< 1 Wakorintho 14 >
1 Utafuteni upendo na kutamani sana karama za rohoni, zaidi sana mpate kutoa unabii.
Strive to possess love; and desire earnestly the spiritual gifts, but especially that of prophesying.
2 Maana yeye anenaye kwa lugha hasemi na watu bali husema na Mungu. Maana hakuna aelewaye kwa sababu anena mambo yaliyofichika katika Roho.
For he that speaketh in an [[unknown]] tongue speaketh not to men, but to God; for no one heareth; but in the Spirit he speaketh mysteries;
3 Lakini yeye atoaye unabii, asema na watu na kuwajenga, kuwatia moyo, na kuwafariji.
but he that prophesieth speaketh to men edification, and exhortation, and comfort.
4 Yeye anenaye kwa lugha hujijenga mwenyewe, lakini yeye atoaye unabii hulijenga kanisa.
He that speaketh in an [[unknown]] tongue edifieth himself; but he that prophesieth edifieth the church.
5 Sasa natamani kwamba ninyi nyote mnene kwa lugha. Lakini zaidi ya hayo, natamani ya kwamba mtoe unabii. Yeye atoaye unabii ni mkuu kuliko yeye anenaye kwa lugha (labda awepo wa kutafasiri), ili kwamba kanisa lipate kujengwa.
I would that ye all spoke with tongues, but rather that ye prophesied; for greater is he that prophesieth than he that speaketh with tongues, unless he interpret, that the church may receive edification.
6 Lakini sasa, kaka na dada zangu, nikija kwenu na kunena kwa lugha, nitawafaidia nini ninyi? Siwezi, isipokuwa nasema nanyi kwa njia ya ufunuo, au kwa njia ya maarifa, au unabii, au kwa njia ya fundisho.
But now, brethren, if I come to you speaking with tongues, what shall I profit you, unless I speak to you either by revelation, or by knowledge, or by prophesying, or by teaching?
7 Ikiwa vitu visivyo na uhai kama filimbi au kinubi visipotoa sauti zilizo na tofauti, itatambulikanaje ni chombo gani kinachezwa?
And even things without life that give sound, whether pipe or harp, if they make no distinction in the sounds, how shall that be known which is piped or harped?
8 Kwa maana ikiwa baragumu itatoa sauti isiyojulikana, ni jinsi gani mtu atatambua ya kuwa ni muda wa kujiandaa kwa vita?
For if the trumpet give an uncertain sound, who will prepare himself for the battle?
9 Vivyo hivyo na ninyi. Mkitoa kwa ulimi neno lisilo dhahiri, ni jinsi gani mtu ataelewa mnachosema? Mtakuwa mkiongea, na hakuna atakayewaelewa.
So also ye, unless ye utter by the tongue words easy to be understood, how shall that be known which is spoken? For ye will be speaking into the air.
10 Hakuna shaka kwamba kuna lugha nyingi mbalimbali duniani, na hakuna hata moja isiyo na maana.
There are, it may be, so many kinds of languages in the world, and not one is without meaning.
11 Lakini ikiwa sijui maana ya lugha, nitakuwa mgeni kwake yeye anenaye, naye anenaye atakuwa mgeni kwangu.
If then I know not the meaning of the language, I shall be to him that speaketh a foreigner, and he that speaketh a foreigner to me.
12 Vivyo hivyo na ninyi. Kwa kuwa mnatamani sana kuona uthihirisho wa Roho, takeni kwamba mzidi sana kulijenga kanisa.
So also ye, since ye are eager to possess spiritual gifts, be earnest to abound in them to the edification of the church.
13 Hivyo, yeye anenaye kwa lugha na aombe apewe kutafasiri.
Wherefore let him that speaketh in an [[unknown]] tongue pray that he may interpret.
14 Kwa maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina matunda.
For if I pray in an [[unknown]] tongue, my spirit prayeth, but my understanding is unfruitful.
15 Nifanye nini? Nitaomba kwa roho yangu, lakini pia nitaomba kwa akili zangu. Nitaimba kwa roho yangu, na nitaimba kwa akili zangu pia.
How stands it then? I will pray with the spirit, and I will pray with the understanding also; I will sing with the spirit, and I will sing with the understanding also.
16 Vinginevyo, ukimsifu Mungu kwa roho, yeye aliye mgeni ataitikaje “Amina” utoapo shukurani, akiwa hayajui usemayo?
Else, if thou bless with the spirit, how shall he that occupieth the place of the unlearned say the Amen at thy giving of thanks, since he understandeth not what thou art saying?
17 Maana ni kweli wewe washukuru vema, lakini yule mwingine hajengwi.
For thou indeed givest thanks well; but the other is not edified.
18 Namshukuru Mungu kwa kuwa nanena kwa lugha zaidi ya ninyi nyote.
I thank God, I speak in an [[unknown]] tongue more than ye all;
19 Lakini katika kanisa ni heri ninene maneno matano kwa ufahamu wangu ili nipate kuwafundisha wengine, zaidi ya kunena maneno kumi elfu kwa lugha.
yet in the church I would rather speak five words with my understanding, that I might also instruct others, than ten thousand words in an [[unknown]] tongue.
20 Kaka na dada zangu, msiwe watoto katika kufikiri kwenu. Badala yake, kuhusiana na uovu, iweni kama watoto wachanga. Lakini katika kufikiri kwenu mkawe watu wazima.
Brethren, do not become children in understanding; yet in malice be children, but in understanding be men.
21 Imeandikwa katika sheria, “Kwa watu wa lugha nyingine na kwa midomo ya wageni nitasema na watu hawa. Wala hata hivyo hawatanisikia,” asema Bwana.
In the Law it is written: “With men of other tongues and with other lips will I speak to this people,
22 Hivyo, ndimi ni ishara, sio kwa walioamini, bali kwa wasioamini. Lakini kutoa unabii ni ishara, sio kwa wasioamini, bali kwa ajili yao waaminio.
and yet for all that will they not hear me, saith the Lord.” Wherefore the tongues are for a sign, not to believers, but to unbelievers; but prophesying is not for unbelievers, but for believers.
23 Haya, ikiwa kanisa lote limekusanyika pamoja na wote wanene kwa lugha, na wageni na wasioamini wameingia, je hawawezi kusema kwamba mna wazimu?
If therefore the whole church be assembled in one place, and all be speaking with tongues, and there come in those who are unlearned, or unbelievers, will they not say that ye are mad?
24 Lakini ikiwa wote mnatoa unabii na asiyeamini au mgeni akaingia, atashawishiwa na yote asikiayo. Atahukumiwa na yote yasemwayo.
But if all prophesy, and there come in one that is an unbeliever, or unlearned, he is convinced by all, he is searched through by all,
25 Siri za moyo wake zingefunuliwa. Matokeo yake, angeanguka kifudifudi na kumwabudu Mungu. Angekiri ya kwamba Mungu yu kati yenu.
the secrets of his heart become manifest; and so falling down on his face, he will worship God, and report that God is indeed within you.
26 Nini kifuatacho basi, kaka na dada zangu? Mnapokutana pamoja, kila mmoja ana Zaburi, mafundisho, mafunuo, lugha au tafsiri. Fanyeni kila kitu ili kwamba mlijenge kanisa.
How is it then, brethren? When ye come together, every one of you hath a psalm, hath a lesson of instruction, hath a revelation, hath a tongue, hath an interpretation; let all things be done for edification.
27 Kama yeyote ananena kwa lugha, wawepo wawili au watatu, na kila mmoja katika zamu. Na mtu lazima atafasiri kilichosemwa.
If any one speak in an [[unknown]] tongue, let it be by two, or, at the most, by three, and in turn; and let one interpret.
28 Lakini kama hakuna mtu wa kutafasiri, basi kila mmoja wao akae kimya ndani ya kanisa. Basi kila mmoja aongee peke yake na kwa Mungu.
But if there be no interpreter, let him keep silence in the church; and let him speak to himself, and to God.
29 Na manabii wawili au watatu wanene, na wengine wasikilize kwa kupambanua kilichosemwa.
And of the prophets let two or three speak, and let the others judge;
30 Lakini aliyeketi akifunuliwa jambo katika huduma, yule ambaye alikuwa ananena na anyamaze.
if anything be revealed to another that sitteth by, let the first speaker be silent.
31 Kwa kuwa kila mmoja wenu anaweza kutoa unabii mmoja baada ya mwingine ili kwamba kila mmoja aweze kujifunza na wote waweze kutiwa moyo.
For one by one ye can all prophesy, that all may learn, and all may be exhorted.
32 Kwa kuwa roho za manabii ziko chini ya uangalizi wa manabii.
And spirits of prophets are subject to prophets;
33 Kwa kuwa Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani. Kama ilivyo katika makanisa yote ya waumini,
for God is not a God of confusion, but of peace. As in all the churches of the saints,
34 imewapasa wanawake wakae kimya katika kanisa. Kwa kuwa hawaruhusiwi kuzungumza. Badala yake, wanapaswa kuwa katika unyenyekevu, kama pia sheria inavyosema.
let your women keep silence in the churches; for it is not permitted them to speak, but they are to be in subjection, as also saith the Law.
35 Kama kuna chochote wanatamani kujifunza, basi wawaulize waume zao nyumbani. Kwa kuwa ni aibu kwa mwanamke kuongea katika kanisa.
And if they desire to learn anything, let them ask their own husbands at home; for it is a shame for a woman to speak in the church.
36 Je neno la Mungu lilitoka kwenu? Je limewafikia ninyi tu?
What! Did the word of God come forth from you? Or did it come to you alone?
37 Kama mtu akijiona kuwa ni nabii au wa rohoni, inampasa ayatambue mambo ninayowaandikia ya kwamba ni maagizo ya Bwana.
If any one thinketh himself to be a prophet, or spiritual, let him know surely that the directions I am writing to you are the Lord's;
38 Lakini asipotambua haya, mwacheni asitambuliwe.
but if any one be ignorant, let him be ignorant!
39 Hivyo basi, kaka na dada zangu, takeni sana kutoa unabii, na msimzuie mtu yeyote kunena kwa lugha.
Wherefore, brethren, desire earnestly to prophesy, and forbid not to speak with tongues;
40 Lakini mambo yote yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu.
but let all things be done becomingly, and in order.