< 1 Wafalme 20 >
1 Beni Hadadi mfalme wa Shamu akakusanya jeshi lake lote pamoja. Kulikuwa na wafalme thelathini na mbili wasaidizi pamoja naye, na magari na farasi. Akapanda, akaihusuru Samaria na kupigana nayo.
And Ben Hadad [the] king of Aram he gathered all army his and thirty and two king[s] [were] with him and horse[s] and chariotry and he went up and he laid siege on Samaria and he fought against it.
2 Akatuma wajumbe katika mji kwa Ahabu mfalme wa Israeli, akamwambia, “Beni Hadadi anasema hivi:
And he sent messengers to Ahab [the] king of Israel the city towards. And he said to him thus he says Ben Hadad
3 Fedha zako na dhahabu zako ni zangu. Pia wake zako na watoto, wale wazuri, sasa ni wangu.”
silver your and gold your [belongs] to me it and wives your and children your good [belong] to me they.
4 Mfalme wa Israeli akajibu akasema, “Na iwe kama unavyosema, bwana wangu, mfalme. Mimi pamoja na vile nilivyo navyo ni mali yako.”
And he answered [the] king of Israel and he said according to word your O lord my the king [belong] to you I and all that [belongs] to me.
5 Wale wajumbe wakaja tena wakasema, “Beni Hadadi anasema hivi, 'Nilituma neno kwako nikisema kwamba lazima ukabidhi kwangu fedha zako, dhahabu zako, wake zako na watoto wako.
And they returned the messengers and they said thus he says Ben Hadad saying that I sent to you saying silver your and gold your and wives your and children your to me you will give.
6 Lakini kesho nitatuma watumishi wangu kwako wakati kama huu, nao wataichunguza nyumba yako na nyumba za watumishi wako. Nao watatia mikononi mwao na kukichukua kila wakipendacho machoni mwao.'”
That - except about this time tomorrow I will send servants my to you and they will search house your and [the] houses of servants your and it will be every desirable thing of eyes your they will put in hand their and they will take [it].
7 Ndipo mfalme wa Israeli akawaita wazee wote wa nchi pamoja akawaambia, ''Hebu angalieni jinsi huyu mtu anavyotafuta matatizo. Amenitumia ujumbe kwamba anataka kuchukua wake zangu, watoto wangu, fedha na dhahabu zangu, nami sijamkatalia.”
And he summoned [the] king of Israel all [the] elders of the land and he said know please and see that trouble this [man] [is] seeking for he sent to me for wives my and for children my and for silver my and for gold my and not I withheld [them] from him.
8 Wazee wote na watu wote wakamwambia Ahabu, “Usimsikilize wala kukubaliana na matakwa yake.”
And they said to him all the elders and all the people may not you listen and not you must be willing.
9 Ahabu akawaambia wajumbe wa Beni Hadadi, “Mwambieni bwana wangu mfalme kwamba, 'Ninakubaliana na kila kitu ambacho kwanza uliwatuma watumishi wako kufanya kwangu, lakini sikubaliani na matakwa yako haya ya pili.'” Wale watumishi wa Beni Hadadi wakaondoka wakampelekea mrejesho Beni Hadadi.
And he said to [the] messengers of Ben Hadad say to lord my the king all that you sent to servant your at the first I will do and the thing this not I am able to do and they went the messengers and they brought back him word.
10 Naye Beni Hadadi akatuma tena majibu yake kwa Ahabu, akaisema, “basi miungu inifanyie hivyo na zaidi, kama hata mavumbi ya Samaria yatawatosheleza watu watu wote wanaonifuata kuchukua kila mmoja angalau konzi mkononi mwake.”
And he sent to him Ben Hadad and he said thus may they do! to me [the] gods and thus may they add if it will suffice [the] dust of Samaria for handfuls for all the people which [is] at feet my.
11 Naye mfalme wa Israeli akamjibu akisema, “Mwabieni Beni Hadadi, 'Hakuna abebaye silaha yake, atakayejivuna kama wakati wa kuishusha.”'
And he answered [the] king of Israel and he said speak may not he boast [one who] girds on like [one who] loosens.
12 Beni Hadadi aliusikia ujumbe huu wakati alipokuwa akinywa, yeye na wafalme walikuwa pamoja naye waliokuwa kwenye mahema yao. Beni Hadadi akayaamuru majaeshi yake, “Jipangeni katika sehemu zenu kwa ajili ya vita.” Kwa hiyo wakajiandaa kivita ili kuuvamia mji.
And it was when heard the word this and he [was] drinking he and the kings in the booths and he said to servants his set yourselves and they set themselves on the city.
13 Tazama, nabii akaja kwa Ahabu mfalme wa Israeli akasema, “BWANA asema, 'Je umeliona hili jeshi kubwa? Tazama, nitaliweka katika mkono wako leo, nawe utatambua kuwa mimi ni BWANA.'”
And there! - a prophet one he drew near to Ahab [the] king of Israel and he said thus he says Yahweh ¿ do you see all the multitude great this here I [am] about to give it in hand your this day and you will know that I [am] Yahweh.
14 Naye Ahabu akajibu, ''kwa nani? BWANA akamjibu akasema, “kwa kuwatumia viijana wanaotumikia maliwali wa wilaya.” kisha Ahabu akasema, “Ni nani atakayepewa hiyo vita?' BWANA akamwambia, “wewe.”
And he said Ahab by whom? and he said thus he says Yahweh by [the] young men of [the] officials of the provinces and he said who? will he begin the battle and he said you.
15 Ndipo Ahabu alipowataarifu wale vijna wanaowatumikia maliwali wa wilaya. Idadi yao ilikuwa 232. Baada yao aliwahesabu wanajeshi wote, jeshi lote la Israeli; idadi yao ilikuwa elfu saba.
And he mustered [the] young men of [the] officials of the provinces and they were two hundred two and thirty and after them he mustered all the people all [the] people of Israel [were] seven thousand.
16 Nao wakatoka wakati wa adhuhuri. Naye Beni Hadadi alikuwa akinywa na kulewa hemani mwake, yeye na wale wafalme wadogo thelathini na mbili waliokuwa wakimsaidia.
And they went out at the noontide and Ben Hadad [was] drinking drunken in the booths he and the kings thirty and two king[s] [who] was helping him.
17 Wale maakida vijana waliokuwa wakiwasaidia maliwali wa wilaya walitangulia kwanza. Kisha Beni Hadadi alitaarifiwa na wanaskauti aliokuwa amewatuma kwamaba, “kuna watu wanakuja kutoka Samaria.”
And they went out [the] young men of [the] officials of the provinces at the first and he sent Ben Hadad and people told to him saying men they have come out from Samaria.
18 Beni Hadadi akasema, “wawe wamekuja kwa amani au kwa vita, wakamteni wakiwa hai.”
And he said if for peace they have come out seize them alive and if for battle they have come out alive seize them.
19 Kwa hiyo wale vijvana wanaowatumikia maliwali wa wilaya wakaenda mjini na jeshi likawafuata kwa nyuma.
And these [men] they went out from the city [the] young men of [the] officials of the provinces and the army which [was] behind them.
20 Kila mmoja akaua adui wake na wale washami wakakimbia. Israeli ikawashinda. Beni Hadadi mfalme wa Shamu akatoroka kwa farasi pamoja na wapanda farasi.
And they struck down everyone man his and they fled Aram and it pursued them Israel and he escaped Ben Hadad [the] king of Aram on a horse and horsemen.
21 Kisha mfalme wa Israeli akaenda akawashambulia farasi na magari, na kuwaua washami kwa mauaji makubwa.
And he went out [the] king of Israel and he struck down the horse[s] and the chariotry and he struck down among Aram a slaughter great.
22 Yule nabii akaja kwa mfalme wa Israeli akamwambia, “Nenda, ukajiimarishe mwenyewe, uelewa na kupanga kile unachofanya, kwa sababu mwakani mfalme wa Shamu atapanda dhidi yako tena.”
And he drew near the prophet to [the] king of Israel and he said to him go strengthen yourself and know and see [that] which you will do for to [the] return of the year [the] king of Aram [is] coming up on you.
23 Wale watumishi wa mfalme wa Shamu wakamwambia, “Mungu wao ni mungu wa milimani. Hiyo ndiyo sababu walikuwa na nguvu kuliko tulivyokuwa. Lakini sasa hebu tupigane nao katika nchi tambarare, na kwa hakika tutakuwa na nguvu kuliko wao.
And [the] servants of [the] king of Aram they said to him [is] a god of mountains God their there-fore they were strong more than us and but let us do battle with them on the level ground if not we will be strong more than them.
24 Na ufanye hivi: waondoe wafalme; mwondoe kila mmoja mahali pake ukaweke majemedari mahali pao.
And the thing this do remove the kings each from place his and appoint governors in place of them.
25 Kisha ujihesabie jeshi kama lile jeshi ulilopoteza, farasi kwa farasi na gari kwa gari, nasi tutapigana nao katika nchi tambarare. Kwa hakika tutakuwa na nguvu kuliko walivyo.” Kwa hiyo Beni Hadadi akausikiliza ushauri huo naye akafanya kama alivyoshauriwa.
And you you will muster for yourself - an army like the army which fell from you and a horse like the horse - and chariotry like the chariotry and let us fight them on the level ground if not we will be strong more than them and he listened to voice their and he did thus.
26 Baada ya mwanzo wa mwaka mpya, Beni Hadadi akawahesabu Washami na akapanda Afeki kupigana na Israeli.
And it was to [the] return of the year and he mustered Ben Hadad Aram and he went up Aphek towards for battle with Israel.
27 Watu wa Israeli walikuwa wamehesabiwa na walikuwa wamejipanga kupigana nao. Watu wa Israeli wakafanya kambi mbele yao kama makundi mawili madogo ya mbuzi, lakini Washami wakaujaza upande wa nchi.
And [the] people of Israel they were mustered and they were supplied and they went to meet them and they encamped [the] people of Israel before them like two little flocks of goats and Aram they filled the land.
28 Ndipo mtu wa Mungu akaja karibu akaongea mfalme wa Israeli akamwambia, “BWANA anasema: 'Kwa kuwa Washami wamesema kuwa BWANA ni mungu wa milima, na wala si mungu wa mabondeni, nitaliweka hili jeshi kubwa mkononi mwako, nawe utajua kuwa mimi ni BWANA.'”
And he drew near [the] man of God and he said to [the] king of Israel and he said thus he says Yahweh because that they have said Aram [is] a god of mountains Yahweh and not [is] a god of valleys he and I will give all the multitude great this in hand your and you will know that I [am] Yahweh.
29 Kwa hiyo majeshi yakaweka kambi yakikabiliana kwa muda wa siku saba. Kisha siku ya saba vita vikaanza. Watu wa Israeli wakawaua Washami 100, 000 wanajeshi wa ardhini kwa siku moja.
And they encamped these opposite to these seven days and it was - on the day seventh and it drew near the battle and they struck down [the] people of Israel Aram one hundred thousand foot soldier[s] in a day one.
30 Waliobaki wakakimbilia Afeki, mjini, na ule ukuta ukaanguka juu ya watu ishiriinina saba elfu waliobaki. Naye Beni Hadadi akakimbilia mjini. akaingia kwenye chumba cha ndani.
And they fled the [ones who] remained - Aphek towards into the city and it fell the wall on twenty and seven thousand man who remained and Ben Hadad he fled and he went into the city a room in a room.
31 Wale watumishi wa Beni Hadadi wakamwambia, “Tazama sasa, tumesikia kwamba wale wafalme wa nyumba ya Israeli ni wenye rehema. Tafadhali hebu tuvaeni magaunia viunoni mwetu na kamba vichwani mwetu, na twendeni kwa mfalme wa Israeli. Labda atakuokoa roho yako.”
And they said to him servants his here! please we have heard that [the] kings of [the] house of Israel that [are] kings of covenant loyalty they let us put please sackcloth on loins our and ropes on head our and let us go out to [the] king of Israel perhaps he will let live life your.
32 Kwa hiyo wakavaa magunia viunoni mwao na kujifunga kamba vichwani mwao na kisha wakaenda kwa mfalme wa Israeli wakamwambia, “Mtumishi wako Beni Hadadi, anasema, 'tafadhali niachie uhai wangu.” Ahabu akawaambia, “Je, bado yuko hai? Yeye ni ndugu yangu.”
And they girded sackcloth on loins their and ropes on heads their and they went to [the] king of Israel and they said servant your Ben Hadad he says let it live please life my and he said ¿ [is] still he alive [is] brother my he.
33 Sasa wale watu walikuwa wakisikiliza ishara yeyote kutoka kwa Ahabu, kwa hiyo wakamjibu haraka, “Ndiyo ndugu yako Beni Hadadi bado yuko hai.” Ahabu akawaambia, “Nendeni mkamlete.” Ndipo Beni Hadadi alipokuja kwake, na Ahabu akamwacha aje kwenye gari lake.
And the men they observed [the] signs and they hastened and they caught ¿ from him and they said [is] brother your Ben Hadad and he said go fetch him and he came out to him Ben Hadad and he brought up him on the chariot.
34 Beni Hadadi akamwambia Ahabu, “Nitakurudishia miji yako ambayo baba yangu alichukua toka kwa baba yako, na unaweza kutengeneza masoko kwa ajili yako Dameski, kama baba yangu alivyofanya kule Samaria.” Ahabu akajibu, “Nitakuacha uende kwa agano hili.” Kwa hiyo Ahabu akafanya agano naye kisha akamwacha aende.
And he said to him the cities which he took father my from with father your I will return and streets you will make for yourself in Damascus just as he made father my in Samaria and I with the covenant I will let go you and he made to him a covenant and he let go him.
35 Mtu mmoja, mmoja wana wa wana wa manabii, akamwambia mmoja wa wale manabii wenzake kwa neno la BWANA, “Tafadhali nipige.” Lakini yule mtu akakataa kumpiga.
And a man one one of [the] sons of the prophets he said to companion his at [the] word of Yahweh strike me please and he refused the man to strike him.
36 Kisha yule nabii akamwambia nabii mwenzake, “Kwa sababu umekataa kutii sauti ya BWANA, mara tu utakaponiacha, simba atakuua.” na mara tu baad ya yule mtu kumwacha, simba akamkuta na kumwua.
And he said to him because that not you listened to [the] voice of Yahweh here you [are] about to go from with me and it will strike down you the lion and he went from beside him and it met him the lion and it struck down him.
37 Kisha yule nabii akamkuta mtu mwingine akamwambia, “Tafadhali nipige.”Yule mtu akampiga na kumwumiza.
And he found a man another and he said strike me please and he struck him the man completely and wounded.
38 Kisha yule nabii akaondoka akaenda kumsubiri yule mfalme barabarani; naye alikuwa amejibadilisha kwa kilemba machoni pake.
And he went the prophet and he stood for the king (beside *LAB(H)*) the way and he disguised himself with ashes over eyes his.
39 Ikawa mfalme alipokuwa akipita, Yule nabii akamwita mfalme na kumwambia, “Mtumishi wako alienda katikati ya pigano, na askari akasimama akamleta adui kwangu akasema, 'Mwangalie mtu huyu. Na ikiwa kwa vyovyote atatoroka, basi maisha yako yatatolewa kwa ajili ya maisha yake vinginevyo utalipa kilo thelathini za fedha.
And he was the king passing by and he he cried out to the king and he said servant your - he went out in [the] midst of the battle and there! a man he turned aside and he brought to me a man and he said guard the man this if indeed he will be missing and it will be life your in place of life his or a talent of silver you will weigh out.
40 Lakini kwa kuwa mtumishi wako alikuwa na mambo mengi akienda huku na kule, yule askari adui akatoroka.” Basi mfalme wa Israeli akamwambia, Hivyo ndivyo itakavyokuwa hukukmu yako - umejihukumu mwenyewe.”
And he was servant your doing them and them and he there not [was] he and he said to him [the] king of Israel [is] thus sentence your you you have decided.
41 Ndipo yule nabii alipoondoa haraka kile kilemba machoni pake, na mfalme wa Israeli alipotambua kuwa huyo alikuwa mmoja wa manabii.
And he hastened and he removed the bandage (from over *Q(k)*) eyes his and he recognized him [the] king of Israel that [was] one of the prophets he.
42 Yule nabii akamwambia mfalme, “BWANA anasema, 'Kwa sababu umemwachia aende mtu yule niliyekuwa nimemhukumu kifo, maisha yako yatachukua nafasi ya maisha yake.'”
And he said to him thus he says Yahweh because you have let go [the] man of total destruction my from a hand and it will be life your in place of life his and people your in place of people his.
43 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akaenda nyumbani kwake akiwa na moyo mzito na mwenye hasira, akafika Samaria.
And he went [the] king of Israel to house his sullen and furious and he went Samaria towards.