< 1 Wafalme 3 >
1 Sulemani akawa na ushirikiano wa kindoa na Farao mfalme wa Misri. Alimwoa binti wa Farao na kumleta katika mji wa Daudi mpaka alipomaliza kujenga nyumba yake, nyumba ya BWANA, na ukuta wa Yerusalemu.
Salomon fit une alliance matrimoniale avec Pharaon, roi d'Égypte. Il prit la fille de Pharaon et l'amena dans la cité de David jusqu'à ce qu'il ait fini de construire sa propre maison, la maison de Yahvé et la muraille autour de Jérusalem.
2 Watu walikuw wakitoa sadaka kwenye maeneo ya juu, kwa sababu hapakuwa bado na nyumba iliyokuwa imejengwa kwa jina la BWANA.
Cependant, le peuple sacrifiait sur les hauts lieux, car il n'y avait pas encore de maison construite au nom de Yahvé.
3 Sulemani alionyesha upendo wake kwa BWANA kwa kutembea katika maagizo ya Daudi baba yake, isipokuwa tu alitoa dhabihu na kuchoma uvumba mahali pa juu.
Salomon aimait l'Éternel et suivait les lois de David, son père, sauf qu'il offrait des sacrifices et brûlait des parfums sur les hauts lieux.
4 Mfalme akaenda Gibioni kutoa sadaka kule, kwa kuwa hilo ndilo lilikuwa eneo kuu la juu. Sulemani katoa sadaka maelfu katika madhabu hiyo.
Le roi alla à Gabaon pour y sacrifier, car c'était le grand haut lieu. Salomon offrit mille holocaustes sur cet autel.
5 BWANA akaonekana kwa Sulemani huko Gibioni katika ndoto ya usiku; akasema, “Omba! uanataka nikupe nini?”
À Gabeon, Yahvé apparut en songe à Salomon, la nuit, et Dieu lui dit: « Demande ce que je dois te donner. »
6 Kwa hiyo Sulemani akasema, “umeonyesha uaminifu wa agano mkuu kwa mtumishi wako, Daudi baba yangu, kwa sababu alitembea mbele yako kwa ukweli na uaminifu, katika haki ya moyo na katika unyofu wa moyo. Umetunza kwa ajili yake hili agano kuu kwa uaminifu na umempa mwana wake kuketi kwenye kiti chake cha enzi leo.
Salomon dit: « Tu as montré à ton serviteur David, mon père, une grande bonté, parce qu'il a marché devant toi dans la vérité, dans la droiture et dans la droiture de cœur avec toi. Tu as gardé pour lui cette grande bonté, en lui donnant un fils pour s'asseoir sur son trône, comme c'est le cas aujourd'hui.
7 Na sasa, BWANA, Mungu wangu, umemfanya mtumishi wako kuwa mfalme katika nafasi ya Daudi baba yangu, japo mimi ni mtoto mdogo. Sijui namna ya kuiingia na kutoka.
Maintenant, Yahvé mon Dieu, tu as établi ton serviteur comme roi à la place de David, mon père. Je ne suis qu'un petit enfant. Je ne sais ni sortir ni entrer.
8 Mtumishi wako yuko katikati ya watu wako uliowachagua, kundi kubwa, watu wangi wasiohesabika.
Ton serviteur est au milieu de ton peuple que tu as choisi, un grand peuple, qui ne peut être ni dénombré ni compté pour la multitude.
9 Kwa hiyo umpe mtumishi wako moyo wa uelewa wa kuwahukumu watu wako. Kwani ni nani awezaye kuwahukumu watu wako hawa walio wengi?”
Donne donc à ton serviteur un cœur compréhensif pour juger ton peuple, afin que je puisse discerner le bien du mal; car qui est capable de juger ton grand peuple? »
10 Ombi hili la Sulemani likampendeza Bwana.
Cette demande plut à l'Éternel, car Salomon avait demandé cette chose.
11 Kwa hiyo Mungu akamwambia. “Kwa sababu umeomba jambo hili na haujajiombea maisha marefu au utajiri au uhai wa maadui wako, lakini umeomba ufahamu wa kutambua hukumu ya haki,
Dieu lui dit: « Parce que tu as demandé cela, et que tu n'as pas demandé pour toi une longue vie, ni la richesse pour toi-même, ni la vie de tes ennemis, mais que tu as demandé pour toi l'intelligence pour discerner la justice,
12 Tazama sasa nitafanya yote uliyoniomba wakati uliponipa ombi lako. Ninakupa moyo wa hekima na ufahamu, kwa kuwa hapajawahi kuwa na mtu wa kuwa kama wewe kabla yako, na hakuna wa kuwa kama wewe atakayeinuka baada yako.
voici, j'ai fait selon ta parole. Voici, je t'ai donné un cœur sage et compréhensif, de sorte qu'il n'y a eu personne comme toi avant toi, et qu'après toi, il n'y aura personne comme toi.
13 Pia ninakupa hata ambayo hujaomba, vyote heshima na utajiri, ili kwamba pasije pakawa na mfalme wa kuwa kama wewe katika siku zako zote.
Je t'ai aussi donné ce que tu n'as pas demandé, la richesse et la gloire, de sorte qu'il n'y aura pas de roi comme toi pendant toute ta vie.
14 Kama utatembea katika njia zangu na kuyatunza maagizo yangu na maagizo yangu, kama alivyofanya baba yako Daudi, ndipo nitakapoziongeza siku zako.”
Si tu marches dans mes voies, pour observer mes lois et mes commandements, comme a marché ton père David, j'allongerai tes jours. »
15 Kisha Sulemani alipoamka, na tazama, ilikuwa ndoto. Akaja Yerusalemu na akasimama mbele ya sanduku na agano la Bwana. Akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, na akawafanyia sherehe watumishi wake wote.
Salomon se réveilla; et voici, c'était un rêve. Il vint à Jérusalem, se plaça devant l'arche de l'alliance de Yahvé, offrit des holocaustes et des sacrifices de paix, et fit un festin pour tous ses serviteurs.
16 Kisha wanawake wawili waliokuwa makahaba wakaja mbele ya mfalme wakasimama mbele yake.
Alors deux femmes qui se prostituaient vinrent auprès du roi et se présentèrent devant lui.
17 Mwanamke mmoja akasema, “Aa, bwana wangu, mwanamke huyu na mimi tunaishi katika nyumba moja, Nilizaa mtoto tukiwa pamoj na yeye katika nyumba yetu.
L'une d'elles dit: « Oh, mon seigneur, cette femme et moi habitons dans une même maison. J'ai accouché d'un enfant avec elle dans la maison.
18 Ikatokea siku ya tatu baada ya kujifungua na yeye akajifungua. Tulikuwa sisi tu. Hapakuwepo na mtu mwingine yeyote katika nyumba yetu, ila sisi tu wawili katika hiyo nyumba.
Le troisième jour après mon accouchement, cette femme a aussi accouché. Nous étions ensemble. Il n'y avait pas d'étranger avec nous dans la maison, seulement nous deux dans la maison.
19 Kisha mtoto wa mwanamke huyu akafa wakati wa usiku, kwa sababu alimlalia.
L'enfant de cette femme mourut pendant la nuit, parce qu'elle était couchée sur lui.
20 kwa hiyo akamka wakati huo wa usiku wa manane akamchukua mwanangu toka pembeni yangu, wakati mimi mtumishi wako nilipokuwa usingizini, na akamlaza kwenye kifua chake, na akamlaza mtoto wake aliyekufa juu ya kifua changu.
Elle s'est levée à minuit, a pris mon fils à côté de moi, pendant que ton serviteur dormait, et l'a mis dans son sein; elle a mis son enfant mort dans mon sein.
21 Asubuhi nilipoamka ili kumhudumia mwanangu, nikaona kuwa alikuwa amekufa. Lakini nilipomwangalia kwa makini wakati huo wa asubuhi, nikagundua kuwa hakuwa yule mwanangu niliyezaa,”
Lorsque je me levai le matin pour allaiter mon enfant, voici qu'il était mort; mais lorsque je l'eus regardé le matin, voici que ce n'était pas mon fils que j'avais porté. »
22 Yule mwanamke mwingine akasema, “Hapana, Huyu aliye hai ndiye wangu. Na yule aliyekufa ndiye wako.” Yule mwanamke wa kwanza akasema, “Hapana, Yule mtoto aliyekufa ndiye mwanao, na huyu aliye hai ndiye wangu.” Hivi ndivyo walivyoongea mbele ya mfalme.
L'autre femme a dit: « Non! Mais celui qui vit est mon fils, et celui qui est mort est ton fils. » Le premier dit: « Non! Mais le mort est ton fils, et le vivant est mon fils. » Ils se disputèrent ainsi devant le roi.
23 Kisha mfalme akasema, “Mmoja wenu anasema, 'huyu aliye hai ni wangu, na kumbe mwanao ndiye aliye kufa,'na mwingine naye anasema, 'Hapana, mwanao ni yule aliyekufa, na mwanangu ni huyu aliye hai.'”
Alors le roi dit: « L'un dit: C'est mon fils qui vit, et ton fils est le mort; et l'autre dit: Non! Mais ton fils est le mort, et mon fils est le vivant. »
24 Mfalme akasema, ''Nileteeni upanga.” Kwa hiyo wakaleta upanga kwa mfalme.
Le roi dit: « Apportez-moi une épée. » Ils apportèrent donc une épée devant le roi.
25 Kisha mfalme akasema, “Mgawe mtoto aliye hai katika vipande viwili, na huyu mwanamke apewe nusu na yule mwingine naye apewe nusu.”
Le roi dit: « Divisez l'enfant vivant en deux, donnez-en la moitié à l'un et la moitié à l'autre. »
26 Yule mwanamke mwenye mtoto aliyekuwa hai akamwambia mfalme, kwa kuwa moyo wake ulikuwa na huruma sana kwa mwanae, akasema, “Aa, bwana wangu, mpatie huyu mtoto aliye hai, na usimwue kamwe.” Lakini yule mwanamke mwingine akasema, “Hatakuwa wangu wala wako. Mgawe.”
Alors la femme à qui appartenait l'enfant vivant parla au roi, car son cœur se languissait de son fils, et elle dit: « Oh, mon seigneur, donne-lui l'enfant vivant, et ne le tue en aucun cas! ». Mais l'autre a dit: « Il ne sera ni à moi ni à toi. Divise-le. »
27 Ndipo mfalme aliposema, “Mpe yule mwanamke wa kwanza mtoto aliye hai, na kamwe usimwue. Yeye ndiye mama wa mtoto huyu.”
Le roi répondit: « Donne à la première femme l'enfant vivant, et ne le tue surtout pas. Elle est sa mère. »
28 Israeli wote waliposikia hukumu ambayo mafalme ametoa, walimwogopa mfalme, kwa sababu waliona kuwa hekima ya Mungu ilikuwa ndani yake kwa ajili ya kutoa kuhukumu.
Tout Israël apprit le jugement que le roi avait rendu, et ils craignirent le roi, car ils virent que la sagesse de Dieu était en lui pour faire justice.