< 1 Wafalme 20 >

1 Beni Hadadi mfalme wa Shamu akakusanya jeshi lake lote pamoja. Kulikuwa na wafalme thelathini na mbili wasaidizi pamoja naye, na magari na farasi. Akapanda, akaihusuru Samaria na kupigana nayo.
And Ben-hadad the king of Aram gathered all his host together; and there were thirty and two kings with him, and horses and chariots; and he went up and besieged Samaria, and fought against it.
2 Akatuma wajumbe katika mji kwa Ahabu mfalme wa Israeli, akamwambia, “Beni Hadadi anasema hivi:
And he sent messengers to Ahab king of Israel, into the city,
3 Fedha zako na dhahabu zako ni zangu. Pia wake zako na watoto, wale wazuri, sasa ni wangu.”
and said unto him: 'Thus saith Ben-hadad: Thy silver and thy gold is mine; thy wives also and thy children, even the goodliest, are mine.'
4 Mfalme wa Israeli akajibu akasema, “Na iwe kama unavyosema, bwana wangu, mfalme. Mimi pamoja na vile nilivyo navyo ni mali yako.”
And the king of Israel answered and said: 'It is according to thy saying, my lord, O king: I am thine, and all that I have.'
5 Wale wajumbe wakaja tena wakasema, “Beni Hadadi anasema hivi, 'Nilituma neno kwako nikisema kwamba lazima ukabidhi kwangu fedha zako, dhahabu zako, wake zako na watoto wako.
And the messengers came again, and said: 'Thus speaketh Ben-hadad, saying: I sent indeed unto thee, saying: Thou shalt deliver me thy silver, and thy gold, and thy wives, and thy children;
6 Lakini kesho nitatuma watumishi wangu kwako wakati kama huu, nao wataichunguza nyumba yako na nyumba za watumishi wako. Nao watatia mikononi mwao na kukichukua kila wakipendacho machoni mwao.'”
but I will send my servants unto thee tomorrow about this time, and they shall search thy house, and the houses of thy servants; and it shall be, that whatsoever is pleasant in thine eyes, they shall put it in their hand, and take it away.'
7 Ndipo mfalme wa Israeli akawaita wazee wote wa nchi pamoja akawaambia, ''Hebu angalieni jinsi huyu mtu anavyotafuta matatizo. Amenitumia ujumbe kwamba anataka kuchukua wake zangu, watoto wangu, fedha na dhahabu zangu, nami sijamkatalia.”
Then the king of Israel called all the elders of the land, and said: 'Mark, I pray you, and see how this man seeketh mischief; for he sent unto me for my wives, and for my children, and for my silver, and for my gold; and I denied him not.'
8 Wazee wote na watu wote wakamwambia Ahabu, “Usimsikilize wala kukubaliana na matakwa yake.”
And all the elders and all the people said unto him: 'Hearken thou not, neither consent.'
9 Ahabu akawaambia wajumbe wa Beni Hadadi, “Mwambieni bwana wangu mfalme kwamba, 'Ninakubaliana na kila kitu ambacho kwanza uliwatuma watumishi wako kufanya kwangu, lakini sikubaliani na matakwa yako haya ya pili.'” Wale watumishi wa Beni Hadadi wakaondoka wakampelekea mrejesho Beni Hadadi.
Wherefore he said unto the messengers of Ben-hadad: 'Tell my lord the king: All that thou didst send for to thy servant at the first I will do; but this thing I may not do.' And the messengers departed, and brought him back word.
10 Naye Beni Hadadi akatuma tena majibu yake kwa Ahabu, akaisema, “basi miungu inifanyie hivyo na zaidi, kama hata mavumbi ya Samaria yatawatosheleza watu watu wote wanaonifuata kuchukua kila mmoja angalau konzi mkononi mwake.”
And Ben-hadad sent unto him, and said: 'The gods do so unto me, and more also, if the dust of Samaria shall suffice for handfuls for all the people that follow me.'
11 Naye mfalme wa Israeli akamjibu akisema, “Mwabieni Beni Hadadi, 'Hakuna abebaye silaha yake, atakayejivuna kama wakati wa kuishusha.”'
And the king of Israel answered and said: 'Tell him: Let not him that girdeth on his armour boast himself as he that putteth it off.'
12 Beni Hadadi aliusikia ujumbe huu wakati alipokuwa akinywa, yeye na wafalme walikuwa pamoja naye waliokuwa kwenye mahema yao. Beni Hadadi akayaamuru majaeshi yake, “Jipangeni katika sehemu zenu kwa ajili ya vita.” Kwa hiyo wakajiandaa kivita ili kuuvamia mji.
And it came to pass, when Ben-hadad heard this message, as he was drinking, he and the kings, in the booths, that he said unto his servants: 'Set yourselves in array.' And they set themselves in array against the city.
13 Tazama, nabii akaja kwa Ahabu mfalme wa Israeli akasema, “BWANA asema, 'Je umeliona hili jeshi kubwa? Tazama, nitaliweka katika mkono wako leo, nawe utatambua kuwa mimi ni BWANA.'”
And, behold, a prophet came near unto Ahab king of Israel, and said: 'Thus saith the LORD: Hast thou seen all this great multitude? behold, I will deliver it into thy hand this day; and thou shalt know that I am the LORD.'
14 Naye Ahabu akajibu, ''kwa nani? BWANA akamjibu akasema, “kwa kuwatumia viijana wanaotumikia maliwali wa wilaya.” kisha Ahabu akasema, “Ni nani atakayepewa hiyo vita?' BWANA akamwambia, “wewe.”
And Ahab said: 'By whom?' And he said: 'Thus saith the LORD: By the young men of the princes of the provinces.' Then he said: 'Who shall begin the battle?' And he answered: 'Thou.'
15 Ndipo Ahabu alipowataarifu wale vijna wanaowatumikia maliwali wa wilaya. Idadi yao ilikuwa 232. Baada yao aliwahesabu wanajeshi wote, jeshi lote la Israeli; idadi yao ilikuwa elfu saba.
Then he numbered the young men of the princes of the provinces, and they were two hundred and thirty-two; and after them he numbered all the people, even all the children of Israel, being seven thousand.
16 Nao wakatoka wakati wa adhuhuri. Naye Beni Hadadi alikuwa akinywa na kulewa hemani mwake, yeye na wale wafalme wadogo thelathini na mbili waliokuwa wakimsaidia.
And they went out at noon. But Ben-hadad was drinking himself drunk in the booths, he and the kings, the thirty and two kings that helped him.
17 Wale maakida vijana waliokuwa wakiwasaidia maliwali wa wilaya walitangulia kwanza. Kisha Beni Hadadi alitaarifiwa na wanaskauti aliokuwa amewatuma kwamaba, “kuna watu wanakuja kutoka Samaria.”
And the young men of the princes of the provinces went out first; and Ben-hadad sent out, and they told him, saying: 'There are men come out from Samaria.'
18 Beni Hadadi akasema, “wawe wamekuja kwa amani au kwa vita, wakamteni wakiwa hai.”
And he said: 'Whether they are come out for peace, take them alive; or whether they are come out for war, take them alive.'
19 Kwa hiyo wale vijvana wanaowatumikia maliwali wa wilaya wakaenda mjini na jeshi likawafuata kwa nyuma.
So these went out of the city, the young men of the princes of the provinces, and the army which followed them.
20 Kila mmoja akaua adui wake na wale washami wakakimbia. Israeli ikawashinda. Beni Hadadi mfalme wa Shamu akatoroka kwa farasi pamoja na wapanda farasi.
And they slew every one his man; and the Arameans fled, and Israel pursued them; and Ben-hadad the king of Aram escaped on a horse with horsemen.
21 Kisha mfalme wa Israeli akaenda akawashambulia farasi na magari, na kuwaua washami kwa mauaji makubwa.
And the king of Israel went out, and smote the horses and chariots, and slew the Arameans with a great slaughter.
22 Yule nabii akaja kwa mfalme wa Israeli akamwambia, “Nenda, ukajiimarishe mwenyewe, uelewa na kupanga kile unachofanya, kwa sababu mwakani mfalme wa Shamu atapanda dhidi yako tena.”
And the prophet came near to the king of Israel, and said unto him: 'Go, strengthen thyself, and mark, and see what thou doest; for at the return of the year the king of Aram will come up against thee.'
23 Wale watumishi wa mfalme wa Shamu wakamwambia, “Mungu wao ni mungu wa milimani. Hiyo ndiyo sababu walikuwa na nguvu kuliko tulivyokuwa. Lakini sasa hebu tupigane nao katika nchi tambarare, na kwa hakika tutakuwa na nguvu kuliko wao.
And the servants of the king of Aram said unto him: 'Their God is a God of the hills; therefore they were stronger than we; but let us fight against them in the plain, and surely we shall be stronger than they.
24 Na ufanye hivi: waondoe wafalme; mwondoe kila mmoja mahali pake ukaweke majemedari mahali pao.
And do this thing: take the kings away, every man out of his place, and put governors in their room:
25 Kisha ujihesabie jeshi kama lile jeshi ulilopoteza, farasi kwa farasi na gari kwa gari, nasi tutapigana nao katika nchi tambarare. Kwa hakika tutakuwa na nguvu kuliko walivyo.” Kwa hiyo Beni Hadadi akausikiliza ushauri huo naye akafanya kama alivyoshauriwa.
and number thee an army, like the army that thou hast lost, horse for horse, and chariot for chariot; and we will fight against them in the plain, and surely we shall be stronger than they.' And he hearkened unto their voice, and did so.
26 Baada ya mwanzo wa mwaka mpya, Beni Hadadi akawahesabu Washami na akapanda Afeki kupigana na Israeli.
And it came to pass at the return of the year, that Ben-hadad mustered the Arameans, and went up to Aphek, to fight against Israel.
27 Watu wa Israeli walikuwa wamehesabiwa na walikuwa wamejipanga kupigana nao. Watu wa Israeli wakafanya kambi mbele yao kama makundi mawili madogo ya mbuzi, lakini Washami wakaujaza upande wa nchi.
And the children of Israel were mustered, and were victualled, and went against them; and the children of Israel encamped before them like two little flocks of kids; but the Arameans filled the country.
28 Ndipo mtu wa Mungu akaja karibu akaongea mfalme wa Israeli akamwambia, “BWANA anasema: 'Kwa kuwa Washami wamesema kuwa BWANA ni mungu wa milima, na wala si mungu wa mabondeni, nitaliweka hili jeshi kubwa mkononi mwako, nawe utajua kuwa mimi ni BWANA.'”
And a man of God came near and spoke unto the king of Israel, and said: 'Thus saith the LORD: Because the Arameans have said: The LORD is a God of the hills, but he is not a God of the valleys; therefore will I deliver all this great multitude into thy hand, and ye shall know that I am the LORD.'
29 Kwa hiyo majeshi yakaweka kambi yakikabiliana kwa muda wa siku saba. Kisha siku ya saba vita vikaanza. Watu wa Israeli wakawaua Washami 100, 000 wanajeshi wa ardhini kwa siku moja.
And they encamped one over against the other seven days. And so it was, that in the seventh day the battle was joined; and the children of Israel slew of the Arameans a hundred thousand footmen in one day.
30 Waliobaki wakakimbilia Afeki, mjini, na ule ukuta ukaanguka juu ya watu ishiriinina saba elfu waliobaki. Naye Beni Hadadi akakimbilia mjini. akaingia kwenye chumba cha ndani.
But the rest fled to Aphek, into the city; and the wall fell upon twenty and seven thousand men that were left. And Ben-hadad fled, and came into the city, into an inner chamber.
31 Wale watumishi wa Beni Hadadi wakamwambia, “Tazama sasa, tumesikia kwamba wale wafalme wa nyumba ya Israeli ni wenye rehema. Tafadhali hebu tuvaeni magaunia viunoni mwetu na kamba vichwani mwetu, na twendeni kwa mfalme wa Israeli. Labda atakuokoa roho yako.”
And his servants said unto him: 'Behold now, we have heard that the kings of the house of Israel are merciful kings; let us, we pray thee, put sackcloth on our loins, and ropes upon our heads, and go out to the king of Israel; peradventure he will save thy life.'
32 Kwa hiyo wakavaa magunia viunoni mwao na kujifunga kamba vichwani mwao na kisha wakaenda kwa mfalme wa Israeli wakamwambia, “Mtumishi wako Beni Hadadi, anasema, 'tafadhali niachie uhai wangu.” Ahabu akawaambia, “Je, bado yuko hai? Yeye ni ndugu yangu.”
So they girded sackcloth on their loins, and put ropes on their heads, and came to the king of Israel, and said: 'Thy servant Ben-hadad saith: I pray thee, let me live.' And he said: 'Is he yet alive? he is my brother.'
33 Sasa wale watu walikuwa wakisikiliza ishara yeyote kutoka kwa Ahabu, kwa hiyo wakamjibu haraka, “Ndiyo ndugu yako Beni Hadadi bado yuko hai.” Ahabu akawaambia, “Nendeni mkamlete.” Ndipo Beni Hadadi alipokuja kwake, na Ahabu akamwacha aje kwenye gari lake.
Now the men took it for a sign, and hastened to catch it from him; and they said: 'Thy brother Ben-hadad.' Then he said: 'Go ye, bring him.' Then Ben-hadad came forth to him; and he caused him to come up into his chariot.
34 Beni Hadadi akamwambia Ahabu, “Nitakurudishia miji yako ambayo baba yangu alichukua toka kwa baba yako, na unaweza kutengeneza masoko kwa ajili yako Dameski, kama baba yangu alivyofanya kule Samaria.” Ahabu akajibu, “Nitakuacha uende kwa agano hili.” Kwa hiyo Ahabu akafanya agano naye kisha akamwacha aende.
And Ben-hadad said unto him: 'The cities which my father took from thy father I will restore; and thou shalt make streets for thee in Damascus, as my father made in Samaria.' 'And I, said Ahab, will let thee go with this covenant.' So he made a covenant with him, and let him go.
35 Mtu mmoja, mmoja wana wa wana wa manabii, akamwambia mmoja wa wale manabii wenzake kwa neno la BWANA, “Tafadhali nipige.” Lakini yule mtu akakataa kumpiga.
And a certain man of the sons of the prophets said unto his fellow by the word of the LORD: 'Smite me, I pray thee.' And the man refused to smite him.
36 Kisha yule nabii akamwambia nabii mwenzake, “Kwa sababu umekataa kutii sauti ya BWANA, mara tu utakaponiacha, simba atakuua.” na mara tu baad ya yule mtu kumwacha, simba akamkuta na kumwua.
Then said he unto him: 'Because thou hast not hearkened to the voice of the LORD, behold, as soon as thou art departed from me, a lion shall slay thee.' And as soon as he was departed from him, a lion found him; and slew him.
37 Kisha yule nabii akamkuta mtu mwingine akamwambia, “Tafadhali nipige.”Yule mtu akampiga na kumwumiza.
Then he found another man, and said: 'Smite me, I pray thee.' And the man smote him, smiting and wounding him.
38 Kisha yule nabii akaondoka akaenda kumsubiri yule mfalme barabarani; naye alikuwa amejibadilisha kwa kilemba machoni pake.
So the prophet departed, and waited for the king by the way, and disguised himself with his headband over his eyes.
39 Ikawa mfalme alipokuwa akipita, Yule nabii akamwita mfalme na kumwambia, “Mtumishi wako alienda katikati ya pigano, na askari akasimama akamleta adui kwangu akasema, 'Mwangalie mtu huyu. Na ikiwa kwa vyovyote atatoroka, basi maisha yako yatatolewa kwa ajili ya maisha yake vinginevyo utalipa kilo thelathini za fedha.
And as the king passed by, he cried unto the king; and he said: 'Thy servant went out into the midst of the battle; and, behold, a man turned aside, and brought a man unto me, and said: Keep this man; if by any means he be missing, then shall thy life be for his life, or else thou shalt pay a talent of silver.
40 Lakini kwa kuwa mtumishi wako alikuwa na mambo mengi akienda huku na kule, yule askari adui akatoroka.” Basi mfalme wa Israeli akamwambia, Hivyo ndivyo itakavyokuwa hukukmu yako - umejihukumu mwenyewe.”
And as thy servant was busy here and there, he was gone.' And the king of Israel said unto him: 'So shall thy judgment be; thyself hast decided it.'
41 Ndipo yule nabii alipoondoa haraka kile kilemba machoni pake, na mfalme wa Israeli alipotambua kuwa huyo alikuwa mmoja wa manabii.
And he hastened, and took the headband away from his eyes; and the king of Israel discerned him that he was of the prophets.
42 Yule nabii akamwambia mfalme, “BWANA anasema, 'Kwa sababu umemwachia aende mtu yule niliyekuwa nimemhukumu kifo, maisha yako yatachukua nafasi ya maisha yake.'”
And he said unto him: 'Thus saith the LORD: Because thou hast let go out of thy hand the man whom I had devoted to destruction, therefore thy life shall go for his life, and thy people for his people.'
43 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akaenda nyumbani kwake akiwa na moyo mzito na mwenye hasira, akafika Samaria.
And the king of Israel went to his house sullen and displeased, and came to Samaria.

< 1 Wafalme 20 >