< 1 Yohana 1 >

1 Kile kilichokuwapo tangu mwanzo-kile tulichokisikia, kile tulichokiona kwa macho yetu, kile tulichokitazama, na mikono yetu imekishika-kuhusu Neno la uzima.
That which was from the beginning, that which we have heard, that which we have witnessed with our eyes, that which we contemplated and our hands handled with reference to the word of the Life
2 Na ule uzima ulifanywa kujulikana wazi, na tumeuona, na kuushuhudia, na kuwatangazia uzima wa milele, ambao ulikuwa kwa Baba na ulifanywa kujulikana kwetu. (aiōnios g166)
—oh yes, the Life was manifested, and we have seen and testify and declare to you that eternal Life who was in the presence of the Father and was manifested to us— (aiōnios g166)
3 Kile tulichokiona na kukisikia twakitangaza kwenu pia, ili kwamba muweze kujumuika pamoja nasi, na ushirika wetu pamoja na Baba na Mwanae Yesu Kristo.
that which we have seen and heard we declare to you, so that you also may have fellowship with us; indeed, our fellowship is with the Father and with His Son, Jesus Christ.
4 Na tunawandikia mambo haya ninyi ili kwamba furaha yetu iwe timilifu.
Yes, we write these things to you so that our joy may be fulfilled.
5 Huu ndio ujumbe tuliousikia kutoka kwake na kuwatangazia: Mungu ni nuru na ndani yake hakuna giza hata kidogo.
Now this is the message that we have heard from Him and declare to you, that God is light and there is no darkness at all in Him.
6 Kama tukisema kwamba tunaushirika naye na twatembea gizani, twadanganya na hatutendi kweli.
If we claim that we have fellowship with Him while walking in the darkness, we are lying and not living the truth.
7 Lakini tukitembea katika nuru kama alivyo katika nuru, twashirikiana sisi kwa sisi, na damu ya Yesu Kristo, mwanae yatutakasa kutoka dhambi zote.
But if we walk in the light just as He is in the light, we have fellowship with one another, and the blood of Jesus Christ His Son cleanses us from all sin.
8 Kama tukisema hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, na kweli haimo ndani yetu.
If we claim that we have no sin, we are deceiving ourselves and the Truth is not in us.
9 Lakini tukizitubu dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na haki kutusamehe dhambi zetu na kututakasa na uovu wote.
If we confess our sins, He is faithful and righteous so as to forgive us those sins and to cleanse us from all unrighteousness.
10 Tukisema kwamba hatujatenda dhambi, twamfanya yeye kuwa muongo, na neno lake halimo ndani yetu.
If we claim that we have not sinned, we call Him a liar and His Word is not in us.

< 1 Yohana 1 >