< 1 Wakorintho 15 >

1 Sasa ninawakumbusha, akina kaka na akina dada, juu ya injili niliyowahubiria, ambayo mliipokea na kusimama kwayo.
And, brothers, I make known to you the good news that I preached to you, which also ye received, and in which ye stand,
2 Ni katika injili hii mmeokolewa, kama mkilishika imara neno nililowahubiri ninyi, isipokuwa mliamini bure.
by which also ye are saved if ye hold firm that word I preached to you, unless ye believed in vain.
3 Kama kwanza nilivyo ipokea kwa umuhimu niliileta kwenu kama ilivyo: kwamba kutokana na maandiko, Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu,
For I delivered to you at first what I also received, that Christ died for our sins according to the scriptures,
4 kutokana na maandiko alizikwa, na kwamba alifufuka siku ya tatu.
and that he was buried, and that he arose on the third day according to the scriptures,
5 Na kwamba alimtokea Kefa, kisha kwa wale kumi na wawili.
and that he appeared to Cephas, then to the twelve.
6 Kisha aliwatokea kwa wakati mmoja akina kaka na akina dada zaidi ya mia tano. Wengi wao bado wako hai, lakini baadhi yao wamelala usingizi.
Then he appeared to over five hundred brothers at once, of whom the greater part remain until now, but some also slept.
7 Kisha alimtokea Yakobo, kisha mitume wote.
Then he appeared to James, then to all the apostles,
8 Mwisho wa yote, alinitokea mimi, kama vile kwa mtoto aliye zaliwa katika wakati usio sahihi.
and last of all, as to the untimely birth, he also appeared to me.
9 Kwa kuwa mimi ni mdogo kati ya mitume. Sistahili kuitwa mtume, kwa sababu nililitesa kanisa la Mungu.
For I am the least of the apostles, who am not worthy to be called an apostle, because I persecuted the church of God.
10 Lakini kwa neema ya Mungu nipo kama nilivyo, na neema yake kwangu haikuwa bure. Badala yake, nilifanya bidii kuliko wote. Lakini haikuwa mimi, bali neema ya Mungu iliyo ndani yangu.
But by the grace of God I am what I am. And his grace for me did not become empty, but I labored more abundantly than them all, yet not I, but the grace of God with me.
11 Kwa hiyo kama ni mimi au wao, tuna hubiri hivyo na tunaamini hivyo.
Therefore whether I or those men, so we proclaim, and so ye believed.
12 Sasa kama Kristo alihubiriwa kama aliyefufuka kwa wafu, iweje baadhi yenu mseme hakuna ufufuo wa wafu?
Now if Christ is proclaimed that he has risen from the dead, how say some among you that there is no resurrection of the dead?
13 Lakini kama hakuna ufufuo wa wafu, basi hata Kristo pia hakufufuka.
But if there is no resurrection of the dead, neither has Christ risen.
14 Na kama Kristo hakufufuka, hivyo mahubiri yetu ni bure, na imani yenu ni bure.
And if Christ has not risen, then our preaching is empty, and your faith is also empty.
15 Na tumepatikana kuwa mashahidi wa uongo kumuhusu Mungu, kwa sababu tulimshushuhudia Mungu kinyume, kusema alimfufua Kristo, wakati hakumfufua.
And also we are found false witnesses of God, because we witnessed according to God that he raised up the Christ, whom he did not raise up, if therefore the dead are really not raised.
16 Kama ikiwa wafu hawafufuliwi, Yesu pia hakufufuliwa.
For if the dead are not raised, neither has Christ been raised.
17 Na kama Kristo hakufufuliwa, imani yenu ni bure na bado mko kwenye dhambi zenu.
And if Christ has not been raised, your faith is vain. Ye are still in your sins.
18 Hivyo hata wale waliokufa katika Kristo pia wameangamia.
Then also those who slept in Christ have perished.
19 Ikiwa kwa maisha haya peke yake tunaujasiri kwa wakati ujao ndani ya Kristo, watu wote, sisi niwakuhurumiwa zaidi ya watu wote.
If we are men who have hoped in Christ in this life only, we are of all men more miserable.
20 Lakini sasa Kristo amefufuka kutoka kwa wafu, matunda ya kwanza ya wale waliokufa.
But now Christ has been raised from the dead. He became the first fruit of those who are asleep.
21 Kwa kuwa kifo kilikuja kupitia mwanadamu, pia kupitia mwanadamu ufufuo wa wafu.
For since death is because of a man, the resurrection of the dead is also because of a man.
22 Kwa kuwa kama katika Adam wote wanakufa, hivyo pia katika Kristo wote watafanywa hai.
For as by Adam all die, so also by Christ all will be made alive.
23 Lakini kila moja katika mpango wake: Kristo, matunda ya kwanza, na kisha wale walio wa Kristo watafanywa hai wakati wa kuja kwake.
But each in his own order. Christ the first fruit, then those of Christ at his coming.
24 Ndipo utakuwa mwisho, pale Kristo atakapo kabidhi ufalme kwa Mungu Baba. Hii ni pale atakapo komesha utawala wote na mamlaka yote na nguvu.
Afterwards the end, when he delivers up the kingdom to the God and Father, when he will abolish all rule, and all authority and power.
25 Kwa kuwa lazima atawale mpaka atakapoweka maadui zake wote chini ya nyayo zake.
For he must reign until he will put all his enemies under his feet.
26 Adui wa mwisho kuharibiwa ni kifo.
The last enemy abolished is death.
27 Kwa kuwa “ameweka kila kitu chini ya nyayo zake.” Lakini inaposema “ameweka kila kitu,” ni wazi kwamba hii haihusishi wale walioweka kila kitu chini yake mwenyewe.
For he subordinated all things under his feet. But when he says that all things have been subordinated, it is clear that he who subordinated all things under him, is excepted.
28 Wakati vitu vyote vimewekwa chini yake, kisha Mwana mwenyewe atawekwa chini kwake Yeye ambaye aliviweka vitu vyote chini yake. Hii itatokea ili kwamba Mungu Baba awe yote katika vyote.
And when all things are made subordinate to him, then the Son himself will also be made subordinate to him who subordinated all things to him, so that God may be all in all.
29 Au pia watafanya nini wale waliobatizwa kwa ajili ya wafu? Kama wafu hawafufuliwi kabisa, kwa nini tena wanabatizwa kwa ajili yao?
Otherwise what will they do who are immersed for the dead? If the dead do not rise at all, why then are they immersed for the dead?
30 Na kwa nini tuko katika hatari kila saa?
And we, why are we in peril every hour?
31 Kaka na dada zangu, kupitia kujisifu kwangu katika ninyi, ambayo ninayo katika Kristo Yesu Bwana wetu, natangaza hivi: nakufa kila siku.
By the pride that belongs to you, that I keep in Christ Jesus our Lord, I die daily.
32 Inanifaidia nini, katika mtazamo wa wanadamu, kama nilipigana na wanyama wakali huko Efeso, kama wafu hawafufuliwi? “Acha basi tule na kunywa, kwa kuwa kesho tunakufa.”
If in respect to men I fought with beasts at Ephesus, what is the benefit to me if the dead are not raised? Let us eat and drink, for tomorrow we die.
33 Msidanganywe: “Makundi mabaya huharibu tabia njema.
Be not led astray. Evil associations corrupt good habits.
34 “Muwe na kiasi! muishi katika haki! msiendelee kutenda dhambi. Kwa kuwa baadhi yenu hamna maarifa ya Mungu. Nasema hivi kwa aibu yenu.
Sober up rightly, and do not sin, for some have ignorance of God. I speak shame about you.
35 Lakini mtu mwingine atasema, “Jinsi gani wafu wanafufuliwa? Nao watakuja na aina gani ya mwili?”
But some man will say, How are the dead raised, and with what kind of body do they come?
36 Wewe ni mjinga sana! Kile ulichopanda hakiwezi kuanza kukua isipokuwa kimekufa.
Thou foolish man, what thou sow is not made alive unless it dies.
37 Na kile unachopanda sio mwili ambao utakuwa, bali ni mbegu iliyochipua. Inaweza kuwa ngano au kitu kingine.
And what thou sow, thou do not sow the body that it will become, but a bare grain, if it may happen of wheat, or of some other kind.
38 Lakini Mungu ataipa mwili kama apendavyo, na katika kila mbengu mwili wake mwenyewe.
But God gives it a body as he wills, and to each of the seeds its own body.
39 Miili yote haifanani. Isipokuwa, kuna mwili mmoja wa wanadamu, na mwili mwingine wa wanyama, na wili mwingine wa ndege, na mwingine kwa ajili ya samaki.
All flesh is not the same flesh, but one of men, and another flesh of beasts, and another of fishes, and another of birds,
40 Pia kuna miili ya mbinguni na miili ya duniani. Lakini utukufu wa miili ya mbinguni ni aina moja na utukufu wa duniani ni mwingine.
and heavenly bodies, and earthly bodies (but the glory of the heavenly is different, and the glory of the earthly is different),
41 Kuna utukufu mmoja wa jua, na utukufu mwingine wa mwezi, na utukufu mwingine wa nyota. Kwa kuwa nyota moja inatofautiana na nyota nyingine katika utukufu.
another glory is of the sun, and another glory of the moon, and another glory of the stars, for star differs from star in glory.
42 Hivyo ndivyo ulivyo pia ufufuo wa wafu. Kinacho pandwa kinaharibika, na kinacho ota hakiharibiki.
So also is the resurrection of the dead. It is sown in the perishable, it is raised in imperishability.
43 Kimepandwa katika matumizi ya kawaida, kinaoteshwa katika utukufu. Kimepandwa katika udhaifu, kinaoteshwa katika nguvu.
It is sown in dishonor, it is raised in glory. It is sown in weakness, it is raised in power.
44 Kimepandwa katika mwili wa asili, kinaoteshwa katika mwili wa kiroho. Kama kuna mwili wa asili, kuna mwili wa kiroho pia.
It is sown a natural body, it is raised a spiritual body. There is a natural body, and there is a spiritual body.
45 Hivyo pia imeandikwa, “Mtu wa kwanza Adamu alifanyika roho inayo ishi.” Adamu wa mwisho alifanyika roho itoayo uhai.
And so it is written, The first man Adam developed into a living soul. The last Adam a life giving spirit.
46 Lakini wa kiroho hakuja kwanza bali wa asili, na kisha wa kiroho.
Nevertheless the spiritual is not first, but the natural, then the spiritual.
47 Mtu wa kwanza ni wa dunia, alitengenezwa kwa mavumbi. Mtu wa pili anatoka mbinguni.
The first man was of the earth, earthly. The second man is the Lord from heaven.
48 Kama vile yule aliyetengenezwa kwa mavumbi, hivyo pia wale waliotengenezwa kwa mavumbi. Kama vile mtu wa mbinguni alivyo, hivyo pia wale wa mbinguni.
As is the earthly, such also are the earthly. And as is the heavenly, such also are the heavenly.
49 Kama ambavyo tumebeba mfano wa mtu wa mavumbi, tutabeba pia mfano wa mtu wa mbinguni.
And just as we have worn the form of the earthly, we will also wear the form of the heavenly.
50 Sasa nawaambia, kaka na dada zangu, kwamba mwili na damu haviwezi kuurithi ufalme wa Mungu. Wala wakuharibika kurithi wakutoharibika.
Now this I affirm, brothers, that flesh and blood cannot inherit the kingdom of God, nor does the perishable inherit imperishability.
51 Tazama! Nawaambia ninyi siri ya kweli: Hatutakufa wote, bali wote tutabadilishwa.
Behold, I tell you a mystery. We will actually not all sleep, but we will all be transformed,
52 Tutabadilishwa katika wakati, katika kufumba na kufumbua kwa jicho, katika tarumbeta ya mwisho. Kwa kuwa tarumbeta italia, na wafu watafufuliwa na hali ya kutoharibika, na tutabadilishwa.
in an instant, in the blink of an eye, at the last trumpet. For it will sound, and the dead will be raised imperishable, and we will be transformed.
53 Kwani huu wa kuharibika lazima uvae wa kutoharibika, na huu wa kufa lazima uvae wa kutokufa.
For this perishable must put on imperishability, and this mortal put on immortality.
54 Lakini wakati huu wa kuharibika ukivikwa wa kutokuharibika, na huu wa kufa ukivaa wa kutokufa, ndipo utakuja msemo ambao umeandikwa, “Kifo kimemezwa katika ushindi.”
But when this perishable will have put on imperishability, and this mortal will have put on immortality, then will come to pass the saying that is written, Death was swallowed up in victory.
55 “Kifo, ushindi wako uko wapi? Kifo, uko wapi uchungu wako?” (Hadēs g86)
O death, where is thy sting? O Hades, where is thy victory? (Hadēs g86)
56 Uchungu wa kifo ni dhambi, na nguvu ya dhambi ni sheria.
The sting of death is sin, and the power of sin is the law.
57 Lakini shukurani kwa Mungu, atupaye sisi ushindi kupitia Bwana wetu Yesu Kristo!
But thanks is to God who gives us the victory through our Lord Jesus Christ.
58 Kwa hiyo, wapendwa kaka na dada zangu, iweni imara na msitikisike. Daima itendeni kazi ya Bwana, kwa sababu mnajua kuwa kazi yenu katika Bwana siyo bure.
Therefore, my beloved brothers, become ye steadfast, unmovable, always abounding in the work of the Lord, knowing that your labor is not empty in the Lord.

< 1 Wakorintho 15 >