< 1 Wakorintho 1 >
1 Paulo, aliyeitwa na Kristo Yesu kuwa mtume kwa mapenzi ya Mungu, na Sosthene ndugu yetu,
Pavel, poklican, da je po Božji volji apostol Jezusa Kristusa in naš brat Sostén,
2 kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, kwa wale ambao wamewekwa wakfu katika Yesu Kristo, ambao wameitwa kuwa watu watakatifu. Tunawaandikia pia wale wote wanaoliitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo katika mahali pote, Bwana wao na wetu.
Božji cerkvi, ki je v Korintu, tem, ki so posvečeni v Kristusu Jezusu, poklicani, da so sveti, z vsemi, ki na vsakem kraju, tako njihovem kakor našem, kličejo ime Jezusa Kristusa, našega Gospoda:
3 Neema na amani iwe kwenu kutoka kwa Mungu baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
›Milost bodi vam in mir od Boga, našega Očeta in od Gospoda Jezusa Kristusa.‹
4 Siku zote namshukru Mungu wangu kwa ajili yenu, kwa sababu ya neema ya Mungu ambayo Kristo Yesu aliwapa.
Vedno se vam v prid zahvaljujem svojemu Bogu za Božjo milost, ki vam je dana po Jezusu Kristusu,
5 Amewafanya kuwa matajiri katika kila njia, katika usemi na pamoja maarifa yote.
da ste v vsaki stvari obogateni po njem, v vsej izgovarjavi in v vsem spoznanju;
6 Amewafanya matajiri, kama ushuhuda kuhusu Kristo ya kwamba amethibitishwa kuwa kweli miongoni mwenu.
celó kakor je bilo Kristusovo pričevanje potrjeno v vas,
7 Kwa hiyo hampungukiwi karama za kiroho, kama mlivyo na hamu ya kusubiri ufunuo wa Bwana wetu Yesu Kristo.
tako da vam, ki pričakujete prihod našega Gospoda Jezusa Kristusa, ne primanjkuje nobenega daru;
8 Atawaimarisha ninyi pia hadi mwisho, ili msilaumiwe siku ya Bwana wetu Yesu Kristo.
ki vas bo tudi do konca potrdil, da boste lahko brez krivde na dan našega Gospoda Jezusa Kristusa.
9 Mungu ni mwaminifu ambaye aliwaita ninyi katika ushirika wa mwana wake, Yesu Kristo Bwana wetu.
Bog je zvest, po katerem ste bili poklicani v družbo njegovega Sina Jezusa Kristusa, našega Gospoda.
10 Sasa nawasihi kaka na dada zangu, kupitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba wote mkubali, na kwamba kusiwe na migawanyiko miongoni mwenu. Nawasihi kwamba muungane pamoja katika nia moja na katika kusudi moja.
Torej vas rotim, bratje, v imenu našega Gospoda Jezusa Kristusa, da vsi govorite isto stvar in da med vami ne bo nobenih nesoglasij; temveč da boste popolnoma združeni skupaj, v istem mišljenju in v isti sodbi.
11 Kwani watu wa nyumba ya Kloe wamenitaarifu kuwa kuna mgawanyiko unaoendelea miongoni mwenu.
Kajti razodeto mi je bilo o vas, moji bratje, po teh, ki so iz Hloine hiše, da so med vami prepiri.
12 Nina maana hii: Kila mmoja wenu husema, “Mimi ni wa Paulo,” au “Mimi ni wa Apolo”, au “Mimi ni wa Kefa” au “Mimi ni wa Kristo”.
Pravim torej to, da vsak izmed vas govori: »Jaz sem Pavlov, jaz Apolov, jaz Kefov, jaz pa Kristusov.«
13 Je! Kristo amegawanyika? Je! Paulo alisulubiwa kwa ajili yenu? Je! Mlibatizwa kwa jina la Paulo?
Ali je Kristus razdeljen? Ali je bil Pavel križan za vas? Ali ste bili krščeni v Pavlovo ime?
14 Namshukuru Mungu kuwa sikumbatiza yeyote, isipokuwa Krispo na Gayo.
Zahvaljujem se Bogu, da nisem krstil nobenega izmed vas razen Krispa in Gaja,
15 Hii ilikuwa kwamba hakuna yeyote angesema mlibatizwa kwa jina langu.
da ne bi kdorkoli lahko rekel, da sem krščeval v svojem lastnem imenu.
16 (Pia niliwabatiza wa nyumba ya Stephania. Zaidi ya hapo, sijui kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote).
In krstil sem tudi Stefanájevo družino; razen tega ne vem, če sem krstil kogarkoli drugega.
17 Kwa kuwa, Kristo hakunituma kubatiza bali kuhubiri injili. Hakunituma kuhubiri kwa maneno ya hekima ya kibinadamu, ili kwamba nguvu ya msalaba wa Kristo isiondolewe.
Kajti Kristus me ni poslal krščevat, temveč oznanjat evangelij; ne z modrostjo besed, da ne bi bil Kristusov križ storjen brez učinka.
18 Kwa kuwa ujumbe wa msalaba ni upuuzi kwa wale wanaokufa. Lakini kwa wale ambao Mungu anawaokoa, ni nguvu ya Mungu.
Kajti oznanjevanje križa je tem, ki propadajo, nespametnost; toda nam, ki smo rešeni, je Božja moč.
19 Kwa kuwa imeandikwa, “Nitaiharibu hekima ya wenye busara. Nitauharibu ufahamu wa wenye akili.”
Kajti pisano je: ›Uničil bom modrost modrih in zavrgel bom razum razsodnih.‹
20 Yuko wapi mtu mwenye busara? Yuko wapi mwenye elimu? Yuko wapi msemaji mshawishi wa dunia hii? Je, Mungu hakuigeuza hekima ya dunia hii kuwa ujinga? (aiōn )
Kje je modri? Kje je pisar? Kje je razpravljavec tega sveta? Mar ni modrosti tega sveta Bog naredil za nespametnost? (aiōn )
21 Tangu dunia imekuwa katika hekima yake haikumjua Mungu, ilimpendeza Mungu katika ujinga wao wa kuhubiri ili kuokoa wale wanaoamini.
Kajti potem, ko v Božji modrosti svet po modrosti ni spoznal Boga, je Bogu ugajalo, da po nespametnosti oznanjevanja reši te, ki verujejo.
22 Kwa Wayahudi huuliza ishara za miujiza na kwa Wayunani hutafuta hekima.
Kajti Judje zahtevajo znamenje in Grki iščejo modrost,
23 Lakini tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa, aliye kikwazo kwa Wayahudi na ni ujinga kwa Wayunani.
toda mi oznanjamo križanega Kristusa, Judom kamen spotike in Grkom nespametnost;
24 Lakini kwa wale ambao waliitwa na Mungu, Wayahudi na Wayunani, tunamhubiri Kristo kama nguvu na hekima ya Mungu.
toda tem, ki so poklicani, tako Judom kakor Grkom, [je] Kristus Božja moč in Božja modrost.
25 Kwa kuwa ujinga wa Mungu una hekima kuliko ya wanadamu, na udhaifu wa Mungu una nguvu zaidi ya wanadamu.
Kajti Božja nespametnost je modrejša od ljudi in Božja slabost močnejša od ljudi.
26 Angalia wito wa Mungu juu yenu, kaka na dada zangu. Si wengi wenu mlikuwa na hekima katika viwango vya kibinadamu. Si wengi wenu mlikuwa na nguvu. Si wengi wenu mlizaliwa katika ukuu.
Kajti vidite svoj klic, bratje, da ni poklicanih veliko modrih po mesu, ne veliko mogočnih, ne veliko plemenitih;
27 Lakini Mungu alichagua vitu vijinga vya dunia ili kuviaibisha vyenye hekima. Mungu alichagua kilicho dhaifu katika dunia kukiaibisha chenye nguvu.
toda Bog je izbral nespametne stvari sveta, da zbega modre; in Bog je izbral slabotne stvari sveta, da zbega stvari, ki so mogočne;
28 Mungu alichagua kile kilicho cha hali ya chini na kilichodharauliwa katika dunia. Alichagua hata vitu ambavyo havikuhesabiwa kuwa kitu, kwa kuvifanya si kitu vitu vilivyo na thamani.
in nizke stvari sveta in stvari, ki so prezirane, je Bog izbral, da, in stvari, ki niso, da zavrže stvari, ki so,
29 Alifanya hivi ili asiwepo yeyote aliye na sababu ya kujivuna mbele zake.
da se v njegovi prisotnosti ne bi poveličevalo nobeno meso.
30 Kwa sababu ya kile Mungu alichofanya, sasa mko ndani ya Kristo Yesu, ambaye amefanyika hekima kwa ajili yetu kutoka kwa Mungu. Alikuwa haki yetu, utakatifu na ukombozi.
Toda vi ste iz njega v Kristusu Jezusu, ki je za nas postal modrost od Boga in pravičnost in posvečenje in odkupitev;
31 Kama matokeo, kama andiko lisemavyo, “Anayejisifu, ajisifu katika Bwana.”
da, kakor je pisano: ›Kdor se ponaša, naj se ponaša v Gospodu.‹