< 1 Wafalme 2 >

1 Daudi alipokaribia kufa, alimwamuru Sulemani mwanae, akisema,
And they drew near [the] days of David to die and he commanded Solomon son his saying.
2 “Mimi sasa ninaiendea njia ya dunia yote. Kwa hiyo, uwe imara, na ujionyeshe mwenyewe kama mwanamume. Uzilinde amri za BWANA, Mungu wako ukitembea katika njia zake, utii maaagizo yake, amari zake,
I [am] about to go in [the] way of all the earth and you will be strong and you will become a man.
3 maamuzi yake, na maagizo ya maagano yake, uwe mwamngalifu kufanya yale yaliyoandikwa katika sheria za Musa, ili ufanikiwe katika yote utakayoyafanya, popote kule utakakokuwa,
And you will keep [the] charge of - Yahweh God your to walk in ways his to keep statutes his commandments his and judgments his and testimonies his according to [what] is written in [the] law of Moses so that you may cause to prosper all that you will do and every where you will turn there.
4 na BWANA atayatimiza maneno yake aliyosema kuhusu mimi, aliposema, 'kama wanao watajilinda katika tabia zao, wakatembea mbele yangu kwa uaminifu kwa mioyo yao yote na kwa roho zao zote, hawatakoma kuwa na mtu aliyeketi katika kiti cha enzi cha Israeli.
So that he may establish Yahweh word his which he spoke on me saying if they will guard descendants your way their to walk before me in faithfulness with all heart their and with all being their saying not it will be cut off to you a man from on [the] throne of Israel.
5 Wewe pia wajua kile Yoabu mwana wa Seruya alichonifanyia, na kile alichowafnyia majemedari wa majeshi y a Israeli, kwa Abina mwana wa Neri, na kwa Amasa mwana wa Yetheri, ambaye alimwua. Alimwaga damu vitani wakati wa amani na kuiweka ile damu kwenye mshipi uliokuwa kiunoni mwake na kwenye vile viatu miguuni mwake.
And also you you know [that] which he did to me Joab [the] son of Zeruiah [that] which he did to [the] two [the] commanders of [the] armies of Israel to Abner [the] son of Ner and to Amasa [the] son of Jether and he killed them and he put blood of war in peace and he put blood of war on belt his which [was] on loins his and on sandal[s] his which [was] on feet his.
6 Mshughulikie Yoabu kwa hekima ambayo umejifunza, lakini usiache mvi zake ziingie kaburini kwa amani. (Sheol h7585)
And you will act according to wisdom your and not you must bring down grey hair his in peace Sheol. (Sheol h7585)
7 Hata hivyo, uonyeshe utu kwa wana wa Barizilai Mgileadi, na uwaache wawe miongoni mwa wale wanaokula mezani kwako, kwa kuwa walikuja kwangu wakati nilipomkimbia ndugu yangu Absalomu.
And to [the] sons of Barzillai the Gileadite you will do loyalty and they will be among [those who] eat of table your for thus they drew near to me when fled I from before Absalom brother your.
8 Tazama, Shimei mwana wa Gera yuko pamoja na wewe, Wabenjamini wa Bahurimu, walionilaani kwa laana ya fujo siku niliyoenda kwa Mahanaimu. Shimei alishuka kuja kuniona pale Yorodani, na nikamwapia kwa BWANA, nikisema, 'Sitawaua kwa upanga,'
And here! [is] with you Shimei [the] son of Gera [the] Ben-jaminite from Bahurim and he he cursed me a curse grievous on [the] day went I Mahanaim and he he came down to meet me the Jordan and I swore to him by Yahweh saying if I will put to death you by the sword.
9 Kwa hiyo sasa usimwache aiepuke adhabu. Wewe ni mwenye hekima, na utajua jinsi itakavyokupasa kumtendea. Utakileta hicho kichwa chenye mvi chini kaburini.” (Sheol h7585)
And therefore may not you leave unpunished him for [are] a man wise you and you will know [that] which you will do to him and you will bring down grey hair his in blood Sheol. (Sheol h7585)
10 Ndipo Daudi alipolala na mababu zake na alizikwa kwenye mji wa Daudi.
And he lay down David with ancestors his and he was buried in [the] city of David.
11 Siku ambazo Daudi alitwala Israeli zilikuwani miaka arobaini. Alikuwa ametawala kwa miaka saba kule Hebroni na kwa miaka thelethini na tatu kule Yerusalemu.
And the days which he reigned David over Israel [were] forty year[s] in Hebron he reigned seven years and in Jerusalem he reigned thirty and three years.
12 Kisha Sulemani akaketi kwenye kiti cha enzi cha baba yake Daudi, na utawala wake ulikuwa imara.
And Solomon he sat on [the] throne of David father his and it was established reign his exceedingly.
13 Kisha Adoniya mwana wa Hagathi alikuja kwa Bathisheba mama wa Sulemani., Naye akamwuliza, “Je, unakuja kwa amani?” Naye akajiibu. “kwa amani.”
And he came Adonijah [the] son of Haggith to Bath-sheba [the] mother of Solomon and she said ¿ peace [are] coming you and he said peace.
14 Kisha akasema, “Nina jambo la kukuambia.” Naye akajibu, “Sema.”
And he said a word [belongs] to me to you and she said speak.
15 Adoniya amesema, “Unajua kuwa ufalme ulikuwa wangu, na kwamba Israeli yote ilikuwa inanitegemea mimi kuwa mfalme. Hata hivyo, ufalme umegeuzwa na umekuwa wa ndugu yangu, kwani ulikuwa wake toka kwa BWANA.
And he said you you know that to me it belonged the kingship and on me they set all Israel faces their to become king and it has turned round the kingship and it has belonged to brother my for from Yahweh it belonged to him.
16 Sasa nina ombi moja kwako. Usinikatalie.”Bathisheba akamwambia, “Sema.”
And now a petition one I [am] asking from with you may not you turn away face my and she said to him speak.
17 Naye akamwambia, “Tafadhali mwambie mfalme Sulemani, kwa kuwa hatakukatalia, ili kwamba anipatie Abishagi Mshunami awe mke wangu.”
And he said speak please to Solomon the king for not he will turn away face your so he may give to me Abishag the Shunammite to a wife.
18 Bathisheba akamwambia, “Vyema sana, nitamwambia mfalme”
And she said Bath-sheba good I I will speak on you to the king.
19 Kwa hiyo Bathisheba akaenda kumwambia, mfalme Sulemani kwa niaba ya Adoniya. Mfalme akainuka kumlaki na akapiga magoti mbele yake. Kisha akaa kwenye kiti chake cha enzi na kulikuwa na kiti kingine cha enzi kilicholetwa kwa ajili ya mama wa mfalme. Naye akaa mkono wa kuume wa mfalme.
And she went Bath-sheba to the king Solomon to speak to him on Adonijah and he rose the king to meet her and he bowed down to her and he sat on throne his and he placed a throne for [the] mother of the king and she sat to right [hand] his.
20 Ndipo alipomwambia, “Napenda kukuomba ombi moja dogo. Usinikalie.” Mfalme, akamjibu, “Mama omba kwa kuwa sitakukatalia.”
And she said a petition one small I [am] asking from with you may not you turn away face my and he said to her the king ask O mother my for not I will turn away face your.
21 Naya akamwambia, “Naomba Abishagi Mshunami apewe Adoniya ndugu yako awe mke wake.”
And she said let it be given Abishag the Shunammite to Adonijah brother your to a wife.
22 Mfalme Sulemani akamjibu mama yake, “Kwa nini unamwombea Adoniya huyo Abishagi Mshunami? Kwa nini usimwombee ufalme pia, kwa kuwa ni ndugu yangu mkubwa? - au kwa Abiathari kuhani, au Yoabu mwana wa Seruya?”
And he answered the king Solomon and he said to mother his and why? [are] you asking Abishag the Shunammite for Adonijah and ask for him the kingship for he [is] brother my old more than me and for him and for Abiathar the priest and for Joab [the] son of Zeruiah.
23 Kisha mfalme Sulemani akaapa kwa BWANA, akisema, “Mungu wangu na anifanyie hivyo, na zaidi pia, kama Adoniya hajayasema haya kinyume na maisha yake.
And he swore an oath the king Solomon by Yahweh saying thus may he do to me God and thus may he add if by own life his he has spoken Adonijah the word this.
24 Sasa basi kama BWANA aishivyo, ambaye ndiye alinifanya mimi kuwepo na kunipa kiti cha enzi cha Daudi baba yangu, na ambaye amenifanyia nyumba kwa ahadi yake, hakika Adoniya lazima auawe leo.”
And therefore [by] [the] life of Yahweh who he appointed me (and he made sit me *Q(k)*) on [the] throne of David father my and who he has made for me a house just as he spoke that this day he will be put to death Adonijah.
25 Kwa hiyo mfalme Sulemani akamtuma Benaya mwana wa Yehoyada naye akamkuta Adoniya na kumwua.
And he sent the king Solomon by [the] hand of Benaiah [the] son of Jehoiada and he fell on him and he died.
26 Kisha akamwambia Abiathari kuhani, “Nenda kwa Anathothi, kwenye mashamba yako. unastahili kufa, lakini sitakua sasa hivi, kwa sababu ulilbeba sanduku la BWANA mbele ya Daudi baba yangu na kujitabisha kwa namna mbalimbali kama baba yangu alivyopata tabu.”
And to Abiathar the priest he said the king Anathoth go to fields your for [are] a man of death you and on the day this not I will put to death you for you carried [the] ark of [the] Lord Yahweh before David father my and for you were afflicted in all that he was afflicted father my.
27 Kwa hiyo Sulemani akamfukuza Abiathari asiwe kuhani wa BWANA, ili kwamba atimilize maneno ya BWANA, aliyokuwa amesema juu ya nyumba ya Eli.
And he drove out Solomon Abiathar from being a priest of Yahweh to fulfill [the] word of Yahweh which he had spoken on [the] house of Eli in Shiloh.
28 Habari hizo zikamfikia Yoabu, Kwani Yoabu alimuunga mkono Adoniya, ingawa hakumuunga mkono Absalomu. Kwa hiyo Yoabu akakimbilia kwenye hema ya BWANA karibu na madhabahu na akabeba pembe za madhabahu.
And the report it came to Joab for Joab he had turned aside after Adonijah and after Absalom not he had turned aside and he fled Joab to [the] tent of Yahweh and he took hold on [the] horns of the altar.
29 Sulemani alipoambiwa kuwa Yoabu amekimbilia kwenye hema ya BWANA na sasa alikuwa karibu na madhabahu. Ndipo Sulemani alipomtuma Benaya mwana wa Yehoyada, akisema, “Nenda, ukamwue.”
And it was told to the king Solomon that he had fled Joab to [the] tent of Yahweh and there! [he was] beside the altar and he sent Solomon Benaiah [the] son of Jehoiada saying go fall on him.
30 Kwa hiyo Benaya akaenda kwenye hema ya BWANA na kumwambia, “Mfalme anasema utoke hemani.” Yoabu akamjibu, “Hapana, Nitafia hapa,” Kwa hiyo Benaya akarudi kwa mfalme, akasema, “Yoabu amesema atafia kwenye madhabahu,”
And he went Benaiah to [the] tent of Yahweh and he said to him thus he says the king come out and he said - In-deed here I will die and he brought back Benaiah the king word saying thus he spoke Joab and thus he answered me.
31 Naye mfalme akamwambia, “Kafanye kama alivyosema. Muue na ukamzike, ili kwamba uitoe kwangu na kwenye nyumba ya baba yangu damu ambayo Yoabu alimwaga bila sababu.
And he said to him the king do just as he has spoken and fall on him and you will bury him and you will remove - blood of without cause which he has shed Joab from on me and from on [the] house of father my.
32 BWANA na amrudishie damu yake kichwani kwake, kwa sababu aliwaua wanaume wawili wasio na hatia na wema kuliko yeye na akawaua kwa upanga, Abineri mwana wa Neri, Jemedari wa Jeshi la Israeli, na Amasa mwana wa Jetheri, jemedari wa jeshi la Yuda, bila baba yangu Daudi kujua.
And he will bring back Yahweh blood his on head his who he fell on two men righteous and good more than him and he killed them with the sword and father my David not he knew Abner [the] son of Ner [the] commander of [the] army of Israel and Amasa [the] son of Jether [the] commander of [the] army of Judah.
33 Kwa hiyo damu yao na imrudie Yoabu kichwani pake na kwenye vichwa vya uzao wake milele na milele. Lakini kwa Daudi na uzao wake, na nyumba yake, na kwenye kiti chake cha enzi, kuwe na amani ya kudumu kutoka kwa BWANA.”
And they will return blood their on [the] head of Joab and on [the] head of offspring his for ever and to David and to offspring his and to house his and to throne his it will belong peace until perpetuity from with Yahweh.
34 Kisha Benaya mwana wa Yehoyada akaenda akamvamia Yoabu na kumwua. Alizikwa kwenye nyumba yake kule jangwani.
And he went up Benaiah [the] son of Jehoiada and he fell on him and he put to death him and he was buried in own house his in the wilderness.
35 Mfalme akamwinua Benaya mwana wa Yehoyada kuwa juu ya jeshi badala yake, na akamweka Sadoki kuhani kwenye nafasi ya Abiatahari.
And he put the king Benaiah [the] son of Jehoiada in place of him over the army and Zadok the priest he put the king in place of Abiathar.
36 Kisha Mfalme akatuma watu kumwita Shimei, na akamwambia, “Kajijengee nyumba kwa ajili yako kule Yerusalemu na ushi huko, na usitoke nje ya Huo mji na kwenda mahali pengine.
And he sent the king and he summoned Shimei and he said to him build for yourself a house in Jerusalem and you will dwell there and not you must go out from there where? and where?
37 Kwa kuwa siku utakayoenda mahali pengine, na kupita bonde la Kidroni, ujue kwa hakika kuwa utakufa. Damu yako itakuwa juu ya kichwa chako.”
And it will be - on [the] day going out you and you will pass over [the] wadi of Kidron certainly you will know that certainly you will die blood your it will be on own head your.
38 Kwa hiyo Shimei akamwambia mfalme, “Unachosema ni chema. Kama vike mfalme bwana wangu alivyosema, ndivyo ambavyo mtumishi wako atakavyofanya.” Kwa hiyo Shimei akaishi Yerusalemu kwa miaka mingi.
And he said Shimei to the king [is] good the word just as he has spoken lord my the king so he will do servant your and he dwelt Shimei in Jerusalem days many.
39 Lakiini mwishoni mwa mwaka wa tatu, watumishi wawili wa Shimei wakakimbilia kwa Akishi mwana wa Maaka, mfalme wa Gathi. Kwa hiyo wakamwambia Shimei, wakisema, “Tazama, watumishi wako wameenda Gathi,”
And it was from [the] end of three years and they fled two servants of Shimei to Achish [the] son of Maacah [the] king of Gath and people told to Shimei saying there! servants your [are] in Gath.
40 Kisha Shimei akainuka, akapanda punda wake akaenda kwa Akishi huko Gathi kuwatafuta watumishi wake. Akaenda na akawaleta watumishi wake toka Gathi.
And he arose Shimei and he saddled donkey his and he went Gath towards to Achish to seek servants his and he went Shimei and he brought servants his from Gath.
41 Sulemani alipoambiwa kuwa Shimei alikuwa ametoka Yerusalemu kwenda Gathi na amerudi,
And it was told to Solomon that he had gone Shimei from Jerusalem Gath and he had returned.
42 mfalme akatuma wito kwa Shimei na kumwambia, “Je, sikukuapisha kwa BWANA na kushuhudia kwako, nikisema, 'Tambua kuwa siku utakayotoka kwenda nje na kwenda mahali popote, hakika utakufa'? Na ukaniambia kuwa unachosema ni chema.'
And he sent the king and he summoned Shimei and he said to him ¿ not did I make swear you by Yahweh and did I warn? you saying on [the] day going out you and you will go where? and where? certainly you will know that certainly you will die and you said to me [is] good the word I have heard.
43 Kwa nini basi umeshindwa kulinda kiapo chako kwa BWANA na amri niliyokupa?”
And why? not have you kept [the] oath of Yahweh and the command which I commanded to you.
44 Pia mfalme akamwambia Shimei, “Unajua katika moyo wako maovu yote uliyofanya kwa baba yangu Daudi. Kwa hiyo BWANA atakurudishia maovu yako kichwani pako.
And he said the king to Shimei you you know all the evil which it knows heart your which you did to David father my and he will return Yahweh evil your on head your.
45 Lakini Sulemani atabarikiwa na enzi ya Daudi itaimarika mbele ya BWANA milele.”
And the king Solomon [will be] blessed and [the] throne of David it will be established before Yahweh until perpetuity.
46 Kwa hiyo mfalme akamwamuru Benaya mwana wa Yehoyada kwenda kumwua Shimei. Kwa hiyo ule utawala ulikuwa mwema kwa mkono wa Sulemain.
And he commanded the king Benaiah [the] son of Jehoiada and he went out and he fell on him and he died and the kingdom it was established in [the] hand of Solomon.

< 1 Wafalme 2 >