< 1 Wafalme 11 >

1 Basi mfalme Sulemani aliwapenda wanawake wengi wa kigeni: binti wa Farao na wanawake wa Wamoabu, Waamori, Waedomu, Wasidoni, na Wahiti - Haya na
And King Solomon has loved many strange women, and the daughter of Pharaoh, females of Moab, Ammon, Edom, Sidon, [and] of the Hittites,
2 mataifa ambayo BWANA alikuwa amewaambia Waisraeli kwamba, “Msiwaoe, wala binti zenu kuolewa nao, kwani kwa hakika wataigeuza mioyo yenu ili mfuate miungu yao.” Lakini Sulemani aliwapenda wanawake hao.
of the nations of which YHWH said to the sons of Israel, “You do not go in to them, and they do not go in to you; surely they turn aside your heart after their gods”; Solomon has cleaved to them for love.
3 Sulemani alikuwa na wanawake halali mia saba na masuria mia tatu. Wake zake waliugeuza moyo wake.
And he has seven hundred wives, princesses, and three hundred concubines; and his wives turn aside his heart.
4 Kwa kuwa Sulemani alipozeeka, wake zake waliugeuza moyo wake kwa miungu mingine; hakuutoa moyo wake wote kwa BWANA, Mungu wake, kama ulivyokuwa moyo wa Daudi baba yake.
And it comes to pass, at the time of Solomon’s old age, his wives have turned aside his heart after other gods, and his heart has not been perfect with his God YHWH, like the heart of his father David.
5 Kwani Sulemani alimfuata Ashtoreth, mungu mke wa Wasidoni, na alimfuata Milkom, ambayo ni sanamu chukizo ya Waamori.
And Solomon goes after Ashtoreth goddess of the Zidonians, and after Milcom the abomination of the Ammonites;
6 Sulemani akafanya maovu mbele ya BWANA; hakumfuata BWANA kwa moyo wake wote, kama alivyofanya Daudi baba yake.
and Solomon does evil in the eyes of YHWH, and has not been fully after YHWH, like his father David.
7 Kisha Sulemani akajenga mahali pa juu pa Kemoshi, ambayo ni sanamu chukizo ya Wamoabu, mashariki mwa Yerusalemu juu ya kilima, na vivyo hivyo na Moleki, Sanamu chukizo ya Waamoni.
Then Solomon builds a high place for Chemosh the abomination of Moab, in the hill that [is] on the front of Jerusalem, and for Molech the abomination of the sons of Ammon;
8 Na kadhalika ndivyo alivyowafanyia wake zake wa kigeni, ambao walifukiza uvumba na kutoa sadaka kwa miungu yao.
and so he has done for all his strange women, who are perfuming and sacrificing to their gods.
9 BWANA alichukizwa na Sulemani, kwa sababu moyo wake ulikuwa umemwacha Mungu wa Israeli, ingawa alikuwa amejionyesha kwake mara mbili
And YHWH shows Himself angry with Solomon, for his heart has turned aside from YHWH, God of Israel, who had appeared to him twice,
10 na kumwamuru juu ya mambo haya, kwamba asiwaendee miungu wengine. Bali Sulemani hakutii kile ambacho BWANA alikuwa amemwamuru.
and given a charge to him concerning this thing, not to go after other gods; and he has not kept that which YHWH commanded,
11 Kwa hiyo BWANA akamwambia Sulemani, “Kwa kuwa umeyafanya haya haukulishika agano langu na maagizo ambayo nilikuamuru, basi nitaugawa ufalme kutoka kwako na kuwapatia watumishi wako.
and YHWH says to Solomon, “Because that this has been with you, and you have not kept My covenant and My statutes that I charged on you, I surely tear the kingdom from you, and have given it to your servant.
12 Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi, sitalifanya hilo wakati wa uhai wako, bali nitaugawa wakati ukiwa chini ya mwanao.
Only, I do not do it in your days, for the sake of your father David; I tear it out of the hand of your son;
13 Bado sitaugawanya ufalme wote; Nitampa mwanao kabila moja kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, na kwa ajili ya Yerusalemu, ambayo nimeichagua.”
only, I do not tear away all of the kingdom; I give one tribe to your son, for the sake of My servant David, and for the sake of Jerusalem that I have chosen.”
14 Kisha BWANA akamwinulia uadui Sulemani, Hadadi Mwedomu. Alikuwa anatoka kwenye familiia ya mfalme wa Edomu.
And YHWH raises up an adversary against Solomon, Hadad the Edomite; he [is] of the seed of the king in Edom;
15 Daudi alipokuwa Edomu, Yoabu mkuu wa jeshi alikuwa ameenda kuzika mfu, kila mtu aliyekuwa ameuawa kule Edomu.
and it comes to pass, in David’s being with Edom, in the going up of Joab head of the host to bury the slain, that he strikes every male in Edom—
16 Yoabu na Israeli yote walibaki huko kwa miezi sita mpaka alipokuwa amewaua wanaume wote wa Edomu.
for six months Joab abided there, and all Israel, until the cutting off of every male in Edom—
17 Lakini Hadadi alichulukuliwa na Waedomu wengine na watumishi wa baba yake hadi Misri, kuanzia Hadadi alipokuwa mtoto mdogo.
and Hadad flees, he and certain Edomites, of the servants of his father, with him, to go to Egypt, and Hadad [is] a little youth,
18 Waliondoka Midiani wakaja Parani, ambapo walichukuliwa na wanaume mpaka Misri, kwa Farao wa Misri, ambaye alimpa nyumba na ardhi yenye chakula.
and they rise out of Midian, and come into Paran, and take men with them out of Paran, and come into Egypt, to Pharaoh king of Egypt, and he gives a house to him, and has commanded bread for him, and has given land to him.
19 Hadadi alipata neema kubwa machoni pa Farao, kwa hiyoFarao akampatia mke, umbu wa mke wake mwenyewe, umbu la Tapenesi aliyekuwa Malkia.
And Hadad finds grace in the eyes of Pharaoh exceedingly, and he gives to him a wife, the sister of his own wife, sister of Tahpenes the mistress;
20 Naye huyo umbu la Tapenesi alimzalia Hadadi mwana. Wakamwita jina lake Genubathi. Tapenesi akamlea katika ikulu ya Farao. Kwa hiyo Genubathi alikulia kwenye ikulu ya Farao pamoja na watoto wa Farao.
and the sister of Tahpenes bears to him his son Genubath, and Tahpenes weans him within the house of Pharaoh, and Genubath is in the house of Pharaoh in the midst of the sons of Pharaoh.
21 Naye alipokuwa huko Misri, Hadadi alisikia kuwa Daudi alishalala na mababu zake na kwamba Yoabu mkuu wa majeshi alishakufa, Hadadi akamwambia Farao, “Acha niondoke nirudi nchini kwangu.”
And Hadad has heard in Egypt that David has lain with his fathers, and that Joab head of the host is dead, and Hadad says to Pharaoh, “Send me away, and I go to my land.”
22 Lakini Farao alimwambia, “Umepungukiwa nini kwangu, kwamba sasa unatafuta kurudi nchini kwako?” Naye Hadadi akamjibu, “Hapana kitu lakini tafadhali niache niende.”
And Pharaoh says to him, “But what are you lacking with me, that behold, you are seeking to go to your own land?” And he says, “Nothing, but you certainly send me away.”
23 Pia Mungu akamwinulia Sulemani adui mwingine, Rezoni mwana wa Eliada, aliyekuwa amemkimbia bwana wake Hadadezeri mfalme wa Soba.
And God raises an adversary against him, Rezon son of Eliadah, who has fled from Hadadezer king of Zobah, his lord,
24 Rezoni alijikusanyia wanaume naye akawa mkuu wa jeshi dogo, Daudi ali owapiga wanaume wa Soba. Wale wanume Rezoni walienda Dameski kuishi huko, na Rezoni aliitawala Dameski.
and gathers men to himself, and is head of a troop in David’s slaying them, and they go to Damascus, and dwell in it, and reign in Damascus;
25 Yeye akawa adui wa Israeli katika siku zote za mfalme Sulemani, zaidi ya madhara ambayo Hadadi alisababisha. Rezoni akawachukia Israeli na akawa juu ya Shamu
and he is an adversary against Israel all the days of Solomon (besides the evil that Hadad [did]), and he cuts off in Israel, and reigns over Aram.
26 Kisha Yeroboamu mwana wa Nebati, mwefraimu wa Sereda, akida wa Sulemani, ambaye jina la mama yake lilikuwa Serua, mjane, pia akainua mkono wake dhidi ya mfalme.
And Jeroboam son of Nebat, an Ephraimite of Zereda—the name of whose mother [is] Zeruah, a widow woman—servant to Solomon, he also lifts up a hand against the king;
27 Kisa cha kuinua mkono wake kinyume cha mfalme ilikuwa ni mfalme Sulemani kujenga Milo na kufunga mahali palipobomoka katika mji wa Daudi baba yake.
and this [is] the thing [for] which he lifted up a hand against the king: Solomon built Millo—he shut up the breach of the city of his father David,
28 Yeroboamu alikuwa mtu hodari na shujaa. Sulemani akaona kuwa huyo kijana alikuwa na bidii, kwa hiyo akampa kuwa na mamlaka juu ya wafanyakazi katika nyumba ya Yusufu.
and the man Jeroboam [is] mighty in valor, and Solomon sees that the young man is doing business, and appoints him over all the burden of the house of Joseph.
29 Wakati huo, Yeroboamu alipokuwa akitoka katika Yerusalemu, nabii Ahiya Mshilo akamkuta barabarani. Sasa Ahiya alikuwa amevaa vazi jipya na kwamba hawa wawili walikuwa pekee yao kondeni.
And it comes to pass, at that time, that Jeroboam has gone out from Jerusalem, and Ahijah the Shilonite, the prophet, finds him in the way, and he is covering himself with a new garment; and both of them [are] by themselves in a field,
30 Kisha Ahiya akalishika lile vazi jipya ambalo alikuwa nalo na akalichana katika vipande kumi na viwili.
and Ahijah lays hold on the new garment that [is] on him, and tears it [into] twelve pieces,
31 Akamwambia Yeroboamu. “Chukua vipande kumi, kwani BWANA, Mungu wa Israeli, anasema, 'Tazama, Nitaugawa ufalme toka katika mkono wa Sulemani nami nitakupa makabila kumi.
and says to Jeroboam, “Take ten pieces for yourself, for thus said YHWH, God of Israel: Behold, I am tearing the kingdom out of the hand of Solomon, and have given the ten tribes to you,
32 (lakini Sulemani atabaki na kabila moja, kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi na kwa ajili ya mji wangu Yerusalemu - mji ambao nimeuchagua toka kwenye kabila zote za Israeli),
but he has the one tribe for My servant David’s sake, and for Jerusalem’s sake, the city which I have fixed on, out of all the tribes of Israel,
33 kwa kuwa ameniacha na kumwabudu Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, Kemoshi Mungu wa Wamoabu, na Milikomu mungu wa watu wa Amoni. Wameziacha njia zangu, hawakufanya kilicho chema katika macho yangu, wala hawa kuzishika amri na maagizo yangu, kama alivyofanya Daudi baba yake.
because they have forsaken Me, and bow themselves to Ashtoreth, goddess of the Zidonians, to Chemosh god of Moab, and to Milcom god of the sons of Ammon, and have not walked in My ways, to do that which [is] right in My eyes, and My statutes and My judgments, like his father David.
34 Hata hivyo. Stauchukua ufalme wote toka kwenye mkono wa Sulemani. Badala yake, nimemfanya kuwa mtawala katika siku zake zote za uhai wake, kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu ambaye nilimchagua, mtu ambaye alizishika amri na maagizo yangu.
And I do not take the whole of the kingdom out of his hand, for I make him prince all [the] days of his life, for the sake of My servant David whom I chose, who kept My commands and My statutes;
35 Bali nitauchukua ufalme ukiwa chini ya mkono wa mwanae na nitakupa wewe, makabila kumi.
and I have taken the kingdom out of the hand of his son, and given it to you—the ten tribes;
36 Nitampa kabila moja mwana wa Sulemani ili kwamba Daudi mtumishi wagu atabaki kuwa nuru mbele yangu huko Yerusalemu, mji ambao nimeuchagua ili niweke jina langu.
and to his son I give one tribe, for there being a lamp before Me for My servant David in Jerusalem [for] all the days, the city that I have chosen for Myself to put My Name there.
37 Nami nitakuchukua, nawe utatawala ili kutimiza haja yako, nawe utakuwa mfalme juu ya Israeli.
And I take you, and you have reigned over all that your soul desires, and you have been king over Israel;
38 Kama utasikiliza yote ninayokuagaza, na kama utatembea katika njia zangu na kufanya kinachopendeza mbele ya macho yangu, ukayashika maagizo na amri zangu, kama Daudi mtumishi wangu alivyofanya, ndipo nitakapokuwa na wewe na nitakujengea nyumba ya uhakika, kama niliyomjengea Daudi, nami nitakupa Israeli.
and it has been, if you hear all that I command you, and have walked in My ways, and done that which is right in My eyes, to keep My statutes and My commands, as My servant David did, that I have been with you, and have built a steadfast house for you, as I built for David, and have given Israel to you,
39 Nitawaadhibu uzao wa Daudi, lakini si milele.”
and I humble the seed of David for this; only, not [for] all the days.”
40 Kwa hiyo Sulemani akajaribu kumwua Yeroboamu. Lakini Yeroboamu akaamka na kukimbilia Misri, Kwa Shishaki mfalme wa Misri, naye akabaki Misri mpaka Sulemani alipokufa.
And Solomon seeks to put Jeroboam to death, and Jeroboam rises and flees to Egypt, to Shishak king of Egypt, and he is in Egypt until the death of Solomon.
41 Na kwa mambo mengine yanayomhusu Sulemani, Yote ambayo alifanya na hekima zake, je, hayakuandikwa katika kitabu cha matukio ya
And the rest of the matters of Solomon, and all that he did, and his wisdom, are they not written on the scroll of the matters of Solomon?
42 Sulemani? Sulemani alitawala Yerusalemu juu ya Israeli yote kwa miaka arobaini.
And the days that Solomon has reigned in Jerusalem over all Israel [are] forty years,
43 Naye akalala na mababu zake na alizikwa katika mji wa Daudi baba yake. Rehoboamu mwanae akawa mfalme mahali pake.
and Solomon lies with his fathers, and is buried in the city of his father David, and his son Rehoboam reigns in his stead.

< 1 Wafalme 11 >