< 1 Wakorintho 3 >

1 Na mimi, kaka na dada zangu, sikusema nanyi kama watu kiroho, lakini kama na watu wa kimwili. Kama na watoto wadogo katika Kristo.
Aussi, mes frères, je n’ai pu moi-même vous parler comme à des hommes spirituels, mais comme à des hommes charnels. Comme à de petits enfants en Jésus-Christ,
2 Niliwanywesha maziwa na si nyama, kwa kuwa hamkuwa tayari kwa kula nyama. Na hata sasa hamjawa tayari.
Je vous ai abreuvés de lait, mais je ne vous ai point donné à manger, parce que vous ne le pouviez pas encore; et à présent même, vous ne le pouvez point, parce que vous êtes encore charnels.
3 Kwa kuwa ninyi bado ni wa mwilini. Kwa kuwa wivu na majivuno yanaonekana miongoni mwenu. Je, hamuishi kulingana na mwili, na je, hamtembei kama kawaida ya kibinadamu?
Car, puisqu’il y a parmi vous jalousie et esprit de contention, n’êtes-vous pas charnels, et ne marchez-vous pas selon l’homme?
4 Kwa kuwa mmoja husema, “Namfuata Paulo” Mwingine husema “Namfuata Apolo,” hamuishi kama wanadamu?
En effet, puisque l’un dit: Moi je suis à Paul; et un autre: Moi à Apollo; n’êtes-vous pas des hommes? Qu’est donc Apollo? et qu’est Paul?
5 Apolo ni nani? na Paulo ni nani? Watumishi wa yule mliyemwamini, kwa kila ambaye Bwana alimpa jukumu.
Des ministres de celui en qui vous avez cru, et chacun l’est selon le don que le Seigneur lui a départi.
6 Mimi nilipanda, Apolo akatia maji, lakini Mungu akakuza.
Moi, j’ai planté, Apollo a arrosé; mais Dieu a donné la croissance.
7 Kwa hiyo, si aliye panda wala aliyetia maji ana chochote. Lakini ni Mungu anayekuza.
C’est pourquoi, ni celui qui plante n’est quelque chose, ni celui qui arrose; mais celui qui donne la croissance. Dieu.
8 Sasa apandaye na atiaye maji wote ni sawa, na kila mmoja atapokea ujira wake kulingana na kazi yake.
Or celui qui plante et celui qui arrose sont une seule chose. Mais chacun recevra son propre salaire selon son travail.
9 Kwa kuwa sisi tu watendakazi wa Mungu, ninyi ni bustani ya Mungu, jengo la Mungu.
Car nous sommes les coopérateurs de Dieu; vous êtes le champ que Dieu cultive, l’édifice que Dieu bâtit.
10 Kutokana na neema ya Mungu niliyopewa kama mjenzi mkuu, niliuweka msingi, na mwingine anajenga juu yake. Lakini mtu awe makini jinsi ajengavyo juu yake.
Selon la grâce que Dieu m’a donnée, j’ai, comme un sage architecte, posé le fondement, et un autre a bâti dessus. Que chacun donc regarde comment il y bâtira encore.
11 Kwa kuwa hakuna mwingine awezaye kujenga msingi mwingine zaidi ya uliojengwa, ambao ni Yesu Kristo.
Car personne ne peut poser d’autre fondement que celui qui a été posé, lequel est le Christ Jésus.
12 Sasa, kama mmoja wenu ajenga juu yake kwa dhahabu, fedha, mawe ya thamani, miti, nyasi, au majani,
Que si on élève sur ce fondement un édifice d’or, d’argent, de pierres précieuses, de bois, de foin, de chaume,
13 kazi yake itafunuliwa, kwa mwanga wa mchana utaidhihirisha. Kwa kuwa itadhihirishwa na moto. Moto utajaribu ubora wa kazi wa kila mmoja alichofanya.
L’ouvrage de chacun sera manifesté; car le jour du Seigneur le mettra en lumière, et il sera révélé par le feu; ainsi le feu éprouvera l’œuvre de chacun.
14 Kama chochote mtu alichojenga kitabaki, yeye atapokea zawadi.
Si l’ouvrage de celui qui a bâti sur le fondement demeure, celui-ci recevra son salaire.
15 Lakini kama kazi ya mtu ikiteketea kwa moto, atapata hasara. Lakini yeye mwenyewe ataokolewa, kama vile kuepuka katika moto.
Si l’œuvre de quelqu’un brûle, il en souffrira la perte; cependant il sera sauvé, mais comme par le feu.
16 Hamjui kuwa ninyi ni hekalu la Mungu na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
Ne savez-vous pas que vous êtes le temple de Dieu, et que l’Esprit de Dieu habite en vous?
17 Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu yule. Kwa kuwa hekalu la Mungu ni takatifu, na hivyo na ninyi.
Si donc quelqu’un profane le temple de Dieu, Dieu le perdra. Car le temple de Dieu est saint, et vous êtes ce temple.
18 Mtu asijidanganye mwenyewe, kama yeyote miongoni mwenu anadhani ana hekima katika nyakati hizi, awe kama “mjinga” ndipo atakuwa na hekima. (aiōn g165)
Que personne ne s’abuse: si quelqu’un d’entre vous paraît sage selon ce siècle, qu’il devienne fou pour être sage; (aiōn g165)
19 Kwa kuwa hekima ya dunia hii ni ujinga mbele za Mungu, Kwa kuwa imeandikwa, “Huwanasa wenye hekima kwa hila zao”
Attendu que la sagesse de ce siècle est folie devant Dieu. Car il est écrit: J’enlacerai les sages dans leurs propres ruses.
20 Na tena “Bwana anajua mawazo ya wenye busara ni ubatili.”
Et encore: Le Seigneur sait que les pensées des sages sont vaines.
21 Hivyo mtu asijivunie wanadamu! Kwa kuwa vitu vyote ni vyenu.
Que personne donc ne se glorifie dans les hommes.
22 Kama ni Paulo, au Apolo, au Kefa, au dunia, au maisha, au kifo, au vitu vilivyopo, au vitakavyokuwepo. Vyote ni vyenu,
Car tout est à vous, soit Paul, soit Apollo, soit Céphas, soit vie, soit mort, soit choses présentes, soit choses futures; oui, tout est à vous;
23 na ninyi ni wa Kristo na Kristo ni wa Mungu.
Mais vous au Christ, et le Christ à Dieu.

< 1 Wakorintho 3 >