< 1 Wafalme 3 >

1 Sulemani akawa na ushirikiano wa kindoa na Farao mfalme wa Misri. Alimwoa binti wa Farao na kumleta katika mji wa Daudi mpaka alipomaliza kujenga nyumba yake, nyumba ya BWANA, na ukuta wa Yerusalemu.
Mais le peuple sacrifiait encore sur les hauts lieux, parce que le temple du Seigneur n'était pas encore bâti.
2 Watu walikuw wakitoa sadaka kwenye maeneo ya juu, kwa sababu hapakuwa bado na nyumba iliyokuwa imejengwa kwa jina la BWANA.
Mais le peuple sacrifiait encore sur les hauts lieux, parce que le temple du Seigneur n'était pas encore bâti.
3 Sulemani alionyesha upendo wake kwa BWANA kwa kutembea katika maagizo ya Daudi baba yake, isipokuwa tu alitoa dhabihu na kuchoma uvumba mahali pa juu.
Or, Salomon aimait le Seigneur, et marchait en la voie des commandements du roi David son père; seulement il sacrifiait et encensait sur, les hauts lieux.
4 Mfalme akaenda Gibioni kutoa sadaka kule, kwa kuwa hilo ndilo lilikuwa eneo kuu la juu. Sulemani katoa sadaka maelfu katika madhabu hiyo.
Et il partit pour Gabaon, afin d'y offrir un sacrifice; car c'était le lieu le plus élevé et le plus célèbre. Salomon offrit en holocauste mille victimes sur l'autel de Gabaon.
5 BWANA akaonekana kwa Sulemani huko Gibioni katika ndoto ya usiku; akasema, “Omba! uanataka nikupe nini?”
Et la nuit venue, le Seigneur apparut à Salomon pendant son sommeil, et le Seigneur lui dit: Demande-moi quelque chose pour toi.
6 Kwa hiyo Sulemani akasema, “umeonyesha uaminifu wa agano mkuu kwa mtumishi wako, Daudi baba yangu, kwa sababu alitembea mbele yako kwa ukweli na uaminifu, katika haki ya moyo na katika unyofu wa moyo. Umetunza kwa ajili yake hili agano kuu kwa uaminifu na umempa mwana wake kuketi kwenye kiti chake cha enzi leo.
Et Salomon répondit: Vous avez usé d'une grande miséricorde envers mon père David votre serviteur, parce qu'il avait marché devant vous dans les voies de la vérité et de la justice, et dans la droiture du cœur. Et gardant envers lui cette grande miséricorde, vous avez fait monter son fils sur le trône où il est aujourd'hui.
7 Na sasa, BWANA, Mungu wangu, umemfanya mtumishi wako kuwa mfalme katika nafasi ya Daudi baba yangu, japo mimi ni mtoto mdogo. Sijui namna ya kuiingia na kutoka.
Vous venez, Seigneur mon Dieu, de mettre à la place de David mon père, moi votre serviteur, moi qui suis encore un jeune adolescent, et qui ne sais encore ni entrer, ni sortir.
8 Mtumishi wako yuko katikati ya watu wako uliowachagua, kundi kubwa, watu wangi wasiohesabika.
Et votre serviteur se trouve au milieu de votre peuple, du peuple nombreux que vous vous êtes choisi, d'un peuple innombrable.
9 Kwa hiyo umpe mtumishi wako moyo wa uelewa wa kuwahukumu watu wako. Kwani ni nani awezaye kuwahukumu watu wako hawa walio wengi?”
Donnez donc à votre serviteur un cœur qui écoute, qui juge votre peuple selon la justice, et qui sache discerner le bien et le mal; car qui pourrait juger votre peuple, ce peuple puissant?
10 Ombi hili la Sulemani likampendeza Bwana.
Et il fut agréable au Seigneur que Salomon eût fait cette demande.
11 Kwa hiyo Mungu akamwambia. “Kwa sababu umeomba jambo hili na haujajiombea maisha marefu au utajiri au uhai wa maadui wako, lakini umeomba ufahamu wa kutambua hukumu ya haki,
Et le Seigneur lui dit: Parce que tu m'as demandé cette chose, et que tu ne m'as pas demandé pour toi de longs jours, que tu ne m'as pas demandé des richesses, que tu ne m'as pas demandé la mort de tes ennemis, mais que tu m'as demandé pour toi la sagesse, afin de discerner ce qui est juste,
12 Tazama sasa nitafanya yote uliyoniomba wakati uliponipa ombi lako. Ninakupa moyo wa hekima na ufahamu, kwa kuwa hapajawahi kuwa na mtu wa kuwa kama wewe kabla yako, na hakuna wa kuwa kama wewe atakayeinuka baada yako.
J'ai déjà fait selon ta parole: voilà que je t'ai doué d'un cœur prudent et sage; il n'a existé avant toi personne qui te ressemble, et après toi, on ne verra jamais ton semblable.
13 Pia ninakupa hata ambayo hujaomba, vyote heshima na utajiri, ili kwamba pasije pakawa na mfalme wa kuwa kama wewe katika siku zako zote.
Je t'ai donné, en outre, ce que tu n'as pas demandé, la richesse et la gloire, au point que nul des rois ne t'a jamais égalé.
14 Kama utatembea katika njia zangu na kuyatunza maagizo yangu na maagizo yangu, kama alivyofanya baba yako Daudi, ndipo nitakapoziongeza siku zako.”
Si tu marches en ma voie comme a marché David ton père, en gardant mes commandements et mes ordonnances, je t'accorderai, de plus, de longs jours.
15 Kisha Sulemani alipoamka, na tazama, ilikuwa ndoto. Akaja Yerusalemu na akasimama mbele ya sanduku na agano la Bwana. Akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, na akawafanyia sherehe watumishi wake wote.
Et Salomon s'éveilla, et il n'oublia point ce songe; il se leva, et rentra dans Jérusalem; il se plaça debout devant l'autel et devant l'arche du Seigneur en Sion; puis, il sacrifia des holocaustes et des hosties pacifiques; enfin il fit préparer un grand festin pour lui-même et pour tous ses serviteurs.
16 Kisha wanawake wawili waliokuwa makahaba wakaja mbele ya mfalme wakasimama mbele yake.
Alors, deux femmes prostituées apparurent en présence du roi, et elles se tinrent debout devant lui.
17 Mwanamke mmoja akasema, “Aa, bwana wangu, mwanamke huyu na mimi tunaishi katika nyumba moja, Nilizaa mtoto tukiwa pamoj na yeye katika nyumba yetu.
L'une des deux femmes dit: Je te prie, Seigneur: Moi et cette femme nous habitons la même maison, et dans cette maison nous avons enfanté.
18 Ikatokea siku ya tatu baada ya kujifungua na yeye akajifungua. Tulikuwa sisi tu. Hapakuwepo na mtu mwingine yeyote katika nyumba yetu, ila sisi tu wawili katika hiyo nyumba.
Trois jours après que je fus accouchée, cette femme est accouchée aussi; nous étions ensemble, et il n'y avait personne que nous deux dans la maison.
19 Kisha mtoto wa mwanamke huyu akafa wakati wa usiku, kwa sababu alimlalia.
Or, l'enfant de cette femme est mort la nuit dernière, parce qu'elle s'était couchée sur lui.
20 kwa hiyo akamka wakati huo wa usiku wa manane akamchukua mwanangu toka pembeni yangu, wakati mimi mtumishi wako nilipokuwa usingizini, na akamlaza kwenye kifua chake, na akamlaza mtoto wake aliyekufa juu ya kifua changu.
Et elle s'est levée au milieu de la nuit; et elle a pris mon enfant dans mes bras, et elle l'a mis en son sein; et son fils mort elle l'a placé en mon sein.
21 Asubuhi nilipoamka ili kumhudumia mwanangu, nikaona kuwa alikuwa amekufa. Lakini nilipomwangalia kwa makini wakati huo wa asubuhi, nikagundua kuwa hakuwa yule mwanangu niliyezaa,”
Je me suis réveillée de grand matin pour allaiter mon fils, et l'enfant était mort; or, comme je le regardais bien attentivement aux premières lueurs du jour, je vis que ce n'était pas le fils que j'avais enfanté.
22 Yule mwanamke mwingine akasema, “Hapana, Huyu aliye hai ndiye wangu. Na yule aliyekufa ndiye wako.” Yule mwanamke wa kwanza akasema, “Hapana, Yule mtoto aliyekufa ndiye mwanao, na huyu aliye hai ndiye wangu.” Hivi ndivyo walivyoongea mbele ya mfalme.
L'autre femme s'écria: Du tout, mais mon fils est vivant, c'est ton fils qui est mort. Et elles parlaient ainsi devant le roi.
23 Kisha mfalme akasema, “Mmoja wenu anasema, 'huyu aliye hai ni wangu, na kumbe mwanao ndiye aliye kufa,'na mwingine naye anasema, 'Hapana, mwanao ni yule aliyekufa, na mwanangu ni huyu aliye hai.'”
Et le roi dit à l'une: Tu dis: Celui-ci, le vivant, est mon fils, et le fils de cette femme est mort; puis il dit à l'autre: Tu dis: Du tout, mais mon fils est vivant, et c'est ton fils qui est mort.
24 Mfalme akasema, ''Nileteeni upanga.” Kwa hiyo wakaleta upanga kwa mfalme.
Et le roi ajouta: Que l'on prenne un glaive. Et l'on apporta un glaive devant le roi.
25 Kisha mfalme akasema, “Mgawe mtoto aliye hai katika vipande viwili, na huyu mwanamke apewe nusu na yule mwingine naye apewe nusu.”
Et le roi dit: Coupez en deux cet enfant vivant qui est à la mamelle, donnez-en la moitié à celle-ci, la moitié à celle-là.
26 Yule mwanamke mwenye mtoto aliyekuwa hai akamwambia mfalme, kwa kuwa moyo wake ulikuwa na huruma sana kwa mwanae, akasema, “Aa, bwana wangu, mpatie huyu mtoto aliye hai, na usimwue kamwe.” Lakini yule mwanamke mwingine akasema, “Hatakuwa wangu wala wako. Mgawe.”
Et la femme à qui était l'enfant vivant se hâta de parler au roi, car ses entrailles étaient troublées à cause de son fils, et elle dit: Je te prie, Seigneur, qu'on lui donne l'enfant, qu'on ne le fasse pas mourir. Mais l'autre dit: Qu'il ne soit ni pour elle, ni pour moi, partagez-le.
27 Ndipo mfalme aliposema, “Mpe yule mwanamke wa kwanza mtoto aliye hai, na kamwe usimwue. Yeye ndiye mama wa mtoto huyu.”
Et le roi prit la parole, et il dit: Donnez l'enfant à celle qui a dit: Donnez-lui l'enfant, ne le faites pas mourir; celle-là est sa mère.
28 Israeli wote waliposikia hukumu ambayo mafalme ametoa, walimwogopa mfalme, kwa sababu waliona kuwa hekima ya Mungu ilikuwa ndani yake kwa ajili ya kutoa kuhukumu.
Et tout Israël citât le jugement qu'avait rendu le roi, et ils eurent crainte du roi, car ils virent que la sagesse de Dieu était en lui quand il rendait la justice.

< 1 Wafalme 3 >