< 1 Wakorintho 10 >

1 Nataka ninyi mjue kaka na dada zangu, ya kuwa baba zetu walikuwa chini ya wingu na wote walipita katika bahari.
But I want you not to be ignorant, brothers, that all our fathers were under the cloud, and all passed through the sea,
2 Wote walibatizwa wawe wa Musa ndani ya wingu na ndani ya bahari,
and all in Moses were immersed in the cloud and in the sea.
3 na wote walikula chakula kile kile cha roho.
And they all ate the same spiritual food,
4 Wote walikunywa kinywaji kile kile cha roho. Maana walikunywa kutoka katika mwamba wa roho uliowafuata, na mwamba ule ulikuwa ni Kristo.
and they all drank the same spiritual drink, for they drank from a spiritual rock that followed them. And the rock was the Christ.
5 Lakini Mungu hakupendezwa sana na wengi wao, na maiti zao zilisambazwa jangwani.
However with most of them God was not well pleased, for they were strewn in the wilderness.
6 Basi mambo haya yote yalikuwa mifano kwetu, ili sisi tusiwe watu wa kutamani mabaya kama na wao walivyofanya.
But these things became our examples, for us not to be men who lust for evil things as those also lusted.
7 Msiwe waabudu sanamu, kama wengine wao walivyokuwa. Hii ni kama ilivyoandikwa, “Watu walikaa chini wakila na kunywa, na waliinuka kucheza kwa tamaa za mapenzi.”
Neither become ye idolaters as some of them, as it is written, The people sat down to eat and drink, and rose up to revel.
8 Tusifanye uasherati kama wengi wao walivyofanya. Wakafa siku moja watu ishirini na tatu elfu kwa sababu hiyo.
Nor should we fornicate as some of them fornicated, and twenty-three thousand fell in one day.
9 Wala tusimjaribu Kristo, kama wengi wao walivyofanya na wakaharibiwa kwa nyoka.
Nor should we challenge the Christ as some of them also challenged, and were destroyed by the serpents.
10 Na pia msinung'unike, kama wengi wao walivyonung'unika na kuharibiwa na malaika wa mauti.
And ye should not grumble as some of them grumbled, and were destroyed by the destroyer.
11 Basi mambo hayo yalitendeka kama mifano kwetu. Yakaandikwa ili kutuonya sisi - tuliofikiliwa na miisho ya zamani. (aiōn g165)
Now all these things happened to those men for examples, and they were written for our admonition, to whom the ends of the ages came. (aiōn g165)
12 Kwa hiyo kila ajionaye amesimama awe makini asije akaanguka.
Therefore let him who seems to stand take heed lest he fall.
13 Hakuna jaribu lililowapata ninyi lisilo kawaida ya wanadamu. Ila Mungu ni mwaminifu. Hatawaacha mjaribiwe kupita uwezo wenu. Pamoja na jaribu yeye atawapa mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.
No temptation has taken you except is common to man. But God is faithful who will not allow you to be tempted above what ye are able, but with the temptation will also make the way to escape, to enable you to endure.
14 Kwa hiyo, wapendwa wangu, ikimbieni ibada ya sanamu.
Therefore, my beloved, flee from idolatry.
15 Nasema nanyi kama watu wenye akili, ili muamue juu ya ninalosema.
I speak as to wise men, judge ye what I say.
16 Kikombe cha baraka tubarikicho, si ushirika wa damu ya Kristo? Mkate ule tuumegao, si ushirika wa mwili wa Kristo?
The cup of the blessing that we bless, is it not a participation of the blood of the Christ? The bread that we break, is it not a participation of the body of the Christ?
17 Kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja. Sisi sote twapokea mkate mmoja kwa pamoja.
Because we, the many, are one bread, one body, for we are all partakers of the one bread.
18 Watazameni watu wa Israeli: Je! Wale wote walao dhabihu si washiriki katika madhabahu?
Look at Israel according to flesh. Those who eat the sacrifices, are they not partakers of the altar?
19 Nasema nini basi? Ya kuwa sanamu ni kitu? Au ya kuwa chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu ni kitu?
What therefore do I say, that an idol is anything, or that a sacrifice to an idol is anything?
20 Lakini nasema juu ya vitu vile wavitoavyo sadaka watu wapagani wa Mataifa, ya kuwa wanatoa vitu hivi kwa mapepo na sio kwa Mungu. Nami sitaki ninyi kushirikiana na mapepo!
Rather, that which the Gentiles sacrifice, they sacrifice to demons and not to God, and I do not want you to become partakers of demons.
21 Hamwezi kunywea kikombe cha Bwana na kikombe cha mapepo. Hamwezi kuwa na ushirika katika meza ya Bwana na katika meza ya mapepo.
Ye cannot drink the cup of the Lord, and the cup of demons. Ye cannot be partakers of a table of the Lord, and of a table of demons.
22 Au twamtia Bwana wivu? Tuna nguvu zaidi yake?
Or do we provoke the Lord to jealousy? Are we stronger than he?
23 “Vitu vyote ni halali,” lakini si vyote vifaavyo. “Vitu vyote ni halali,” lakini si vyote viwajengavyo watu.
All things are permitted for me, but not all things are expedient. All things are permitted for me, but not all things are constructive.
24 Hakuna hata mmoja angetafuta mazuri yake tu. Badala yake, kila mmoja angetafuta mazuri ya mwenzake.
Let not one man seek that of himself, but each man that of the other.
25 Mnaweza kula kila kitu kiuzwacho sokoni bila kuuliza -uliza kwa ajili ya dhamiri.
Eat everything being sold in a meat market, inquiring of nothing because of the conscience,
26 Maana “dunia ni mali ya Bwana, na vyote viijazavyo.”
for the earth is the Lord's, and the fullness of it.
27 Na mtu asiyeamini akiwaalika kula, na mnataka kwenda, kuleni chochote awapacho pasipo kuuliza maswali ya dhamiri.
If any of those unbelievers invites you, and ye want to go, eat everything being set before you, inquiring of nothing because of the conscience.
28 Lakini mtu akiwaambia, “Chakula hiki kimetokana na sadaka ya wapagani,” msile. Hii ni kwa ajili yake aliyewaambia, na kwa ajili ya dhamiri.
But if any man says to you, This is a sacrifice to an idol, do not eat for the sake of that man who informed, and the conscience, for the earth is the Lord's, and the fullness of it.
29 Nami simaanishi dhamiri zenu, bali dhamiri ya yule mwingine. Maana kwanini uhuru wangu uhukumiwe na dhamiri ya mtu mwingine?
And I say conscience, not the one of himself, but the one of the other man. For why is my liberty judged by another conscience?
30 Ikiwa mimi natumia chakula kwa shukrani, kwanini nitukanwe kwa kitu ambacho nimeshukuru kwacho?
If I partake with thankfulness, why am I maligned about which I express thanks?
31 Kwa hiyo, chochote mnachokula au kunywa, au chochote mfanyacho, fanyeni yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.
Therefore whether ye eat, or drink, or anything ye do, do all to the glory of God.
32 Msiwakoseshe Wayahudi au Wayunani, au kanisa la Mungu.
Become ye inoffensive both to Jews and to Greeks, and to the church of God,
33 Jaribuni kama mimi ninavyojaribu kuwapendeza watu wote kwa mambo yote. Sitafuti faida yangu mwenyewe, bali ya wengi. Nami nafanya hivi ili wapate kuokolewa.
just as I also strive to please in all things for all men, not seeking my own advantage, but that of the many, so that they may be saved.

< 1 Wakorintho 10 >