< 1 Wakorintho 15 >
1 Sasa ninawakumbusha, akina kaka na akina dada, juu ya injili niliyowahubiria, ambayo mliipokea na kusimama kwayo.
Now I am calling to your remembrance, brothers, the gospel which I preached to you, which you also received, and on which you have taken your stand,
2 Ni katika injili hii mmeokolewa, kama mkilishika imara neno nililowahubiri ninyi, isipokuwa mliamini bure.
by which also you are saved, if you are holding fast the message which I preached to you; unless indeed you have believed in vain.
3 Kama kwanza nilivyo ipokea kwa umuhimu niliileta kwenu kama ilivyo: kwamba kutokana na maandiko, Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu,
For the very first thing I taught you was that I had myself been taught, that Christ died for our sins according to the Scripture,
4 kutokana na maandiko alizikwa, na kwamba alifufuka siku ya tatu.
that he was buried, and that he was raised the third day, according to the Scriptures,
5 Na kwamba alimtokea Kefa, kisha kwa wale kumi na wawili.
and was seen by Cephas, and then by the Twelve.
6 Kisha aliwatokea kwa wakati mmoja akina kaka na akina dada zaidi ya mia tano. Wengi wao bado wako hai, lakini baadhi yao wamelala usingizi.
Afterward he was seen at one time by more than five hundred brethren, most of whom are still alive, but some are fallen asleep.
7 Kisha alimtokea Yakobo, kisha mitume wote.
Then he was seen by James, then by all the apostles,
8 Mwisho wa yote, alinitokea mimi, kama vile kwa mtoto aliye zaliwa katika wakati usio sahihi.
and last of all, as by one born out of due time, he was seen by me also.
9 Kwa kuwa mimi ni mdogo kati ya mitume. Sistahili kuitwa mtume, kwa sababu nililitesa kanisa la Mungu.
For I am the least of the apostles, I who am not worthy to be called an apostle, because I persecuted the church of God.
10 Lakini kwa neema ya Mungu nipo kama nilivyo, na neema yake kwangu haikuwa bure. Badala yake, nilifanya bidii kuliko wote. Lakini haikuwa mimi, bali neema ya Mungu iliyo ndani yangu.
But by the grace of God I am what I am, and that grace of his, bestowed upon me, did not prove ineffectual. I labored more abundantly than all the rest, yet not I, but by the grace of God that is with me.
11 Kwa hiyo kama ni mimi au wao, tuna hubiri hivyo na tunaamini hivyo.
But whether it is I or they, thus do I preach, and thus you came to believe.
12 Sasa kama Kristo alihubiriwa kama aliyefufuka kwa wafu, iweje baadhi yenu mseme hakuna ufufuo wa wafu?
If then, we are preaching Christ, that he rose from the dead, how are some of you saying that there is no resurrection from the dead?
13 Lakini kama hakuna ufufuo wa wafu, basi hata Kristo pia hakufufuka.
But if there is no resurrection from the dead, then not even Christ has been raised;
14 Na kama Kristo hakufufuka, hivyo mahubiri yetu ni bure, na imani yenu ni bure.
and if Christ has not been raised, then our preaching is vain, and vain also is your faith.
15 Na tumepatikana kuwa mashahidi wa uongo kumuhusu Mungu, kwa sababu tulimshushuhudia Mungu kinyume, kusema alimfufua Kristo, wakati hakumfufua.
More than that, we are detected in bearing false witness against God; because we testified of God that he raised Christ from the dead, whom he did not raise, if indeed the dead rise not.
16 Kama ikiwa wafu hawafufuliwi, Yesu pia hakufufuliwa.
For if the dead rise not, neither has Christ arisen;
17 Na kama Kristo hakufufuliwa, imani yenu ni bure na bado mko kwenye dhambi zenu.
and if Christ be not risen, your faith is vain, you are still in your sins.
18 Hivyo hata wale waliokufa katika Kristo pia wameangamia.
More than that, those who are sleeping in Christ have perished.
19 Ikiwa kwa maisha haya peke yake tunaujasiri kwa wakati ujao ndani ya Kristo, watu wote, sisi niwakuhurumiwa zaidi ya watu wote.
If in this life only we have hope in Christ, we are of all mankind most pitiable.
20 Lakini sasa Kristo amefufuka kutoka kwa wafu, matunda ya kwanza ya wale waliokufa.
But now, now, Christ is risen from the dead, the first-fruit of those who have fallen asleep.
21 Kwa kuwa kifo kilikuja kupitia mwanadamu, pia kupitia mwanadamu ufufuo wa wafu.
For since by man came to death, by man came also the resurrection from the dead.
22 Kwa kuwa kama katika Adam wote wanakufa, hivyo pia katika Kristo wote watafanywa hai.
For just as in Adam all die, so also in Christ all will be made alive.
23 Lakini kila moja katika mpango wake: Kristo, matunda ya kwanza, na kisha wale walio wa Kristo watafanywa hai wakati wa kuja kwake.
But each in his own order; Christ the first-fruits, then those who belong to Christ at his appearing.
24 Ndipo utakuwa mwisho, pale Kristo atakapo kabidhi ufalme kwa Mungu Baba. Hii ni pale atakapo komesha utawala wote na mamlaka yote na nguvu.
And then the end, when he shall hand over his kingdom to God his Father, after he has abolished all rule and authority and power.
25 Kwa kuwa lazima atawale mpaka atakapoweka maadui zake wote chini ya nyayo zake.
For he must rule until he has put all his enemies under his feet.
26 Adui wa mwisho kuharibiwa ni kifo.
The last enemy that will be destroyed is Death.
27 Kwa kuwa “ameweka kila kitu chini ya nyayo zake.” Lakini inaposema “ameweka kila kitu,” ni wazi kwamba hii haihusishi wale walioweka kila kitu chini yake mwenyewe.
For He hast put all things under his feet, but in that quotation All things are put under him, it is evident that God is excepted, who put all things under Him.
28 Wakati vitu vyote vimewekwa chini yake, kisha Mwana mwenyewe atawekwa chini kwake Yeye ambaye aliviweka vitu vyote chini yake. Hii itatokea ili kwamba Mungu Baba awe yote katika vyote.
For when everything is subjected to him, then the Son himself shall subject himself to Him who made them subject, that God may be all in all.
29 Au pia watafanya nini wale waliobatizwa kwa ajili ya wafu? Kama wafu hawafufuliwi kabisa, kwa nini tena wanabatizwa kwa ajili yao?
Else what shall they do who are baptized for the dead? If the dead are really not raised, why are they baptized for them?
30 Na kwa nini tuko katika hatari kila saa?
Yes, and why am I myself exposed to danger every hour?
31 Kaka na dada zangu, kupitia kujisifu kwangu katika ninyi, ambayo ninayo katika Kristo Yesu Bwana wetu, natangaza hivi: nakufa kila siku.
Every day I am facing death, my brothers, I affirm it by that pride in you which I have through Christ Jesus our Lord.
32 Inanifaidia nini, katika mtazamo wa wanadamu, kama nilipigana na wanyama wakali huko Efeso, kama wafu hawafufuliwi? “Acha basi tule na kunywa, kwa kuwa kesho tunakufa.”
If after the manner of men I have fought with wild beasts at Ephesus, what good does it do me? If the dead do not rise, Let us eat and drink, For we shall be dead tomorrow.
33 Msidanganywe: “Makundi mabaya huharibu tabia njema.
Do not deceive yourselves. Evil companions ruin good morals.
34 “Muwe na kiasi! muishi katika haki! msiendelee kutenda dhambi. Kwa kuwa baadhi yenu hamna maarifa ya Mungu. Nasema hivi kwa aibu yenu.
Wake up, do justly, cease from sin; for I say to your shame that some of you have no acquaintance with God.
35 Lakini mtu mwingine atasema, “Jinsi gani wafu wanafufuliwa? Nao watakuja na aina gani ya mwili?”
But some one will ask. "How are the dead raised? and with what body are they coming?"
36 Wewe ni mjinga sana! Kile ulichopanda hakiwezi kuanza kukua isipokuwa kimekufa.
Foolish man! The seed you sow does not come to life unless it dies.
37 Na kile unachopanda sio mwili ambao utakuwa, bali ni mbegu iliyochipua. Inaweza kuwa ngano au kitu kingine.
And when you sow the seed you are not sowing the body that it will become, but bare grain, of wheat perhaps, or some other grain.
38 Lakini Mungu ataipa mwili kama apendavyo, na katika kila mbengu mwili wake mwenyewe.
But God gives it what body he pleases, and to each kind of seed its own body.
39 Miili yote haifanani. Isipokuwa, kuna mwili mmoja wa wanadamu, na mwili mwingine wa wanyama, na wili mwingine wa ndege, na mwingine kwa ajili ya samaki.
All flesh is not the same flesh; there is human flesh, another of fishes of animals, another of birds, another of fishes.
40 Pia kuna miili ya mbinguni na miili ya duniani. Lakini utukufu wa miili ya mbinguni ni aina moja na utukufu wa duniani ni mwingine.
There are both celestial bodies and bodies terrestrial; but the splendor of the celestial is one thing, and the splendor of the terrestrial is another.
41 Kuna utukufu mmoja wa jua, na utukufu mwingine wa mwezi, na utukufu mwingine wa nyota. Kwa kuwa nyota moja inatofautiana na nyota nyingine katika utukufu.
There is one glory of the sun, another of the moon, and another of the stars; for star differs from star in glory.
42 Hivyo ndivyo ulivyo pia ufufuo wa wafu. Kinacho pandwa kinaharibika, na kinacho ota hakiharibiki.
So it is in the resurrection of the dead. It is sown in corruption, It is raised in incorruption;
43 Kimepandwa katika matumizi ya kawaida, kinaoteshwa katika utukufu. Kimepandwa katika udhaifu, kinaoteshwa katika nguvu.
Sown in weakness, It is raised in power;
44 Kimepandwa katika mwili wa asili, kinaoteshwa katika mwili wa kiroho. Kama kuna mwili wa asili, kuna mwili wa kiroho pia.
The body sown is animal The body is raised is spiritual. If there is an animal body, there is also a spiritual body.
45 Hivyo pia imeandikwa, “Mtu wa kwanza Adamu alifanyika roho inayo ishi.” Adamu wa mwisho alifanyika roho itoayo uhai.
Thus it is written. The first man, Adam, became a living being, the last Adam, a life-giving Spirit.
46 Lakini wa kiroho hakuja kwanza bali wa asili, na kisha wa kiroho.
Now it is not the spiritual which is first, but the animal, and then the spiritual.
47 Mtu wa kwanza ni wa dunia, alitengenezwa kwa mavumbi. Mtu wa pili anatoka mbinguni.
The first man is of the earth, earthly; the second Man is of heaven.
48 Kama vile yule aliyetengenezwa kwa mavumbi, hivyo pia wale waliotengenezwa kwa mavumbi. Kama vile mtu wa mbinguni alivyo, hivyo pia wale wa mbinguni.
Like him who was of earth, are the earthy; and like Him who is of heaven, are the heavenly;
49 Kama ambavyo tumebeba mfano wa mtu wa mavumbi, tutabeba pia mfano wa mtu wa mbinguni.
As we have borne the likeness of him who was of earth, so also let us bear the likeness of Him who is of heaven.
50 Sasa nawaambia, kaka na dada zangu, kwamba mwili na damu haviwezi kuurithi ufalme wa Mungu. Wala wakuharibika kurithi wakutoharibika.
I tell you this, brothers, that flesh and blood cannot inherit the kingdom of God; nor can corruption inherit incorruption.
51 Tazama! Nawaambia ninyi siri ya kweli: Hatutakufa wote, bali wote tutabadilishwa.
Lo, I tell you a secret truth. we shall not all be sleeping, but we shall be changed,
52 Tutabadilishwa katika wakati, katika kufumba na kufumbua kwa jicho, katika tarumbeta ya mwisho. Kwa kuwa tarumbeta italia, na wafu watafufuliwa na hali ya kutoharibika, na tutabadilishwa.
in a moment, in the twinkling of an eye, when the last trumpet sounds. For the trumpet will sound, and the dead will be raised, incorruptible, and we shall be changed.
53 Kwani huu wa kuharibika lazima uvae wa kutoharibika, na huu wa kufa lazima uvae wa kutokufa.
For this corruptible must be clothed with incorruption, and this mortal must be clothed with immortality.
54 Lakini wakati huu wa kuharibika ukivikwa wa kutokuharibika, na huu wa kufa ukivaa wa kutokufa, ndipo utakuja msemo ambao umeandikwa, “Kifo kimemezwa katika ushindi.”
And when this mortal has been clothed with immortality, then will the words of Scripture come to pass, Death has been swallowed up in victory.
55 “Kifo, ushindi wako uko wapi? Kifo, uko wapi uchungu wako?” (Hadēs )
Where, Death, is thy victory? Where, Death, is thy sting? (Hadēs )
56 Uchungu wa kifo ni dhambi, na nguvu ya dhambi ni sheria.
Now the sting of death is sin, and the power of sin is the Law.
57 Lakini shukurani kwa Mungu, atupaye sisi ushindi kupitia Bwana wetu Yesu Kristo!
But thanks be to God, who has given us the victory through our Lord Jesus Christ.
58 Kwa hiyo, wapendwa kaka na dada zangu, iweni imara na msitikisike. Daima itendeni kazi ya Bwana, kwa sababu mnajua kuwa kazi yenu katika Bwana siyo bure.
So, my brothers beloved, stand firm, immovable, always abounding in work for the Lord, because you know that your toil is not fruitless in the Lord.