Haande Fjerkræ paa Sti.
24 Kwa kuwa utawala wake ulikuwa zaidi ya nchi yote upande huu wa mto, kutoka Tifsa mpaka Gaza, juu ya wafalme wote wa upande huu wa mto, naye alikuwa na amani pande zote.
Thi han herskede i alt det, som laa paa denne Side af Floden, fra Thipsa og indtil Gaza, over alle Konger paa denne Side af Floden; og han havde Fred trindt omkring paa alle sine Sider.
25 Yuda na Israeli waliishi kwa usalama, kila mtu chini y a mzabibu wake na chini ya mtini wake, kutoka Dani mpaka Beerisheba, siku zote za Sulemani.
Og Juda og Israel boede tryggelig, hver under sit Vintræ og under sit Figentræ, fra Dan og indtil Beersaba, alle Salomos Dage.
26 Sulemani alikuwa na mabanda ya farasi arobaini elfu kwa ajili ya magari yake, na wapanda farasi elfu kumi na mbili.
Salomo havde og fyrretyve Tusinde Stalde til sine Vognheste og tolv Tusinde Ryttere.
27 Na maakida walileta chakula kwa Sulemani na kwa wale walioketi kwenye meza ya mfalme Sulemani, kila mtu katika mwezi wake. Walihakikisha hakuna kinachopungua.
Og disse Befalingsmænd forsynede Kong Salomo og hver den, som nærmede sig til Kong Salomos Bord, hver i sin Maaned; de lode ikke fattes paa noget.
28 Na pia walileta kwenye eneo husika shayiri na majani kwa ajili ya wale farasi wa magari na kwa wale farasi wa mbio kila mmoja alileta kadri alivyoweza.
Og Byg og Straa til Kørehestene og til Ridehestene førte de hen til det Sted, hvor det skulde være, hver efter Anvisningen.
29 Mungu alimpa Sulemani hekima kubwa, ufahamu, na upana wa uelewa kama mchanga wa baharini.
Og Gud gav Salomo Visdom og saare megen Indsigt og en omfattende Forstand, som Sand, der er ved Havets Bred.
30 Hekima ya Sulemani ilizidi hekima ya watu wote wa mashariki na hekima yote ya Misri.
Og Salomos Visdom var større end alle Østerlændernes Visdom og end alle Ægypternes Visdom.
31 Alikuwa na hekima kuliko wanaume wote - kuliko Ethani Muezrahi, Hemani, Kaliko, na Darda, wana wa Maholi - na habari zake zikaenea hadi kwenye mataifa yote yaliyomzunguka.
Og han var visere end alle Mennesker, end Esrahiteren Ethan, og Heman og Kalkol og Darda, Mahols Sønner, og hans Navn var berømt hos alle Hedninger trindt omkring.
32 Aliongea mithali elfu tatu na idadi ya nyimbo zake zilikuwa elfu moja na tano.
Og han fremsatte tre Tusinde Ordsprog, og hans Sange vare Tusinde og fem.
33 Aliifafanua mimea, kuanzia mierezi iliyoko Lebanoni hadi Hisopo imeao ukutani. Aliwafafanua wanyama, ndege, vitu vitambaavyo na samaki. Watu walikuja kutoka mataifa yote kuisikia hekima ya Sulemani.
Og han talede om Træerne fra Cederen, som er paa Libanon, og indtil Isopen, som vokser ud af Væggen; og han talede om Dyrene og om Fuglene og om krybende Dyr og om Fiskene.
34 Watu walikuja kutoka falme zote za duniani waliosikia juu ya hekima yake.
Og man kom fra alle Folk for at høre Salomos Visdom, fra alle Konger paa Jorden, som havde hørt om hans Visdom.

< 1 Wafalme 4 >