< 1 Wafalme 19 >
1 Ahabu akamwambia Yezebeli mambo yote ambayo Eliya amefanya na jinsi alivyowaua manabii wote kwa upanga.
Achab raconta à Jézabel tout ce qu'Élie avait fait, et comment il avait tué par l'épée tous les prophètes.
2 Ndipo Yezebeli alipotuma mjumbe kwa Eliya, akisema, “miungu wanifanye hivyo na mimi, na zaidi yake, kama kesho muda kama huu sitayafanya maisha yako kuwa kama mmoja wa hao manabii waliokufa.”
Alors Jézabel envoya un messager à Élie, en disant: « Que les dieux me fassent ainsi, et plus encore, si je ne fais pas de ta vie la vie de l'un d'eux, demain à cette heure-ci! ».
3 Eliya aliposikia hayo, akaiinuka na akakimbia kwa ajili ya kuokoa maisha yake akaja mpaka Beerisheba, ambao ni mji wa Yuda, na akamwacha mtumishi wake huko.
Dès qu'il vit cela, il se leva et courut pour sauver sa vie, et il arriva à Beersheba, qui appartient à Juda, et il y laissa son serviteur.
4 Lakini yeye mwenyewe akaenda mwendo wa siku moja huko jangwani, akaja akakaa chini ya mti wa mretemu. Akajiombea mwenyewe kufa, akasema, “Sasa yatosha, BWANA, ichukue roho yangu, kwa kuwa mimi si mzuri kuliko mababu zangu waliokufa.”
Mais lui-même fit une journée de marche dans le désert, et vint s'asseoir sous un genévrier. Puis il demanda pour lui-même à mourir, et dit: « C'est assez. Maintenant, Yahvé, ôte-moi la vie, car je ne suis pas meilleur que mes pères. »
5 Kwa hiyo akalala chini ya mretemu. Ghafula malaika akamgusa na akamwambia, “Inuka ule.”
Il se coucha et dormit sous un genévrier; et voici qu'un ange le toucha et lui dit: « Lève-toi et mange! »
6 Eliya akatazama, karibu na kichwa chake kulikuwa na mkate uliokuwa umeokwa kwa mkaa na gudulia la maji. Kwa hiyo akala na kunywa na kulala tena.
Il regarda, et voici qu'il y avait à sa tête un gâteau cuit sur les charbons, et une cruche d'eau. Il mangea et but, puis il se recoucha.
7 Malaika wa BWANA akaja tena mara ya pili akamgusa na kumwambia, “Inuka ule, kwa sababu safari bado ndefu kwako.”
L'ange de Yahvé revint une seconde fois, le toucha et lui dit: « Lève-toi et mange, car le voyage est trop long pour toi. »
8 Kwa hiyo akainuka na kula na kunywa, naye akasafiri kwa nguvu ya chakula hicho kwa siku arobaini mchana na usiku hata akafika Horebu, mlima wa Mungu.
Il se leva, mangea et but, et alla, à la force de cette nourriture, quarante jours et quarante nuits, à Horeb, la montagne de Dieu.
9 Akaingia kwenye pango akakaa humo. Kisha neno la BWANA likamjia likimwambia, “Unafanya nini hapa, Eliya?”
Il arriva dans une caverne, où il campa. Et voici que la parole de Yahvé lui fut adressée, et il lui dit: « Que fais-tu ici, Elie? »
10 Eliya akajibu, “Nimeona wivu mwingi kwa BWANA, Mungu wa majeshi, kwa kuwa watu wa Israeli wameliacha agano lako, wameziharibu madhabahu zako, na wamewaua manabii wako kwa upanga. Sasa ni mimi, pekee yangu, nimebaki na wanataka kuichukua roho yangu.
Il dit: « J'ai été très jaloux de Yahvé, le Dieu des armées, car les enfants d'Israël ont abandonné ton alliance, renversé tes autels et tué tes prophètes par l'épée. Il ne reste que moi, moi seul, et ils cherchent à m'enlever la vie. »
11 BWANA akamwambia, “Nenda nje ukasimame kwenye mlima mbele yangu.” Kisha BWANA akapita, na upepo mkali ukaupiga mlima ukavunja miamba katika vipande vipande mbele ya BWANA, lakini BWANA hakuwemo kwenye huo mlima. Kisha baada ya upepo, tetemeko lakaja, lakini BWANA hakuwemo kwenye hilo tetemeko.
Il dit: « Sors et tiens-toi sur la montagne devant Yahvé. » Voici que Yahvé passait, et un vent grand et fort déchirait les montagnes et brisait les rochers devant Yahvé; mais Yahvé n'était pas dans le vent. Après le vent, il y eut un tremblement de terre; mais Yahvé n'était pas dans le tremblement de terre.
12 Kisha baada ya tetemeko, moto ukaja, lakini BWANA hakuwemo kwenye moto. Ndipo baada ya moto, sauti ya upole ikaja.
Après le tremblement de terre, il y eut un feu; mais Yahvé n'était pas dans le feu. Après le feu, il y eut une petite voix calme.
13 Naye Eliya alipoisikia sauti, akafunika uso wake kwa vazi lake, akatoka nje, akasimama kwenye lango la hilo pango. Na sauti ikaja kwake ikisema, “unafanya nini hapa?,
Lorsque Élie l'entendit, il enveloppa son visage dans son manteau, sortit et se tint à l'entrée de la caverne. Et voici qu'une voix s'approcha de lui et dit: « Que fais-tu ici, Élie? »
14 Eliya akajibu, “nimeona wivu sana kwa ajili ya BWANA, Muungu wa majeshi, kwa kuwa watu wa Israeli wameliacha agano lako, wamezihariibu madhabahu zako, na wamewaua manabii kwa upanga. Sasa, ni mimi pekee yangu, nimebaki na wanajaribu kuichukua roho yangu.”
Il dit: « J'ai été très jaloux de Yahvé, le Dieu des armées, car les enfants d'Israël ont abandonné ton alliance, jeté tes autels et tué tes prophètes par l'épée. Il ne reste que moi, moi seul, et ils cherchent à m'enlever la vie. »
15 Kisha BWANA akamwambia, “Nenda, rudi kwa njia yako kwenye jangwa la Dameski, na utakapofika utamtia mafuta Hazaeli awe Mfalme wa Shamu,
Yahvé lui dit: « Va, retourne sur ton chemin dans le désert de Damas. A ton arrivée, oint Hazaël comme roi de Syrie.
16 na utamtia mafuta Yehu mwana wa Nimshi kuwa mfalme wa Israeli, na utamtia mafuta Elisha mwana wa Shafeti wa Abeli Mehola kuwa nabii mahali pako.
Oint Jéhu, fils de Nimshi, comme roi d'Israël, et oint Élisée, fils de Shaphat, d'Abel Meholah, comme prophète à ta place.
17 Itakuwa hivi Yehu atamwua kila mmoja atakayejaribu kutoroka upanga wa Hazaeli, na kwamba Elisha atamwua kila atakayejaribu kukwepa upanga wa Yehu.
Celui qui échappera à l'épée de Hazaël, Jehu le tuera; et celui qui échappera à l'épée de Jehu, Élisée le tuera.
18 Lakini nitawaacha watu elfu saba katika Israeli kwa ajili yangu, ambao magoti yao hayajawahi kupigwa kwa Baali, na ambao midomo yao haijambusu.”
Mais j'en ai réservé sept mille en Israël, tous ceux dont les genoux n'ont pas fléchi devant Baal et toutes les bouches qui ne l'ont pas baisé. »
19 Kwa hiyo Eliya akaondoka mahali pale na akamkuta Elisha mwana wa Shafati, akilima na jozi za makisai kumi na mbili mbele yake, na yeye mwenyewe alikuwa akilima na ile jozi ya kumi na mbili. Eliya akaenda mpaka kwa Elisha akamtupia vazi lake juu yake.
Et il partit de là et trouva Élisée, fils de Shaphat, qui labourait avec douze jougs de bœufs devant lui, et lui avec le douzième. Élie s'approcha de lui et le revêtit de son manteau.
20 Elisha naye akawaacha wale makisai akamkimbilia Eliya; akamwambia, “Tafadhali naomba nikambusu baba yangu na mama yangu kisha nitakufuata.” Naye Eliya akamwambia, “Rudi, lakini fikiria juu ya kile nilichokufanyia.”
Élisée laissa les bœufs, courut après Élie et dit: « Laisse-moi, s'il te plaît, embrasser mon père et ma mère, et ensuite je te suivrai. » Il lui dit: « Va-t'en, car que t'ai-je fait? »
21 Kwa hiyo Elisha akarudi toka kwa Eliya na akachukua ile jozi ya makisai, akawaua wale wanyama, na akapika ile nyama kwa kuni za ile nira. Kisha akawapa watu wakala. Kisha akaamka, akamfuata Eliya akamtumikia.
Il s'en retourna après l'avoir suivi, prit le joug des bœufs, les tua, fit bouillir leur viande avec l'équipement des bœufs, et la donna au peuple; et ils mangèrent. Puis il se leva, alla après Élie, et le servit.