< 1 Wakorintho 1 >

1 Paulo, aliyeitwa na Kristo Yesu kuwa mtume kwa mapenzi ya Mungu, na Sosthene ndugu yetu,
Paul by vocacion an Apostle of Iesus Christ thorow the will of God and brother Sostenes.
2 kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, kwa wale ambao wamewekwa wakfu katika Yesu Kristo, ambao wameitwa kuwa watu watakatifu. Tunawaandikia pia wale wote wanaoliitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo katika mahali pote, Bwana wao na wetu.
Vnto the congregacion of God which is at Corinthum. To them that are sanctified in Christ Iesu sainctes by callynge with all that call on the name of oure lorde Iesus Christ in every place both of theirs and of oures
3 Neema na amani iwe kwenu kutoka kwa Mungu baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
Grace be with you and peace fro God oure father and from the lorde Iesus Christ.
4 Siku zote namshukru Mungu wangu kwa ajili yenu, kwa sababu ya neema ya Mungu ambayo Kristo Yesu aliwapa.
I thanke my God all wayes on youre behalfe for ye grace of God which is geuen you by Iesus Christ
5 Amewafanya kuwa matajiri katika kila njia, katika usemi na pamoja maarifa yote.
that in all thinges ve are made riche by him in all lerninge and in all knowledge
6 Amewafanya matajiri, kama ushuhuda kuhusu Kristo ya kwamba amethibitishwa kuwa kweli miongoni mwenu.
even as the testimony of Iesus Christ was confermed in you)
7 Kwa hiyo hampungukiwi karama za kiroho, kama mlivyo na hamu ya kusubiri ufunuo wa Bwana wetu Yesu Kristo.
so that ye are behynde in no gyft and wayte for the apperynge of oure lorde Iesus Christ
8 Atawaimarisha ninyi pia hadi mwisho, ili msilaumiwe siku ya Bwana wetu Yesu Kristo.
which shall streght you vnto ye ende that ye maye be blamelesse in ye daye of oure lorde Iesus Christ.
9 Mungu ni mwaminifu ambaye aliwaita ninyi katika ushirika wa mwana wake, Yesu Kristo Bwana wetu.
ffor god is faythfull by whom ye are called vnto ye fellishyppe of his sonne Iesus Christe oure lorde
10 Sasa nawasihi kaka na dada zangu, kupitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba wote mkubali, na kwamba kusiwe na migawanyiko miongoni mwenu. Nawasihi kwamba muungane pamoja katika nia moja na katika kusudi moja.
I beseche you brethre in ye name of oure lorde Iesus Christ that ye all speake one thynge and that there be no dissencion amoge you: but be ye knyt together in one mynde and in one meaynge.
11 Kwani watu wa nyumba ya Kloe wamenitaarifu kuwa kuna mgawanyiko unaoendelea miongoni mwenu.
It is shewed vnto me (my brethren) of you by them that are of the housse of Cloe that ther is stryfe amonge you. And this is it that I meane:
12 Nina maana hii: Kila mmoja wenu husema, “Mimi ni wa Paulo,” au “Mimi ni wa Apolo”, au “Mimi ni wa Kefa” au “Mimi ni wa Kristo”.
how that comelie amonge you one sayeth: I holde of Paul: another I holde of Apollo: ye thyrde I holde of Cephas: ye four ye I holde of Christ.
13 Je! Kristo amegawanyika? Je! Paulo alisulubiwa kwa ajili yenu? Je! Mlibatizwa kwa jina la Paulo?
Ys Christ devided? was Paul crucified for you? ether were ye baptised in ye name of Paul?
14 Namshukuru Mungu kuwa sikumbatiza yeyote, isipokuwa Krispo na Gayo.
I thanke God that I christened none of you but Crispus and Gayus
15 Hii ilikuwa kwamba hakuna yeyote angesema mlibatizwa kwa jina langu.
lest eny shulde saye that I had baptised in myne awne name.
16 (Pia niliwabatiza wa nyumba ya Stephania. Zaidi ya hapo, sijui kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote).
I baptised also the housse of Stephana. Forthermore knowe I not whether I baptised eny man or no.
17 Kwa kuwa, Kristo hakunituma kubatiza bali kuhubiri injili. Hakunituma kuhubiri kwa maneno ya hekima ya kibinadamu, ili kwamba nguvu ya msalaba wa Kristo isiondolewe.
For Christ sent me not to baptyse but to preache ye gospell not with wysdome of wordes lest the crosse of Christ shuld have bene made of none effecte.
18 Kwa kuwa ujumbe wa msalaba ni upuuzi kwa wale wanaokufa. Lakini kwa wale ambao Mungu anawaokoa, ni nguvu ya Mungu.
For ye preachinge of the crosse is to them yt perisshe folishnes: but vnto vs which are saved it is ye power of God.
19 Kwa kuwa imeandikwa, “Nitaiharibu hekima ya wenye busara. Nitauharibu ufahamu wa wenye akili.”
For it is written: I will destroye the wysdome of the wyse and will cast awaye the vnderstondinge of the prudet.
20 Yuko wapi mtu mwenye busara? Yuko wapi mwenye elimu? Yuko wapi msemaji mshawishi wa dunia hii? Je, Mungu hakuigeuza hekima ya dunia hii kuwa ujinga? (aiōn g165)
Where is the wyse? Where is the scrybe? Where is the searcher of this worlde? Hath not God made the wysdome of this worlde folisshnes? (aiōn g165)
21 Tangu dunia imekuwa katika hekima yake haikumjua Mungu, ilimpendeza Mungu katika ujinga wao wa kuhubiri ili kuokoa wale wanaoamini.
For when the worlde thorow wysdome knew not God in ye wysdome of God: it pleased God thorow folisshnes of preachinge to save them yt beleve.
22 Kwa Wayahudi huuliza ishara za miujiza na kwa Wayunani hutafuta hekima.
For ye Iewes requyre a signe and the Grekes seke after wysdome.
23 Lakini tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa, aliye kikwazo kwa Wayahudi na ni ujinga kwa Wayunani.
But we preache Christ crucified vnto the Iewes an occasion of fallinge and vnto the Grekes folisshnes:
24 Lakini kwa wale ambao waliitwa na Mungu, Wayahudi na Wayunani, tunamhubiri Kristo kama nguvu na hekima ya Mungu.
but vnto the which are called both of Iewes and Grekes we preache Christ ye power of God and the wysdome of God.
25 Kwa kuwa ujinga wa Mungu una hekima kuliko ya wanadamu, na udhaifu wa Mungu una nguvu zaidi ya wanadamu.
For the folishnes of God is wyser then me: and the weakenes of God is stronger then men.
26 Angalia wito wa Mungu juu yenu, kaka na dada zangu. Si wengi wenu mlikuwa na hekima katika viwango vya kibinadamu. Si wengi wenu mlikuwa na nguvu. Si wengi wenu mlizaliwa katika ukuu.
Brethren loke on youre callinge how that not many wyse men after the flesshe not many myghty not many of hye degre are called:
27 Lakini Mungu alichagua vitu vijinga vya dunia ili kuviaibisha vyenye hekima. Mungu alichagua kilicho dhaifu katika dunia kukiaibisha chenye nguvu.
but God hath chosen the folysshe thinges of the worlde to confounde the wyse. And God hath chosyn the weake thinges of the worlde to confounde thinges which are mighty.
28 Mungu alichagua kile kilicho cha hali ya chini na kilichodharauliwa katika dunia. Alichagua hata vitu ambavyo havikuhesabiwa kuwa kitu, kwa kuvifanya si kitu vitu vilivyo na thamani.
And vile thinges of the worlde and thinges which are despysed hath God chosen yee and thinges of no reputacion for to brynge to nought thinges of reputacion
29 Alifanya hivi ili asiwepo yeyote aliye na sababu ya kujivuna mbele zake.
that no flesshe shulde reioyce in his presence.
30 Kwa sababu ya kile Mungu alichofanya, sasa mko ndani ya Kristo Yesu, ambaye amefanyika hekima kwa ajili yetu kutoka kwa Mungu. Alikuwa haki yetu, utakatifu na ukombozi.
And vnto him partayne ye in Christ Iesu which of God is made vnto vs wysdome and also rightewesnes and saunctifyinge and redempcion.
31 Kama matokeo, kama andiko lisemavyo, “Anayejisifu, ajisifu katika Bwana.”
That accordinge as it is written: he which reioyseth shulde reioyce in the Lorde.

< 1 Wakorintho 1 >