< 1 Wakorintho 3 >
1 Na mimi, kaka na dada zangu, sikusema nanyi kama watu kiroho, lakini kama na watu wa kimwili. Kama na watoto wadogo katika Kristo.
Brothers, I could not address you as spiritual, but as worldly—as infants in Christ.
2 Niliwanywesha maziwa na si nyama, kwa kuwa hamkuwa tayari kwa kula nyama. Na hata sasa hamjawa tayari.
I gave you milk, not solid food, for you were not yet ready for solid food. In fact, you are still not ready,
3 Kwa kuwa ninyi bado ni wa mwilini. Kwa kuwa wivu na majivuno yanaonekana miongoni mwenu. Je, hamuishi kulingana na mwili, na je, hamtembei kama kawaida ya kibinadamu?
for you are still worldly. For since there is jealousy and dissension among you, are you not worldly? Are you not walking in the way of man?
4 Kwa kuwa mmoja husema, “Namfuata Paulo” Mwingine husema “Namfuata Apolo,” hamuishi kama wanadamu?
For when one of you says, “I follow Paul,” and another, “I follow Apollos,” are you not mere men?
5 Apolo ni nani? na Paulo ni nani? Watumishi wa yule mliyemwamini, kwa kila ambaye Bwana alimpa jukumu.
What then is Apollos? And what is Paul? They are servants through whom you believed, as the Lord has assigned to each his role.
6 Mimi nilipanda, Apolo akatia maji, lakini Mungu akakuza.
I planted the seed and Apollos watered it, but God made it grow.
7 Kwa hiyo, si aliye panda wala aliyetia maji ana chochote. Lakini ni Mungu anayekuza.
So neither he who plants nor he who waters is anything, but only God, who makes things grow.
8 Sasa apandaye na atiaye maji wote ni sawa, na kila mmoja atapokea ujira wake kulingana na kazi yake.
He who plants and he who waters are one in purpose, and each will be rewarded according to his own labor.
9 Kwa kuwa sisi tu watendakazi wa Mungu, ninyi ni bustani ya Mungu, jengo la Mungu.
For we are God’s fellow workers; you are God’s field, God’s building.
10 Kutokana na neema ya Mungu niliyopewa kama mjenzi mkuu, niliuweka msingi, na mwingine anajenga juu yake. Lakini mtu awe makini jinsi ajengavyo juu yake.
By the grace God has given me, I laid a foundation as an expert builder, and someone else is building on it. But each one must be careful how he builds.
11 Kwa kuwa hakuna mwingine awezaye kujenga msingi mwingine zaidi ya uliojengwa, ambao ni Yesu Kristo.
For no one can lay a foundation other than the one already laid, which is Jesus Christ.
12 Sasa, kama mmoja wenu ajenga juu yake kwa dhahabu, fedha, mawe ya thamani, miti, nyasi, au majani,
If anyone builds on this foundation using gold, silver, precious stones, wood, hay, or straw,
13 kazi yake itafunuliwa, kwa mwanga wa mchana utaidhihirisha. Kwa kuwa itadhihirishwa na moto. Moto utajaribu ubora wa kazi wa kila mmoja alichofanya.
his workmanship will be evident, because the Day will bring it to light. It will be revealed with fire, and the fire will prove the quality of each man’s work.
14 Kama chochote mtu alichojenga kitabaki, yeye atapokea zawadi.
If what he has built survives, he will receive a reward.
15 Lakini kama kazi ya mtu ikiteketea kwa moto, atapata hasara. Lakini yeye mwenyewe ataokolewa, kama vile kuepuka katika moto.
If it is burned up, he will suffer loss. He himself will be saved, but only as if through the flames.
16 Hamjui kuwa ninyi ni hekalu la Mungu na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
Do you not know that you yourselves are God’s temple, and that God’s Spirit dwells in you?
17 Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu yule. Kwa kuwa hekalu la Mungu ni takatifu, na hivyo na ninyi.
If anyone destroys God’s temple, God will destroy him; for God’s temple is holy, and you are that temple.
18 Mtu asijidanganye mwenyewe, kama yeyote miongoni mwenu anadhani ana hekima katika nyakati hizi, awe kama “mjinga” ndipo atakuwa na hekima. (aiōn )
Let no one deceive himself. If any of you thinks he is wise in this age, he should become a fool, so that he may become wise. (aiōn )
19 Kwa kuwa hekima ya dunia hii ni ujinga mbele za Mungu, Kwa kuwa imeandikwa, “Huwanasa wenye hekima kwa hila zao”
For the wisdom of this world is foolishness in God’s sight. As it is written: “He catches the wise in their craftiness.”
20 Na tena “Bwana anajua mawazo ya wenye busara ni ubatili.”
And again, “The Lord knows that the thoughts of the wise are futile.”
21 Hivyo mtu asijivunie wanadamu! Kwa kuwa vitu vyote ni vyenu.
Therefore, stop boasting in men. All things are yours,
22 Kama ni Paulo, au Apolo, au Kefa, au dunia, au maisha, au kifo, au vitu vilivyopo, au vitakavyokuwepo. Vyote ni vyenu,
whether Paul or Apollos or Cephas or the world or life or death or the present or the future. All of them belong to you,
23 na ninyi ni wa Kristo na Kristo ni wa Mungu.
and you belong to Christ, and Christ belongs to God.