< 1 Wakorintho 10 >
1 Nataka ninyi mjue kaka na dada zangu, ya kuwa baba zetu walikuwa chini ya wingu na wote walipita katika bahari.
For I would not have you ignorant, brethren, that all our fathers were under the cloud, and all passed through the sea;
2 Wote walibatizwa wawe wa Musa ndani ya wingu na ndani ya bahari,
and all were baptised unto Moses in the cloud and in the sea;
3 na wote walikula chakula kile kile cha roho.
and all ate the same spiritual food,
4 Wote walikunywa kinywaji kile kile cha roho. Maana walikunywa kutoka katika mwamba wa roho uliowafuata, na mwamba ule ulikuwa ni Kristo.
and all drank the same spiritual drink, for they drank of a spiritual rock which followed [them]: (now the rock was the Christ; )
5 Lakini Mungu hakupendezwa sana na wengi wao, na maiti zao zilisambazwa jangwani.
yet God was not pleased with the most of them, for they were strewed in the desert.
6 Basi mambo haya yote yalikuwa mifano kwetu, ili sisi tusiwe watu wa kutamani mabaya kama na wao walivyofanya.
But these things happened [as] types of us, that we should not be lusters after evil things, as they also lusted.
7 Msiwe waabudu sanamu, kama wengine wao walivyokuwa. Hii ni kama ilivyoandikwa, “Watu walikaa chini wakila na kunywa, na waliinuka kucheza kwa tamaa za mapenzi.”
Neither be ye idolaters, as some of them; as it is written, The people sat down to eat and to drink, and rose up to play.
8 Tusifanye uasherati kama wengi wao walivyofanya. Wakafa siku moja watu ishirini na tatu elfu kwa sababu hiyo.
Neither let us commit fornication, as some of them committed fornication, and fell in one day three and twenty thousand.
9 Wala tusimjaribu Kristo, kama wengi wao walivyofanya na wakaharibiwa kwa nyoka.
Neither let us tempt the Christ, as some of them tempted, and perished by serpents.
10 Na pia msinung'unike, kama wengi wao walivyonung'unika na kuharibiwa na malaika wa mauti.
Neither murmur ye, as some of them murmured, and perished by the destroyer.
11 Basi mambo hayo yalitendeka kama mifano kwetu. Yakaandikwa ili kutuonya sisi - tuliofikiliwa na miisho ya zamani. (aiōn )
Now all these things happened to them [as] types, and have been written for our admonition, upon whom the ends of the ages are come. (aiōn )
12 Kwa hiyo kila ajionaye amesimama awe makini asije akaanguka.
So that let him that thinks that he stands take heed lest he fall.
13 Hakuna jaribu lililowapata ninyi lisilo kawaida ya wanadamu. Ila Mungu ni mwaminifu. Hatawaacha mjaribiwe kupita uwezo wenu. Pamoja na jaribu yeye atawapa mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.
No temptation has taken you but such as is according to man's nature; and God is faithful, who will not suffer you to be tempted above what ye are able [to bear], but will with the temptation make the issue also, so that [ye] should be able to bear [it].
14 Kwa hiyo, wapendwa wangu, ikimbieni ibada ya sanamu.
Wherefore, my beloved, flee from idolatry.
15 Nasema nanyi kama watu wenye akili, ili muamue juu ya ninalosema.
I speak as to intelligent [persons]: do ye judge what I say.
16 Kikombe cha baraka tubarikicho, si ushirika wa damu ya Kristo? Mkate ule tuumegao, si ushirika wa mwili wa Kristo?
The cup of blessing which we bless, is it not [the] communion of the blood of the Christ? The bread which we break, is it not [the] communion of the body of the Christ?
17 Kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja. Sisi sote twapokea mkate mmoja kwa pamoja.
Because we, [being] many, are one loaf, one body; for we all partake of that one loaf.
18 Watazameni watu wa Israeli: Je! Wale wote walao dhabihu si washiriki katika madhabahu?
See Israel according to flesh: are not they who eat the sacrifices in communion with the altar?
19 Nasema nini basi? Ya kuwa sanamu ni kitu? Au ya kuwa chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu ni kitu?
What then do I say? that what is sacrificed to an idol is anything, or that an idol is anything?
20 Lakini nasema juu ya vitu vile wavitoavyo sadaka watu wapagani wa Mataifa, ya kuwa wanatoa vitu hivi kwa mapepo na sio kwa Mungu. Nami sitaki ninyi kushirikiana na mapepo!
But that what [the nations] sacrifice they sacrifice to demons, and not to God. Now I do not wish you to be in communion with demons.
21 Hamwezi kunywea kikombe cha Bwana na kikombe cha mapepo. Hamwezi kuwa na ushirika katika meza ya Bwana na katika meza ya mapepo.
Ye cannot drink [the] Lord's cup, and [the] cup of demons: ye cannot partake of [the] Lord's table, and of [the] table of demons.
22 Au twamtia Bwana wivu? Tuna nguvu zaidi yake?
Do we provoke the Lord to jealousy? are we stronger than he?
23 “Vitu vyote ni halali,” lakini si vyote vifaavyo. “Vitu vyote ni halali,” lakini si vyote viwajengavyo watu.
All things are lawful, but all are not profitable; all things are lawful, but all do not edify.
24 Hakuna hata mmoja angetafuta mazuri yake tu. Badala yake, kila mmoja angetafuta mazuri ya mwenzake.
Let no one seek his own [advantage], but that of the other.
25 Mnaweza kula kila kitu kiuzwacho sokoni bila kuuliza -uliza kwa ajili ya dhamiri.
Everything sold in the shambles eat, making no inquiry for conscience sake.
26 Maana “dunia ni mali ya Bwana, na vyote viijazavyo.”
For the earth [is] the Lord's and its fulness.
27 Na mtu asiyeamini akiwaalika kula, na mnataka kwenda, kuleni chochote awapacho pasipo kuuliza maswali ya dhamiri.
But if any one of the unbelievers invite you, and ye are minded to go, all that is set before you eat, making no inquiry for conscience sake.
28 Lakini mtu akiwaambia, “Chakula hiki kimetokana na sadaka ya wapagani,” msile. Hii ni kwa ajili yake aliyewaambia, na kwa ajili ya dhamiri.
But if any one say to you, This is offered to holy purposes, do not eat, for his sake that pointed it out, and conscience sake;
29 Nami simaanishi dhamiri zenu, bali dhamiri ya yule mwingine. Maana kwanini uhuru wangu uhukumiwe na dhamiri ya mtu mwingine?
but conscience, I mean, not thine own, but that of the other: for why is my liberty judged by another conscience?
30 Ikiwa mimi natumia chakula kwa shukrani, kwanini nitukanwe kwa kitu ambacho nimeshukuru kwacho?
If I partake with thanksgiving, why am I spoken evil of for what I give thanks for?
31 Kwa hiyo, chochote mnachokula au kunywa, au chochote mfanyacho, fanyeni yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.
Whether therefore ye eat, or drink, or whatever ye do, do all things to God's glory.
32 Msiwakoseshe Wayahudi au Wayunani, au kanisa la Mungu.
Give no occasion to stumbling, whether to Jews, or Greeks, or the assembly of God.
33 Jaribuni kama mimi ninavyojaribu kuwapendeza watu wote kwa mambo yote. Sitafuti faida yangu mwenyewe, bali ya wengi. Nami nafanya hivi ili wapate kuokolewa.
Even as I also please all in all things; not seeking my own profit, but that of the many, that they may be saved.