< 1 Wakorintho 14 >

1 Utafuteni upendo na kutamani sana karama za rohoni, zaidi sana mpate kutoa unabii.
Follow after divine love; and seek the spiritual gifts, but rather that you may prophesy.
2 Maana yeye anenaye kwa lugha hasemi na watu bali husema na Mungu. Maana hakuna aelewaye kwa sababu anena mambo yaliyofichika katika Roho.
For the one speaking with a tongue speaks not to men, but to God; for no one hears him; but he speaks mysteries in the spirit:
3 Lakini yeye atoaye unabii, asema na watu na kuwajenga, kuwatia moyo, na kuwafariji.
but the one prophesying speaks to men edification, exhortation, and comfort.
4 Yeye anenaye kwa lugha hujijenga mwenyewe, lakini yeye atoaye unabii hulijenga kanisa.
The one speaking with a tongue edifies himself; but the one prophesying edifies the church.
5 Sasa natamani kwamba ninyi nyote mnene kwa lugha. Lakini zaidi ya hayo, natamani ya kwamba mtoe unabii. Yeye atoaye unabii ni mkuu kuliko yeye anenaye kwa lugha (labda awepo wa kutafasiri), ili kwamba kanisa lipate kujengwa.
But I wish you all to speak with tongues, but rather that you may prophesy: but greater is the one prophesying, than the one speaking with tongues, unless he may interpret, in order that the church may receive edification.
6 Lakini sasa, kaka na dada zangu, nikija kwenu na kunena kwa lugha, nitawafaidia nini ninyi? Siwezi, isipokuwa nasema nanyi kwa njia ya ufunuo, au kwa njia ya maarifa, au unabii, au kwa njia ya fundisho.
But now, brethren, if I may come unto you speaking with tongues, what shall I profit you, unless I shall speak to you either in revelation, or knowledge, or prophecy, or in instruction?
7 Ikiwa vitu visivyo na uhai kama filimbi au kinubi visipotoa sauti zilizo na tofauti, itatambulikanaje ni chombo gani kinachezwa?
Nevertheless things without life, giving forth a voice, whether pipe or harp, if it may not give a distinction to the sounds, how shall it be known what is piped, or what is harped?
8 Kwa maana ikiwa baragumu itatoa sauti isiyojulikana, ni jinsi gani mtu atatambua ya kuwa ni muda wa kujiandaa kwa vita?
For if indeed the trumpet may give an uncertain sound, who will prepare himself for the war?
9 Vivyo hivyo na ninyi. Mkitoa kwa ulimi neno lisilo dhahiri, ni jinsi gani mtu ataelewa mnachosema? Mtakuwa mkiongea, na hakuna atakayewaelewa.
Thus also if you through the tongue may give an indistinct word, how will that which is spoken be known? for you will be speaking into the air.
10 Hakuna shaka kwamba kuna lugha nyingi mbalimbali duniani, na hakuna hata moja isiyo na maana.
If it so happens that there are so many kinds of voices in the world, and nothing without a voice;
11 Lakini ikiwa sijui maana ya lugha, nitakuwa mgeni kwake yeye anenaye, naye anenaye atakuwa mgeni kwangu.
if then I do not understand the power of the voice, I will be a barbarian to the one speaking, and the one speaking will be a barbarian to me.
12 Vivyo hivyo na ninyi. Kwa kuwa mnatamani sana kuona uthihirisho wa Roho, takeni kwamba mzidi sana kulijenga kanisa.
So also you, since you are zealots of spirits, seek that you may abound unto the edification of the church.
13 Hivyo, yeye anenaye kwa lugha na aombe apewe kutafasiri.
Therefore let the one speaking with a tongue, pray that one may interpret.
14 Kwa maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina matunda.
For if I pray with a tongue, my spirit is praying, but my mind is not fruitful.
15 Nifanye nini? Nitaomba kwa roho yangu, lakini pia nitaomba kwa akili zangu. Nitaimba kwa roho yangu, na nitaimba kwa akili zangu pia.
Then what is it? I will pray with my spirit, and I will pray with my mind also: I will sing with my spirit, and I will sing with my mind also.
16 Vinginevyo, ukimsifu Mungu kwa roho, yeye aliye mgeni ataitikaje “Amina” utoapo shukurani, akiwa hayajui usemayo?
Since if you may bless with the spirit, how will one occupying the place of the unlearned say Amen to your blessing? since he does not know what you are saying.
17 Maana ni kweli wewe washukuru vema, lakini yule mwingine hajengwi.
For you indeed bless beautifully, but the other is not edified.
18 Namshukuru Mungu kwa kuwa nanena kwa lugha zaidi ya ninyi nyote.
I thank God, I speak with tongue more than you all:
19 Lakini katika kanisa ni heri ninene maneno matano kwa ufahamu wangu ili nipate kuwafundisha wengine, zaidi ya kunena maneno kumi elfu kwa lugha.
but I would rather speak five words in the church with my understanding, so that I may indeed teach others, than ten thousand words in a tongue.
20 Kaka na dada zangu, msiwe watoto katika kufikiri kwenu. Badala yake, kuhusiana na uovu, iweni kama watoto wachanga. Lakini katika kufikiri kwenu mkawe watu wazima.
Brethren, be not children in intellect: but be infants in evil, but be perfect in intellect.
21 Imeandikwa katika sheria, “Kwa watu wa lugha nyingine na kwa midomo ya wageni nitasema na watu hawa. Wala hata hivyo hawatanisikia,” asema Bwana.
It has been written in the law; I will speak to this people with other tongues and with the lips of others; and thus they will not hearken unto me, says the Lord.
22 Hivyo, ndimi ni ishara, sio kwa walioamini, bali kwa wasioamini. Lakini kutoa unabii ni ishara, sio kwa wasioamini, bali kwa ajili yao waaminio.
So tongues are for a sign, not to those who believe, but to the unbelievers: and prophecy is not for the unbelievers, but for the believers.
23 Haya, ikiwa kanisa lote limekusanyika pamoja na wote wanene kwa lugha, na wageni na wasioamini wameingia, je hawawezi kusema kwamba mna wazimu?
Then if the whole church may come together, and all may speak with tongues, and the unlearned or unbelievers may come in, will they not say that you are gone mad?
24 Lakini ikiwa wote mnatoa unabii na asiyeamini au mgeni akaingia, atashawishiwa na yote asikiayo. Atahukumiwa na yote yasemwayo.
But if all may prophesy, and some unbeliever or unlearned person may come in, he is convicted by all, he is discerned by all;
25 Siri za moyo wake zingefunuliwa. Matokeo yake, angeanguka kifudifudi na kumwabudu Mungu. Angekiri ya kwamba Mungu yu kati yenu.
the secrets of his heart are made manifest; and thus falling upon his face he will worship God, proclaiming that God is truly in you.
26 Nini kifuatacho basi, kaka na dada zangu? Mnapokutana pamoja, kila mmoja ana Zaburi, mafundisho, mafunuo, lugha au tafsiri. Fanyeni kila kitu ili kwamba mlijenge kanisa.
Then what is it, brethren? When you may come together, each one has a psalm, has a lesson, has a revelation, has a tongue, has an interpretation. Let all things be done to edification.
27 Kama yeyote ananena kwa lugha, wawepo wawili au watatu, na kila mmoja katika zamu. Na mtu lazima atafasiri kilichosemwa.
If one speaks with a tongue, let it he by twos, or at most by threes, and separately; and let one interpret;
28 Lakini kama hakuna mtu wa kutafasiri, basi kila mmoja wao akae kimya ndani ya kanisa. Basi kila mmoja aongee peke yake na kwa Mungu.
but if there may be no interpreter, let him keep silent in the church; but let him speak to himself, and to God.
29 Na manabii wawili au watatu wanene, na wengine wasikilize kwa kupambanua kilichosemwa.
But let two or three prophets speak, and let the others give audience;
30 Lakini aliyeketi akifunuliwa jambo katika huduma, yule ambaye alikuwa ananena na anyamaze.
but if something may be revealed to another sitting down, let the first be silent.
31 Kwa kuwa kila mmoja wenu anaweza kutoa unabii mmoja baada ya mwingine ili kwamba kila mmoja aweze kujifunza na wote waweze kutiwa moyo.
For you are all able to prophesy one by one, in order that all may learn, and all may be comforted.
32 Kwa kuwa roho za manabii ziko chini ya uangalizi wa manabii.
Truly the spirits of the prophets are subject to the prophets;
33 Kwa kuwa Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani. Kama ilivyo katika makanisa yote ya waumini,
for he is not a God of confusion, but of peace. So in all the churches of the saints,
34 imewapasa wanawake wakae kimya katika kanisa. Kwa kuwa hawaruhusiwi kuzungumza. Badala yake, wanapaswa kuwa katika unyenyekevu, kama pia sheria inavyosema.
let the women be silent in the churches: for it is not permitted to them to talk; but let them be subordinate, as the law also says.
35 Kama kuna chochote wanatamani kujifunza, basi wawaulize waume zao nyumbani. Kwa kuwa ni aibu kwa mwanamke kuongea katika kanisa.
But if they wish to learn something, let them ask their own husbands at home: for it is disgraceful for a woman to talk in church.
36 Je neno la Mungu lilitoka kwenu? Je limewafikia ninyi tu?
Whether did the word of God come out from you? or has it reached unto you alone?
37 Kama mtu akijiona kuwa ni nabii au wa rohoni, inampasa ayatambue mambo ninayowaandikia ya kwamba ni maagizo ya Bwana.
If any one seems to be a prophet, or spiritual, let him understand the things which I write to you, that they are of the Lord;
38 Lakini asipotambua haya, mwacheni asitambuliwe.
but if any one ignores, he is ignored.
39 Hivyo basi, kaka na dada zangu, takeni sana kutoa unabii, na msimzuie mtu yeyote kunena kwa lugha.
So, my brethren, be zealous to prophesy, and do not forbid to speak with tongues;
40 Lakini mambo yote yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu.
but let all things be done decently and in order.

< 1 Wakorintho 14 >