< 1 Wafalme 13 >

1 Mtu wa Mungu alikuja tokea Yuda kwa neno la BWANA kule Betheli. Naye Yeroboamu alikuwa amesimama karibu na madhabahu ili kufukiza uvumba.
Et voilà qu’un homme de Dieu vint avec les paroles du Seigneur, de Juda à Béthel, Jéroboam étant près de l’autel et jetant de l’encens.
2 Akalia kinyume na zile madhabahu kwa neno la BWANA: “Ee madhabahu, madhabahu” hivi ndivyo asemavyo BWANA, 'Tazama, mwana aitwaye Yosia atazaliwa katika familia ya Daudi, na juu yenu atawachinja makuhani ambao sasa wanafukiza uvumba mahali hapa pa juu kwa ajili yako. Juu yako watachoma mifupa ya watu.'”
Et il s’écria contre l’autel, avec les paroles du Seigneur, et il dit: Autel, autel, le Seigneur dit ceci: Voilà qu’un fils naîtra dans la maison de David, du nom de Josias, et il immolera sur toi les prêtres des hauts lieux, qui maintenant brûlent sur toi de l’encens, et il brûlera sur toi des os d’hommes.
3 Kisha mtu wa Mungu akatoa ishara siku hiyohiyo, akisema, “Hii ndiyo isharaya kwamba BWANA amesema: 'Tazama, madhabahu zitavuunjika, na majivu yaliyo juu yatamwagika.”
Et il donna en ce jour-là ce signe, disant: Ceci sera le signe que le Seigneur a parlé: Voilà que l’autel sera brisé, et que sera répandue la cendre qui est sur lui.
4 Naye mfalme aliposikia kile mtu wa Mungu alichosema, kwamba amelia kinyume cha zile madhabahu kule Betheli, Yeroboamu akanyosha mkono wake kutoka madhabahuni, akisema, “mkamateni.” Ndipo ule mkono aliokuwa ameunyosha dhidi ya mtu wa Mungu ukakauka, kiasi kwamba hakuweza kuurudisha mwenyewe.
Or lorsque le roi eut entendu la parole que l’homme de Dieu avait dite en criant contre l’autel à Béthel, il étendit sa main de dessus l’autel, disant: Saisissez-le. Et sa main qu’il avait étendue contre le prophète se sécha, et il ne put pas la retirer à lui.
5 Na ile madhabahu ikavunjika vipande vipande, na yale majivu yakamwagika kutoka madhabahuni, kama ilivyokuwa imefafanuliwa kuwa ndiyo ishara ya kwamba mtu wa Mungu alikuwa amepewa kwa neno la BWANA.
L’autel aussi se brisa, et la cendre se répandit de l’autel, selon le signe que l’homme de Dieu avait prédit avec les paroles du Seigneur.
6 Mfalme Yeroboamu akajibu akimwambia mtu wa Mungu, “Msihi BWANA, Mungu wako akupe neema ili uniombee, ili kwamba mkono wangu urejee kwangu tena.” Kwa hiyo mtu wa Mungu akamwomba BWANA, na mkono wa mfalme ukarejea katika hali yake tena, na ukawa kama ulivyokuwa mwanzoni.
Alors le roi dit à l’homme de Dieu: Implore la face du Seigneur ton Dieu, et prie pour moi, afin que ma main me soit rendue. Et l’homme de Dieu pria la face du Seigneur, et la main du roi revint à lui, et elle devint comme elle était auparavant.
7 Yule mfalme akamwambia mtu wa Mungu, “twende nyumbani kwangu upate chakula, nami nitakupa zawadi.”
Or le roi dit à l’homme de Dieu: Viens avec moi en ma maison pour dîner, et je te donnerai des présents.
8 Yule mtu wa Mungu akamwambia mfalme, “Hata kama utanipa nusu ya miliki yako. staende na wewe, wala sitakula au kunywa maji mahali hapa,
Et l’homme de Dieu répondit au roi: Quand vous me donneriez la moitié de votre maison, je n’irai point avec vous, et je ne mangerai point de pain ni ne boirai point d’eau en ce lieu;
9 kwa sababu BWANA ameniamuru kwa neno lake, 'hutakula mkate wala kunywa maji, wala kurudi kwa njia ulioijia.'”
Car c’est ainsi qu’il m’a été commandé avec les paroles du Seigneur, qui a donné cet ordre: Tu ne mangeras point de pain, tu ne boiras point d’eau, et tu ne retourneras point par la voie par laquelle tu es venu.
10 Kwa hiyo mtu wa Mungu akaondoka na hakurudi nyumbani kwa njia aliyokuja nayo huko Betheli.
Il s’en alla donc par une autre voie, et il ne retourna pas par le chemin par lequel il était venu à Béthel.
11 Sasa kulikuwa na nabii mwingine mzee aliyekuwa akiishi Betheli, na mmoja wa wana wake akaja kumwambia mambo yote ambayo mtu wa Mungu amefanya siku hiyo kule Betheli. Wana wake wakamwambia pia maneno ambayo Yule mtu wa Mungu alimwambia mfalme.
Or un certain vieux prophète habitait à Béthel, et ses fils vinrent vers lui, et lui racontèrent toutes les œuvres qu’avait faites l’homme de Dieu ce jour-là à Béthel; et les paroles qu’il avait dites au roi, ils les racontèrent à leur père.
12 Baba yao akawaambia, “Alienda kwa njia gani?” Wale wanawe walikuwa wamemwona yule mtu wa Mungu kutoka Yuda njia aliyotumia kurudi.
Et leur père leur dit: Par quelle voie s’en est-il allé? Ses fils lui montrèrent la voie par laquelle s’en était allé l’homme de Dieu qui était venu de Juda.
13 Kwa hiyo akawaambia wanawe, “Nitandikeni punda.” Kwa hiyo wakamtandikia punda naye akampanda.
Et il dit à ses fils: Préparez-moi l’âne. Et lorsque ceux-ci l’eurent préparé, il monta dessus.
14 Yule nabii mzee akamfuata yule mtu wa Mungu na akamkuta amekaa chini ya mti wa mwaloni; akamwambia, “Je, wewe ndiye mtu wa Mungu aliyetoka Yuda?” Naye akamjibu, “Mimi ndiye.”
Et il s’en alla après l’homme de Dieu, et il le trouva assis sous le térébinthe, et il lui dit: Es-tu l’homme de Dieu qui es venu de Juda? Celui-ci répondit; Je le suis.
15 Kisha yule nabii mzee akamwambia, “twende nyumbani kwangu ukale chakula.”
Viens, dit-il, avec moi en ma maison pour manger du pain.
16 Yule mtu wa Mungu akamjibu, “Siwezi kurudi na wewe wala kuingia ndani na wewe, tena sitakula chakula wala kunywa maji pamoja na wewe mahali hapa,
L’homme de Dieu lui répondit: Je ne puis retourner ni aller avec toi, et je ne mangerai point de pain et ne boirai point d’eau en ce lieu;
17 kwa sababu niliamuriwa hivyo kwa neno la BWANA, 'Hautakula chakula wala kunywa maji kule, wala kurudi kwa njia utakayokuja nayo.'”
Parce que le Seigneur m’a parlé avec les paroles du Seigneur, disant: tu ne mangeras point de pain et ne boiras point d’eau là, et tu ne retourneras point par la voie par laquelle tu seras allé.
18 Kwa hiyo yule nabii mzee akamwambia, “Mimi pia ni nabii kama ulivyo, na malaika amesema na mimi neno la BWANA, akisema, 'Mrudishe aje na wewe katika nyumba yako, ili aweze kula chakula na kunywa maji.'” Lakini alikuwa anamdanganya mtu wa Mungu.
Cet homme lui répondit: Moi aussi, je suis prophète, semblable à toi, et un ange m’a parlé avec les paroles du Seigneur, disant: Ramène-le avec toi en ta maison, afin qu’il mange du pain et qu’il boive de l’eau. Il le trompa,
19 Kwa hiyo yule mtu wa Mungu akarudi pamoja na yule nabii mzee na akala chakula nyumbani kwake na akanywa maji.
Et le ramena avec lui: il mangea donc du pain en sa maison, et il but de l’eau.
20 Walipokuwa wamekaa mezani, neno la BWANA likamjia yule nabii aliyemrudisha,
Et, lorsqu’ils étaient assis à table, la parole du Seigneur fut adressée au prophète qui l’avait ramené,
21 naye akalia kwa mtu wa Mungu aliyetoka Yuda, akisema “BWANA anasema, 'Kwa kuwa umeshindwa kutii nenola BWANA na umeshindwa kuishika amri ya BWANA ambayo Mungu wako alikupa,
Et il cria à l’homme de Dieu qui était venu de Juda, disant: Voici ce que dit le Seigneur: Parce que tu n’as pas été obéissant à la parole du Seigneur, et que tu n’as point gardé le commandement que t’a prescrit le Seigneur ton Dieu,
22 bali umerudi na umekula chakula na kunywa maji mahali ambapo BWANA alikwambia usile chakula wala kunywa maji, basi mwili wako hautazikwa kwenye makaburi ya baba zako.'”
Et que tu es retourné, et que tu as mangé du pain et bu de l’eau dans le lieu dans lequel je t’ai ordonné de ne point manger de pain et de ne point boire d’eau, ton cadavre ne sera pas porté dans le sépulcre de tes pères.
23 Baada ya kula chakula na kunywa maji, Yule nabii akatandika punda wa mtu wa Mungu, yule mtu aliyerudi naye.
Lors donc qu’il eut mangé et bu, le vieux prophète sella son âne pour le prophète qu’il avait ramené.
24 Baada ya mtu wa Mungu kuondoka, akakutana na simba njiani na kumwua barabarani, na mwili wake uliachwa barabarani. Na yule punda akasimama pembeni yake, na yule simba naye akasimama pembeni ya ule mwili.
Et lorsque celui-ci s’en fut allé, un lion le rencontra et le tua, et son cadavre était étendu dans le chemin: l’âne se tenait auprès de lui, et le lion se tenait auprès du cadavre.
25 Watu walipopita na kuuona ule mwili umeachwa barabarani, na yule simba akisimama karibu na ule mwili, walikuja wakaeleza habari hiyo mjini kule ambako yule nabii mzee aliishi.
Et voilà que des hommes qui passaient virent son cadavre étendu sur la voie, et le lion qui se tenait auprès du cadavre. Et ils vinrent, et le publièrent dans la ville dans laquelle ce vieux prophète demeurait.
26 Yule nabii aliyemrudisha toka njiani aliposikia, akasema, “Yeye mtu wa Muugu ndiye aliyeshindwa kutii neno la BWANA. Kwa hiyo BWANA alimtoa kwa simba, ambaye amemrarua katika vipande vipande na kumwua, kama vile neno la BWANA lilivyokuwa limemwonya.”
Ce qu’ayant appris, ce prophète qui l’avait détourné de sa voie, dit: C’est l’homme de Dieu qui a été désobéissant à la parole du Seigneur, et le Seigneur l’a livré au lion, qui l’a brisé et l’a tué, selon la parole que le Seigneur lui avait dite.
27 Kwa hiyo yule nabii mzee akawaamnbia wanawe, akisema, “Tandikeni punda wangu,” nao wakamtandikia.
Et il dit à ses fils: Sellez-moi l’âne. Lorsque ceux-ci l’eurent sellé,
28 Akaenda akaukuta mwili umeachwa barabarani, punda na simba wamesimama pembeni ya ule mwili. Yule simba hakuula ule mwili, wala hakumshambulia yule punda.
Et que lui s’en fut allé, il trouva le cadavre étendu sur la voie, et l’âne et le lion qui se tenaient auprès du cadavre: le lion ne mangea pas du cadavre et ne fit pas de mal à l’âne.
29 Yule nabii akauchukua ule mwili wa mtu wa Mungu, akaulaza juu ya punda, na akaurudisha. Akaja kwenye mji wake kuomboleza na kuuzika.
Le prophète prit donc le cadavre de l’homme de Dieu, le mit sur l’âne, et le ramena dans la ville du vieux prophète, pour le pleurer.
30 Akaulaza mwili kwenye kaburi lake, nao wakamwombolezea, wakisema, “Aa! ndugu yangu!”
Et il mit son cadavre dans son sépulcre; et ils le pleurèrent, disant: Hélas! hélas! mon frère!
31 Kisha baada ya kumzika, yule nabii mzee akawaambia wanawe, akasema, “Nitakapokufa, mtanizika kwenye kaburi ambalo tumemzika mtu wa Mungu. Mtalaza mifupa yangu pembeni mwa mifupa yake.
Et lorsqu’ils l’eurent pleuré, il dit à ses fils: Lorsque je serai mort, ensevelissez-moi dans le sépulcre dans lequel l’homme de Dieu est enseveli; mettez mes os auprès de ses os.
32 Kwa kuwa ule ujumbe uliosemwa na BWANA, dhidi ya madhabahu kule Betheli na dhidi ya nyumba zote za mahali pa juu katika mji wa Samaria, hakika yatatokea.
Car certainement il arrivera ce qu’il a prédit avec les paroles du Seigneur, contre l’autel qui est à Béthel, et contre tous les temples des hauts lieux qui sont dans les villes de Samarie.
33 Baada ya haya Yeroboamu hakuuacha uovu wake, aliendelea kuchagua makuhani wa kawaida kwa ajili ya mahali pa juu kutoka kwa watu wa kila aina. Yeyote ambaye angeweza kutumika alimtakasa kuwa kuhani.
Après cela, Jéroboam ne revint point de ses voies très mauvaises; mais au contraire, il fit des derniers du peuple des prêtres des hauts lieux: à quiconque le voulait il remplissait sa main, et celui-ci devenait prêtre des hauts lieux.
34 Jambo hili likawa dhambi kwenye familia ya Yeroboamu na kusababisha familia yake kuangamizwa na kuondolewa kabisa katika uso wa dunia.
Et c’est pour ce motif que pécha la maison de Jéroboam, et qu’elle fut détruite et exterminée de la surface de la terre.

< 1 Wafalme 13 >