< 1 Yohana 3 >

1 Oneni ni pendo la namna gani ametupatia Baba, kwamba tunaitwa watoto wa Mungu, na hivi ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui kwa kuwa haukumtambua yeye.
Behold, how great love the Father has bestowed on us, that we should be called the children of God! For this reason, the world knows us not, because it knew him not.
2 Wapendwa sisi sasa ni watoto wa Mungu, na haijadhihirika bado jinsi tutakavyokuwa. Twajua kwamba Kristo atakapoonekana, tutafanana naye, kwani tutamuona kama alivyo.
Beloved, now are we the children of God, and it does not yet appear what we shall be: but we know that, when he shall appear, we shall be like him; for we shall see him as he is.
3 Na kila mmoja ambaye ana ujasiri huu kuhusu wakati ujao ulioelekezwa kwake, hujitakasa mwenyewe kama yeye alivyo mtakatifu.
And every one that has this hope in Him purifies himself, even as He is pure.
4 Kila mtu anayeendelea kutenda dhambi huvunja sheria. Kwa sababu dhambi ni uvunjaji sheria.
Every one that works sin, works also transgression of law: and sin is transgression of law.
5 Mnajua Kristo alidhihilishwa ili kuziondoa dhambi kabisa. Na ndani yake hamna dhambi.
And you know that he was manifested, that he might take away our sins; and in him there is no sin.
6 Hakuna hata mmoja adumue ndani yake na kuendelea kutenda dhambi. Hakuna mtu hata mmoja adumuye katika dhambi ikiwa amemuona au kumfahamu yeye.
Whoever abides in him, sins not. Whoever sins, has neither seen him nor known him.
7 Watoto wapendwa, msikubali kupotoshwa na mtu yeyote. Atendaye haki ni mwenye haki, kama vile Kristo naye alivyo mwenye haki.
Little children, let no one deceive you: he that works righteousness is righteous, even as he is righteous.
8 Atendaye dhambi ni wa ibilisi, kwa sababu ibilisi ni mtenda dhambi tangu mwanzo. Kwa sababu hii Mwana wa Mungu alidhihilishwa ili aweze kuziharibu kazi za ibilisi.
He that works sin is of the devil, for the devil sins from the beginning: for this purpose was the son of God manifested, that he might destroy the works of the devil.
9 Yeyote aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu mbegu ya Mungu hukaa ndani yake. Hawezi kuendelea kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa na Mungu.
Whoever has been begotten of God does not work sin; because his seed remains in him: and he can not sin, because he has been begotten of God.
10 Katika hili watoto wa Mungu na watoto wa ibilisi wanafahamika. Yeyote asiyetenda kilicho cha haki, siyo wa Mungu, wala yule ambaye hawezi kumpenda ndugu yake.
By this the children of God are manifest, and the children of the devil. Whoever does not work righteousness is not of God; neither is he that loves not his brother.
11 Kwani huu ndio ujumbe mliousikia kutoka mwanzo, kwamba tunapaswa kupendana sisi kwa sisi,
For this is the message that you have heard from the beginning, that we should love one another.
12 siyo kama Kaini ambaye alikuwa wa mwovu na alimuua ndugu yake. Na kwa nini alimuua? Kwa sababu matendo yake yalikuwa maovu, na yale ya ndugu yake yalikuwa ya haki.
Not as Cain, who was of the wicked one, and slew his brother: and for what reason did he slay him? because his own works were evil, and his brother’s, righteous.
13 Ndugu zangu, msishangae, endapo ulimwengu utawachukia.
Wonder not, my brethren, if the world hates you.
14 Twajua tumekwisha toka mautini na kuingia uzimani, kwa sababu tunawapenda ndugu. Yeyote ambaye hana upendo hudumu katika mauti.
We know that we have passed from death to life, because we love the brethren: he that loves not his brother, abides in death.
15 Mtu yeyote anaye mchukia ndugu yake ni muuaji. Na mnajua kuwa uzima wa milele haukai ndani ya muuaji. (aiōnios g166)
Whoever hates his brother, is a murderer: and you know that no murderer has eternal life abiding in him. (aiōnios g166)
16 Katika hili tunalijua pendo, kwa sababu kristo aliutoa uhai wake kwa ajili yetu. Nasi yatupasa kuyatoa maisha yetu kwa ajili ya ndugu.
By this we know the love of Christ, because he laid down his life for us: and we ought to lay down our lives for the brethren.
17 Lakini yeyote aliye na vitu, na anamuona ndugu yake mwenye uhitaji, lakini huuzuia moyo wake wa huruma kwa ajili yake; je, upendo wa Mungu unakaaje ndani yake?
Whoever has this world’s goods, and sees his brother have need, and shuts his heart against him, how dwells the love of God in him?
18 Watoto wangu wapenzi, tusipende kwa midomo wala kwa maneno matupu bali katika vitendo na kweli.
My little children, let us not love in word, nor in tongue, but in deed, and in truth.
19 Katika hili tunajua kwamba sisi tuko katika kweli, na mioyo yetu inathibitika katika yeye.
And by this we know that we are of the truth; and we shall have our hearts at rest before him:
20 Ikiwa kama mioyo yetu yatuhukumu, Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu, na yeye hujua mambo yote.
for if our heart condemn us, we know that God is greater than our heart, and knows all things.
21 Wapenzi, kama mioyo yetu haituhukumu, tunao ujasiri kwa Mungu.
Beloved, if our heart condemn us not, we have confidence toward God,
22 Na chochote tuombacho tutakipokea kutoka kwake, kwa sababu tunazishika amri zake na tunafanya mambo yanayopendeza mbele zake.
and whatever we ask, we receive from him, because we keep his commandments, and do the things that are pleasing in his sight.
23 Na hii ndiyo amri yake- ya kwamba yatupasa kuamini katika jina la Mwanaye Yesu Kristo na kupendana sisi kwa sisi-kama alivyotupatia amri yake.
And this is his commandment: That we should believe on the name of his Son Jesus Christ, and love one another, as he gave us commandment.
24 Anayezitii amri zake hudumu ndani yake, na Mungu hukaa ndani yake. Na kwa sababu hii twajua kuwa hukaa ndani yetu, Kwa yule Roho aliyetupa.
And he that keeps his commandments abides in him, and he in him. And by this we know that he abides in us, by the Spirit which he has given us.

< 1 Yohana 3 >