< 1 Wafalme 13 >
1 Mtu wa Mungu alikuja tokea Yuda kwa neno la BWANA kule Betheli. Naye Yeroboamu alikuwa amesimama karibu na madhabahu ili kufukiza uvumba.
One day a prophet, obeying what Yahweh commanded him to do, went from Judah [north] to Bethel. He arrived there right at the time that Jeroboam was standing at the altar, ready to burn incense.
2 Akalia kinyume na zile madhabahu kwa neno la BWANA: “Ee madhabahu, madhabahu” hivi ndivyo asemavyo BWANA, 'Tazama, mwana aitwaye Yosia atazaliwa katika familia ya Daudi, na juu yenu atawachinja makuhani ambao sasa wanafukiza uvumba mahali hapa pa juu kwa ajili yako. Juu yako watachoma mifupa ya watu.'”
Saying what Yahweh told him to say, the prophet shouted, “This is what Yahweh says [about this] altar [APO]: ‘I want you to know that [some day] a descendant [MTY] of King David will be born. His name will be Josiah, and he will come here. He will slaughter at this altar the priests who are burning incense for sacrifices on the hills [in this area], and he will burn the bones of dead people on this altar.’” [APO]
3 Kisha mtu wa Mungu akatoa ishara siku hiyohiyo, akisema, “Hii ndiyo isharaya kwamba BWANA amesema: 'Tazama, madhabahu zitavuunjika, na majivu yaliyo juu yatamwagika.”
Then the prophet also said, “This is what will prove to you that Yahweh has said this: This altar will be split apart, and the ashes that are on it will be scattered.’”
4 Naye mfalme aliposikia kile mtu wa Mungu alichosema, kwamba amelia kinyume cha zile madhabahu kule Betheli, Yeroboamu akanyosha mkono wake kutoka madhabahuni, akisema, “mkamateni.” Ndipo ule mkono aliokuwa ameunyosha dhidi ya mtu wa Mungu ukakauka, kiasi kwamba hakuweza kuurudisha mwenyewe.
When King Jeroboam heard the prophet say that, he pointed his finger at him and said to his servants, “Seize that man!” But immediately the king’s arm became paralyzed/stiff, with the result that he could not move it.
5 Na ile madhabahu ikavunjika vipande vipande, na yale majivu yakamwagika kutoka madhabahuni, kama ilivyokuwa imefafanuliwa kuwa ndiyo ishara ya kwamba mtu wa Mungu alikuwa amepewa kwa neno la BWANA.
And the altar immediately split apart, and the ashes spilled out [on the ground], which is what the prophet said that Yahweh [MTY] had predicted would happen.
6 Mfalme Yeroboamu akajibu akimwambia mtu wa Mungu, “Msihi BWANA, Mungu wako akupe neema ili uniombee, ili kwamba mkono wangu urejee kwangu tena.” Kwa hiyo mtu wa Mungu akamwomba BWANA, na mkono wa mfalme ukarejea katika hali yake tena, na ukawa kama ulivyokuwa mwanzoni.
Then the king said to the prophet, “Please pray that Yahweh will be merciful to me and heal my arm!” So the prophet prayed, and Yahweh completely healed the king’s arm.
7 Yule mfalme akamwambia mtu wa Mungu, “twende nyumbani kwangu upate chakula, nami nitakupa zawadi.”
Then the king said to the prophet, “Come home with me and eat some food. And I will also give you a reward [for what you have done]!”
8 Yule mtu wa Mungu akamwambia mfalme, “Hata kama utanipa nusu ya miliki yako. staende na wewe, wala sitakula au kunywa maji mahali hapa,
But the prophet replied, “Even if you would [promise to] give me half of everything that you own [MTY], I will not go with you, and I will not eat or drink anything with you here,
9 kwa sababu BWANA ameniamuru kwa neno lake, 'hutakula mkate wala kunywa maji, wala kurudi kwa njia ulioijia.'”
because Yahweh commanded me not to eat or drink anything here. He also commanded me not to return home on the road on which I came here.”
10 Kwa hiyo mtu wa Mungu akaondoka na hakurudi nyumbani kwa njia aliyokuja nayo huko Betheli.
So he started to return home, but he did not go on the road on which he came to Bethel. He went on a different road.
11 Sasa kulikuwa na nabii mwingine mzee aliyekuwa akiishi Betheli, na mmoja wa wana wake akaja kumwambia mambo yote ambayo mtu wa Mungu amefanya siku hiyo kule Betheli. Wana wake wakamwambia pia maneno ambayo Yule mtu wa Mungu alimwambia mfalme.
At that time there was an old man living in Bethel who was a prophet. His sons came and told him what the prophet [from Judah] had done there on that day, and they also told him what the prophet had said to the king.
12 Baba yao akawaambia, “Alienda kwa njia gani?” Wale wanawe walikuwa wamemwona yule mtu wa Mungu kutoka Yuda njia aliyotumia kurudi.
Their father said, “On which road did he go?” So his sons showed him the road on which the prophet from Judah had gone [when he left Bethel].
13 Kwa hiyo akawaambia wanawe, “Nitandikeni punda.” Kwa hiyo wakamtandikia punda naye akampanda.
Then he said to his sons, “Put a saddle on my donkey.” So they did that, and he got on the donkey.
14 Yule nabii mzee akamfuata yule mtu wa Mungu na akamkuta amekaa chini ya mti wa mwaloni; akamwambia, “Je, wewe ndiye mtu wa Mungu aliyetoka Yuda?” Naye akamjibu, “Mimi ndiye.”
He went along the road to (find/catch up with) the prophet from Judah. He found him sitting under an oak tree. He said to him, “Are you the prophet who came from Judah?” He replied, “Yes, I am.”
15 Kisha yule nabii mzee akamwambia, “twende nyumbani kwangu ukale chakula.”
The old prophet said to him, “Come home with me and eat some food.”
16 Yule mtu wa Mungu akamjibu, “Siwezi kurudi na wewe wala kuingia ndani na wewe, tena sitakula chakula wala kunywa maji pamoja na wewe mahali hapa,
He replied, “No, I am not allowed to go with you into your house, or to eat or drink anything with you,
17 kwa sababu niliamuriwa hivyo kwa neno la BWANA, 'Hautakula chakula wala kunywa maji kule, wala kurudi kwa njia utakayokuja nayo.'”
because Yahweh told me, ‘Do not eat or drink anything here, and do not return home on the road on which you came.’”
18 Kwa hiyo yule nabii mzee akamwambia, “Mimi pia ni nabii kama ulivyo, na malaika amesema na mimi neno la BWANA, akisema, 'Mrudishe aje na wewe katika nyumba yako, ili aweze kula chakula na kunywa maji.'” Lakini alikuwa anamdanganya mtu wa Mungu.
Then the old prophet said to him, “I also am a prophet, like you are. Yahweh sent an angel to tell me that I should take you home with me and give you some food and drink.” But the old man was lying [when he said that].
19 Kwa hiyo yule mtu wa Mungu akarudi pamoja na yule nabii mzee na akala chakula nyumbani kwake na akanywa maji.
But because of what the old prophet said, the prophet from Judah returned with him to his home and ate some food and drank some water with him.
20 Walipokuwa wamekaa mezani, neno la BWANA likamjia yule nabii aliyemrudisha,
While they were sitting at the table, Yahweh spoke to the old man.
21 naye akalia kwa mtu wa Mungu aliyetoka Yuda, akisema “BWANA anasema, 'Kwa kuwa umeshindwa kutii nenola BWANA na umeshindwa kuishika amri ya BWANA ambayo Mungu wako alikupa,
Then he cried out to the prophet from Judah, “This is what Yahweh says: ‘You have disobeyed him, and you have not done what he commanded you to do.
22 bali umerudi na umekula chakula na kunywa maji mahali ambapo BWANA alikwambia usile chakula wala kunywa maji, basi mwili wako hautazikwa kwenye makaburi ya baba zako.'”
Instead, you have come back here and had things to eat and drink in a place where he commanded you not to do that. As a result, you will be killed, and your body will not be buried in the grave where your ancestors are buried.’”
23 Baada ya kula chakula na kunywa maji, Yule nabii akatandika punda wa mtu wa Mungu, yule mtu aliyerudi naye.
When they had finished eating, the old man put a saddle on the donkey for the prophet from Judah, [and the prophet from Judah left].
24 Baada ya mtu wa Mungu kuondoka, akakutana na simba njiani na kumwua barabarani, na mwili wake uliachwa barabarani. Na yule punda akasimama pembeni yake, na yule simba naye akasimama pembeni ya ule mwili.
But as he was going, a lion met him and killed him. The prophet’s corpse was lying on the road, and the donkey was standing beside it, and the lion was also standing beside the corpse.
25 Watu walipopita na kuuona ule mwili umeachwa barabarani, na yule simba akisimama karibu na ule mwili, walikuja wakaeleza habari hiyo mjini kule ambako yule nabii mzee aliishi.
Some men passed by and were surprised to see the corpse on the road and the lion standing next to the corpse. So they went into Bethel and reported what they had seen.
26 Yule nabii aliyemrudisha toka njiani aliposikia, akasema, “Yeye mtu wa Muugu ndiye aliyeshindwa kutii neno la BWANA. Kwa hiyo BWANA alimtoa kwa simba, ambaye amemrarua katika vipande vipande na kumwua, kama vile neno la BWANA lilivyokuwa limemwonya.”
When the old man who had brought the prophet from Judah to his home heard about it, he said, “That is the prophet who disobeyed what Yahweh told him to do! That is why Yahweh allowed the lion to attack him and kill him. That is what Yahweh said would happen!”
27 Kwa hiyo yule nabii mzee akawaamnbia wanawe, akisema, “Tandikeni punda wangu,” nao wakamtandikia.
Then he said to his sons, “Put a saddle on my donkey.” So they did that.
28 Akaenda akaukuta mwili umeachwa barabarani, punda na simba wamesimama pembeni ya ule mwili. Yule simba hakuula ule mwili, wala hakumshambulia yule punda.
Then he rode on the donkey and found the prophet’s corpse on the road, and his donkey and the lion were still standing there alongside the corpse. But the lion had not eaten any of the flesh of the prophet and had not attacked the donkey.
29 Yule nabii akauchukua ule mwili wa mtu wa Mungu, akaulaza juu ya punda, na akaurudisha. Akaja kwenye mji wake kuomboleza na kuuzika.
The old man picked up the corpse of the prophet and put it on his donkey and brought it back to Bethel, in order to mourn for him and to bury his corpse.
30 Akaulaza mwili kwenye kaburi lake, nao wakamwombolezea, wakisema, “Aa! ndugu yangu!”
He buried the prophet’s corpse in the grave where other people in his family [had been buried]. Then he and his sons mourned for him, saying, “[We are very sorry], my brother!”
31 Kisha baada ya kumzika, yule nabii mzee akawaambia wanawe, akasema, “Nitakapokufa, mtanizika kwenye kaburi ambalo tumemzika mtu wa Mungu. Mtalaza mifupa yangu pembeni mwa mifupa yake.
After they had buried him, the old man said to his sons, “When I die, bury my corpse in the grave where we buried the prophet from Judah. Lay my corpse next to his corpse.
32 Kwa kuwa ule ujumbe uliosemwa na BWANA, dhidi ya madhabahu kule Betheli na dhidi ya nyumba zote za mahali pa juu katika mji wa Samaria, hakika yatatokea.
[And do not forget what he said, because] the things that Yahweh told him to say about the altar in Bethel, and about the shrines on the hills in the towns in Samaria, will surely happen.”
33 Baada ya haya Yeroboamu hakuuacha uovu wake, aliendelea kuchagua makuhani wa kawaida kwa ajili ya mahali pa juu kutoka kwa watu wa kila aina. Yeyote ambaye angeweza kutumika alimtakasa kuwa kuhani.
But King Jeroboam still did not turn away from continuing to do evil things. Instead, he appointed more priests [who were not descended from Levi]. Anyone who wanted to be a priest, he appointed to be a priest, in order that he could offer sacrifices on the hills.
34 Jambo hili likawa dhambi kwenye familia ya Yeroboamu na kusababisha familia yake kuangamizwa na kuondolewa kabisa katika uso wa dunia.
Because he committed that sin, [a few years later] God got rid of most of Jeroboam’s descendants and did not allow them to become kings of Israel.