< 1 Wafalme 18 >

1 Kwa hiyo baada ya siku nyingi neno la BWANA likamjia Eliya, katika mwaka wa tatu wa ukame, likisema, “Nenda ukajionyeshe mwenyewe kwa Ahabu nami nitainyeshea ardhi mvua.”
For almost three years there was no rain in Samaria. Then Yahweh said this to Elijah: “Go and meet with King Ahab and [tell him that] I will soon send rain.”
2 Eliya akaenda kujionyesha mwenyewe kwa Ahabu; sasa njaa ilikuwa kali sana kule Samaria.
So Elijah went to talk to Ahab. In Samaria there was almost no food for anyone to eat.
3 Ahabu akamwita Obadia, aliyekuwa mkuu wa ikulu. Obadia alimheshimu sana BWANA,
There was a man there named Obadiah. He was in charge of the king’s palace. He greatly revered Yahweh.
4 kwa kuwa wakati Yezebeli alipokuwa akiwaua manabii wa BWANA, Obadia alichukua manabii mia akawaficha katika makundi ya hamsini hamsini katika pango na akawalisha kwa mikate na maji.
One time when [Queen] Jezebel had [tried to] kill all Yahweh’s prophets, Obadiah hid 100 of them in two caves. He put 50 prophets in each cave, and he brought food and water to them.
5 Ahabu akamwambia Obadia, “Pita katika nchi yote na katika chemichemi zote za maji na vijito. Yamkini tunaweza kupata maji na nyasi ili tuwaokoa hawa farasi na nyumbu, ili tusiwakose wanyama wote.”
[By this time, the (famine/lack of food and water) had become very severe in Samaria]. So Ahab summoned Obadiah and said to him, “We must check/look near every spring and in every valley to see if we can find enough grass to give to some of my horses and mules, so that they will not all die.”
6 Kwa hiyo wakaigawa nchi kati yao ili wapite kati yake wakitafuta maji. Ahabu akaenda njia yake mwenyewe na Obadia naye akaenda njia yake.
So they both started walking throughout the land. Obadiah went in one direction by himself, and Ahab went in another direction by himself.
7 Wakati Obadia akiwa njiani, akakutana na Eliya pasipo kutegemea. Obadia akamtambua na akalala kifudifudi chini. Akamwambia, “Ndiye wewe, bwana wangu Eliya?”
While Obadiah was walking along, he saw Elijah coming toward him. Obadiah recognized Elijah and bowed down in front of him and said, “Is it really you, Elijah, my master?”
8 Naye Eliya akamjibu, Ni mimi. Nenda umwambie bwana wako, 'Tazama, Eliya yuko hapa.'”
Elijah replied, “Yes. Now go and tell [Ahab, ] your master, that I am here.”
9 Obadia akamjibu. “Nimekoseaje, kwamba umtoe mtumishi wako katika mkono wa Ahabu ili aniue?
Obadiah objected. He said, “Sir, I have not [RHQ] harmed you at all. So why are you sending me back to Ahab? He will kill me!
10 Kama BWANA Mungu wako aishivyo, hakuna taifa wala ufalme ambapo bwana wangu hajatuma watu kukutafuta. Kila taifa au ufalme unaposema, “Eliya hayuko hapa,' Ahabu hufanya waape ni kweli hawajakuona.
Yahweh your God [knows that I am telling the truth when] I solemnly declare that King Ahab has searched in every kingdom all over the world [HYP] to find you. Each time that some king said to him, ‘Elijah is not here,’ Ahab demanded that the king of that country solemnly swear/declare that the king was telling the truth.
11 Na sasa wewe unasema, 'Nenda, ukamwambie bwana wako kwamba Eliya yuko hapa.'
Now you say to me, ‘Go and tell your master that Elijah is here!’
12 Mara tu baada ya kukuacha Roho wa BWANA atakuchukua na kukupeleka mahali ambapo sitapajua. Kisha nikienda na kumwambia Ahabu, na asipokuona, ataniua. Bado, mimi, mtumishi wako, nimekuwa nikimwabudu BWANA kutoka ujana wangu.
But as soon as I leave you, the Spirit of Yahweh will carry you away, and I will not know where he will take you. So when [I tell] Ahab [that you are here and he] comes to me and he does not find you here, he will kill me! But [I do not deserve to die because] I have revered Yahweh since I was a boy.
13 Je, haujaambiwa, bwana wangu, nilichokifanya wakati Yezebeli alipowaua manabii wa BWANA, jinsi nilivyowaficha wale manabii mia moja wa BWANA katika makundi ya hamsini kwenye pango na kuwalisha kwa mikate na maji?
My master, have you not heard about what I did when Jezebel wanted to kill all of Yahweh’s prophets? I hid 100 of them in two caves and took food and water to them.
14 Na sasa unasema, 'Nenda umwambie bwana wako kwamba Eliya yuko hapa,' kwa hiyo ataniua.”
Now, sir, you say, ‘Go and tell your master that Elijah is here.’ But if I do that, [and he comes and you are not here, ] he will kill me!”
15 Ndipo Eliya alipomjibu, “Kama vile BWANA wa majeshi aishivyo, ambaye mimi ninasimama, Kwa hakika nitajionyeshakwa Ahabu leo.”
But Elijah replied, “Yahweh, the Almighty One whom I serve [IDM], knows that [I am telling the truth as] I solemnly declare that I will go to meet with Ahab today.”
16 Kwa hiyo Obadia akaenda kukutana na Ahabu, nakumwambia kile Eliya alichokuwa amemwambia. Ndipo mfalme alipoenda kukutana na Eliya.
So Obadiah went to tell Ahab that Elijah had come. Ahab went to meet with him.
17 Ahabu alipomwona Eliya, akamwambia, “Je, ni wewe? Wewe mtabishaji wa Israeli!”
When he saw Elijah, he said to him, “Is that you, the one who causes trouble for [the people of] Israel?”
18 Eliya akamwambia, “Mimi sijaitabisha Israeli, Lakiini wewe na familia ya baba yako ndio watabishaji kwa kuziacha amri za BWANA na kufuata sanamu za Baali.
Elijah replied, “It is not I who have caused trouble for the people of Israel! You and your family are the ones who have caused trouble! You have refused to obey Yahweh’s commands, and you have worshiped the idols of Baal instead.
19 Kwa hiyo sasa, Tuma neno na unikusanyie Israeli yote katika mlima Kameli, pamoja na manabii 450 wa Baali na wale manabii 400 wa Ashera wanaokula kwenye meza ya Yezebeli.”
So now, command all the Israeli people to come to Carmel Mountain, and [be sure to] bring all the 450 prophets who worship Baal and the 400 prophets who worship [the goddess] Asherah, the ones to whom [your wife] Jezebel brings food and water.”
20 Kwa hiyo Ahabu akatuma neno kwa watu wote wa Israeli na akawakusanya manabii wote kwenye mlima Kameli.
So Ahab summoned all his prophets and all the other [Israeli] people to the top of Carmel Mountain, [and Elijah went up there too.]
21 Eliya akaja karibu na watu wote akasema, “Mtaendelea kubadilisha mawazo yenu mpaka lini? Kama BWANA ni Mungu, mfuateni yeye, Lakini kama Baali ni Mungu, basi mfuateni yeye,” Lakini watu hawakumjibu neno.
Then Elijah stood in front of them and said, “How long [RHQ] are you going to be undecided [about who is truly God]? If Yahweh is [truly] God, then worship/serve him. If Baal is truly God, then worship/serve him!” But the people said nothing [in reply, because they were afraid of what Jezebel would do to them if they admitted that they worshiped Yahweh].
22 Kisha Eliya akawaambia wale watu, “Mimi, pekee yangu, ndiye niliyebaki kuwa nabii wa BWANA, lakini manabii wa Baali wako 450.
Then Elijah said to them, “I am the only true prophet of Yahweh who is left, but Baal has 450 prophets.
23 Hebu tutoleeni ng'ombe wawili. Nao wajichagulie ng'ombe mmoja na wamchinje na kumkatakata katika vipnde, na wamweke kwenye kuni, na wasitie moto chini yake. Nami nitamwandaa yule wa pili na kumweke juu ya kuni nami sitatia moto chini yake.
Bring two bulls. The prophets of Baal may choose the one that they want. They must [kill it and] cut it into pieces and lay the pieces on the wood that is on the altar that they have made. But they must not light a fire [under the wood]. [I will kill the other bull and cut it in pieces and lay the pieces on the altar that I make].
24 Kisha mtaliita jina la mungu wenu, nami nitaliita jina la BWANA, na Mungu atakayejibu kwa moto, huyo ndiye Mungu.” Watu wote wakajibu na kusema, “Hilo ni jambo jema.”
Then they must call to their god [MTY], and I will call to Yahweh. The god who answers by lighting a fire [to the wood that is on that altar] is [the true] God!” Then all the people thought that Elijah’s suggestion was good.
25 Kwa Eliya akawaambia manabii wa Baali, “Chagueni ng'ombe mmoja kwa ajili yenu na mwe wa kwanza kumwamdaa, kwa kuwa ninyi ni wengi, Kisha liiteni jina la mungu wenu, lakini msiwashe moto.”
Then Elijah said to the prophets of Baal, “You call to Baal first, because there are many of you. Choose one of the bulls and prepare it, and then call to your god. But do not light a fire under the wood!”
26 Nao wakamchukua yule ng'ombe waliokuwa wamepewa na wakamwandaa, na ndipo walipoliita jina la Baali kuanzia asubuhi hadi adhuhuri, wakisema, “Baali, tusikie.” Lakini hapakuwepo na Sauti, na wala hakuna aliyejibu. Wakachezacheza kuizunguka madhabahu waliyotengeneza.
So they killed one of the bulls and cut it up and placed the pieces on the altar. Then they called out to Baal all morning. They shouted, “Baal, answer us!” But no one answered. There was no reply at all [DOU]. Then they danced wildly around the altar that they had made.
27 Ilipofika adhuhuri Eliya akawakejeli akisema, “Mwiteni kwa nguvu! Huyo ni mungu! labda anawaza kitu, au amepumzika, au yuko safarini, au pengine amelala sharti aamshwe.”
About noontime, Elijah started to make fun of them. He said, “[Surely] Baal is a god, so it seems that you must shout louder! Perhaps he is thinking about something, or perhaps he has gone to the toilet. Or perhaps he is traveling somewhere, or perhaps he is asleep and you need to wake him up!”
28 Kwa hiyo wakamwita kwa nguvu, wakajikatakata kama kawaida yao ilivyokuwa, kwa upanga na nyembe, mpaka damu ikawachuruzika.
So they shouted louder. Then, doing one of the things that they frequently did [when they worshiped Baal], they slashed/cut themselves with knives and swords until a lot of blood flowed.
29 Ikawa wakati wa adhuhuri ulipopita, na bado walikuwa wakiendelea kutabiri mpaka wakati wa jioni wa kutoa dhabihu, lakini hapakuwepo na sauti wala mtu wa kuwajibu; wala hapakuwepo na yeyote wa kujibu wala wa kuangalia.
They continued calling out to Baal all afternoon. But there was no reply, no answer, no god who paid attention.
30 Kisha Eliya akawaambia watu wote, “Nisogeleeni,” na watu wote wakamsogelea. Naye akatengeneza ile madhabahu ya BWANA ambayo ilikuwa imeharibika.
Then Elijah called to the people saying, “Come closer!” So they all crowded around him. Then Elijah repaired the altar of Yahweh that had previously been (ruined/torn down) [by the prophets of Baal].
31 Eliya akachukua mawe kumi na mawili, kila jiwe moja liliwakilisha kabila moja la wana wa Yakobo - ni kupitia Yakobo kwamba neno la BWANA lilikuja, likisema, “Jina lako litakuwa Israel.”
Then he took twelve [large] stones, each one to represent one of the Israeli tribes. The names of those tribes were given to them by their ancestor Jacob.
32 Kwa kutumia hayo mawe aliijenga ile madhabahu kwa jina la BWANA na akachimba mfereji kuizunguka ile madhabahu kubwa kiasi cha kubeba lita kumi na tano za maji.
With these stones he rebuilt Yahweh’s altar. Then around the altar he dug a little ditch that was large enough to hold about (three gallons/12 liters) of water.
33 Kisha akaweka kuni kwa ajili ya moto na akamkatakata yule ng'ombe katika vipande vipande na akaweka vile vipande juu ya kuni. Na akasema, “Vijazeni maji hivyo vyombo na yamwageni kwenye hiyo sadaka ya kueketezwa na juu ya hizo kuni.”
He piled wood on top of the stones. He killed the bull and cut it in pieces. Then he laid the pieces on top of the wood. Then he said, “Fill four large jars with water, and pour the water on top of the pieces of meat and the wood.” So they did that.
34 Akasema tena fanyeni hivyo mara ya pili,” nao wakafanya kwa mara ya pili. kisha akasema, “Fanyeni mara ya tatu,” nao wakafanya kwa mara ya tatu.
Then he said, “Do the same thing again!” So they did it again. Then he said “Do it a third time!” So they did it again.
35 Maji yakaizunguka ile madhabahu na kuujaza ule mfereji.
As a result, the water flowed down below the altar and filled the ditches.
36 Ikawa wakati wa kutoa dhabihu ya jioni, nabii Eliya akasogea na akasema, “BWANA, Mungu wa Abrahamu, na wa Isaka, na wa Israeli, na ijulikane leo kwamba wewe ndiye Mungu wa Israeli, na kwamba mimi ni mtumishi wako, na kwamba nimeyafanya mambo haya yote kwa jina lako.
When it was time to offer the evening sacrifices, Elijah walked close [to the altar] and prayed. He said, “Yahweh, you who are the God that [our ancestors] Abraham and Isaac and Jacob [worshiped], prove today that you are the God whom the Israeli people [should worship], and prove that I am your servant. Prove that I have done all these things because you told me to do them.
37 Nisikie, BWANA, nisike, ili hawa watu wajue kuwa wewe, BWANA, ndiye Mungu, na kwamba umeirudisha mioyo yao kwako tena.”
Yahweh, answer me! Answer me in order that these people will know that you, Yahweh God, [have the power to do what you say that you will do], and that you have caused them to trust in [IDM] you again!”
38 Ndipo moto wa BWANA ukashuka ukairamba ile sadaka, pamoja na zile kuni, mawe na mavumbi, na kuyaramba yale maji yaliyokuwa kwenye ule mfereji.
Immediately a fire from Yahweh flashed down from the sky. The fire burned up the pieces of meat, the wood, the stones, and the dirt [that was around the altar]. It even dried up all the water in the ditch!
39 watu wote walipoona haya, wakalala kifudifudi chini wakasema, “BWANA, ndiye Mungu! BWANA ndiye Mungu!
When the people saw that, they prostrated themselves on the ground and shouted, “Yahweh is God! Yahweh is God!”
40 Kwa hiyo Eliya akawaambia, “Wakamateni manabii wa Baali. Msimwache hata mmoja wao atoroke.” Kwa hiyo wakawakamata, na Eliya akawaleta manabii wa Baali chini kwenye kijito cha Kishoni na akawaua huko.
Then Elijah commanded them, “Seize all the prophets of Baal! Do not allow any of them to escape!” So the people seized all the prophets of Baal, and took them down the mountain to the Kishon Valley, and Elijah killed them all there.
41 Eliya akamwambia Ahabu, “Inuka, ule na kunywa, kwa kuwa kuna sauti ya mvua kubwa.”
Then Elijah said to Ahab, “Go and get something to eat and drink. [But do it quickly, because] it is soon going to rain very hard!”
42 Kwa hiyo Ahabu akaenda akala na knywa. Kisha Eliya akaenda juu ya mlima Kameli, akasudu chini na akaweka uso wake katikati ya magoti.
So Ahab [and his men] left to prepare a big meal. But Elijah went back up to the top of Carmel Mountain and prayed.
43 Akamwambia mtumishi wake, “Nenda sasa, utazame upande wa bahari.” mtumishi wake akaenda na akasema, “Hakuna kitu,” Eliya akamwambia, “Nenda tena, mpaka mara saba.”
Then he said to his servant, “Go and look out toward the sea, [to see if there are any rain clouds.]” So his servant went and looked, [and came back] and said, “I do not see anything.” This happened six times.
44 Ile mara ya saba mtumishi wake akasema, “Tazama, kuna wingu linapanda kutoka baharini, ni dogo kama mkono wa mtu.” Eliya akamjibu, Nenda ukamwambie Ahabu, 'Andaa gari lako na ushuke kabla mvua haijakuzuia.'”
But when the servant went the seventh time, he came back and said, “I saw a very small cloud above the sea. [As I extend my arm, ] the cloud is about the size of my hand/fist.” Then Elijah shouted to him, “Go and tell King Ahab to get his chariot ready and go home immediately! If he does not do that, the rain will stop him!”
45 Ikatokea baada ya muda mfupi mbingu zikawa nyeusi kwa mawingu na upepo, na kulikuwa na mvua kubwa. Ahabu akapanda gari akaenda zake Yezreeli,
Very soon the sky was full of black clouds. There was a strong wind, and then it began to rain very hard. Ahab got into his chariot and started to return to Jezreel [city].
46 lakini mkono wa BWANA ulikuwa juu ya Eliya. Akalikaza vazi lake kwa mshipi wake na akakimbia mbele ya Ahabu kwenye lango la Yezreeli.
Yahweh gave extra strength to Elijah. He tucked his cloak into his belt [in order to run fast], and he ran ahead of Ahab’s [chariot] all the way [17 miles/26 km.] to Jezreel.

< 1 Wafalme 18 >