< 1 Wakorintho 1 >
1 Paulo, aliyeitwa na Kristo Yesu kuwa mtume kwa mapenzi ya Mungu, na Sosthene ndugu yetu,
Paul, called to be an apostle of Jesus Christ through the will of God, and Sosthenes our brother, to the church of God which is in Corinth,
2 kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, kwa wale ambao wamewekwa wakfu katika Yesu Kristo, ambao wameitwa kuwa watu watakatifu. Tunawaandikia pia wale wote wanaoliitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo katika mahali pote, Bwana wao na wetu.
even to them that are sanctified in Christ Jesus, and called to be saints, with all that in every place call upon the name of our Lord Jesus Christ, who is both their Lord and ours;
3 Neema na amani iwe kwenu kutoka kwa Mungu baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
grace and peace be to you from God our Father, and from our Lord Jesus Christ.
4 Siku zote namshukru Mungu wangu kwa ajili yenu, kwa sababu ya neema ya Mungu ambayo Kristo Yesu aliwapa.
I always give thanks unto my God, on your account, for the grace of God bestowed on you in Christ Jesus; that ye are enriched by Him with every gift,
5 Amewafanya kuwa matajiri katika kila njia, katika usemi na pamoja maarifa yote.
in all utterance and knowledge;
6 Amewafanya matajiri, kama ushuhuda kuhusu Kristo ya kwamba amethibitishwa kuwa kweli miongoni mwenu.
(even as the testimony of Christ was confirmed among you; )
7 Kwa hiyo hampungukiwi karama za kiroho, kama mlivyo na hamu ya kusubiri ufunuo wa Bwana wetu Yesu Kristo.
so that ye are deficient in no gift, expecting the revelation of our Lord Jesus Christ:
8 Atawaimarisha ninyi pia hadi mwisho, ili msilaumiwe siku ya Bwana wetu Yesu Kristo.
who will also confirm you unto the end, that ye may be blameless in the day of our Lord Jesus Christ;
9 Mungu ni mwaminifu ambaye aliwaita ninyi katika ushirika wa mwana wake, Yesu Kristo Bwana wetu.
for God is faithful by whom ye were called into the communion of his son Jesus Christ our Lord.
10 Sasa nawasihi kaka na dada zangu, kupitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba wote mkubali, na kwamba kusiwe na migawanyiko miongoni mwenu. Nawasihi kwamba muungane pamoja katika nia moja na katika kusudi moja.
Now I beseech you, brethren, by the name of our Lord Jesus Christ, that ye would all say alike, and that there may be no schisms among you, but that ye be perfectly united in the same mind and in the same judgement.
11 Kwani watu wa nyumba ya Kloe wamenitaarifu kuwa kuna mgawanyiko unaoendelea miongoni mwenu.
For I have been informed concerning you, my brethren, by some of Chloe's family, that there are contentions among you.
12 Nina maana hii: Kila mmoja wenu husema, “Mimi ni wa Paulo,” au “Mimi ni wa Apolo”, au “Mimi ni wa Kefa” au “Mimi ni wa Kristo”.
I mean, that each of you saith, as if of different parties, I am of Paul, and I of Apollos, I of Cephas, and I of Christ.
13 Je! Kristo amegawanyika? Je! Paulo alisulubiwa kwa ajili yenu? Je! Mlibatizwa kwa jina la Paulo?
Is Christ divided? was Paul crucified for you? or were ye baptized into the name of Paul?
14 Namshukuru Mungu kuwa sikumbatiza yeyote, isipokuwa Krispo na Gayo.
I thank God that I baptized none of you, except Crispus and Gaius:
15 Hii ilikuwa kwamba hakuna yeyote angesema mlibatizwa kwa jina langu.
so that no one can say I baptized in my own name.
16 (Pia niliwabatiza wa nyumba ya Stephania. Zaidi ya hapo, sijui kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote).
I also baptized indeed the family of Stephanas: but I know not whether I baptized any other.
17 Kwa kuwa, Kristo hakunituma kubatiza bali kuhubiri injili. Hakunituma kuhubiri kwa maneno ya hekima ya kibinadamu, ili kwamba nguvu ya msalaba wa Kristo isiondolewe.
For Christ sent me not to baptize, but to preach the gospel: not in fine speech, least the cross of Christ should be made of no effect.
18 Kwa kuwa ujumbe wa msalaba ni upuuzi kwa wale wanaokufa. Lakini kwa wale ambao Mungu anawaokoa, ni nguvu ya Mungu.
For the doctrine of the cross is to them, that perish, foolishness: but to us, who are saved, it is the power of God.
19 Kwa kuwa imeandikwa, “Nitaiharibu hekima ya wenye busara. Nitauharibu ufahamu wa wenye akili.”
For it is written, "I will destroy the wisdom of the wise, and will bring to nothing the understanding of the prudent."
20 Yuko wapi mtu mwenye busara? Yuko wapi mwenye elimu? Yuko wapi msemaji mshawishi wa dunia hii? Je, Mungu hakuigeuza hekima ya dunia hii kuwa ujinga? (aiōn )
Where is the wise? where is the scribe? where is the disputant of the age? hath not God made foolish the wisdom of this world? (aiōn )
21 Tangu dunia imekuwa katika hekima yake haikumjua Mungu, ilimpendeza Mungu katika ujinga wao wa kuhubiri ili kuokoa wale wanaoamini.
For, since in the wisdom of God the world by it's wisdom knew not God, it pleased God by what they called the folly of preaching to save those that believe.
22 Kwa Wayahudi huuliza ishara za miujiza na kwa Wayunani hutafuta hekima.
And whereas the Jews require a sign, and the Greeks look for wisdom, we preach Christ crucified;
23 Lakini tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa, aliye kikwazo kwa Wayahudi na ni ujinga kwa Wayunani.
to the Jews indeed a stumbling-block, and to the Greeks foolishness; but to them that are called,
24 Lakini kwa wale ambao waliitwa na Mungu, Wayahudi na Wayunani, tunamhubiri Kristo kama nguvu na hekima ya Mungu.
both Jews and Greeks, Christ the power of God and the wisdom of God.
25 Kwa kuwa ujinga wa Mungu una hekima kuliko ya wanadamu, na udhaifu wa Mungu una nguvu zaidi ya wanadamu.
Because the foolishness of God, as they call it, is wiser than men; and the weakness of God is stronger than men.
26 Angalia wito wa Mungu juu yenu, kaka na dada zangu. Si wengi wenu mlikuwa na hekima katika viwango vya kibinadamu. Si wengi wenu mlikuwa na nguvu. Si wengi wenu mlizaliwa katika ukuu.
For ye see by your calling, brethren, that not many wise men according to the flesh, not many mighty, not many noble are called:
27 Lakini Mungu alichagua vitu vijinga vya dunia ili kuviaibisha vyenye hekima. Mungu alichagua kilicho dhaifu katika dunia kukiaibisha chenye nguvu.
but God hath chosen things that are foolish in the eye of the world to put it's wise men to confusion; and God hath chosen the weak things of the world to confound the mighty;
28 Mungu alichagua kile kilicho cha hali ya chini na kilichodharauliwa katika dunia. Alichagua hata vitu ambavyo havikuhesabiwa kuwa kitu, kwa kuvifanya si kitu vitu vilivyo na thamani.
and things in the opinion of the world ignoble, and despicable, and accounted as nothing, hath God chosen, to abolish things that are in esteem among men;
29 Alifanya hivi ili asiwepo yeyote aliye na sababu ya kujivuna mbele zake.
that no flesh may glory in his presence.
30 Kwa sababu ya kile Mungu alichofanya, sasa mko ndani ya Kristo Yesu, ambaye amefanyika hekima kwa ajili yetu kutoka kwa Mungu. Alikuwa haki yetu, utakatifu na ukombozi.
But ye are of Him in Christ Jesus, who from God is made unto us wisdom, and righteousness, and sanctification, and redemption:
31 Kama matokeo, kama andiko lisemavyo, “Anayejisifu, ajisifu katika Bwana.”
that, as it is written, He that glorieth may glory in the Lord.