< 1 Wafalme 22 >

1 Miaka mitatu ilipita bila kuwepo na vita kati ya Washami na Wisraeli.
And they remained three years there not [was] war between Aram and between Israel.
2 Ikawa katika mwaka wa tatu, Yehoshafati mfalme wa Israeli akashuka kwa mfalme wa Isreli.
And it was in the year third and he went down Jehoshaphat [the] king of Judah to [the] king of Israel.
3 Mfalme wa Israeli alikuwa amewaambia watumishi wake, “Je, mnajua kuwa Ramothi Gileadi ni yetu, ila hatufanyi chochote kuitwaa kutoka kwenye mkono wa mfalme wa Shamu?”
And he said [the] king of Israel to servants his ¿ do you know that [belongs] to us Ramoth Gilead and we [are] inactive from taking it from [the] hand of [the] king of Aram.
4 Kwa hiyo akamwambia Yehoshafati, “Je, utakwenda na mimi katika vita huko Ramothi Gileadi?” Yehoshafati akamjibu mfalme wa Israeli, “Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, na farasi wangu ni kama farasi wako.”
And he said to Jehoshaphat ¿ will you go with me for battle Ramoth Gilead and he said Jehoshaphat to [the] king of Israel as me as you as people my as people your as horses my as horses your.
5 Yehoshafati akamwambia mfalme wa Israeli, “Tafadhali tafuta mwongozo kutoka neno la BWANA juu ya kile unachopaswa kufanya kwanza.”
And he said Jehoshaphat to [the] king of Israel seek please as the day [the] word of Yahweh.
6 Ndipo mfalme wa Israeli akawakusanya manabii pamoja, walikuwa wanaume elfu nne, akawaambia, “Je, niende Ramothi Gileadi kupigana, au nisiende?” Nao wakamwambia, “Ivamie, kwa kuwa Bwana ataitoa katika mkono wa mfalme.”
And he gathered [the] king of Israel the prophets about four hundred man and he said to them ¿ will I go on Ramoth Gilead for battle or? will I refrain and they said go up so he may give [it] [the] Lord in [the] hand of the king.
7 Lakini Yehoshafati akasema, “Je, hapa hayupo nabii mwingine wa BWANA ambaye tunaweza kupata ushauri?”
And he said Jehoshaphat ¿ [is] there not here a prophet of Yahweh still so we may enquire from him.
8 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Bado kuna mtu mmoja ambaye tunaweza kupata ushauri toka kwa BWANA ili kusaidia, Makaya mwana wa Imla, lakini namchukia kwa sababu huwa hanitabirii mazuri yanayonihusu, ila hunitabiria matatizo tu.” Lakini Yehoshafat akasema, “mfalme na asiseme hivyo,”
And he said [the] king of Israel - to Jehoshaphat still a man one to consult Yahweh from him and I I hate him for not he prophesies on me good that except evil Micaiah [the] son of Imlah and he said Jehoshaphat may not he speak the king thus.
9 Kisha mfalme wa Israeli akmwita akida na akamwamuru, “Kamlete Makaya mwana wa Imla, sasa hivi.”
And he summoned [the] king of Israel a court-official one and he said bring quickly! Micaiah [the] son of Imlah.
10 Wakati huo Ahabu mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wameketi kila mmoja kwenye kiti cha enzi, wamevaa mavazi yao, katika eneo la wazi kwenye lango la kuingilia Samaria, na manabii walikuwa wakiwatabiria.
And [the] king of Israel and Jehoshaphat [the] king of Judah [were] sitting each on throne his clothed garments at [the] threshing floor [the] entrance of [the] gate of Samaria and all the prophets [were] prophesying before them.
11 Sedekia mwana wa Kenaana akajitengenezea pembe za chuma akasema, “BWANA asema hivi: 'Kwa hili utawasukuma Washami mpaka watakapoisha.'”
And he made for himself Zedekiah [the] son of Kenaanah horns of iron and he said thus he says Yahweh with these you will gore Aram until destroy them.
12 Na manabii wengine wote wakasema hivyo, wakisema, “Ishambulie Ramothi Gileadi na ushinde, kwa kuwa BWANA ameiweka kwenye mkono wa mfalme.”
And all the prophets [were] prophesying thus saying go up Ramoth Gilead and succeed and he will give [it] Yahweh in [the] hand of the king.
13 Yule mjumbe aliyeenda kumwita Makaya akamwambia, akisema, “Tazama sasa, maneno ya manabii kwa kinywa kimoja wanatabiri mambo mema kwa mfalme. Tafadhali maneno yako yawe kama yao ukaseme mambo mazuri.”
And the messenger who he had gone - to summon Micaiah he spoke to him saying here! please [the] words of the prophets a mouth one [is] good to the king let it be please (word your *Q(K)*) like [the] word of one from them and you will speak good.
14 Makaya akajibu, “Kama BWANA aishivyo, kile BWANA atakachosema kwangu ndicho nitakachosema.'”
And he said Micaiah [by] [the] life of Yahweh for [that] which he will say Yahweh to me it I will speak.
15 Naye alipokuja kwa mfalme, mfalme akamwambia, “Makaya, je twende Ramothi Gileadi kupigana, au tusiende?” Makaya akamjibu, “Ivamie na ushinde. BWANA ataitoa kwenye mkono wa mfalme.”
And he came to the king and he said the king to him O Micaiah ¿ will we go against Ramoth Gilead for battle or? will we refrain and he said to him go up and succeed and he will give [it] Yahweh in [the] hand of the king.
16 Kisha mfalme akamwambia. “Je, nikutake mara ngapi ili kuniapia ukweli kwa jna la BWANA?”
And he said to him the king until how many? times [will] I make swear you that not you must speak to me only truth in [the] name of Yahweh.
17 Makaya akasema, “Ninaiona Israeli yote imesambaa kwenye milima, kama kondoo wasiokuwa na mchungaji, na BWANA amesema, 'Hawa hawana mchungaji. Kila mtu na arudi nyumbani kwake kwa amani.'”
And he said I saw all Israel scattered to the mountains like flock which not [belongs] to them a shepherd and he said Yahweh not masters [belong] to these let them return each to house his in peace.
18 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Je sikukwambia kuwa huwa hanitabirii mambo mema yanayonihusu, ila majanga tu?”
And he said [the] king of Israel to Jehoshaphat ¿ not did I say to you not he prophesies on me good that except evil.
19 Kisha Makaya akasema, “Kwa hiyo sikiliza neno la BWANA: Nimemwona BWANA akiwa ameketi kwenye kiti chake cha enzi, na majeshi yote ya mbinguni yalikuwa yamesimama karibu yake upande wake wa kulia na upande wake wa kushoto.
And he said therefore hear [the] word of Yahweh I saw Yahweh sitting on throne his and all [the] host of the heavens [was] standing at him from right his and from left his.
20 BWANA akasema, 'Ni nani atakayemdanganya Ahabu, ili kwamba apande akafie Ramothi Gileadi? Na mtu mmoja akajibu kwa njia hii, na mwingine akajbu kwa njia ile.
And he said Yahweh who? will he deceive Ahab so he may go up and he may fall at Ramoth Gilead and it said this [one] by thus and this [one] [was] saying by thus.
21 Ndipo pepo moja akajitokeza, akasimama mbele ya BWANA, akasema, 'Mimi nitamdanganya.' BWANA akmwuliza, 'Kwa jinsi gani?'
And it came forth the spirit and it stood before Yahweh and it said I I will deceive him
22 Yule pepo akamjibu, 'Nitakwenda na kuwa roho idanganyayo katika vinywa vya manabii wake,' BWANA akamjibu, 'utaweza kumdanganya, na utafanikiwa. Nenda sasa ukafanye hivyo.'
and he said Yahweh to it how? And it said I will go out and I will be a spirit of falsehood in [the] mouth of all prophets his and he said you will deceive and also you will prevail go out and do thus.
23 Tazama sasa, BWANA ameweka roho idangayo kwenye vinywa vya hawa manabii wako, na BWANA ametangaza janga kwako.”
And therefore here! he has put Yahweh a spirit of falsehood in [the] mouth of all prophets your these and Yahweh he has spoken on you evil.
24 Kisha Sedekia mwana wa Kenaana, akaja, akamzabua Makaya shavuni, akasema, “Je, yule roho wa Bwana alitokaje kwangu ili asema na wewe?”
And he drew near Zedekiah [the] son of Kenaanah and he struck Micaiah on the cheek and he said where? this did it pass on [the] spirit of Yahweh from with me to speak with you.
25 Makaya akasema, “Tazama, “utatambua hilo katika siku hiyo, utakapokimbilia katika chumba cha ndani kujificha.”
And he said Micaiah there you [are] about to see on the day that when you will go a room in a room to hide yourself.
26 Mfalme wa Israeli akamwambia mtumishi wake, “Mkamate Makaya umpeleke kwa Amoni, liwali wa mji, na kwa mwanangu, Yoashi.
And he said [the] king of Israel take Micaiah and take back him to Amon [the] official of the city and to Joash [the] son of the king.
27 Mwambie, 'mfalme anasema mweke huyo gerezani na awe anampa mkate kidogo na maji kidogo, mpaka nitakaporudi salama.'”
And you will say thus he says the king put this [one] [the] house of imprisonment and feed him bread oppression and water oppression until come I in peace.
28 Naye Makaya akasema, “Kama utarudi salama basi BWANA hajasema kupitia kinywa changu.” Na akaongeza, “Sikilizeni hili, ninyi watu.”
And he said Micaiah certainly [if] you will return in peace not he has spoken Yahweh by me and he said listen O peoples all of them.
29 Ahabu, mfalme wa Israeli, na Yehoshafati mfalme wa Yuda, wamepanda Ramothi Gileadi.
And he went up [the] king of Israel and Jehoshaphat [the] king of Judah Ramoth Gilead.
30 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Nitajibadilisha mwenyewe niende vitani, lakini wewe uvae vazi lako la kifalme.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli akajibadilisha na akaenda vitani.
And he said [the] king of Israel to Jehoshaphat I will disguise myself and I will go in the battle and you wear own clothes your and he disguised himself [the] king of Israel and he went in the battle.
31 Naye mfalme wa Shamu alikuwa amewaamuru majemedari thelathini na mbili wa magari yake, akisema, “Msimwamgamize askari wa muhimu au ambaye si wa muhimu, badala yake mshambulieni mfalme wa Israeli tu.”
And king of Aram he had commanded [the] commanders of the chariotry which [belonged] to him thirty and two saying not you must do battle with [the] small and with [the] great that except with [the] king of Israel to only him.
32 Ikawa wakati majemedari wa magari walipomwona Yehoshafati wakasema, “Hakika huyu ndiye mfalme wa Israeli.” Wakageuka ili kumshambulia, kwahiyo Yehoshafati akapiga kelele.
And it was when saw [the] commanders of the chariotry Jehoshaphat and they they said surely [is] [the] king of Israel he and they turned aside on him to do battle and he cried out Jehoshaphat.
33 Ikawa majemedari wa magari walipoona kuwa yeye hakuwa mfalme wa Israeli, wakamwacha.
And it was when saw [the] commanders of the chariotry that not [was] [the] king of Israel he and they turned back from after him.
34 Lakini mtu mmoja akavuta upinde wake kwa kubahatisha na akampiga mfalme wa Israeli katikati ya mwunganiko wa mavazi yake ya chuma. Ahabu akamawambia dereva wa gari lake, “geuza unirudishe kutoka vitani, kwa kuwa nimeumizwa sana.”
And someone he drew on the bow to innocence his and he struck [the] king of Israel between the joints and between the body armor and he said to charioteer his turn around hand your and take out me from the camp for I have been wounded.
35 Vita ikawa mbaya sana siku hiyo na mfalme akalazwazwa garini mwake akiwakabili Washami. Akafa jioni hiyo. Damu ilimwagika kutoka kwenye jeraha lake ndani ya gari.
And it went up the battle on the day that and the king he was placed in the chariot opposite to Aram and he died in the evening and it flowed [the] blood of the wound into [the] bottom of the chariot.
36 Ikawa wakati wa kuzama jua, kilio kikatawala kwa jeshi lote, wakisema, “Kila mtu arudi kwenye mji wake; na kila mtu arudi kwenye mkoa wake!”
And it passed the cry in the camp when went the sun saying everyone to city his and everyone to land his.
37 Kwa hiyo mfalme Ahabu akafa na akaletwa Samaria, wakamzika huko Samaria.
And he died the king and he came Samaria and people buried the king in Samaria.
38 Wakaliosha lile gari kwenye birika la Samaria, na mbwa wakaramba damu yake (hapa ni mahali ambapo makahaba waliogea), kama vile neno la BWANA lilivyokuwa limesema.
And someone washed off the chariot at - [the] pool of Samaria and they licked up the dogs blood his and the prostitutes they bathed according to [the] word of Yahweh which he had spoken.
39 Kwa mambo mengine yanayohusisana na Ahabu, yote ambayo alifanya, ile nyumba ya pembe aliyojenga, na miji yote aliyojenga, je, hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio cha wafalme wa Israeli?
And [the] rest of [the] matters of Ahab and all that he did and [the] house of ivory which he built and all the cities which he built ¿ not [are] they written on [the] scroll of [the] matters of the days of [the] kings of Israel.
40 Kwa hiyo Ahabu akalala pamoja na mababu zake, na Ahaziya mwanae akawa mfalme mahali pake.
And he lay down Ahab with ancestors his and he became king Ahaziah son his in place of him.
41 Kisha Yehoshafati mwana wa Asa alianza kutawala juu ya Yuda katika mwaka wa nne wa Ahabu mfalme wa Israeli.
And Jehoshaphat [the] son of Asa he became king over Judah in year four of Ahab [the] king of Israel.
42 Yehoshafati alikuwa na umri wa miaka thelathini na tano alipoanza kutawala, na akatawala Yerusalemu kwa miaka ishirini na mitano. Mama yake alikuwa Azuba, binti wa Shilhi.
Jehoshaphat [was] a son of thirty and five year[s] when became king he and twenty and five year[s] he reigned in Jerusalem and [the] name of mother his [was] Azubah [the] daughter of Shilhi.
43 Akatembea katika njia za Asa, baba yake, hakuziacha; akafanya yaliyokuwa mema mbele ya macho ya BWANA. Lakini bado mahali pa juu palikuwa hapajabomolewa. Watu walikuwa bado wanaendelea kutoa dhabihu na kufukiza uvumba mahali pa juu.
And he walked in all [the] way of Asa father his not he turned aside from it to do the right in [the] eyes of Yahweh. Only the high places not they were removed still the people [were] sacrificing and making smoke at the high places.
44 Yehoshafati akafanya amani na mfalme wa Israeli.
And he made peace Jehoshaphat with [the] king of Israel.
45 Kwa mambo mengine kuhusiana na Yehoshafati, na nguvu zake alizoonyesha, na jinsi alivyopigana vita, je, hayajaandikwa katika kitabu cha matukio cha wafalme wa Israeli?
And [the] rest of [the] matters of Jehoshaphat and might his which he did and which he waged war ¿ not [are] they written on [the] scroll of [the] matters of the days of [the] kings of Judah.
46 Aliwaondoa kutoka katka nchi wale makahaba wa kipagani waliokuwa wamebaki katika siku za baba yake Asa.
And [the] rest of the cult prostitute[s] which it remained in [the] days of Asa father his he destroyed from the land.
47 Hapakuwepo mfalme katika Edomu isipokuwa kaimu mtawala.
And [was] a king there not in Edom a deputy [was] king.
48 Yehoshafati alijenga merikebu: ziende Tarshishi na Ofri kuleta dhahabu, lakini hazikusafiri kwa sababu zile merikebu zilivunjika kule Esioni Geberi. Kisha
Jehoshaphat (he made *Q(K)*) ships of Tarshish to go Ophir towards for gold and not it went for (they were broken *Q(K)*) [the] ships at Ezion Geber.
49 Ahazia mwana wa Ahabu akamwambia Yehoshafati, “Naomba watumishi wangu waende pamoja na watumishi wako merikebuni. “Lakini Yehoshafati hakuruhusu hilo.
Then he said Ahaziah [the] son of Ahab to Jehoshaphat let them go servants my with servants your in [the] ships and not he was willing Jehoshaphat.
50 Yehoshafati akalala na mababu zake na akazikwa pamoja nao katika mji wa Daudi, babu yake; Yoramu mwanawe akawa mfalme mahali pake.
And he lay down Jehoshaphat with ancestors his and he was buried with ancestors his in [the] city of David ancestor his and he became king Jehoram son his in place of him.
51 Ahazia mwana Ahabu alianza kutawala juu ya Israeli ya Samaria katika mwaka wa kumi na saba wa mfalme Yehoshafati mfalme wa Yuda, na akatawala kwa mika miwili juu ya Israeli.
Ahaziah [the] son of Ahab he became king over Israel in Samaria in year seven-teen of Jehoshaphat [the] king of Judah and he reigned over Israel two years.
52 Naye akafanya yaliyo maovu mbele ya macho ya BWANA akatembea katika njia za baba yake, katika njia za mama yake na katika njia za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo kwazo aliifanya Israeli kufanya dhambi.
And he did the evil in [the] eyes of Yahweh and he walked in [the] way of father his and in [the] way of mother his and in [the] way of Jeroboam [the] son of Nebat who he caused to sin Israel.
53 Alimtumikia Baali na kumwabudu na kwa hiyo akamghadhabisha BWANA, Mungu wa Israeli, katika hasira, kama vile baba yake alivyofanya.
And he served Baal and he bowed down to it and he provoked to anger Yahweh [the] God of Israel according to all that he had done father his.

< 1 Wafalme 22 >