< 1 Yohana 1 >

1 Kile kilichokuwapo tangu mwanzo-kile tulichokisikia, kile tulichokiona kwa macho yetu, kile tulichokitazama, na mikono yetu imekishika-kuhusu Neno la uzima.
We declare to you what was from the beginning, what we have heard, what we have seen with our eyes, what we have looked at and touched with our hands, concerning the word of life.
2 Na ule uzima ulifanywa kujulikana wazi, na tumeuona, na kuushuhudia, na kuwatangazia uzima wa milele, ambao ulikuwa kwa Baba na ulifanywa kujulikana kwetu. (aiōnios g166)
This life was revealed; we have seen it, and we testify and declare to you the eternal life that was with the Father and that was revealed to us. (aiōnios g166)
3 Kile tulichokiona na kukisikia twakitangaza kwenu pia, ili kwamba muweze kujumuika pamoja nasi, na ushirika wetu pamoja na Baba na Mwanae Yesu Kristo.
What we have seen and heard we declare to you, so that you also may have fellowship with us, and indeed our fellowship is with the Father and with his Son Jesus Christ.
4 Na tunawandikia mambo haya ninyi ili kwamba furaha yetu iwe timilifu.
We are writing these things to you so that our joy may be full.
5 Huu ndio ujumbe tuliousikia kutoka kwake na kuwatangazia: Mungu ni nuru na ndani yake hakuna giza hata kidogo.
This is the message that we have heard from him and proclaim to you, that God is light, and in him there is no darkness at all.
6 Kama tukisema kwamba tunaushirika naye na twatembea gizani, twadanganya na hatutendi kweli.
If we say that we have fellowship with him and yet walk in the darkness, we lie and do not live by the truth.
7 Lakini tukitembea katika nuru kama alivyo katika nuru, twashirikiana sisi kwa sisi, na damu ya Yesu Kristo, mwanae yatutakasa kutoka dhambi zote.
But if we walk in the light, as he is in the light, we have fellowship with one another, and the blood of Jesus Christ his Son cleanses us from all sin.
8 Kama tukisema hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, na kweli haimo ndani yetu.
If we say that we do not have sin, we deceive ourselves, and the truth is not in us.
9 Lakini tukizitubu dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na haki kutusamehe dhambi zetu na kututakasa na uovu wote.
If we confess our sins, he is faithful and just to forgive us our sins and cleanse us from all unrighteousness.
10 Tukisema kwamba hatujatenda dhambi, twamfanya yeye kuwa muongo, na neno lake halimo ndani yetu.
If we say that we have not sinned, we make him a liar, and his word is not in us.

< 1 Yohana 1 >