< 1 Wakorintho 12 >
1 Kuhusu karama za rohoni, kaka na dada zangu sitaki mkose kufahamu.
But concerning spiritual [manifestations], brethren, I do not wish you to be ignorant.
2 Mwajua ya kuwa mlipokuwa wapagani mliongozwa kufuata sanamu zisizoongea, kwa njia zozote mliongozwa nazo.
Ye know that when ye were [of the] nations [ye were] led away to dumb idols, in whatever way ye might be led.
3 Kwa hiyo, nataka mfahamu kwamba hakuna yeyote anenaye kwa Roho wa Mungu akisema, “Yesu amelaaniwa.” Hakuna yeyote atakayesema, “Yesu ni Bwana,” isipokuwa katika Roho Mtakatifu.
I give you therefore to know, that no one, speaking in [the power of the] Spirit of God, says, Curse [on] Jesus; and no one can say, Lord Jesus, unless in [the power of the] Holy Spirit.
4 Basi kuna karama tofauti tofauti, bali Roho ni yeye yule.
But there are distinctions of gifts, but the same Spirit;
5 Na kuna huduma tofauti tofauti, bali Bwana ni yeye yule.
and there are distinctions of services, and the same Lord;
6 Na kuna aina mbalimbali za kazi, lakini Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote.
and there are distinctions of operations, but the same God who operates all things in all.
7 Basi kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa faida ya wote.
But to each the manifestation of the Spirit is given for profit.
8 Maana mtu mmoja amepewa na Roho neno la hekima, na mwingine neno la maarifa kwa Roho yule yule.
For to one, by the Spirit, is given [the] word of wisdom; and to another [the] word of knowledge, according to the same Spirit;
9 Kwa mwingine humpa imani kwa Roho yeye yule, na kwa mwingine karama ya uponyaji kwa Roho mmoja.
and to a different one faith, in [the power of] the same Spirit; and to another gifts of healing in [the power of] the same Spirit;
10 Kwa mwingine matendo ya nguvu, na mwingine unabii. Na kwa mwingine uwezo wa kupambanua roho, mwingine aina mbalimbali za lugha, na kwa mwingnine tafsiri za lugha.
and to another operations of miracles; and to another prophecy; and to another discerning of spirits; and to a different one kinds of tongues; and to another interpretation of tongues.
11 Lakini Roho ni yule yule atendaye kazi hizi zote, kumpa kila mtu karama kwa kadiri ya uchaguzi wake mwenyewe.
But all these things operates the one and the same Spirit, dividing to each in particular according as he pleases.
12 Kwa maana kama vile mwili ni mmoja, nao una viungo vingi, na viungo vyote ni vya mwili ule ule, vivyo hivyo na Kristo.
For even as the body is one and has many members, but all the members of the body, being many, are one body, so also [is] the Christ.
13 Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi au Wayunani, kwamba tu watumwa au huru, na wote tulinyweshwa Roho mmoja.
For also in [the power of] one Spirit we have all been baptised into one body, whether Jews or Greeks, whether bondmen or free, and have all been given to drink of one Spirit.
14 Kwa maana mwili si kiungo kimoja, bali ni vingi.
For also the body is not one member but many.
15 Ikiwa mguu utasema, “kwa kuwa mimi si mkono, mimi si sehemu ya mwili,” hiyo haiufanyi kutokuwa sehemu ya mwili.
If the foot say, Because I am not a hand I am not of the body, is it on account of this not indeed of the body?
16 Na ikiwa sikio litasema, “kwa kuwa mimi si jicho, mimi si sehemu ya mwili,” hiyo hailifanyi kutokuwa sehemu ya mwili.
And if the ear say, Because I am not an eye I am not of the body, is it on account of this not indeed of the body?
17 Kama mwili wote utakuwa jicho, kungekuwa wapi kusikia? Kama mwili wote ukiwa sikio, kungekuwa wapi kunusa?
If the whole body [were] an eye, where the hearing? if all hearing, where the smelling?
18 Lakini Mungu aliweka kila kiungo cha mwili mahali pake kama alivyopanga mwenyewe.
But now God has set the members, each one of them in the body, according as it has pleased [him].
19 Na kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
But if all were one member, where the body?
20 Hivyo sasa viungo ni vingi, lakini mwili ni mmoja.
But now the members [are] many, and the body one.
21 Jicho haliwezi kuuambia mkono, “sina haja na wewe.” Wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu, sina haja na ninyi.”
The eye cannot say to the hand, I have not need of thee; or again, the head to the feet, I have not need of you.
22 Lakini viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa na heshima kidogo vyahitajika zaidi.
But much rather, the members of the body which seem to be weaker are necessary;
23 Na viungo vya mwili tunavyodhani vina heshima kidogo, twavipa heshima zaidi, na viungo vyetu visivyo na mvuto vina uzuri zaidi.
and those [parts] of the body which we esteem to be the more void of honour, these we clothe with more abundant honour; and our uncomely [parts] have more abundant comeliness;
24 Na sasa viungo vyetu vilivyo na mvuto havina haja ya kupewa heshima, kwa kuwa tayari vina heshima. Lakini Mungu ameviunganisha viungo vyote pamoja, na amevipa heshima zaidi vile visivyo heshimiwa.
but our comely [parts] have not need. But God has tempered the body together, having given more abundant honour to [the part] that lacked;
25 Alifanya hivyo ili pasiwepo mgawanyiko katika mwili, bali viungo vyote vitunzane kwa upendo wa mmoja.
that there might be no division in the body, but that the members might have the same concern one for another.
26 Na wakati kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote vyaumia kwa pamoja. Au wakati kiungo kimoja kikiheshimiwa, viungo vyote vifurahi kwa pamoja.
And if one member suffer, all the members suffer with [it]; and if one member be glorified, all the members rejoice with [it].
27 Sasa ninyi ni mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake.
Now ye are Christ's body, and members in particular.
28 Na Mungu ameweka katika kanisa kwanza mitume, pili manabii, tatu waalimu, kisha wale wote watendao matendo makuu, kisha karama za uponyaji, wale wasaidiao, wale wafanyao kazi ya kuongoza, na wote walio na aina mbalimbali za lugha.
And God has set certain in the assembly: first, apostles; secondly, prophets; thirdly, teachers; then miraculous powers; then gifts of healings; helps; governments; kinds of tongues.
29 Je sisi sote ni mitume? Sisi sote ni manabii? Sisi sote ni waalimu? Je sisi sote tunafanya matendo ya miujiza?
[Are] all apostles? [are] all prophets? [are] all teachers? [are] all [in possession of] miraculous powers?
30 Je sisi sote tuna karama ya uponyaji? Sisi sote tunaongea kwa lugha? Sisi sote tunatafsiri lugha?
have all gifts of healings? do all speak with tongues? do all interpret?
31 Tafuteni sana karama zilizo kuu. Nami nitawaonesha njia iliyo bora zaidi.
But desire earnestly the greater gifts, and yet shew I unto you a way of more surpassing excellence.