< 1 Wafalme 18 >
1 Kwa hiyo baada ya siku nyingi neno la BWANA likamjia Eliya, katika mwaka wa tatu wa ukame, likisema, “Nenda ukajionyeshe mwenyewe kwa Ahabu nami nitainyeshea ardhi mvua.”
Aftir many daies the word of the Lord was maad to Elie, in the thridde yeer, and seide, Go, and schewe thee to Achab, that Y yyue reyn on the face of erthe.
2 Eliya akaenda kujionyesha mwenyewe kwa Ahabu; sasa njaa ilikuwa kali sana kule Samaria.
Therfor Elie yede to schewe hym silf to Achab; forsothe greet hungur was in Samarie.
3 Ahabu akamwita Obadia, aliyekuwa mkuu wa ikulu. Obadia alimheshimu sana BWANA,
And Achab clepide Abdie, dispendere, ether stiward, of his hows; forsothe Abdie dredde greetli the Lord God of Israel.
4 kwa kuwa wakati Yezebeli alipokuwa akiwaua manabii wa BWANA, Obadia alichukua manabii mia akawaficha katika makundi ya hamsini hamsini katika pango na akawalisha kwa mikate na maji.
For whanne Jezabel killide the prophetis of the Lord, he took an hundrid prophetis, and hidde hem, bi fifties and fifties, in dennes, and fedde hem with breed and watir.
5 Ahabu akamwambia Obadia, “Pita katika nchi yote na katika chemichemi zote za maji na vijito. Yamkini tunaweza kupata maji na nyasi ili tuwaokoa hawa farasi na nyumbu, ili tusiwakose wanyama wote.”
Therfor Achab seide to Abdie, Go thou in to the lond, to alle wellis of watris, and in to alle valeis, if in hap we moun fynde gras, and saue horsis and mulis; and werk beestis perische not outirli.
6 Kwa hiyo wakaigawa nchi kati yao ili wapite kati yake wakitafuta maji. Ahabu akaenda njia yake mwenyewe na Obadia naye akaenda njia yake.
Therfor thei departiden the cuntreis to hem silf, that thei schulden cumpasse tho; Achab yede bi o weye, and Abdie yede bi another weie, `bi hym silf.
7 Wakati Obadia akiwa njiani, akakutana na Eliya pasipo kutegemea. Obadia akamtambua na akalala kifudifudi chini. Akamwambia, “Ndiye wewe, bwana wangu Eliya?”
And whanne Abdie was in the weie, Elie mette hym; and whanne he hadde knowe Elie, he felde on his face, and seide, Whethir thou art my lord Elie?
8 Naye Eliya akamjibu, Ni mimi. Nenda umwambie bwana wako, 'Tazama, Eliya yuko hapa.'”
To whom he answeride, Y am. And Elie seide, Go thou, and seie to thi lord, Elie is present.
9 Obadia akamjibu. “Nimekoseaje, kwamba umtoe mtumishi wako katika mkono wa Ahabu ili aniue?
And Abdie seide, What `synnede Y, for thou bitakist me in the hond of Achab, that he sle me?
10 Kama BWANA Mungu wako aishivyo, hakuna taifa wala ufalme ambapo bwana wangu hajatuma watu kukutafuta. Kila taifa au ufalme unaposema, “Eliya hayuko hapa,' Ahabu hufanya waape ni kweli hawajakuona.
Thi Lord God lyueth, for no folk ethir rewme is, whidur my lord, sekynge thee, sente not; and whanne alle men answeriden, He is not here, he chargide greetli alle rewmes and folkis, for thou were not foundun; and now thou seist to me,
11 Na sasa wewe unasema, 'Nenda, ukamwambie bwana wako kwamba Eliya yuko hapa.'
Go, and seie to thi lord, Elie is present.
12 Mara tu baada ya kukuacha Roho wa BWANA atakuchukua na kukupeleka mahali ambapo sitapajua. Kisha nikienda na kumwambia Ahabu, na asipokuona, ataniua. Bado, mimi, mtumishi wako, nimekuwa nikimwabudu BWANA kutoka ujana wangu.
And whanne Y schal departe fro thee, the Spirit of the Lord schal bere thee awey in to a place which Y knowe not; and Y schal entre, and `Y schal telle to Achab, and he schal not fynde thee, and he schal sle me; forsothe thi seruaunt dredith the Lord fro his yong childhod.
13 Je, haujaambiwa, bwana wangu, nilichokifanya wakati Yezebeli alipowaua manabii wa BWANA, jinsi nilivyowaficha wale manabii mia moja wa BWANA katika makundi ya hamsini kwenye pango na kuwalisha kwa mikate na maji?
Whether it is not schewid to thee, my lord, what Y dide, whanne Jesabel killide the prophetis of the Lord, that Y hidde of the prophetis of the Lord an hundrid men, bi fifty and bi fifti, in dennes, and Y fedde hem with breed and watir?
14 Na sasa unasema, 'Nenda umwambie bwana wako kwamba Eliya yuko hapa,' kwa hiyo ataniua.”
And now thou seist, Go, and seie to thi lord, Elie is present, that he sle me.
15 Ndipo Eliya alipomjibu, “Kama vile BWANA wa majeshi aishivyo, ambaye mimi ninasimama, Kwa hakika nitajionyeshakwa Ahabu leo.”
And Elie seide, The Lord of oostis lyueth, bifor whos siyt Y stonde, for to dai Y schal appere to hym.
16 Kwa hiyo Obadia akaenda kukutana na Ahabu, nakumwambia kile Eliya alichokuwa amemwambia. Ndipo mfalme alipoenda kukutana na Eliya.
Therfor Abdie yede in to the metyng of Achab, and schewide to hym; and Achab cam in to the meetyng of Elie.
17 Ahabu alipomwona Eliya, akamwambia, “Je, ni wewe? Wewe mtabishaji wa Israeli!”
And whanne he hadde seyn Elie, he seide, Whether thou art he, that disturblist Israel?
18 Eliya akamwambia, “Mimi sijaitabisha Israeli, Lakiini wewe na familia ya baba yako ndio watabishaji kwa kuziacha amri za BWANA na kufuata sanamu za Baali.
And he seide, Not Y disturble Israel, but thou, and the hows of thi fadir, whiche han forsake the comaundementis of the Lord, and sueden Baalym, `disturbliden Israel.
19 Kwa hiyo sasa, Tuma neno na unikusanyie Israeli yote katika mlima Kameli, pamoja na manabii 450 wa Baali na wale manabii 400 wa Ashera wanaokula kwenye meza ya Yezebeli.”
Netheles now sende thou, and gadere to me al Israel, in the hil of Carmele, and foure hundrid and fifti prophetis of Baal, and foure hundrid prophetis of woodis, that eten of the table of Jezabel.
20 Kwa hiyo Ahabu akatuma neno kwa watu wote wa Israeli na akawakusanya manabii wote kwenye mlima Kameli.
Achab sente to alle the sones of Israel, and gaderide prophetis in the hil of Carmele.
21 Eliya akaja karibu na watu wote akasema, “Mtaendelea kubadilisha mawazo yenu mpaka lini? Kama BWANA ni Mungu, mfuateni yeye, Lakini kama Baali ni Mungu, basi mfuateni yeye,” Lakini watu hawakumjibu neno.
Forsothe Elie neiyede to al the puple of Israel, and seide, Hou long halten ye in to twey partis? If the Lord is God, sue ye hym; forsothe if Baal is God, sue ye hym. And the puple answeride not o word to hym.
22 Kisha Eliya akawaambia wale watu, “Mimi, pekee yangu, ndiye niliyebaki kuwa nabii wa BWANA, lakini manabii wa Baali wako 450.
And Elie seide eft to the puple, Y dwellide aloone a prophete of the Lord; sotheli the prophetis of Baal ben foure hundrid and fifti, and the prophetis of woodis ben foure hundrid men.
23 Hebu tutoleeni ng'ombe wawili. Nao wajichagulie ng'ombe mmoja na wamchinje na kumkatakata katika vipnde, na wamweke kwenye kuni, na wasitie moto chini yake. Nami nitamwandaa yule wa pili na kumweke juu ya kuni nami sitatia moto chini yake.
Tweyne oxis be youun to us; and chese thei oon oxe, and thei schulen kitte in to gobetis, and schulen putte on trees, but putte thei not fier vndur; and Y schal make the tother oxe in to sacrifice, and Y schal putte on the trees, and Y schal not putte fier vnder.
24 Kisha mtaliita jina la mungu wenu, nami nitaliita jina la BWANA, na Mungu atakayejibu kwa moto, huyo ndiye Mungu.” Watu wote wakajibu na kusema, “Hilo ni jambo jema.”
Clepe ye the name of youre goddis, and Y schal clepe the name of my God; and the God that herith bi fier, be he God. And al the puple answeride, and seide, The resoun is best, `which resoun Elie spak.
25 Kwa Eliya akawaambia manabii wa Baali, “Chagueni ng'ombe mmoja kwa ajili yenu na mwe wa kwanza kumwamdaa, kwa kuwa ninyi ni wengi, Kisha liiteni jina la mungu wenu, lakini msiwashe moto.”
Therfor Elie seide to the prophetis of Baal, Chese ye oon oxe to you, and make ye first, for ye ben the mo; and clepe ye the names of youre goddis, and putte ye not fier vnder.
26 Nao wakamchukua yule ng'ombe waliokuwa wamepewa na wakamwandaa, na ndipo walipoliita jina la Baali kuanzia asubuhi hadi adhuhuri, wakisema, “Baali, tusikie.” Lakini hapakuwepo na Sauti, na wala hakuna aliyejibu. Wakachezacheza kuizunguka madhabahu waliyotengeneza.
And whanne thei hadden take the oxe, whom Elie yaf to hem, thei maden sacrifice, and clepiden the name of Baal, fro the morewtid `til to myddai, and seiden, Baal, here vs! And no vois was, nether ony that answerd; and thei skippiden ouer the auter, which thei hadden maad.
27 Ilipofika adhuhuri Eliya akawakejeli akisema, “Mwiteni kwa nguvu! Huyo ni mungu! labda anawaza kitu, au amepumzika, au yuko safarini, au pengine amelala sharti aamshwe.”
And whanne it was thanne myddai, Elie scornede hem, and seide, Crie ye with gretter vois, for Baal is youre god, and in hap he spekith with an other, ethir he is in a herborgerie, ether in weie, ether certis he slepith, that he be reisid.
28 Kwa hiyo wakamwita kwa nguvu, wakajikatakata kama kawaida yao ilivyokuwa, kwa upanga na nyembe, mpaka damu ikawachuruzika.
Therfor thei crieden with greet vois, and thei kerueden hem silf with knyues and launcetis, bi her custom, til thei weren bisched with blood.
29 Ikawa wakati wa adhuhuri ulipopita, na bado walikuwa wakiendelea kutabiri mpaka wakati wa jioni wa kutoa dhabihu, lakini hapakuwepo na sauti wala mtu wa kuwajibu; wala hapakuwepo na yeyote wa kujibu wala wa kuangalia.
Sotheli after that mydday passide, and while thei prophesieden, the tyme cam, in which the sacrifice is wont to be offrid, nether vois was herd `of her goddis, nether ony answeride, nether perceyuede hem preiynge.
30 Kisha Eliya akawaambia watu wote, “Nisogeleeni,” na watu wote wakamsogelea. Naye akatengeneza ile madhabahu ya BWANA ambayo ilikuwa imeharibika.
Elie seide to al the puple, Come ye to me. And whanne the puple cam to him, he arrayede the auter of the Lord, that was distried.
31 Eliya akachukua mawe kumi na mawili, kila jiwe moja liliwakilisha kabila moja la wana wa Yakobo - ni kupitia Yakobo kwamba neno la BWANA lilikuja, likisema, “Jina lako litakuwa Israel.”
And he took twelue stonys, bi the noumbre of lynagis of sones of Jacob, to which Jacob the word of the Lord was maad, and seide, Israel schal be thi name.
32 Kwa kutumia hayo mawe aliijenga ile madhabahu kwa jina la BWANA na akachimba mfereji kuizunguka ile madhabahu kubwa kiasi cha kubeba lita kumi na tano za maji.
And he bildide an auter of stonys, in the name of the Lord, and he made a ledyng to of watir, `ether a dich, as bi twei litle dichis in the cumpas of the auter.
33 Kisha akaweka kuni kwa ajili ya moto na akamkatakata yule ng'ombe katika vipande vipande na akaweka vile vipande juu ya kuni. Na akasema, “Vijazeni maji hivyo vyombo na yamwageni kwenye hiyo sadaka ya kueketezwa na juu ya hizo kuni.”
And he dresside trees, and he departide the oxe bi membris, and puttide on the trees,
34 Akasema tena fanyeni hivyo mara ya pili,” nao wakafanya kwa mara ya pili. kisha akasema, “Fanyeni mara ya tatu,” nao wakafanya kwa mara ya tatu.
and seide, Fille ye foure pottis with watir, and schede ye on the brent sacrifice, and on the trees. And eft he seide, Also the secounde tyme do ye this. `And thei diden the secounde tyme. And he seide, Do ye the same thing the thridde tyme; and thei diden the thridde tyme.
35 Maji yakaizunguka ile madhabahu na kuujaza ule mfereji.
And the watris runnen aboute the auter, and the dich of ledyng to `of watir was fillid.
36 Ikawa wakati wa kutoa dhabihu ya jioni, nabii Eliya akasogea na akasema, “BWANA, Mungu wa Abrahamu, na wa Isaka, na wa Israeli, na ijulikane leo kwamba wewe ndiye Mungu wa Israeli, na kwamba mimi ni mtumishi wako, na kwamba nimeyafanya mambo haya yote kwa jina lako.
And whanne the tyme was thanne, that the brent sacrifice schulde be offrid, Elye the prophete neiyede, and seide, Lord God of Abraham, of Isaac, and of Israel, schewe thou to dai that thou art God of Israel, and that Y am thi seruaunt, and haue do alle these wordis bi thi comaundement.
37 Nisikie, BWANA, nisike, ili hawa watu wajue kuwa wewe, BWANA, ndiye Mungu, na kwamba umeirudisha mioyo yao kwako tena.”
Lord, here thou me; Lord, here thou me; that this puple lerne, that thou art the Lord God, and that thou hast conuertid eft the herte of hem.
38 Ndipo moto wa BWANA ukashuka ukairamba ile sadaka, pamoja na zile kuni, mawe na mavumbi, na kuyaramba yale maji yaliyokuwa kwenye ule mfereji.
Sotheli fier of the Lord felde doun, and deuouride brent sacrifice, and trees, and stonus, and lickide vp also the poudre, and the water that was in the `leding of water.
39 watu wote walipoona haya, wakalala kifudifudi chini wakasema, “BWANA, ndiye Mungu! BWANA ndiye Mungu!
And whanne al the puple hadde seyn this, it felde in to his face, and seide, The Lord he is God; the Lord he is God.
40 Kwa hiyo Eliya akawaambia, “Wakamateni manabii wa Baali. Msimwache hata mmoja wao atoroke.” Kwa hiyo wakawakamata, na Eliya akawaleta manabii wa Baali chini kwenye kijito cha Kishoni na akawaua huko.
And Elie seide to hem, Take ye the prophetis of Baal; not oon sotheli ascape of hem. And whanne thei hadden take hem, Elie ledde hem to the stronde of Cison, and killide hem there.
41 Eliya akamwambia Ahabu, “Inuka, ule na kunywa, kwa kuwa kuna sauti ya mvua kubwa.”
And Elie seide to Achab, Stie thou, ete, and drynke, for the sown of myche reyn is.
42 Kwa hiyo Ahabu akaenda akala na knywa. Kisha Eliya akaenda juu ya mlima Kameli, akasudu chini na akaweka uso wake katikati ya magoti.
Achab stiede to ete and drynke; forsothe Elie stiede in to the hil of Carmele, and he settide lowli his face to the erthe, bitwixe hise knees;
43 Akamwambia mtumishi wake, “Nenda sasa, utazame upande wa bahari.” mtumishi wake akaenda na akasema, “Hakuna kitu,” Eliya akamwambia, “Nenda tena, mpaka mara saba.”
and seide to his child, Stie thou, and biholde ayens the see. And whanne he hadde stied, and hadde biholde, he seide, No thing is. And eft Elie seide to hym, Turne thou ayen bi seuene tymes.
44 Ile mara ya saba mtumishi wake akasema, “Tazama, kuna wingu linapanda kutoka baharini, ni dogo kama mkono wa mtu.” Eliya akamjibu, Nenda ukamwambie Ahabu, 'Andaa gari lako na ushuke kabla mvua haijakuzuia.'”
Sotheli in the seuenthe tyme, lo! a litil cloude as the step of a man stiede fro the see. And Elie seide, Stie thou, and seie to Achab, Ioyne thi chare, and go doun, lest the reyn byfor ocupie thee.
45 Ikatokea baada ya muda mfupi mbingu zikawa nyeusi kwa mawingu na upepo, na kulikuwa na mvua kubwa. Ahabu akapanda gari akaenda zake Yezreeli,
And whanne thei turneden hem hidur and thidur, lo! heuenes weren maad derk, and cloud, and wynd, and greet reyn was maad. Therfor Achab stiede, and yede in to Jezrael;
46 lakini mkono wa BWANA ulikuwa juu ya Eliya. Akalikaza vazi lake kwa mshipi wake na akakimbia mbele ya Ahabu kwenye lango la Yezreeli.
and the hond of the Lord was maad on Elie, and whanne the leendis weren gird, he ran bifor Achab, til he cam in to Jezrael.