< 1 Wafalme 13 >

1 Mtu wa Mungu alikuja tokea Yuda kwa neno la BWANA kule Betheli. Naye Yeroboamu alikuwa amesimama karibu na madhabahu ili kufukiza uvumba.
و اینک مرد خدایی به فرمان خداوند ازیهودا به بیت ئیل آمد و یربعام به جهت سوزانیدن بخور نزد مذبح ایستاده بود.۱
2 Akalia kinyume na zile madhabahu kwa neno la BWANA: “Ee madhabahu, madhabahu” hivi ndivyo asemavyo BWANA, 'Tazama, mwana aitwaye Yosia atazaliwa katika familia ya Daudi, na juu yenu atawachinja makuhani ambao sasa wanafukiza uvumba mahali hapa pa juu kwa ajili yako. Juu yako watachoma mifupa ya watu.'”
پس به فرمان خداوند مذبح را ندا کرده، گفت: «ای مذبح! ای مذبح! خداوند چنین می‌گوید: اینک پسری که یوشیا نام دارد به جهت خاندان داود زاییده می‌شود و کاهنان مکانهای بلند را که بر تو بخورمی سوزانند، بر تو ذبح خواهد نمود واستخوانهای مردم را بر تو خواهند سوزانید.»۲
3 Kisha mtu wa Mungu akatoa ishara siku hiyohiyo, akisema, “Hii ndiyo isharaya kwamba BWANA amesema: 'Tazama, madhabahu zitavuunjika, na majivu yaliyo juu yatamwagika.”
ودر آن روز علامتی نشان داده، گفت: «این است علامتی که خداوند فرموده است، اینک این مذبح چاک خواهد شد و خاکستری که بر آن است، ریخته خواهد گشت.»۳
4 Naye mfalme aliposikia kile mtu wa Mungu alichosema, kwamba amelia kinyume cha zile madhabahu kule Betheli, Yeroboamu akanyosha mkono wake kutoka madhabahuni, akisema, “mkamateni.” Ndipo ule mkono aliokuwa ameunyosha dhidi ya mtu wa Mungu ukakauka, kiasi kwamba hakuweza kuurudisha mwenyewe.
و واقع شد که چون پادشاه، سخن مرد خدا را که مذبح را که دربیت ئیل بود، ندا کرده بود، شنید، یربعام دست خود را از جانب مذبح دراز کرده، گفت: «او را بگیرید.» و دستش که به سوی او دراز کرده بود، خشک شد به طوری که نتوانست آن را نزد خودباز بکشد.۴
5 Na ile madhabahu ikavunjika vipande vipande, na yale majivu yakamwagika kutoka madhabahuni, kama ilivyokuwa imefafanuliwa kuwa ndiyo ishara ya kwamba mtu wa Mungu alikuwa amepewa kwa neno la BWANA.
و مذبح چاک شد و خاکستر از روی مذبح ریخته گشت بر‌حسب علامتی که آن مردخدا به فرمان خداوند نشان داده بود.۵
6 Mfalme Yeroboamu akajibu akimwambia mtu wa Mungu, “Msihi BWANA, Mungu wako akupe neema ili uniombee, ili kwamba mkono wangu urejee kwangu tena.” Kwa hiyo mtu wa Mungu akamwomba BWANA, na mkono wa mfalme ukarejea katika hali yake tena, na ukawa kama ulivyokuwa mwanzoni.
و پادشاه، مرد خدا را خطاب کرده، گفت: «تمنا اینکه نزدیهوه، خدای خود تضرع نمایی و برای من دعاکنی تا دست من به من باز داده شود.» پس مرد خدانزد خداوند تضرع نمود، و دست پادشاه به او بازداده شده، مثل اول گردید.۶
7 Yule mfalme akamwambia mtu wa Mungu, “twende nyumbani kwangu upate chakula, nami nitakupa zawadi.”
و پادشاه به آن مردخدا گفت: «همراه من به خانه بیا و استراحت نما وتو را اجرت خواهم داد.»۷
8 Yule mtu wa Mungu akamwambia mfalme, “Hata kama utanipa nusu ya miliki yako. staende na wewe, wala sitakula au kunywa maji mahali hapa,
اما مرد خدا به پادشاه گفت: «اگر نصف خانه خود را به من بدهی، همراه تو نمی آیم، و در اینجا نه نان می‌خورم و نه آب می‌نوشم.۸
9 kwa sababu BWANA ameniamuru kwa neno lake, 'hutakula mkate wala kunywa maji, wala kurudi kwa njia ulioijia.'”
زیرا خداوند مرا به کلام خود چنین امر فرموده و گفته است نان مخور و آب منوش وبه راهی که آمده‌ای بر مگرد.»۹
10 Kwa hiyo mtu wa Mungu akaondoka na hakurudi nyumbani kwa njia aliyokuja nayo huko Betheli.
پس به راه دیگربرفت و از راهی که به بیت ئیل آمده بود، مراجعت ننمود.۱۰
11 Sasa kulikuwa na nabii mwingine mzee aliyekuwa akiishi Betheli, na mmoja wa wana wake akaja kumwambia mambo yote ambayo mtu wa Mungu amefanya siku hiyo kule Betheli. Wana wake wakamwambia pia maneno ambayo Yule mtu wa Mungu alimwambia mfalme.
و نبی سالخورده‌ای در بیت ئیل ساکن می‌بود و پسرانش آمده، او را از هر کاری که آن مرد خدا آن روز در بیت ئیل کرده بود، مخبرساختند، و نیز سخنانی را که به پادشاه گفته بود، برای پدر خود بیان کردند.۱۱
12 Baba yao akawaambia, “Alienda kwa njia gani?” Wale wanawe walikuwa wamemwona yule mtu wa Mungu kutoka Yuda njia aliyotumia kurudi.
و پدر ایشان به ایشان گفت: «به کدام راه رفته است؟» و پسرانش دیده بودند که آن مرد خدا که از یهودا آمده بود به کدام راه رفت.۱۲
13 Kwa hiyo akawaambia wanawe, “Nitandikeni punda.” Kwa hiyo wakamtandikia punda naye akampanda.
پس به پسران خود گفت: «الاغ را برای من بیارایید.» و الاغ را برایش آراستند و برآن سوار شد.۱۳
14 Yule nabii mzee akamfuata yule mtu wa Mungu na akamkuta amekaa chini ya mti wa mwaloni; akamwambia, “Je, wewe ndiye mtu wa Mungu aliyetoka Yuda?” Naye akamjibu, “Mimi ndiye.”
و از عقب مرد خدا رفته، او را زیردرخت بلوط نشسته یافت. پس او را گفت: «آیا توآن مرد خدا هستی که از یهودا آمده‌ای؟» گفت: «من هستم.»۱۴
15 Kisha yule nabii mzee akamwambia, “twende nyumbani kwangu ukale chakula.”
وی را گفت: «همراه من به خانه بیا و غذا بخور.»۱۵
16 Yule mtu wa Mungu akamjibu, “Siwezi kurudi na wewe wala kuingia ndani na wewe, tena sitakula chakula wala kunywa maji pamoja na wewe mahali hapa,
او در جواب گفت که «همراه تونمی توانم برگردم و با تو داخل شوم، و در اینجا باتو نه نان می‌خورم و نه آب می‌نوشم.۱۶
17 kwa sababu niliamuriwa hivyo kwa neno la BWANA, 'Hautakula chakula wala kunywa maji kule, wala kurudi kwa njia utakayokuja nayo.'”
زیرا که به فرمان خداوند به من گفته شده است که در آنجانان مخور و آب منوش و از راهی که آمده‌ای مراجعت منما.»۱۷
18 Kwa hiyo yule nabii mzee akamwambia, “Mimi pia ni nabii kama ulivyo, na malaika amesema na mimi neno la BWANA, akisema, 'Mrudishe aje na wewe katika nyumba yako, ili aweze kula chakula na kunywa maji.'” Lakini alikuwa anamdanganya mtu wa Mungu.
او وی را گفت: «من نیز مثل تونبی هستم و فرشته‌ای به فرمان خداوند با من متکلم شده، گفت او را با خود به خانه ات برگردان تا نان بخورد و آب بنوشد.» اما وی را دروغ گفت.۱۸
19 Kwa hiyo yule mtu wa Mungu akarudi pamoja na yule nabii mzee na akala chakula nyumbani kwake na akanywa maji.
پس همراه وی در خانه‌اش برگشته، غذا خوردو آب نوشید.۱۹
20 Walipokuwa wamekaa mezani, neno la BWANA likamjia yule nabii aliyemrudisha,
و هنگامی که ایشان بر سفره نشسته بودند، کلام خداوند به آن نبی که او را برگردانیده بودآمد،۲۰
21 naye akalia kwa mtu wa Mungu aliyetoka Yuda, akisema “BWANA anasema, 'Kwa kuwa umeshindwa kutii nenola BWANA na umeshindwa kuishika amri ya BWANA ambayo Mungu wako alikupa,
و به آن مرد خدا که از یهودا آمده بود، نداکرده، گفت: «خداوند چنین می‌گوید: چونکه ازفرمان خداوند تمرد نموده، حکمی را که یهوه، خدایت به تو امر فرموده بود نگاه نداشتی،۲۱
22 bali umerudi na umekula chakula na kunywa maji mahali ambapo BWANA alikwambia usile chakula wala kunywa maji, basi mwili wako hautazikwa kwenye makaburi ya baba zako.'”
وبرگشته، در جایی که به تو گفته شده بود غذامخور و آب منوش، غذا خوردی و آب نوشیدی، لهذا جسد تو به قبر پدرانت داخل نخواهد شد.»۲۲
23 Baada ya kula chakula na kunywa maji, Yule nabii akatandika punda wa mtu wa Mungu, yule mtu aliyerudi naye.
پس بعد از اینکه او غذا خورد وآب نوشید الاغ را برایش بیاراست، یعنی به جهت نبی که برگردانیده بود.۲۳
24 Baada ya mtu wa Mungu kuondoka, akakutana na simba njiani na kumwua barabarani, na mwili wake uliachwa barabarani. Na yule punda akasimama pembeni yake, na yule simba naye akasimama pembeni ya ule mwili.
و چون رفت، شیری اورا در راه یافته، کشت و جسد او در راه انداخته شد، و الاغ به پهلویش ایستاده، و شیر نیز نزد لاش ایستاده بود.۲۴
25 Watu walipopita na kuuona ule mwili umeachwa barabarani, na yule simba akisimama karibu na ule mwili, walikuja wakaeleza habari hiyo mjini kule ambako yule nabii mzee aliishi.
و اینک بعضی راه گذران جسد رادر راه انداخته شده، و شیر را نزد جسد ایستاده دیدند، پس آمدند و در شهری که آن نبی پیر درآن ساکن می‌بود، خبر دادند.۲۵
26 Yule nabii aliyemrudisha toka njiani aliposikia, akasema, “Yeye mtu wa Muugu ndiye aliyeshindwa kutii neno la BWANA. Kwa hiyo BWANA alimtoa kwa simba, ambaye amemrarua katika vipande vipande na kumwua, kama vile neno la BWANA lilivyokuwa limemwonya.”
و چون نبی که او را از راه برگردانیده بودشنید، گفت: «این آن مرد خداست که از حکم خداوند تمرد نمود، لهذا خداوند او را به شیر داده که او را دریده و کشته است، موافق کلامی که خداوند به او گفته بود.۲۶
27 Kwa hiyo yule nabii mzee akawaamnbia wanawe, akisema, “Tandikeni punda wangu,” nao wakamtandikia.
پس پسران خود راخطاب کرده، گفت: «الاغ را برای من بیارایید.» وایشان آن را آراستند.۲۷
28 Akaenda akaukuta mwili umeachwa barabarani, punda na simba wamesimama pembeni ya ule mwili. Yule simba hakuula ule mwili, wala hakumshambulia yule punda.
و او روانه شده، جسد اورا در راه انداخته، و الاغ و شیر را نزد جسدایستاده یافت، و شیر جسد را نخورده و الاغ راندریده بود.۲۸
29 Yule nabii akauchukua ule mwili wa mtu wa Mungu, akaulaza juu ya punda, na akaurudisha. Akaja kwenye mji wake kuomboleza na kuuzika.
و آن نبی جسد مرد خدا رابرداشت و بر الاغ گذارده، آن را بازآورد و آن نبی پیر به شهر آمد تا ماتم گیرد و او را دفن نماید.۲۹
30 Akaulaza mwili kwenye kaburi lake, nao wakamwombolezea, wakisema, “Aa! ndugu yangu!”
وجسد او را در قبر خویش گذارد و برای او ماتم گرفته، گفتند: «وای‌ای برادر من!»۳۰
31 Kisha baada ya kumzika, yule nabii mzee akawaambia wanawe, akasema, “Nitakapokufa, mtanizika kwenye kaburi ambalo tumemzika mtu wa Mungu. Mtalaza mifupa yangu pembeni mwa mifupa yake.
و بعد ازآنکه او را دفن کرد به پسران خود خطاب کرده، گفت: «چون من بمیرم مرا در قبری که مرد خدا درآن مدفون است، دفن کنید، و استخوانهایم را به پهلوی استخوانهای وی بگذارید.۳۱
32 Kwa kuwa ule ujumbe uliosemwa na BWANA, dhidi ya madhabahu kule Betheli na dhidi ya nyumba zote za mahali pa juu katika mji wa Samaria, hakika yatatokea.
زیرا کلامی را که درباره مذبحی که در بیت ئیل است و درباره همه خانه های مکانهای بلند که در شهرهای سامره می‌باشد، به فرمان خداوند گفته بود، البته واقع خواهد شد.۳۲
33 Baada ya haya Yeroboamu hakuuacha uovu wake, aliendelea kuchagua makuhani wa kawaida kwa ajili ya mahali pa juu kutoka kwa watu wa kila aina. Yeyote ambaye angeweza kutumika alimtakasa kuwa kuhani.
و بعد از این امر، یربعام از طریق ردی خودبازگشت ننمود، بلکه کاهنان برای مکانهای بلند ازجمیع قوم تعیین نمود، و هرکه می‌خواست، او راتخصیص می‌کرد تا از کاهنان مکانهای بلند بشود.۳۳
34 Jambo hili likawa dhambi kwenye familia ya Yeroboamu na kusababisha familia yake kuangamizwa na kuondolewa kabisa katika uso wa dunia.
و این کار باعث گناه خاندان یربعام گردید تا آن را از روی زمین منقطع و هلاک ساخت.۳۴

< 1 Wafalme 13 >