< 1 Wakorintho 7 >
1 Kuhusu mambo mliyoniandikia: Kuna wakati ambapo ni vizuri mwanaume asilale na mke wake.
論到你們信上所寫的事,我認為男人不親近女人倒好。
2 Lakini kwa sababu ya majaribu mengi ya zinaa kila mwanaume awe na mkewe, na kila mwanamke awe na mmewe.
可是為了避免淫亂,男人當各有自己的妻子女人當各有自己的丈夫。
3 Mume anapaswa kumpa mke haki yake ya ndoa, na vile vile mke naye kwa mmewe.
丈夫對妻子該盡他應盡的義務,妻子對丈夫也如此。
4 Si mke aliye na mamlaka juu ya mwili wake, ni mme. Na vile vile, mme naye hana mamlaka juu ya mwili wake, bali mke anayo.
妻子對自己的身體沒有主權,而是丈夫有;同樣丈夫對自己的身體也沒有主權,而是妻子有。
5 Msinyimane mnapolala pamoja, isipokuwa mmekubaliana kwa muda maalum. Fanyeni hivyo ili kupata muda wa maombi. Kisha mnaweza kurudiana tena pamoja, Ili kwamba Shetani asije akawajaribu kwa kukosa kiasi.
你們切不要彼此虧負,除非兩相情願,暫時分房,為專務祈禱;但事後仍要歸到一處,免得撒殫因你們不能節制,而誘惑你們。
6 Lakini nasema haya mambo kwa hiari na si kama amri.
我說這話,原是出於寬容,並不是出於命令。
7 Natamani kila mmoja angekuwa kama mimi nilivyo. Lakini kila mmoja ana karama yake kutoka kwa Mungu. Huyu ana karama hii, na yule ana karama ile.
我本來願意眾人都如同我一樣,可是,每人都有他各自得自天主的恩寵:有人這樣,有人那樣。
8 Kwa wasioolewa na wajane ninasema kwamba, ni vizuri kwao kama wakibaki bila kuolewa, kama nilivyo mimi.
我對那些尚未結婚的人,特別對寡婦說:如果她們能止於現狀,像我一樣,為她們倒好。
9 Lakini kama hawawezi kujizuia, wanapaswa kuolewa. Kwa kuwa heri kwao kuolewa kuliko kuwaka tamaa.
但若她們節制不住,就讓她們婚嫁,因為與其慾火中燒,倒不如結婚為妙。
10 Sasa kwa wale walioolewa nawapa amri, si mimi bali ni Bwana. “Mke asitengane na mme wake.”
至於那些已經結婚的,我命令──其實不是我,而是主命令:妻子不可丈夫;
11 Lakini kama akijitenga kutoka kwa mmewe, abaki hivyo bila kuolewa au vinginevyo apatane na mmewe. Na “Mme asimpe talaka mke wake.”
若是離開了,就應該持身不嫁,或是仍與丈夫和好;丈夫也不可離棄妻子。
12 Lakini kwa waliobaki, nasema- mimi, si Bwana- kwamba kama ndugu yeyote ana mke asiyeamini na anaridhika kuishi naye, hapaswi kumwacha.
對其餘的人,是我說,而不是主說:倘若某弟兄有不信主的妻子,妻子也同意與他同居,就不應該離棄她;
13 Kama mwanamke ana mme asiyeamini, na kama anaridhika kuishi naye, asimwache.
倘若某婦人有不信主的丈夫,丈夫也同意與她同居,就不應該離棄丈夫,
14 Kwa mme asiyeamini anatakaswa kwa sababu ya imani ya mkewe. Na mwanamke asiyeamini anatakaswa kwa sababu ya mmewe aaminiye. Vinginevyo watoto wenu wangekuwa si safi, lakini kwa kweli wametakaswa.
因為不信主的丈夫因妻子而成了聖潔的,不信主的妻子也因口1而成了聖潔的;不然你們的兒女就是不潔的,其實他們卻是聖潔的。
15 Lakini mwenzi asiyeamini akiondoka na aende. Kwa namna hiyo, kaka au dada hafungwi na viapo vyao. Mungu ametuita tuishi kwa amani.
但若不信主的一方要離去,就由他離去;在這種情形之下,兄弟或姐妹不必受拘束,天主召叫了我們原是為平安。
16 Unajuaje kama mwanamke, huenda utamwokoa mmeo? Au unajuaje kama mwanaume, huenda utamwokoa mkeo?
因為妳這為妻子的,怎麼知道妳能救丈夫呢?或者,你這為丈夫的,怎麼知道你能救妻子呢?
17 Kila mmoja tu aishi maisha kama Bwana alivyowagawia, kila mmoja kama Mungu alivyowaita wao. Huu ni mwongozo wangu kwa makanisa yote.
此外,主怎麼分給了各人,天主怎樣召選了各人,各人就該怎樣生活下去:這原是我在各教會內所訓示的。
18 Yupo aliyekuwa ametahiriwa alipoitwa kuamini? Asijaribu kuondoa alama ya tohara yake. Yupo yeyote aliyeitwa katika imani hajatahiriwa? Hapaswi kutahiriwa.
有人受割損後蒙召的嗎?他就不該掩割損的記號;有人是未受割損蒙召的嗎?他就不該受割損。
19 Kwa hili aidha ametahiriwa wala asiye tahiriwa hakuna matatizo. Chenye matatizo ni kutii amri za Mungu.
受割損算不得什麼,不受割損也算不得什麼,只該遵持天主的誡命。
20 Kila mmoja abaki katika wito alivyokuwa alipoitwa na Mungu kuamini.
各人在什麼身份上蒙召,就該安於這身份。
21 Ulikuwa mtumwa wakati Mungu alipokuita? Usijali kuhusu hiyo. Lakini kama unaweza kuwa huru, fanya hivyo.
你是作奴隸蒙召的嗎?你不要介意,而且既使你們能成為自由人,你也寧要守住你原有的身份,
22 Kwa mmoja aliyeitwa na Bwana kama mtumwa ni mtu huru katika Bwana. Kama vile, mmoja aliye huru alipoitwa kuamini ni mtumwa wa Kristo.
因為作奴隸而在主內蒙召,就是主所釋放的人;同樣,那有自由而蒙召的人,就是基督的奴隸。
23 Mmekwisha nunuliwa kwa thamani, hivyo msiwe watumwa wa wanadamu.
你們是用高價買來的,切不要做人的奴隸。
24 Kaka na dada zangu, katika maisha yoyote kila mmoja wetu tulipoitwa kuamini, tubaki kama vile.
弟兄們,各人在什麼身份上蒙召,就在天主前安於這身份罷!
25 Sasa, wale wote ambao hawajaoa kamwe, sina amri kutoka kwa Bwana. Lakini nawapa maoni yangu kama nilivyo. Kwa huruma za Bwana, zinazo aminika
詮到童身的人,我沒有主的命令,只就我蒙主的仁慈,作為一個忠信的人,說出我的意見:
26 Kwa hiyo, ninafikiri hivyo kwa sababu ya usumbufu, ni vyema mwanaume abaki kama alivyo.
為了現時的急難,依我看來,為人這倒好。
27 Umefungwa kwa mwanamke na kiapo cha ndoa? Usitake uhuru kutoka kwa hiyo. Una uhuru kutoka kwa mke au hujaolewa? Usitafute mke.
你有妻子的束縳嗎?不要尋求解脫;你沒有妻子的束縳嗎?不要尋求妻屋。
28 Lakini kama ukioa, hujafanya dhambi. Na kama mwanamke hajolewa akiolewa, hajafanya dhambi. Bado wale wanaoana wanapata masumbufu ya aina mbalimbali. Nami nataka niwaepushe hayo.
但是你若娶妻,你並沒有犯罪,童女若出嫁,也沒有犯罪;不過這等人要遭受肉身上的痛苦。
29 Lakini nasema hivi, kaka na dada zangu, muda ni mfupi. Tangu sasa na kuendelea, wale walio na wake waishi kama hawana.
弟兄們,我給你們說:時間是很短促的,今後有妻子的,要像沒有一樣;
30 Wote walio na huzuni wajifanye kama walikuwa hawana huzuni, na wote wanaofurahi, kama walikuwa hawafurahi, na wote wanaonunua kitu chochote, kama hawakumiliki chochote.
哭泣的,要像不哭泣的一樣;歡樂的,要像不歡樂的;購買的,要像一無所得的;
31 Na wote wanaoshughulika na ulimwengu, wawe kama hawakushughulika nao. Kwa kuwa mitindo ya dunia inafikia mwisho wake.
享用這世界的,要像不享用的,因為這世界的局面正在逝去。
32 Ninataka muwe huru kwa masumbufu yote. Mwanaume asiyeoa anajihusisha na vitu vinavyo mhusu Bwana, namna ya kumpendeza yeye.
我願你們無所掛慮:沒有妻子的,所掛慮的是主的事,想怎樣悅樂主;
33 Lakini mwanaume aliyeoa hujihusisha na mambo ya dunia, namna ya kumpendeza mkewe,
娶了妻子的,所掛慮的是怎樣悅樂妻子:這樣他的心就分散了。
34 amegawanyika. Mwanawake asiyeolewa au bikira hujihusisha na vitu kuhusu Bwana, namna ya kujitenga katika mwili na katika roho. Lakini mwanamke aliyeolewa hujihusisha kuhusu vitu dunia, namna ya kumfurahisha mme wake.
沒有丈夫的婦女和童女,所掛慮的是主的事,一心使身心聖潔;至於已出嫁的,所掛慮的是世俗的事,想怎樣悅樂丈夫。
35 Nasema hivi kwa faida yenu wenyewe, na siweki mtego kwenu. Nasema hivi kwa vile ni haki, ili kwamba mnaweza kujiweka wakfu kwa Bwana bila kikwazo chochote.
我所這話,是為你們的益處,並不是要設下圈奪陷害你們,而只為叫你們更齊全,得以不斷地專心事主。
36 Lakini kama mtu anafikiri hawezi kumtendea kwa heshima mwanawali wake, kwa sababu ya hisia zake zina nguvu sana, acha aoane naye kama apendavyo. Siyo dhambi.
若有人以為對自己的童女待的不合宜,怕她過了韶華年齡,而事又在必行,他就可以隨意辦理,讓她們成新,不算犯罪。
37 Lakini kama amefanya maamuzi kutokuoa, na hakuna haja ya lazima, na kama anaweza kutawala hamu yake, atafanya vyema kama hatamwoa.
但是誰若心意堅定,沒有不得已的事,而又能隨自己的意願處置,這樣心裏決定了要保存自己的童女,的確做的好;
38 Hivyo, anayemwoa mwanamwali wake afanya vyema, na yeyote ambaye anachagua kutooa atafanya vyema zaidi.
所以誰若嫁叫自己的童女出嫁,作得好;誰若不叫她出嫁,作得更好。
39 Mwanamke amefungwa na mmewe wakati yu hai. Lakini kama mmewe akifa, yuko huru kuolewa na yeyote ampendaye, lakini katika Bwana tu.
丈夫活著的時候,妻子是被束縳的;但如果丈夫死了,她便自由了,可以隨意嫁人,只要是在主內的人。
40 Bado katika maamuzi yangu, atakuwa na furaha zaidi kama akiishi kama alivyo. Na ninafikiri kuwa nami pia nina Roho wa Mungu.
可是按我的意見,如果她仍能這樣守下去,她更為有福:我想我也有天主的聖神。