< 1 Wafalme 13 >

1 Mtu wa Mungu alikuja tokea Yuda kwa neno la BWANA kule Betheli. Naye Yeroboamu alikuwa amesimama karibu na madhabahu ili kufukiza uvumba.
And behold, by the word of the Lord, a man of God went from Judah to Bethel, when Jeroboam was standing over the altar, and burning incense.
2 Akalia kinyume na zile madhabahu kwa neno la BWANA: “Ee madhabahu, madhabahu” hivi ndivyo asemavyo BWANA, 'Tazama, mwana aitwaye Yosia atazaliwa katika familia ya Daudi, na juu yenu atawachinja makuhani ambao sasa wanafukiza uvumba mahali hapa pa juu kwa ajili yako. Juu yako watachoma mifupa ya watu.'”
And by the word of the Lord, he cried out against the altar. And he said: “O altar, O altar! Thus says the Lord: ‘Behold, a son will be born to the house of David, Josiah by name. And upon you, he will immolate the priests of the high places, who now burn incense upon you. And upon you, he will burn up the bones of men.’”
3 Kisha mtu wa Mungu akatoa ishara siku hiyohiyo, akisema, “Hii ndiyo isharaya kwamba BWANA amesema: 'Tazama, madhabahu zitavuunjika, na majivu yaliyo juu yatamwagika.”
And he gave a sign on the same day, saying: “This will be the sign that the Lord has spoken. Behold, the altar shall be torn apart, and the ashes that are upon it shall be poured out.”
4 Naye mfalme aliposikia kile mtu wa Mungu alichosema, kwamba amelia kinyume cha zile madhabahu kule Betheli, Yeroboamu akanyosha mkono wake kutoka madhabahuni, akisema, “mkamateni.” Ndipo ule mkono aliokuwa ameunyosha dhidi ya mtu wa Mungu ukakauka, kiasi kwamba hakuweza kuurudisha mwenyewe.
And when the king had heard the word of the man of God, which he had cried out against the altar at Bethel, he extended his hand from the altar, saying, “Apprehend him!” But his hand, which he had extended against him, withered. And he was unable to draw it back to himself.
5 Na ile madhabahu ikavunjika vipande vipande, na yale majivu yakamwagika kutoka madhabahuni, kama ilivyokuwa imefafanuliwa kuwa ndiyo ishara ya kwamba mtu wa Mungu alikuwa amepewa kwa neno la BWANA.
Also, the altar was torn apart, and the ashes were poured out from the altar, in accord with the sign that the man of God had predicted by the word of the Lord.
6 Mfalme Yeroboamu akajibu akimwambia mtu wa Mungu, “Msihi BWANA, Mungu wako akupe neema ili uniombee, ili kwamba mkono wangu urejee kwangu tena.” Kwa hiyo mtu wa Mungu akamwomba BWANA, na mkono wa mfalme ukarejea katika hali yake tena, na ukawa kama ulivyokuwa mwanzoni.
And the king said to the man of God, “Entreat the face of the Lord your God, and pray for me, so that my hand may be restored to me.” And the man of God prayed before the face of the Lord, and the hand of the king was restored to him, and it became as it had been before.
7 Yule mfalme akamwambia mtu wa Mungu, “twende nyumbani kwangu upate chakula, nami nitakupa zawadi.”
Then the king said to the man of God: “Come home with me, so that you may dine. And I will give you gifts.”
8 Yule mtu wa Mungu akamwambia mfalme, “Hata kama utanipa nusu ya miliki yako. staende na wewe, wala sitakula au kunywa maji mahali hapa,
And the man of God responded to the king: “Even if you will give me one half part of your house, I will not go with you, nor eat bread, nor drink water in this place.
9 kwa sababu BWANA ameniamuru kwa neno lake, 'hutakula mkate wala kunywa maji, wala kurudi kwa njia ulioijia.'”
For so it was commanded to me by the word of the Lord, ordering: ‘You shall not eat bread, and you shall not drink water, nor shall you return by the way that you came.’”
10 Kwa hiyo mtu wa Mungu akaondoka na hakurudi nyumbani kwa njia aliyokuja nayo huko Betheli.
Then he departed by another way, and he did not return along the way that he had traveled to Bethel.
11 Sasa kulikuwa na nabii mwingine mzee aliyekuwa akiishi Betheli, na mmoja wa wana wake akaja kumwambia mambo yote ambayo mtu wa Mungu amefanya siku hiyo kule Betheli. Wana wake wakamwambia pia maneno ambayo Yule mtu wa Mungu alimwambia mfalme.
Now a certain elderly prophet was living in Bethel. His sons went to him, and they described to him all the works which the man of God had accomplished on that day in Bethel. And they described to their father the words that he had spoken to the king.
12 Baba yao akawaambia, “Alienda kwa njia gani?” Wale wanawe walikuwa wamemwona yule mtu wa Mungu kutoka Yuda njia aliyotumia kurudi.
And their father said to them, “By which way did he depart?” His sons showed him the way by which the man of God, who had come from Judah, had departed.
13 Kwa hiyo akawaambia wanawe, “Nitandikeni punda.” Kwa hiyo wakamtandikia punda naye akampanda.
And he said to his sons, “Saddle the donkey for me.” And when they had saddled it, he climbed on,
14 Yule nabii mzee akamfuata yule mtu wa Mungu na akamkuta amekaa chini ya mti wa mwaloni; akamwambia, “Je, wewe ndiye mtu wa Mungu aliyetoka Yuda?” Naye akamjibu, “Mimi ndiye.”
and he went away after the man of God. And he found him sitting under a terebinth tree. And he said to him, “Are you the man of God who came from Judah?” And he responded, “I am.”
15 Kisha yule nabii mzee akamwambia, “twende nyumbani kwangu ukale chakula.”
And he said to him, “Come home with me, so that you may eat bread.”
16 Yule mtu wa Mungu akamjibu, “Siwezi kurudi na wewe wala kuingia ndani na wewe, tena sitakula chakula wala kunywa maji pamoja na wewe mahali hapa,
But he said: “I am not able to turn back, nor to go with you. Neither will I eat bread, or drink water in this place.
17 kwa sababu niliamuriwa hivyo kwa neno la BWANA, 'Hautakula chakula wala kunywa maji kule, wala kurudi kwa njia utakayokuja nayo.'”
For the Lord has spoken to me, by the word of the Lord, saying, “You shall not eat bread, and you shall not drink water in that place, nor shall you return by the way that you arrived.”
18 Kwa hiyo yule nabii mzee akamwambia, “Mimi pia ni nabii kama ulivyo, na malaika amesema na mimi neno la BWANA, akisema, 'Mrudishe aje na wewe katika nyumba yako, ili aweze kula chakula na kunywa maji.'” Lakini alikuwa anamdanganya mtu wa Mungu.
And he said to him: “I, too, am a prophet like you. And an Angel spoke to me, by the word of the Lord, saying, ‘Lead him back with you to your house, so that he may eat bread, and drink water.’” And so he deceived him.
19 Kwa hiyo yule mtu wa Mungu akarudi pamoja na yule nabii mzee na akala chakula nyumbani kwake na akanywa maji.
And he led him back with him. Then he ate bread and drank water in his house.
20 Walipokuwa wamekaa mezani, neno la BWANA likamjia yule nabii aliyemrudisha,
And while they were sitting at table, the word of the Lord came to the prophet who had led him back.
21 naye akalia kwa mtu wa Mungu aliyetoka Yuda, akisema “BWANA anasema, 'Kwa kuwa umeshindwa kutii nenola BWANA na umeshindwa kuishika amri ya BWANA ambayo Mungu wako alikupa,
And he cried out to the man of God who had arrived from Judah, saying: “Thus says the Lord: Because you were not obedient to the mouth of the Lord, and you did not keep the commandment that the Lord your God instructed to you,
22 bali umerudi na umekula chakula na kunywa maji mahali ambapo BWANA alikwambia usile chakula wala kunywa maji, basi mwili wako hautazikwa kwenye makaburi ya baba zako.'”
and you turned back, and ate bread, and drank water in the place where he commanded you that you should not eat bread, nor drink water: your dead body shall not be carried back to the sepulcher of your fathers.”
23 Baada ya kula chakula na kunywa maji, Yule nabii akatandika punda wa mtu wa Mungu, yule mtu aliyerudi naye.
And when he had eaten and had drunk, he saddled his donkey for the prophet whom he had led back.
24 Baada ya mtu wa Mungu kuondoka, akakutana na simba njiani na kumwua barabarani, na mwili wake uliachwa barabarani. Na yule punda akasimama pembeni yake, na yule simba naye akasimama pembeni ya ule mwili.
And when he had departed, a lion found him along the way, and it killed him, and his dead body was left upon the road. Now the donkey was standing beside him. And the lion was standing beside the dead body.
25 Watu walipopita na kuuona ule mwili umeachwa barabarani, na yule simba akisimama karibu na ule mwili, walikuja wakaeleza habari hiyo mjini kule ambako yule nabii mzee aliishi.
And behold, men who were passing by saw the dead body lying in the road, with the lion standing beside the body. And they went and made it widely known in the city where that elderly prophet was living.
26 Yule nabii aliyemrudisha toka njiani aliposikia, akasema, “Yeye mtu wa Muugu ndiye aliyeshindwa kutii neno la BWANA. Kwa hiyo BWANA alimtoa kwa simba, ambaye amemrarua katika vipande vipande na kumwua, kama vile neno la BWANA lilivyokuwa limemwonya.”
And when that prophet, who had led him back from the way, had heard it, he said: “It is the man of God, who was disobedient to the mouth of the Lord. And the Lord has delivered him to the lion. And it has torn him apart and killed him, in accord with the word of the Lord, which he spoke to him.”
27 Kwa hiyo yule nabii mzee akawaamnbia wanawe, akisema, “Tandikeni punda wangu,” nao wakamtandikia.
And he said to his sons, “Saddle a donkey for me.” And when they had saddled it,
28 Akaenda akaukuta mwili umeachwa barabarani, punda na simba wamesimama pembeni ya ule mwili. Yule simba hakuula ule mwili, wala hakumshambulia yule punda.
and he had departed, he found the dead body lying on the road, with the donkey and the lion standing beside the dead body. The lion did not eat from the dead body, nor did it harm the donkey.
29 Yule nabii akauchukua ule mwili wa mtu wa Mungu, akaulaza juu ya punda, na akaurudisha. Akaja kwenye mji wake kuomboleza na kuuzika.
Then the prophet took the dead body of the man of God, and he placed it upon the donkey, and returning, he brought it into the city of the elderly prophet, so that he might mourn for him.
30 Akaulaza mwili kwenye kaburi lake, nao wakamwombolezea, wakisema, “Aa! ndugu yangu!”
And he placed his dead body in his own sepulcher. And they mourned for him, saying: “Alas! Alas! My brother!”
31 Kisha baada ya kumzika, yule nabii mzee akawaambia wanawe, akasema, “Nitakapokufa, mtanizika kwenye kaburi ambalo tumemzika mtu wa Mungu. Mtalaza mifupa yangu pembeni mwa mifupa yake.
And when they had mourned over him, he said to his sons: “When I will have died, bury me in the sepulcher in which the man of God was buried. Place my bones beside his bones.
32 Kwa kuwa ule ujumbe uliosemwa na BWANA, dhidi ya madhabahu kule Betheli na dhidi ya nyumba zote za mahali pa juu katika mji wa Samaria, hakika yatatokea.
For certainly, the word will arrive, which he predicted by the word of the Lord, against the altar, which is in Bethel, and against all the shrines of the high places, which are in the cities of Samaria.”
33 Baada ya haya Yeroboamu hakuuacha uovu wake, aliendelea kuchagua makuhani wa kawaida kwa ajili ya mahali pa juu kutoka kwa watu wa kila aina. Yeyote ambaye angeweza kutumika alimtakasa kuwa kuhani.
After these words, Jeroboam did not turn back from his very evil way. Instead, to the contrary, he made priests for the high places out of the least of the people. Whosoever was willing, he filled his hand, and he became a priest of the high places.
34 Jambo hili likawa dhambi kwenye familia ya Yeroboamu na kusababisha familia yake kuangamizwa na kuondolewa kabisa katika uso wa dunia.
And for this reason, the house of Jeroboam sinned, and was uprooted, and was wiped from the face of the earth.

< 1 Wafalme 13 >