< 1 Wafalme 20 >

1 Beni Hadadi mfalme wa Shamu akakusanya jeshi lake lote pamoja. Kulikuwa na wafalme thelathini na mbili wasaidizi pamoja naye, na magari na farasi. Akapanda, akaihusuru Samaria na kupigana nayo.
Or Bénadad, roi de Syrie, assembla toute son armée, et trente-deux rois avec lui, des chevaux et des chars; puis montant, il combattait contre Samarie, et l’assiégeait.
2 Akatuma wajumbe katika mji kwa Ahabu mfalme wa Israeli, akamwambia, “Beni Hadadi anasema hivi:
Et envoyant dans la ville des messagers à Achab, roi d’Israël,
3 Fedha zako na dhahabu zako ni zangu. Pia wake zako na watoto, wale wazuri, sasa ni wangu.”
Il dit: Voici ce que dit Bénadad: Votre argent et votre or est à moi; vos femmes et vos enfants les meilleurs sont à moi.
4 Mfalme wa Israeli akajibu akasema, “Na iwe kama unavyosema, bwana wangu, mfalme. Mimi pamoja na vile nilivyo navyo ni mali yako.”
Et le roi d’Israël lui répondit: Selon votre parole, ô roi mon seigneur, je suis à vous, moi et tout ce que j’ai.
5 Wale wajumbe wakaja tena wakasema, “Beni Hadadi anasema hivi, 'Nilituma neno kwako nikisema kwamba lazima ukabidhi kwangu fedha zako, dhahabu zako, wake zako na watoto wako.
Et revenant, les messagers dirent: Voici ce que dit Bénadad, qui nous a envoyés vers vous: Vous me donnerez votre argent, votre or, vos femmes et vos fils.
6 Lakini kesho nitatuma watumishi wangu kwako wakati kama huu, nao wataichunguza nyumba yako na nyumba za watumishi wako. Nao watatia mikononi mwao na kukichukua kila wakipendacho machoni mwao.'”
Demain donc, à cette même heure, j’enverrai mes serviteurs vers vous, et ils fouilleront votre maison et la maison de vos serviteurs, et tout ce qui leur plaira, ils le prendront en leurs mains et l’emporteront.
7 Ndipo mfalme wa Israeli akawaita wazee wote wa nchi pamoja akawaambia, ''Hebu angalieni jinsi huyu mtu anavyotafuta matatizo. Amenitumia ujumbe kwamba anataka kuchukua wake zangu, watoto wangu, fedha na dhahabu zangu, nami sijamkatalia.”
Mais le roi d’Israël appela tous les anciens du pays, et dit: Considérez et voyez qu’il nous tend un piège; car il m’a envoyé pour mes femmes, pour mes fils, pour mon argent et mon or, et je n’ai pas refusé.
8 Wazee wote na watu wote wakamwambia Ahabu, “Usimsikilize wala kukubaliana na matakwa yake.”
Tous les anciens et tout le peuple lui répondirent: Ne l’écoûtez point, et ne lui cédez point.
9 Ahabu akawaambia wajumbe wa Beni Hadadi, “Mwambieni bwana wangu mfalme kwamba, 'Ninakubaliana na kila kitu ambacho kwanza uliwatuma watumishi wako kufanya kwangu, lakini sikubaliani na matakwa yako haya ya pili.'” Wale watumishi wa Beni Hadadi wakaondoka wakampelekea mrejesho Beni Hadadi.
C’est pourquoi Achab répondit aux messagers de Bénadad: Dites à mon seigneur le roi: Tout ce que vous m’avez demandé, à moi votre serviteur, au commencement, je le ferai, mais, quant à ceci, je ne le puis faire.
10 Naye Beni Hadadi akatuma tena majibu yake kwa Ahabu, akaisema, “basi miungu inifanyie hivyo na zaidi, kama hata mavumbi ya Samaria yatawatosheleza watu watu wote wanaonifuata kuchukua kila mmoja angalau konzi mkononi mwake.”
Et, étant revenus, les messagers firent leur rapport à Bénadad, et Bénadad les envoya de nouveau, et dit: Que les dieux me fassent ceci, et qu’ils ajoutent cela, si la poussière de Samarie suffit pour remplir le creux de la main de tout le peuple qui me suit!
11 Naye mfalme wa Israeli akamjibu akisema, “Mwabieni Beni Hadadi, 'Hakuna abebaye silaha yake, atakayejivuna kama wakati wa kuishusha.”'
Et répondant, le roi d’Israël dit: Dites-lui: Que celui qui a mis sa ceinture, ne se glorifie point comme celui qui l’a ôtée.
12 Beni Hadadi aliusikia ujumbe huu wakati alipokuwa akinywa, yeye na wafalme walikuwa pamoja naye waliokuwa kwenye mahema yao. Beni Hadadi akayaamuru majaeshi yake, “Jipangeni katika sehemu zenu kwa ajili ya vita.” Kwa hiyo wakajiandaa kivita ili kuuvamia mji.
Or il arriva que lorsque Bénadad reçut cette réponse, il buvait, lui et les autres rois, dans leurs pavillons, et il dit à ses serviteurs: Investissez la ville. Et ils l’investirent.
13 Tazama, nabii akaja kwa Ahabu mfalme wa Israeli akasema, “BWANA asema, 'Je umeliona hili jeshi kubwa? Tazama, nitaliweka katika mkono wako leo, nawe utatambua kuwa mimi ni BWANA.'”
Et voilà qu’un prophète, s’approchant d’Achab, roi d’Israël, lui dit: Voici ce que dit le Seigneur: Sans doute que tu as vu toute cette multitude innombrable? voilà que moi je la livrerai en ta main aujourd’hui, afin que tu saches que c’est moi qui suis le Seigneur.
14 Naye Ahabu akajibu, ''kwa nani? BWANA akamjibu akasema, “kwa kuwatumia viijana wanaotumikia maliwali wa wilaya.” kisha Ahabu akasema, “Ni nani atakayepewa hiyo vita?' BWANA akamwambia, “wewe.”
Et Achab lui demanda: Par qui? Et il lui répondit: Voici ce que dit le Seigneur: Par les serviteurs des princes des provinces. Achab ajouta: Qui commencera le combat? Et le prophète répondit: Toi.
15 Ndipo Ahabu alipowataarifu wale vijna wanaowatumikia maliwali wa wilaya. Idadi yao ilikuwa 232. Baada yao aliwahesabu wanajeshi wote, jeshi lote la Israeli; idadi yao ilikuwa elfu saba.
Achab fit donc la revue des serviteurs des princes des provinces, et il trouva le nombre de deux cent trente-deux; et après eux, il fit la revue du peuple de tous les enfants d’Israël, et il en trouva sept mille.
16 Nao wakatoka wakati wa adhuhuri. Naye Beni Hadadi alikuwa akinywa na kulewa hemani mwake, yeye na wale wafalme wadogo thelathini na mbili waliokuwa wakimsaidia.
Et ils sortirent à midi. Cependant Bénadad buvait, ivre, dans son pavillon, et avec lui les trente-deux rois qui étaient venus à son secours.
17 Wale maakida vijana waliokuwa wakiwasaidia maliwali wa wilaya walitangulia kwanza. Kisha Beni Hadadi alitaarifiwa na wanaskauti aliokuwa amewatuma kwamaba, “kuna watu wanakuja kutoka Samaria.”
Or les serviteurs des princes des provinces sortirent au premier rang. C’est pourquoi Bénadad envoya; et on lui annonça, en disant: Ce sont des hommes sortis de Samarie.
18 Beni Hadadi akasema, “wawe wamekuja kwa amani au kwa vita, wakamteni wakiwa hai.”
Et lui répondit: Si c’est pour la paix qu’ils viennent, saisissez-les vivants; si c’est pour combattre, prenez-les vivants.
19 Kwa hiyo wale vijvana wanaowatumikia maliwali wa wilaya wakaenda mjini na jeshi likawafuata kwa nyuma.
Les serviteurs des princes des provinces sortirent donc, et le reste de l’armée suivait;
20 Kila mmoja akaua adui wake na wale washami wakakimbia. Israeli ikawashinda. Beni Hadadi mfalme wa Shamu akatoroka kwa farasi pamoja na wapanda farasi.
Et chacun d’eux frappa celui qui venait contre lui; alors les Syriens s’enfuirent, et Israël les poursuivit. Bénadad, roi de Syrie, s’enfuit aussi à cheval avec ses cavaliers.
21 Kisha mfalme wa Israeli akaenda akawashambulia farasi na magari, na kuwaua washami kwa mauaji makubwa.
Et même le roi d’Israël, étant sorti, frappa les chevaux et les chariots, et frappa la Syrie d’une grande plaie.
22 Yule nabii akaja kwa mfalme wa Israeli akamwambia, “Nenda, ukajiimarishe mwenyewe, uelewa na kupanga kile unachofanya, kwa sababu mwakani mfalme wa Shamu atapanda dhidi yako tena.”
(Alors le prophète, s’approchant du roi d’Israël, lui dit: Allez, fortifiez-vous, sachez et voyez ce que vous devez faire; car l’année suivante le roi de Syrie montera contre vous.)
23 Wale watumishi wa mfalme wa Shamu wakamwambia, “Mungu wao ni mungu wa milimani. Hiyo ndiyo sababu walikuwa na nguvu kuliko tulivyokuwa. Lakini sasa hebu tupigane nao katika nchi tambarare, na kwa hakika tutakuwa na nguvu kuliko wao.
Mais les serviteurs du roi de Syrie lui dirent: Ce sont les dieux des montagnes, que leurs dieux, et c’est pourquoi ils nous ont vaincus; il vaut donc mieux que nous combattions contre eux dans les plaines, et nous l’emporterons sur eux.
24 Na ufanye hivi: waondoe wafalme; mwondoe kila mmoja mahali pake ukaweke majemedari mahali pao.
Vous donc, faites cette chose-ci: éloignez tous les rois de votre armée, et mettez des officiers en leur place;
25 Kisha ujihesabie jeshi kama lile jeshi ulilopoteza, farasi kwa farasi na gari kwa gari, nasi tutapigana nao katika nchi tambarare. Kwa hakika tutakuwa na nguvu kuliko walivyo.” Kwa hiyo Beni Hadadi akausikiliza ushauri huo naye akafanya kama alivyoshauriwa.
Rétablissez le nombre de ceux de vos soldats qui ont succombé, et autant de chevaux que les premiers chevaux, et autant de chariots que vous avez eu de chariots auparavant; et nous combattrons contre eux dans les plaines, et vous verrez que nous l’emporterons sur eux. Il crut leur conseil, et il fit ainsi.
26 Baada ya mwanzo wa mwaka mpya, Beni Hadadi akawahesabu Washami na akapanda Afeki kupigana na Israeli.
Ainsi après qu’un an fut passé, Bénadad fit la revue des Syriens, et il monta à Aphec pour combattre contre Israël.
27 Watu wa Israeli walikuwa wamehesabiwa na walikuwa wamejipanga kupigana nao. Watu wa Israeli wakafanya kambi mbele yao kama makundi mawili madogo ya mbuzi, lakini Washami wakaujaza upande wa nchi.
Les enfants d’Israël furent aussi passés en revue; et, des vivres pris, ils partirent de leur côté, et campèrent vis-à-vis deux, comme deux petits troupeaux de chèvres, au lieu que les Syriens couvraient toute la terre.
28 Ndipo mtu wa Mungu akaja karibu akaongea mfalme wa Israeli akamwambia, “BWANA anasema: 'Kwa kuwa Washami wamesema kuwa BWANA ni mungu wa milima, na wala si mungu wa mabondeni, nitaliweka hili jeshi kubwa mkononi mwako, nawe utajua kuwa mimi ni BWANA.'”
(Alors s’approchant, un homme de Dieu dit au roi d’Israël: Voici ce que dit le Seigneur: Parce que les Syriens ont dit: C’est le Dieu des montagnes que le Seigneur, et il n’est pas le Dieu des vallées, je mettrai toute cette grande multitude en ta main, et vous saurez que c’est moi qui suis le Seigneur.)
29 Kwa hiyo majeshi yakaweka kambi yakikabiliana kwa muda wa siku saba. Kisha siku ya saba vita vikaanza. Watu wa Israeli wakawaua Washami 100, 000 wanajeshi wa ardhini kwa siku moja.
Or durant sept jours ceux-ci et ceux-là rangèrent les armées en bataille, l’une vis-à-vis de l’autre, mais au septième jour la bataille fut engagée, et les enfants d’Israël tuèrent, parmi les Syriens, cent mille hommes de pied en un seul jour.
30 Waliobaki wakakimbilia Afeki, mjini, na ule ukuta ukaanguka juu ya watu ishiriinina saba elfu waliobaki. Naye Beni Hadadi akakimbilia mjini. akaingia kwenye chumba cha ndani.
Et ceux qui étaient restés s’enfuirent dans la ville d’Aphec, et le mur tomba sur vingt-sept mille hommes qui étaient restés. Quant à Bénadad, fuyant, il entra dans la ville, et se retira dans une chambre, qui était dans sa chambre;
31 Wale watumishi wa Beni Hadadi wakamwambia, “Tazama sasa, tumesikia kwamba wale wafalme wa nyumba ya Israeli ni wenye rehema. Tafadhali hebu tuvaeni magaunia viunoni mwetu na kamba vichwani mwetu, na twendeni kwa mfalme wa Israeli. Labda atakuokoa roho yako.”
Et ses serviteurs lui dirent: Voilà que nous avons ouï dire que les rois de la maison d’Israël sont cléments: mettons donc des sacs sur nos reins et des cordes à nos têtes, et sortons vers le roi d’Israël; peut-être qu’il sauvera nos âmes.
32 Kwa hiyo wakavaa magunia viunoni mwao na kujifunga kamba vichwani mwao na kisha wakaenda kwa mfalme wa Israeli wakamwambia, “Mtumishi wako Beni Hadadi, anasema, 'tafadhali niachie uhai wangu.” Ahabu akawaambia, “Je, bado yuko hai? Yeye ni ndugu yangu.”
Ils ceignirent donc de sacs leurs reins, mirent des cordes à leurs têtes, vinrent vers le roi d’Israël, et lui dirent: Votre serviteur Bénadad dit: Je vous prie, que mon âme vive. Et lui répondit: S’il vit encore, il est mon frère.
33 Sasa wale watu walikuwa wakisikiliza ishara yeyote kutoka kwa Ahabu, kwa hiyo wakamjibu haraka, “Ndiyo ndugu yako Beni Hadadi bado yuko hai.” Ahabu akawaambia, “Nendeni mkamlete.” Ndipo Beni Hadadi alipokuja kwake, na Ahabu akamwacha aje kwenye gari lake.
Ce que les Syriens prirent pour un heureux présage; et, se hâtant, ils saisirent cette parole de sa bouche et dirent: Bénadad est votre frère. Et il leur répondit: Allez, et amenez-le-moi. Bénadad sortit donc vers Achab, qui le fit monter sur son char.
34 Beni Hadadi akamwambia Ahabu, “Nitakurudishia miji yako ambayo baba yangu alichukua toka kwa baba yako, na unaweza kutengeneza masoko kwa ajili yako Dameski, kama baba yangu alivyofanya kule Samaria.” Ahabu akajibu, “Nitakuacha uende kwa agano hili.” Kwa hiyo Ahabu akafanya agano naye kisha akamwacha aende.
Et Bénadad lui dit: Je vous rendrai les villes que mon père a prises à votre père; et faites-vous des places publiques dans Damas, comme s’en fit mon père dans Samarie; et moi, ainsi allié, je me retirerai d’auprès de vous. Achab fit donc alliance, et le laissa aller.
35 Mtu mmoja, mmoja wana wa wana wa manabii, akamwambia mmoja wa wale manabii wenzake kwa neno la BWANA, “Tafadhali nipige.” Lakini yule mtu akakataa kumpiga.
Alors un certain homme d’entre les fils des prophètes dit à son compagnon avec la parole du Seigneur: Frappe-moi. Mais comme celui-ci ne voulut pas le frapper,
36 Kisha yule nabii akamwambia nabii mwenzake, “Kwa sababu umekataa kutii sauti ya BWANA, mara tu utakaponiacha, simba atakuua.” na mara tu baad ya yule mtu kumwacha, simba akamkuta na kumwua.
Il lui dit: Parce que tu n’as pas voulu écouter la voix du Seigneur, tu t’éloigneras de moi, et le lion te tuera. Lorsqu’il fut un peu éloigné de lui, le lion le trouva et le tua.
37 Kisha yule nabii akamkuta mtu mwingine akamwambia, “Tafadhali nipige.”Yule mtu akampiga na kumwumiza.
Mais rencontrant aussi un autre homme, il lui dit: Frappe-moi. Cet homme le frappa et le blessa.
38 Kisha yule nabii akaondoka akaenda kumsubiri yule mfalme barabarani; naye alikuwa amejibadilisha kwa kilemba machoni pake.
Le prophète s’en alla donc, et vint à la rencontre du roi dans la voie, et il changea, en y répandant de la poussière, son visage et ses yeux.
39 Ikawa mfalme alipokuwa akipita, Yule nabii akamwita mfalme na kumwambia, “Mtumishi wako alienda katikati ya pigano, na askari akasimama akamleta adui kwangu akasema, 'Mwangalie mtu huyu. Na ikiwa kwa vyovyote atatoroka, basi maisha yako yatatolewa kwa ajili ya maisha yake vinginevyo utalipa kilo thelathini za fedha.
Et lorsque le roi fut passé, il cria après lui, et dit: Votre serviteur est sorti pour combattre de près, et, comme un homme s’est enfui, quelqu’un me l’a amené, et a dit: Garde cet homme; et, s’il s’échappe, ton âme sera pour son âme, ou tu pèseras un talent d’argent.
40 Lakini kwa kuwa mtumishi wako alikuwa na mambo mengi akienda huku na kule, yule askari adui akatoroka.” Basi mfalme wa Israeli akamwambia, Hivyo ndivyo itakavyokuwa hukukmu yako - umejihukumu mwenyewe.”
Mais tandis que moi, troublé, je me tournais ici et là, il a subitement disparu. Et le roi d’Israël lui dit: C’est ton jugement que toi-même tu as prononcé.
41 Ndipo yule nabii alipoondoa haraka kile kilemba machoni pake, na mfalme wa Israeli alipotambua kuwa huyo alikuwa mmoja wa manabii.
Mais lui aussitôt essuya la poussière de son visage, et le roi d’Israël reconnut qu’il était du nombre des prophètes.
42 Yule nabii akamwambia mfalme, “BWANA anasema, 'Kwa sababu umemwachia aende mtu yule niliyekuwa nimemhukumu kifo, maisha yako yatachukua nafasi ya maisha yake.'”
Il dit au roi: Voici ce que dit le Seigneur: Parce que tu as laissé échapper de ta main un homme digne de mort, ta vie sera pour sa vie, et ton peuple pour son peuple.
43 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akaenda nyumbani kwake akiwa na moyo mzito na mwenye hasira, akafika Samaria.
Le roi d’Israël retourna donc en sa maison, dédaignant d’entendre, et, plein de fureur, il vint dans Samarie.

< 1 Wafalme 20 >