< 1 Wafalme 14 >
1 Wakati huo Abiya mwana wa Yeroboamu akawa mgonjwa sana.
At that time Abiyah the son of Jerobo'am fell sick.
2 Yeroboamu akamwambia mke wake, “amka ujibadilishe, ili wasikutambue kuwa wewe ndiye mke wangu, na uende Shilo, kwa sababu nabii Ahiya yuko huko, yeye ndiye aliyeninea mimi kuwa nitakuwa mfalme juu ya watu hawa.
And Jerobo'am said to his wife, Arise, I pray thee, and disguise thyself, that people may not know that thou art the wife of Jerobo'am; and go to Shiloh: behold, there is Achiyahu the prophet, who spoke of me that [I should become] king over this people.
3 Uchukue mikate kumi, na kaki na mtungi wa asali, na uende kwa Ahiya. Naye atakuambia kitakachotokea kwa mtoto.”
And take with thee ten loaves of bread and spice-cakes, and a cruise of honey, and go to him: he will tell thee what is to become of the lad.
4 Mke wa Yeroboamu akafanya hivyo; akaenda Shilo mpaka kwenye nyumba ya Ahiya. Wakati huo Ahiya alikuwa hawezi kuona, kwa kuwa macho yake yalikuwa yameishiwa nguvu kwa sababu ya umri wake.
And Jerobo'am's wife did so, and arose, and went to Shiloh, and came to the house of Achiyahu. But Achiyahu was not able to see; for his eyes were set by reason of his high age.
5 BWANA akamwambia Ahiya, “Tazama mke wa Ahiya anakuja kutafuta kutaka ushauri toka kwako kuhusiana na mwanae, kwa kuwa ni mgonjwa. Mwambie hivi na hivi, kwa sababu atakapofika atajifanya kuwa ni mwanamke mwingine.”
And the Lord had said unto Achiyahu, Behold the wife of Jerobo'am is coming to inquire a word of thee about her son; for he is sick: thus and thus shalt thou speak unto her; for it will be, when she cometh in, that she will feign to be another.
6 Naye Ahiya aliposikia sauti za miguu yake alipokuwa akiukaribia mlango, akasema, “karibu, mke wa Yeroboamu. Kwa nini unajifanya kuwa mtu mwingine? Nimetumwa kwako nikiwa na habaari mbaya.
And it happened, when Achiyahu heard the sound of her feet, as she came in at the door, that he said, Come in, thou wife of Jerobo'am; why is this, that thou feignest to be another? but I am sent to thee with a hard message.
7 Nenda ukamwambia Yeroboamu kwamba BWANA, Mungu wa Israeli, anasema, 'Nilikuinua kutoka kati ya watu na kukufanya uwe kiongozi wa watu wangu Israeli.
Go, say to Jerobo'am, Thus hath said the Lord the God of Israel, Forasmuch as I exalted thee from the midst of the people, and made thee prince over my people Israel,
8 Niliugawa ufalme kutoka kwa Daudi na kukupa wewe, lakini bado hutaki kuwa kama mtumishi wangu Daudi, ambaye alizishika amri zangu na kunifuata kwa moyo wake wote, na kufanya kilichokuwa sawa mbele ya macho yangu.
And I rent the kingdom away from the house of David, and gave it unto thee; whereas thou hast not been like my servant David, who kept my commandments, and who followed after me with all his heart, to do only what is right in my eyes;
9 Badala yake, umefanya maovu, zaidi ya wote waliokutangulia. Umetengeneza miungu mingine, na umetengeneza sanamu za kuyeyushwa ili kunikasirisha na kunitupa nyuma yako.
And thou hast done more evil than all that were before thee; and thou art gone and hast made unto thyself other gods, and molten images, to provoke me to anger, and me hast thou cast behind thy back:
10 Kwa hiyo, tazama, Nitaleta majanga kwenye familia yako; Nitawatupilia mbali watoto wako wote wa kiume katika Israeli, kama ni mtumwa au ni huru, na nitaiondoa familia yako, kama mtu anayechoma mavi mpaka yaishe.
Therefore, behold, will I bring evil upon the house of Jerobo'am, and will cut off from Jerobo'am every male, [also] the guarded and fortified in Israel; and I will sweep out after the house of Jerobo'am as one sweepeth away the dung till there be nothing left of it.
11 Yeyote ambaye ni mwanafamilia yako atakayefia mjini ataliwa na mbwa, na yeyote atakayefia shamabani ataliwa na ndege wa angani, kwa kuwa Mimi BWANA, nimesema;
Him that dieth of Jerobo'am in the city shall the dogs eat; and him that dieth in the field shall the fowls of the heavens eat; for the Lord hath spoken it.
12 Kwa hiyo inuka wewe mke wa Yeroboamu, na uende nyumbani kwako; na mguu wako utakapokanyaga mjini, yule mtoto wa Abiya atakufa.
But thou, arise now, go to thy own house: when thy feet enter into the city, the child shall die.
13 Na Israeli yote itamwombolezea na kumzika. Ni yeye pekee katika familia ya Abiya atakayepelekwa makaburini, kwa sababu ni yeye pekee yake kutoka kwenye nyumba ya Abiya, ambaye BWANA, Mungu wa Israeli alimwona kuwa ni mwema.
And all Israel shall mourn for him, and bury him; for this one alone shall come of Jerobo'am's [family] to the grave; because there hath been found in him some good thing toward the Lord the God of Israel in the house of Jerobo'am.
14 Pia BWANA atainua mfalme katika Israeli ambaye ataifutilia mbali familia ya Yeroboamu katika siku hiyo. Leo ndiyo siku hiyo, sasa hivi.
And the Lord will raise up unto himself a king over Israel, who shall cut off the house of Jerobo'am what is here this day, and what will be after this.
15 Kwa kuwa BWANA ataishambulia Israeli kama vile majani yanavyotikiswa majini, na ataing'oa Israeli katika nchi hii njema ambayo aliwpa mababu. Atawatawanya hata ng'ambo ya Mto Frati, kwa sababu wamefanya nguzo za Ashera kumkasirisha BWANA.
And the Lord will smite Israel, as the reed is shaken in the water, and he will pull up Israel out of this good land, which he gave to their fathers, and will scatter them on the other side of the river; because they have made their groves, provoking the Lord to anger.
16 Ataiacha Israeli kwa sababu ya dhambi ya Yeroboamu, dhambi ambazo ametenda, na kwa hizo ameifanya Israeli kufanya dhambi.
And he will give Israel up for the sake of the sins of Jerobo'am, who did sin, and who induced Israel to sin.
17 Kwa hiyo mke wa Yeroboamu akainuka na akaondoka na akaenda mpaka Tirza. Naye alipofika kizingitini kwa nyumba yake, yule mtoto akafa.
And Jerobo'am's wife arose, and departed, and came to Thirzah; [and] as she came to the threshold of the door, the lad died:
18 Isareli wote wakamzika na kumwombolezea, kama vile alivyokuwa ameambiwa kwa neno la BWANA ambalo amelisema kupitia mtumishi wake nabii Ahiya.
And they buried him; and all Israel mourned for him, according to the word of the Lord, which he had spoken by the hand of his servant Achiyahu the prophet.
19 Na kwa mambo mengine yanayOmhusu Yeroboamu, jinsi alivyopigana vita na jinsi alivyotawala, tazama yameandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli.
And the rest of the acts of Jerobo'am, how he warred, and how he reigned, behold, they are written in the book of the chronicles of the kings of Israel.
20 Yeroboamu alitawala kwa miaka ishirini na mbili naye akalala na babu zake, na Nadabu mwanawe akawa mfalme mahali pake.
And the days which Jerobo'am reigned were two and twenty years; and he slept with his fathers, and Nadab his son became king in his stead.
21 Sasa Rehoboamu mwana wa Sulemani alikuwa mtawala wa Yuda. Rehoboamu alikuwa na umri wa miaka arobaini na moja alipokuwa mfalme, na akatawala kwa miaka kumi na saba kule Yerusalemu, mji ambao BWANA alikuwa ameuchagua kati ya makabila yote ya Israeli ili aweke jina lake kule. Jina la mama yake alikuwa Naama Mwamori.
And Rehobo'am the son of Solomon reigned in Judah. Rehobo'am was forty and one years old when he became king, and seventeen years did he reign in Jerusalem, the city which the Lord had chosen out of all the tribes of Israel, to put his name there. And his mother's name was Na'amah the 'Ammonitess.
22 Yuda ikafanya yaliyo maovu mbele ya macho ya BWANA; wakamtia wivu kwa makosa yao, zaidi ya yote ambayo baba zao walikuwa wamefanya
And Judah did what is evil in the eyes of the Lord, and they moved him to wrath more than all that their fathers had done, with their sins which they committed.
23 Kwa kuwa walijijengea wenyewe mahali pa juu, nguzo za mawe, na nguzo za Ashera katika kila mahali pa juu na katika kila mti wenye majani mabichi.
And they also built themselves high-places, and standing images, and groves, on every high hill, and under every green tree.
24 Pia kulikuwepo na ukahaba wa kipagani katika nchi. Walifanya machukizo yaleyale kama wa mataifa yale ambayo BWANA alikuwa amewafukuza kutoka kwa watu wa Israeli.
And sodomites also were in the land: they acted in accordance with all the abominable deeds of the nations which the Lord had driven out before the children of Israel.
25 Ilitokea wakati wa mwaka wa tano wa mfalme Rehoboamu wakati Shishaki akiwa mfalme wa Misri, akaja kinyume na Yerusalemu.
And it came to pass in the fifth year of king Rehobo'am, that Shishak the king of Egypt came up against Jerusalem:
26 Akaichukua hazina iliyokuwa kwenye nyumba ya BWANA, na ile hazina iliyokuwa kwenye nyumba ya Mfalme. Akachukua kila kitu; Pia alizichukua zile ngao za dhahabu ambazo Sulemani alikuwa ametengeneza.
And he took away the treasures of the house of the Lord, and the treasures of the king's house; yea, every thing did he take away; and he took away all the shields of gold which Solomon had made.
27 Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba mahali pake na akazikabidhi kwa wakuu wa walinzi, ambao walilinda malango ya kuingia kwa mfalme.
And king Rehobo'am made in their stead shields of copper, and committed them for keeping into the hand of the chiefs of the runners, who kept guard at the door of the king's house.
28 Na ikawa kila mfalme alipoingia kwenye nyumba ya BWANA, wale walinzi walizibeba na baadaye walizirudisha katika chumba cha walinzi.
And it happened whenever the king went into the house of the Lord, that the runners used to bear them, and carried them then back into the apartment of the runners.
29 Lakini katika mambo mengine kuhusiana na Rehoboamu, na yote yale aliyofanya, je, hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
And the rest of the acts of Rehobo'am, and all that he did, behold, they are written in the book of the chronicles of the kings of Judah.
30 Kulikuwa na mapigano yasiyokoma kati ya nyumba ya Rehoboamu na nyumba ya Yeroboamu.
And there was war between Rehobo'am and Jerobo'am all the days.
31 Kwa hiyo Rehoboamu akalala na mababu zake naye akazikwa pamoja nao katika mji wa Daudi Jina la mama yake alikuwa Naama Mwamori. Abiya mwanawe akawa mfalme mahali pake
And Rehobo'am slept with his fathers, and was buried with his fathers in the city of David. And his mother's name was Na'amah the 'Ammonitess. And Abiyam his son became king in his stead.