< 1 Wafalme 3 >
1 Sulemani akawa na ushirikiano wa kindoa na Farao mfalme wa Misri. Alimwoa binti wa Farao na kumleta katika mji wa Daudi mpaka alipomaliza kujenga nyumba yake, nyumba ya BWANA, na ukuta wa Yerusalemu.
Salomon je sklenil svaštvo s faraonom, egiptovskim kraljem in vzel faraonovo hčer ter jo privedel v Davidovo mesto, dokler ni končal gradnje svoje lastne hiše, Gospodove hiše in obzidja okoli Jeruzalema.
2 Watu walikuw wakitoa sadaka kwenye maeneo ya juu, kwa sababu hapakuwa bado na nyumba iliyokuwa imejengwa kwa jina la BWANA.
Vendar pa je ljudstvo žrtvovalo na visokih krajih, ker do tistih dni ni bilo zgrajene hiše Gospodovemu imenu.
3 Sulemani alionyesha upendo wake kwa BWANA kwa kutembea katika maagizo ya Daudi baba yake, isipokuwa tu alitoa dhabihu na kuchoma uvumba mahali pa juu.
Salomon je ljubil Gospoda, hodeč po zakonih svojega očeta Davida, vendar je žrtvoval in zažigal kadilo na visokih krajih.
4 Mfalme akaenda Gibioni kutoa sadaka kule, kwa kuwa hilo ndilo lilikuwa eneo kuu la juu. Sulemani katoa sadaka maelfu katika madhabu hiyo.
Kralj je odšel do Gibeóna, da tam žrtvuje, kajti to je bil ugleden visok kraj [in] na tistem oltarju je Salomon daroval tisoč žgalnih daritev.
5 BWANA akaonekana kwa Sulemani huko Gibioni katika ndoto ya usiku; akasema, “Omba! uanataka nikupe nini?”
V Gibeónu se je Gospod v sanjah ponoči prikazal Salomonu in Bog je rekel: »Prosi, kaj naj ti dam.«
6 Kwa hiyo Sulemani akasema, “umeonyesha uaminifu wa agano mkuu kwa mtumishi wako, Daudi baba yangu, kwa sababu alitembea mbele yako kwa ukweli na uaminifu, katika haki ya moyo na katika unyofu wa moyo. Umetunza kwa ajili yake hili agano kuu kwa uaminifu na umempa mwana wake kuketi kwenye kiti chake cha enzi leo.
Salomon je rekel: »Svojemu služabniku, mojemu očetu Davidu, si izkazal veliko milost, kakor je hodil pred teboj v resnici, v pravičnosti in v iskrenosti srca s teboj in si zanj ohranil to veliko prijaznost, da si mu dal sina, da sedi na njegovem prestolu, kakor je to ta dan.
7 Na sasa, BWANA, Mungu wangu, umemfanya mtumishi wako kuwa mfalme katika nafasi ya Daudi baba yangu, japo mimi ni mtoto mdogo. Sijui namna ya kuiingia na kutoka.
Sedaj, oh Gospod, moj Bog, svojega služabnika si naredil kralja namesto mojega očeta Davida. Jaz pa sem samo majhen otrok. Ne vem kako odhajati ali prihajati.
8 Mtumishi wako yuko katikati ya watu wako uliowachagua, kundi kubwa, watu wangi wasiohesabika.
Tvoj služabnik je v sredi tvojega ljudstva, ki si ga izbral, velikega ljudstva, ki zaradi množice ne more biti niti našteto niti prešteto.
9 Kwa hiyo umpe mtumishi wako moyo wa uelewa wa kuwahukumu watu wako. Kwani ni nani awezaye kuwahukumu watu wako hawa walio wengi?”
Daj torej svojemu služabniku razumevajoče srce, da sodi tvoje ljudstvo, da bom lahko razločeval med dobrim in slabim, kajti kdo je zmožen soditi to tvoje tako veliko ljudstvo?«
10 Ombi hili la Sulemani likampendeza Bwana.
Govor je ugajal Gospodu, da je Salomon prosil to stvar.
11 Kwa hiyo Mungu akamwambia. “Kwa sababu umeomba jambo hili na haujajiombea maisha marefu au utajiri au uhai wa maadui wako, lakini umeomba ufahamu wa kutambua hukumu ya haki,
Bog mu je rekel: »Ker si prosil to stvar in zase nisi prosil dolgega življenja, niti zase nisi prosil bogastev, niti nisi prosil za življenja svojih sovražnikov, temveč si zase prosil razumevanje, da razsojaš sodbo;
12 Tazama sasa nitafanya yote uliyoniomba wakati uliponipa ombi lako. Ninakupa moyo wa hekima na ufahamu, kwa kuwa hapajawahi kuwa na mtu wa kuwa kama wewe kabla yako, na hakuna wa kuwa kama wewe atakayeinuka baada yako.
glej, storil sem glede na tvoje besede, glej, dal sem ti modrost in razumevajoče srce, tako da pred teboj ni bilo nikogar podobnega tebi niti za teboj ne bo vstal nihče podoben tebi.
13 Pia ninakupa hata ambayo hujaomba, vyote heshima na utajiri, ili kwamba pasije pakawa na mfalme wa kuwa kama wewe katika siku zako zote.
Dal sem ti tudi to, česar nisi prosil, tako bogastva kakor čast, tako da vse tvoje dni med kralji ne bo nobenega kralja podobnega tebi.
14 Kama utatembea katika njia zangu na kuyatunza maagizo yangu na maagizo yangu, kama alivyofanya baba yako Daudi, ndipo nitakapoziongeza siku zako.”
Če boš hodil po mojih poteh, da varuješ moje zakone in moje zapovedi, kakor je hodil tvoj oče David, potem bom podaljšal tvoje dni.«
15 Kisha Sulemani alipoamka, na tazama, ilikuwa ndoto. Akaja Yerusalemu na akasimama mbele ya sanduku na agano la Bwana. Akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, na akawafanyia sherehe watumishi wake wote.
Salomon se je prebudil in glej, to so bile sanje. Prišel je v Jeruzalem, stopil pred skrinjo Gospodove zaveze in daroval žgalne daritve, mirovne daritve in vsem svojim služabnikom priredil gostijo.
16 Kisha wanawake wawili waliokuwa makahaba wakaja mbele ya mfalme wakasimama mbele yake.
Potem sta prišli h kralju dve ženski, ki sta bili pocestnici in obstali pred njim.
17 Mwanamke mmoja akasema, “Aa, bwana wangu, mwanamke huyu na mimi tunaishi katika nyumba moja, Nilizaa mtoto tukiwa pamoj na yeye katika nyumba yetu.
Ena ženska je rekla: »Oh moj gospod, jaz in ta ženska stanujeva v eni hiši in rodila sem otroka, z njo v hiši.
18 Ikatokea siku ya tatu baada ya kujifungua na yeye akajifungua. Tulikuwa sisi tu. Hapakuwepo na mtu mwingine yeyote katika nyumba yetu, ila sisi tu wawili katika hiyo nyumba.
Tretji dan pa se je pripetilo, potem ko sem rodila, da je tudi ta ženska rodila in bili sva skupaj. Z nama v hiši ni bilo nobenega tujca, razen naju dveh v hiši.
19 Kisha mtoto wa mwanamke huyu akafa wakati wa usiku, kwa sababu alimlalia.
Otrok te ženske pa je ponoči umrl, ker ga je prekrila.
20 kwa hiyo akamka wakati huo wa usiku wa manane akamchukua mwanangu toka pembeni yangu, wakati mimi mtumishi wako nilipokuwa usingizini, na akamlaza kwenye kifua chake, na akamlaza mtoto wake aliyekufa juu ya kifua changu.
Ona pa je opolnoči vstala in mojega sina vzela od mene, medtem ko je tvoja pomočnica spala in si ga položila v svoje naročje, svojega mrtvega pa je položila v moje naročje.
21 Asubuhi nilipoamka ili kumhudumia mwanangu, nikaona kuwa alikuwa amekufa. Lakini nilipomwangalia kwa makini wakati huo wa asubuhi, nikagundua kuwa hakuwa yule mwanangu niliyezaa,”
Ko sem zjutraj vstala, da podojim svojega otroka, glej, je bil ta mrtev. Toda ko sem to zjutraj preudarjala, glej, to ni bil moj sin, ki sem ga rodila.«
22 Yule mwanamke mwingine akasema, “Hapana, Huyu aliye hai ndiye wangu. Na yule aliyekufa ndiye wako.” Yule mwanamke wa kwanza akasema, “Hapana, Yule mtoto aliyekufa ndiye mwanao, na huyu aliye hai ndiye wangu.” Hivi ndivyo walivyoongea mbele ya mfalme.
Druga ženska pa je rekla: »Ne, temveč živi je moj sin, mrtvi pa je tvoj sin.« Ta pa je rekla: »Ne, temveč mrtvi je tvoj sin, živi pa je moj sin.« Tako sta govorili pred kraljem.
23 Kisha mfalme akasema, “Mmoja wenu anasema, 'huyu aliye hai ni wangu, na kumbe mwanao ndiye aliye kufa,'na mwingine naye anasema, 'Hapana, mwanao ni yule aliyekufa, na mwanangu ni huyu aliye hai.'”
Potem je kralj rekel: »Ena pravi: ›Ta je moj sin, ki živi, tvoj sin pa je mrtev.‹ Druga pa pravi: ›Ne, temveč je mrtvi tvoj sin, moj sin pa živi.‹«
24 Mfalme akasema, ''Nileteeni upanga.” Kwa hiyo wakaleta upanga kwa mfalme.
Kralj je rekel: »Prinesite mi meč.« Meč so prinesli pred kralja.
25 Kisha mfalme akasema, “Mgawe mtoto aliye hai katika vipande viwili, na huyu mwanamke apewe nusu na yule mwingine naye apewe nusu.”
Kralj je rekel: »Živega otroka razdelite na pol in polovico dajte eni, polovico pa drugi.«
26 Yule mwanamke mwenye mtoto aliyekuwa hai akamwambia mfalme, kwa kuwa moyo wake ulikuwa na huruma sana kwa mwanae, akasema, “Aa, bwana wangu, mpatie huyu mtoto aliye hai, na usimwue kamwe.” Lakini yule mwanamke mwingine akasema, “Hatakuwa wangu wala wako. Mgawe.”
Potem je kralju spregovorila ženska, od katere je bil živi otrok, kajti njena notranjost je hrepenela za svojim sinom in rekla: »Oh moj gospod, izročite ji živega otroka in nikakor ga ne ubijte.« Druga pa je rekla: »Naj ne bo niti moj niti tvoj, temveč ga razdelite.«
27 Ndipo mfalme aliposema, “Mpe yule mwanamke wa kwanza mtoto aliye hai, na kamwe usimwue. Yeye ndiye mama wa mtoto huyu.”
Potem je kralj odgovoril in rekel: »Njej dajte živega otroka in ga nikakor ne ubijte. Ona je njegova mati.«
28 Israeli wote waliposikia hukumu ambayo mafalme ametoa, walimwogopa mfalme, kwa sababu waliona kuwa hekima ya Mungu ilikuwa ndani yake kwa ajili ya kutoa kuhukumu.
Ves Izrael je slišal o sodbi, ki jo je kralj razsodil in bali so se kralja, kajti videli so, da je bila v njem Božja modrost, da razsoja.