< 1 Wakorintho 4 >
1 Hivi ndivyo mtu atuhesabu sisi, kama watumishi wa Kristo na mawakili wa siri za kweli za Mungu.
Niech więc każdy uważa nas za sługi Chrystusa i szafarzy tajemnic Boga.
2 Katika hili, kinachotakiwa kwa uwakili ni kwamba wawe wa kutumainiwa.
A od szafarzy wymaga się, aby każdy [z nich] okazał się wierny.
3 Lakini kwangu mimi ni kitu kidogo sana kuwa ninahukumiwa na ninyi au hukumu ya kibinadamu. Kwa kuwa sijihukumu hata mimi mwenyewe.
Mnie jednak najmniej zależy na tym, czy będę przez was sądzony, czy przez sąd ludzki. Nawet sam siebie nie sądzę.
4 Sijihukumu mimi mwenyewe, hii haina maana kuwa mimi ni mwenye haki. Ni Bwana anihukumuye.
Niczego bowiem w sobie nie dostrzegam, jednak nie jestem przez to usprawiedliwiony, lecz tym, który mnie sądzi, jest Pan.
5 Kwa hiyo, msitamke hukumu juu ya lolote kabla ya wakati, kabla ya kuja kwa Bwana. Atayaleta nuruni mambo yaliyofichika gizani na kufunua makusudi ya mioyo. Ndipo kila mmoja atapokea sifa yake kutoka kwa Mungu.
Dlatego nie sądźcie przed czasem, dopóki nie przyjdzie Pan, który oświetli to, co ukryte w ciemności, i ujawni zamiary serc. Wtedy każdy otrzyma pochwałę od Boga.
6 Sasa, kaka na dada zangu, mimi mwenyewe na Apolo nimetumia kanuni hizi kwa ajili yenu. Ili kwamba kutoka kwetu mnaweza kujifunza maana ya usemi, “Usiende zaidi ya kilivyoandikwa.” Hii ni kwamba hakuna mmoja wenu ajivunaye juu ya mwingine.
To wszystko zaś, bracia, odniosłem do samego siebie i do Apollosa ze względu na was, abyście się nauczyli na naszym przykładzie nie wykraczać ponad to, co jest napisane, żeby jeden nie pysznił się drugim przeciw innemu.
7 Maana ni nani aonaye tofauti kati yenu na mwingine? Ni nini ulicho nacho hukukipokea bure? Kama umekwisha kupokea bure, kwa nini mnajivuna kama hamkufanya hivyo?
Kto bowiem czyni cię różnym? Cóż masz, czego byś nie otrzymał? A jeśli otrzymałeś, to dlaczego się chlubisz, jakbyś nie otrzymał?
8 Tayari mnavyo vyote ambavyo mngetaka! Tayari mmekuwa na utajiri! Mmeanza kutawala-na kwamba mnamiliki zaidi yetu sisi! Kweli, nawatakia umililki mwema ili kwamba tumiliki pamoja nanyi.
Już jesteście nasyceni, już jesteście bogaci, bez nas królujecie. I obyście królowali, abyśmy i my z wami królowali.
9 Kwa hiyo ninadhani Mungu ametuweka sisi mitume kama kutuonyesha wa mwisho katika mustari wa maandamano na kama watu waliohukumiwa kuuawa. Tumekuwa kama tamasha kwa ulimwengu, kwa malaika na kwa wanadamu.
Bo uważam, że Bóg nas, apostołów, wyznaczył jako ostatnich, jakby na śmierć skazanych. Staliśmy się bowiem widowiskiem dla świata, aniołów i ludzi.
10 Sisi ni wajinga kwa ajili ya Kristo, lakini ninyi ni wenye hekima katika Kristo. Tu wanyonge, lakini ninyi mna nguvu. Mnaheshimiwa, lakina sisi tunadharauliwa.
My jesteśmy głupi dla Chrystusa, ale wy mądrzy w Chrystusie, my jesteśmy słabi, ale wy mocni, wy szanowani, a my wzgardzeni.
11 Hata saa hii tuna njaa na kiu, hatuna nguo, tuna mapigo, na tena hatuna makazi.
Aż do tej chwili cierpimy głód i pragnienie, jesteśmy nadzy, policzkowani i tułamy się;
12 Tunafanya kazi kwa bidii, kwa mikono yetu wenyewe. Tunapodharauliwa, twabariki. Wakati tunapoteswa, twavumilia.
I trudzimy się, pracując własnymi rękami. Gdy nas znieważają – błogosławimy, gdy nas prześladują – znosimy;
13 Tunapotukanwa, twarudisha kwa upole. Tumekuwa, na tu bado tunahesabiwa kuwa kama kukataliwa na dunia na takataka kwa mambo yote.
Gdy nam złorzeczą – modlimy się [za nich]. Staliśmy się jak śmiecie tego świata, [jak] odpadki u wszystkich, aż do tej chwili.
14 Siandiki mambo haya kuwaaibisha ninyi, lakini kuwarudi ninyi kama watoto wangu niwapendao.
Nie piszę tego po to, aby was zawstydzić, ale napominam [was] jako moje umiłowane dzieci.
15 Hata kama mna waalimu makumi elfu katika Kristo, hamna baba wengi. Kwa kuwa nimekuwa baba yenu katika Yesu Kristo kupitia injili.
Choćbyście bowiem mieli dziesięć tysięcy wychowawców w Chrystusie, to jednak nie [macie] wielu ojców. Ja bowiem przez ewangelię zrodziłem was w Chrystusie Jezusie.
16 Hivyo ninawasihi mniige mimi.
Proszę was więc, bądźcie moimi naśladowcami.
17 Hiyo ndiyo sababu nilimtuma kwenu Timotheo, mpendwa wangu na mtoto mwaminifu katika Bwana. Atawakumbusheni njia zangu katika Kristo, kama ninavyofundisha kila mahali na kila kanisa.
Dlatego to posłałem do was Tymoteusza, który jest moim umiłowanym synem i wiernym w Panu. On wam przypomni moje drogi w Chrystusie, jak nauczam wszędzie, w każdym kościele.
18 Sasa baadhi yenu wanajisifu, wakitenda kana kwamba sitakuja kwenu.
A niektórzy wbili się w pychę, jakbym nie miał przyjść do was.
19 Lakini nitakuja kwenu kitambo, kama Bwana akipenda. Ndipo nitajua si maneno yao tu wanaojisifu, lakini nitaona nguvu zao.
Lecz przyjdę do was wkrótce, jeśli Pan zechce, i poznam nie słowa pysznych, ale [ich] moc.
20 Kwa kuwa ufalme wa Mungu hauwi katika maneno bali katika nguvu.
Królestwo Boże bowiem [przejawia się] nie w słowie, ale w mocy.
21 Mnataka nini? Nije kwenu na fimbo au kwa upendo na katika roho ya upole?
Co chcecie? Czy mam przyjść do was z rózgą, czy z miłością i w duchu łagodności?