< 1 Wakorintho 4 >

1 Hivi ndivyo mtu atuhesabu sisi, kama watumishi wa Kristo na mawakili wa siri za kweli za Mungu.
Thus let a man regard us as of helpers of Christ, and managers of mysteries of God.
2 Katika hili, kinachotakiwa kwa uwakili ni kwamba wawe wa kutumainiwa.
And beyond that, it is sought in managers that any man should be found faithful.
3 Lakini kwangu mimi ni kitu kidogo sana kuwa ninahukumiwa na ninyi au hukumu ya kibinadamu. Kwa kuwa sijihukumu hata mimi mwenyewe.
But it is a very small thing to me that I might be appraised by you or by a day of mankind. Yet neither do I appraise myself,
4 Sijihukumu mimi mwenyewe, hii haina maana kuwa mimi ni mwenye haki. Ni Bwana anihukumuye.
for I know nothing on myself. Yet I have not been made righteous in this, but he who appraises me is the Lord.
5 Kwa hiyo, msitamke hukumu juu ya lolote kabla ya wakati, kabla ya kuja kwa Bwana. Atayaleta nuruni mambo yaliyofichika gizani na kufunua makusudi ya mioyo. Ndipo kila mmoja atapokea sifa yake kutoka kwa Mungu.
Therefore do not judge anything before the time, until the Lord comes who will both bring to light the hidden things of darkness, and make public the deliberations of the hearts. And then praise will come to each man from God.
6 Sasa, kaka na dada zangu, mimi mwenyewe na Apolo nimetumia kanuni hizi kwa ajili yenu. Ili kwamba kutoka kwetu mnaweza kujifunza maana ya usemi, “Usiende zaidi ya kilivyoandikwa.” Hii ni kwamba hakuna mmoja wenu ajivunaye juu ya mwingine.
Now these things, brothers, I applied to myself and Apollos for your sakes, so that in us ye might learn not to think above that which is written, so that ye may not be puffed up, one over the one against the other.
7 Maana ni nani aonaye tofauti kati yenu na mwingine? Ni nini ulicho nacho hukukipokea bure? Kama umekwisha kupokea bure, kwa nini mnajivuna kama hamkufanya hivyo?
For who makes thee different? And what have thou that thou did not receive? And also if thou received it, why do thou boast as not having received it?
8 Tayari mnavyo vyote ambavyo mngetaka! Tayari mmekuwa na utajiri! Mmeanza kutawala-na kwamba mnamiliki zaidi yetu sisi! Kweli, nawatakia umililki mwema ili kwamba tumiliki pamoja nanyi.
Already ye are filled. Already ye have become rich. Ye reigned without us, and O that ye did indeed reign, so that we also might reign with you.
9 Kwa hiyo ninadhani Mungu ametuweka sisi mitume kama kutuonyesha wa mwisho katika mustari wa maandamano na kama watu waliohukumiwa kuuawa. Tumekuwa kama tamasha kwa ulimwengu, kwa malaika na kwa wanadamu.
For I think God has exhibited us the apostles least, as men sentenced to die, because we became a spectacle to the world, both to agents and to men.
10 Sisi ni wajinga kwa ajili ya Kristo, lakini ninyi ni wenye hekima katika Kristo. Tu wanyonge, lakini ninyi mna nguvu. Mnaheshimiwa, lakina sisi tunadharauliwa.
We are foolish for the sake of Christ, but ye are wise in Christ. We are weak, but ye are strong. Ye are esteemed, but we are disreputable.
11 Hata saa hii tuna njaa na kiu, hatuna nguo, tuna mapigo, na tena hatuna makazi.
As far as the present hour we both hunger, and thirst, and are ill clothed, and are treated roughly, and are homeless.
12 Tunafanya kazi kwa bidii, kwa mikono yetu wenyewe. Tunapodharauliwa, twabariki. Wakati tunapoteswa, twavumilia.
And we toil, working with our own hands. Being reviled, we bless; being persecuted, we endure;
13 Tunapotukanwa, twarudisha kwa upole. Tumekuwa, na tu bado tunahesabiwa kuwa kama kukataliwa na dunia na takataka kwa mambo yote.
being slandered, we entreat. We became as trash of the world, an offscouring of all things, until now.
14 Siandiki mambo haya kuwaaibisha ninyi, lakini kuwarudi ninyi kama watoto wangu niwapendao.
I do not write these things shaming you, but I warn you as my beloved children.
15 Hata kama mna waalimu makumi elfu katika Kristo, hamna baba wengi. Kwa kuwa nimekuwa baba yenu katika Yesu Kristo kupitia injili.
For though ye have countless instructors in Christ, yet not many fathers. For in Christ Jesus I begot you through the good news.
16 Hivyo ninawasihi mniige mimi.
I beseech you therefore, become followers of me.
17 Hiyo ndiyo sababu nilimtuma kwenu Timotheo, mpendwa wangu na mtoto mwaminifu katika Bwana. Atawakumbusheni njia zangu katika Kristo, kama ninavyofundisha kila mahali na kila kanisa.
Because of this I sent Timothy to you, who is my beloved and faithful child in the Lord, who will remind you of my ways in Christ, just as I teach everywhere in every congregation.
18 Sasa baadhi yenu wanajisifu, wakitenda kana kwamba sitakuja kwenu.
But as of me not coming to you, some men are puffed up.
19 Lakini nitakuja kwenu kitambo, kama Bwana akipenda. Ndipo nitajua si maneno yao tu wanaojisifu, lakini nitaona nguvu zao.
But I will come to you shortly, if the Lord should will, and I will know, not the word of those who are puffed up, but the power.
20 Kwa kuwa ufalme wa Mungu hauwi katika maneno bali katika nguvu.
For the kingdom of God is not in word, but in power.
21 Mnataka nini? Nije kwenu na fimbo au kwa upendo na katika roho ya upole?
What do ye want? Should I come to you with a rod, or in love and a spirit of meekness?

< 1 Wakorintho 4 >