< 1 Wafalme 14 >
1 Wakati huo Abiya mwana wa Yeroboamu akawa mgonjwa sana.
In that time Abijah, the son of Jeroboam, became ill.
2 Yeroboamu akamwambia mke wake, “amka ujibadilishe, ili wasikutambue kuwa wewe ndiye mke wangu, na uende Shilo, kwa sababu nabii Ahiya yuko huko, yeye ndiye aliyeninea mimi kuwa nitakuwa mfalme juu ya watu hawa.
And Jeroboam said to his wife: “Rise up, and change clothing, so that you will not be recognized to be the wife of Jeroboam. And go to Shiloh, where the prophet Ahijah is, who said to me that I should reign over this people.
3 Uchukue mikate kumi, na kaki na mtungi wa asali, na uende kwa Ahiya. Naye atakuambia kitakachotokea kwa mtoto.”
Also, take in your hand ten loaves, and dried bread, and a container of honey, and go to him. For he will reveal to you what will happen to this boy.”
4 Mke wa Yeroboamu akafanya hivyo; akaenda Shilo mpaka kwenye nyumba ya Ahiya. Wakati huo Ahiya alikuwa hawezi kuona, kwa kuwa macho yake yalikuwa yameishiwa nguvu kwa sababu ya umri wake.
The wife of Jeroboam did just as he had said. And rising up, she went away to Shiloh. And she arrived at the house of Ahijah. But he was unable to see, because his eyes had dimmed due to old age.
5 BWANA akamwambia Ahiya, “Tazama mke wa Ahiya anakuja kutafuta kutaka ushauri toka kwako kuhusiana na mwanae, kwa kuwa ni mgonjwa. Mwambie hivi na hivi, kwa sababu atakapofika atajifanya kuwa ni mwanamke mwingine.”
Then the Lord said to Ahijah: “Behold, the wife of Jeroboam enters, so that she may consult you over her son, who is ill. You shall say one thing and another to her.” Therefore, as she was entering, not presenting herself to be who she was,
6 Naye Ahiya aliposikia sauti za miguu yake alipokuwa akiukaribia mlango, akasema, “karibu, mke wa Yeroboamu. Kwa nini unajifanya kuwa mtu mwingine? Nimetumwa kwako nikiwa na habaari mbaya.
Ahijah heard the sound of her feet, entering through the door. And he said: “Enter, O wife of Jeroboam. Why do you pretend to be someone you are not? But I have been sent to you with harsh news.
7 Nenda ukamwambia Yeroboamu kwamba BWANA, Mungu wa Israeli, anasema, 'Nilikuinua kutoka kati ya watu na kukufanya uwe kiongozi wa watu wangu Israeli.
Go, and tell Jeroboam: ‘Thus says the Lord, the God of Israel: Although I exalted you from the midst of the people, and I granted to you to be the leader over my people Israel,
8 Niliugawa ufalme kutoka kwa Daudi na kukupa wewe, lakini bado hutaki kuwa kama mtumishi wangu Daudi, ambaye alizishika amri zangu na kunifuata kwa moyo wake wote, na kufanya kilichokuwa sawa mbele ya macho yangu.
and I tore the kingdom away from the house of David, and I gave it to you, yet you have not been like David, my servant, who kept my commandments, and who followed me with his whole heart, doing what was pleasing in my sight.
9 Badala yake, umefanya maovu, zaidi ya wote waliokutangulia. Umetengeneza miungu mingine, na umetengeneza sanamu za kuyeyushwa ili kunikasirisha na kunitupa nyuma yako.
Instead, you have worked evil beyond all those who were before you. And you have made for yourself strange gods and molten images, so that you provoke me to anger. And you have cast me behind your back.
10 Kwa hiyo, tazama, Nitaleta majanga kwenye familia yako; Nitawatupilia mbali watoto wako wote wa kiume katika Israeli, kama ni mtumwa au ni huru, na nitaiondoa familia yako, kama mtu anayechoma mavi mpaka yaishe.
For this reason, behold, I will lead evils over the house of Jeroboam, and I will strike down from Jeroboam that which urinates against a wall, and that which is lame, and that which is last in Israel. And I will cleanse that which remains of the house of Jeroboam, just as dung is usually cleaned away, until there is purity.
11 Yeyote ambaye ni mwanafamilia yako atakayefia mjini ataliwa na mbwa, na yeyote atakayefia shamabani ataliwa na ndege wa angani, kwa kuwa Mimi BWANA, nimesema;
Those who will have died of Jeroboam in the city, the dogs will devour them. And those who will have died in the field, the birds of the heavens will devour them. For the Lord has spoken.’
12 Kwa hiyo inuka wewe mke wa Yeroboamu, na uende nyumbani kwako; na mguu wako utakapokanyaga mjini, yule mtoto wa Abiya atakufa.
Therefore, you must rise up, and go to your house. And in the city, at the very entrance of your feet, the boy will die.
13 Na Israeli yote itamwombolezea na kumzika. Ni yeye pekee katika familia ya Abiya atakayepelekwa makaburini, kwa sababu ni yeye pekee yake kutoka kwenye nyumba ya Abiya, ambaye BWANA, Mungu wa Israeli alimwona kuwa ni mwema.
And all of Israel will mourn him, and will bury him. For he alone of Jeroboam shall be brought into a sepulcher. For concerning him, there has been found a good word from the Lord, the God of Israel, in the house of Jeroboam.
14 Pia BWANA atainua mfalme katika Israeli ambaye ataifutilia mbali familia ya Yeroboamu katika siku hiyo. Leo ndiyo siku hiyo, sasa hivi.
But the Lord has appointed for himself a king over Israel, who will strike down the house of Jeroboam, in this day and in this time.
15 Kwa kuwa BWANA ataishambulia Israeli kama vile majani yanavyotikiswa majini, na ataing'oa Israeli katika nchi hii njema ambayo aliwpa mababu. Atawatawanya hata ng'ambo ya Mto Frati, kwa sababu wamefanya nguzo za Ashera kumkasirisha BWANA.
And the Lord God shall strike Israel, just as a reed is usually shaken in the water. And he will uproot Israel from this good land, which he gave to their fathers. And he will winnow them beyond the river. For they have made for themselves sacred groves, so that they have provoked the Lord.
16 Ataiacha Israeli kwa sababu ya dhambi ya Yeroboamu, dhambi ambazo ametenda, na kwa hizo ameifanya Israeli kufanya dhambi.
And the Lord will hand over Israel, because of the sins of Jeroboam, who has sinned and caused Israel to sin.”
17 Kwa hiyo mke wa Yeroboamu akainuka na akaondoka na akaenda mpaka Tirza. Naye alipofika kizingitini kwa nyumba yake, yule mtoto akafa.
And so, the wife of Jeroboam rose up, and she went away. And she arrived at Tirzah. And as she was entering the threshold of the house, the boy died.
18 Isareli wote wakamzika na kumwombolezea, kama vile alivyokuwa ameambiwa kwa neno la BWANA ambalo amelisema kupitia mtumishi wake nabii Ahiya.
And they buried him, and all of Israel mourned for him, in accord with the word of the Lord, which he spoke by the hand of his servant Ahijah, the prophet.
19 Na kwa mambo mengine yanayOmhusu Yeroboamu, jinsi alivyopigana vita na jinsi alivyotawala, tazama yameandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli.
Now the rest of the words of Jeroboam, the manner in which he fought, and the manner in which he reigned, behold, these were written in the book of the words of the days of the kings of Israel.
20 Yeroboamu alitawala kwa miaka ishirini na mbili naye akalala na babu zake, na Nadabu mwanawe akawa mfalme mahali pake.
And the days during which Jeroboam reigned were twenty-two years. And he slept with his fathers. And Nadab, his son, reigned in his place.
21 Sasa Rehoboamu mwana wa Sulemani alikuwa mtawala wa Yuda. Rehoboamu alikuwa na umri wa miaka arobaini na moja alipokuwa mfalme, na akatawala kwa miaka kumi na saba kule Yerusalemu, mji ambao BWANA alikuwa ameuchagua kati ya makabila yote ya Israeli ili aweke jina lake kule. Jina la mama yake alikuwa Naama Mwamori.
Now Rehoboam, the son of Solomon, reigned in Judah. Rehoboam was forty-one years old when he had begun to reign. And he reigned for seventeen years in Jerusalem, the city that the Lord chose, out of all the tribes of Israel, so that he might place his name there. And the name of his mother was Naamah, an Ammonite.
22 Yuda ikafanya yaliyo maovu mbele ya macho ya BWANA; wakamtia wivu kwa makosa yao, zaidi ya yote ambayo baba zao walikuwa wamefanya
And Judah did evil in the sight of the Lord, and they provoked him beyond all that their fathers had done, by their sins that they committed.
23 Kwa kuwa walijijengea wenyewe mahali pa juu, nguzo za mawe, na nguzo za Ashera katika kila mahali pa juu na katika kila mti wenye majani mabichi.
For they, too, built for themselves altars, and statues, and sacred groves, upon every high hill and under every leafy tree.
24 Pia kulikuwepo na ukahaba wa kipagani katika nchi. Walifanya machukizo yaleyale kama wa mataifa yale ambayo BWANA alikuwa amewafukuza kutoka kwa watu wa Israeli.
Moreover, the effeminate were in the land, and they committed all the abominations of the peoples that the Lord had destroyed before the face of the sons of Israel.
25 Ilitokea wakati wa mwaka wa tano wa mfalme Rehoboamu wakati Shishaki akiwa mfalme wa Misri, akaja kinyume na Yerusalemu.
Then, in the fifth year of the reign of Rehoboam, Shishak, the king of Egypt, ascended against Jerusalem.
26 Akaichukua hazina iliyokuwa kwenye nyumba ya BWANA, na ile hazina iliyokuwa kwenye nyumba ya Mfalme. Akachukua kila kitu; Pia alizichukua zile ngao za dhahabu ambazo Sulemani alikuwa ametengeneza.
And he took away the treasures of the house of the Lord, and the royal treasures, and he plundered everything, including the shields of gold that Solomon had made.
27 Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba mahali pake na akazikabidhi kwa wakuu wa walinzi, ambao walilinda malango ya kuingia kwa mfalme.
In place of these, king Rehoboam made shields of brass, and he delivered them into the hand of the commanders of the shield bearers, and of those who were keeping the night watch before the gate of the king’s house.
28 Na ikawa kila mfalme alipoingia kwenye nyumba ya BWANA, wale walinzi walizibeba na baadaye walizirudisha katika chumba cha walinzi.
And when the king entered into the house of the Lord, these were carried by those who held the office to go before him. And afterward, they carried them back to the armory of the shield bearers.
29 Lakini katika mambo mengine kuhusiana na Rehoboamu, na yote yale aliyofanya, je, hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
Now the rest of the words of Rehoboam, and all that he did, behold, these were written in the book of the words of the days of the kings of Judah.
30 Kulikuwa na mapigano yasiyokoma kati ya nyumba ya Rehoboamu na nyumba ya Yeroboamu.
And there was war between Rehoboam and Jeroboam, during all the days.
31 Kwa hiyo Rehoboamu akalala na mababu zake naye akazikwa pamoja nao katika mji wa Daudi Jina la mama yake alikuwa Naama Mwamori. Abiya mwanawe akawa mfalme mahali pake
And Rehoboam slept with his fathers, and he was buried with them in the city of David. And his mother’s name was Naamah, an Ammonite. And his son Abijam reigned in his place.