< 1 Wakorintho 2 >
1 Nilipokuja kwenu kaka na dada zangu, sikuja kwa maneno ya ushawishi na hekima kama nilivyohubiri kweli iliyofichika kuhusu Mungu.
And I, brethren, when I came to you, came not with excellency of speech or of wisdom, declaring unto you the testimony of YHWH.
2 Niliamua kutojua chochote nilipokuwa miongoni mwenu isipokuwa Yesu Kristo, na yeye aliyesulubiwa.
For I determined not to know any thing among you, save Yahushua the Messiah, and him crucified.
3 Na nilikuwa nanyi katika udhaifu, na katika hofu, na katika kutetemeka sana.
And I was with you in weakness, and in fear, and in much trembling.
4 Na ujumbe wangu na kuhubiri kwangu hakukuwa katika maneno ya ushawishi na hekima. Badala yake, yalikuwa katika kumdhihirisha Roho na ya nguvu,
And my speech and my preaching was not with enticing words of man's wisdom, but in demonstration of the Spirit and of power:
5 ili kwamba imani yenu isiwe katika hekima ya wanadadamu, bali katika nguvu ya Mungu.
That your faith should not stand in the wisdom of men, but in the power of YHWH.
6 Sasa tunaizungumza hekima miongoni mwa watu wazima, lakini si hekima ya dunia hii, au ya watawala wa nyakati hizi, ambao wanaopita. (aiōn )
Howbeit we speak wisdom among them that are perfect: yet not the wisdom of this world, nor of the princes of this world, that come to nought: (aiōn )
7 Badala yake, tunaizungumza hekima ya Mungu katika ukweli uliofichika, hekima iliyofichika ambayo Mungu aliichagua kabla ya nyakati za utukufu wetu. (aiōn )
But we speak the wisdom of YHWH in a mystery, even the hidden wisdom, which YHWH ordained before the world unto our glory: (aiōn )
8 Hakuna yeyote wa watawala wa nyakati hizi aliyeijua hekima hii, Kama wangeifahamu katika nyakati zile, wasingelimsulubisha Bwana wa utukufu. (aiōn )
Which none of the princes of this world knew: for had they known it, they would not have crucified the King of glory. (aiōn )
9 Lakini kama ilivyoandikwa, “Mambo mbayo hakuna jicho limeyaona, hakuna sikio lililoyasikia, mawazo hayakufikiri, mambo ambayo Mungu ameyaandaa kwa ajili ya wale wampendao yeye.”
But as it is written, Eye hath not seen, nor ear heard, neither have entered into the heart of man, the things which Elohim hath prepared for them that love him.
10 Haya ni mambo ambayo Mungu ameyafunua kwetu kupitia Roho, Kwa kuwa Roho huchunguza kila kitu, hata mambo ya ndani ya Mungu.
But YHWH hath revealed them unto us by his Spirit: for the Spirit searcheth all things, yea, the deep things of YHWH.
11 Kwa kuwa nani afahamuye mawazo ya mtu, isipokuwa roho ya mtu ndani yake? Hivyo pia, hakuna ajuaye mambo ya ndani ya Mungu, isipokuwa Roho wa Mungu.
For what man knoweth the things of a man, save the spirit of man which is in him? even so the things of Elohim knoweth no man, but the Spirit of Elohim.
12 Lakini hatukupokea roho ya dunia, lakini Roho ambaye anatoka kwa Mungu, ili kwamba tuweze kujua kwa uhuru mambo tuliyopewa na Mungu.
Now we have received, not the spirit of the world, but the spirit which is of Elohim; that we might know the things that are freely given to us of YHWH.
13 Tunasema mambo haya kwa maneno, ambayo hekima ya mtu haiwezi kufundisha, lakini ambayo Roho hutufundisha. Roho hutafasiri maneno ya kiroho kwa hekima ya kiroho.
Which things also we speak, not in the words which man's wisdom teacheth, but which the Holy Spirit teacheth; comparing spiritual things with spiritual.
14 Mtu asiye wa kiroho hapokei mambo ambayo ni ya Roho wa Mungu, kwa kuwa hayo ni upuuzi kwake. Hawezi kuyajua kwa sababu yanatambuliwa kiroho.
But the natural man receiveth not the things of the Spirit of YHWH: for they are foolishness unto him: neither can he know them, because they are spiritually discerned.
15 Kwa yule wa kiroho huhukumu mambo yote. Lakini huhukumiwa na wengine.
But he that is spiritual judgeth all things, yet he himself is judged of no man.
16 “Ni nani anaweza kuyajua mawazo ya Bwana, ambaye anaweza kumfundisha yeye?” Lakini tuna mawazo ya Kristo.
For who hath known the mind of YHWH, that he may instruct him? But we have the mind of the Messiah.