< 1 Wakorintho 8 >

1 Sasa kuhusu vyakula vilivyotolewa sadaka kwa sanamu: tunajua ya kwamba “sisi sote tuna maarifa.” Maarifa huleta majivuno, bali upendo hujenga.
Now in regard to food which has been offered to idols, we are sure of course that "we all have knowledge." But knowledge puffs up, while love builds up.
2 Ikiwa mtu yeyote anadhani kwamba anajua jambo fulani, mtu huyo bado hajui kama impasavyo kujua.
If a man thinks that he already has knowledge, he does not yet truly know as he ought to know;
3 Lakini ikiwa mmoja wapo akimpenda Mungu, mtu huyo anajulikana naye.
but if a man loves God, he is known by him.
4 Basi kuhusu kula vyakula vilivyotolewa sadaka kwa sanamu: twajua kuwa “sanamu si kitu katika dunia hii,” na ya kuwa hakuna Mungu ila mmoja tu.”
Now as to eating food that has been offered to idols, we know well that an idol has no real existence in the universe, and that there is no God but One.
5 Kwa maana kuna wengi waitwao miungu ikiwa ni mbinguni au duniani, kama vile walivyo “miungu na mabwana wengi.”
For though there be so-called "gods," celestial of terrestrial, as indeed there are gods many and lords many,
6 “Ijapokuwa kwetu kuna Mungu mmoja tu ambaye ni Baba, vitu vyote vimetoka kwake, nasi tunaishi kwake, na Bwana mmoja Yesu Kristo, ambaye kwake vitu vyote vimekuwapo, na kwa yeye sisi tupo.”
yet for there is one God, the Father, from whom are all things, and we for him; and one Lord Jesus Christ, by whom are all things, and we by him.
7 Hata hivyo, ujuzi huu haupo ndani ya kila mmoja. Badala yake, wengine walishiriki ibada za sanamu hapo zamani, na hata sasa wanakula vyakula hivi kana kwamba ni kitu kilichotolewa sadaka kwa sanamu. Dhamiri zao zimepotoshwa kwa kuwa ni dhaifu.
But that "knowledge" is not possessed by all; but some, accustomed until now to the idol, eat food as that which has actually been offered to an idol, and so their conscience, being still weak, is defiled.
8 Lakini chakula hakitatuthibitisha sisi kwa Mungu. Sisi sio wabaya sana kama tusipo kula, wala wema sana ikiwa tutakula.
Now food does not bring us nearness to God. Neither if we eat do we gain any advantage, nor if we eat not, do we lose any.
9 Lakini iweni makini ya kwamba uhuru wenu usiwe sababu ya kumkwaza aliye dhaifu katika imani.
But see to it lest this right of yours become a stumbling-block to the weak.
10 Hebu fikiri kwamba mtu amekuona, wewe uliye na ujuzi, unakula chakula katika hekalu la sanamu. Dhamiri yake mtu huyo haitathibitika hata yeye naye ale vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu?
For if any one should see you, the possessor of "knowledge," reclining at table in an idol’s temple, would not his conscience, if he were weak, be emboldened to eat things sacrificed to idols?
11 Kwa hiyo kwa sababu ya ufahamu wako wa ukweli juu ya asili ya sanamu, kaka au dada yako aliye dhaifu, ambaye pia Kristo alikufa kwa ajili yake, anaangamizwa.
So he is lost, this weak man, lost by your "knowledge." this brother for whom Christ died.
12 Hivyo, unapofanya dhambi dhidi ya kaka na dada zako na kuzijeruhi dhamiri zao zilizo dhaifu, mnatenda dhambi dhidi ya Kristo.
In so sinning against your brothers, and in ever and again wounding their weak consciences, you are sinning against Christ.
13 Kwa hiyo, ikiwa chakula kinasababisha kumkwaza kaka au dada, sitakula nyama kamwe, ili nisimsababishe kaka au dada yangu kuanguka. (aiōn g165)
Therefore, if what I eat makes my brother to stumble, I will never eat meat again, lest I make my brother to stumble. (aiōn g165)

< 1 Wakorintho 8 >