< 1 Wakorintho 1 >

1 Paulo, aliyeitwa na Kristo Yesu kuwa mtume kwa mapenzi ya Mungu, na Sosthene ndugu yetu,
Paul, [a] called apostle of Jesus Christ, by God's will, and Sosthenes the brother,
2 kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, kwa wale ambao wamewekwa wakfu katika Yesu Kristo, ambao wameitwa kuwa watu watakatifu. Tunawaandikia pia wale wote wanaoliitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo katika mahali pote, Bwana wao na wetu.
to the assembly of God which is in Corinth, to [those] sanctified in Christ Jesus, called saints, with all that in every place call on the name of our Lord Jesus Christ, both theirs and ours:
3 Neema na amani iwe kwenu kutoka kwa Mungu baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
Grace to you and peace from God our Father, and [the] Lord Jesus Christ.
4 Siku zote namshukru Mungu wangu kwa ajili yenu, kwa sababu ya neema ya Mungu ambayo Kristo Yesu aliwapa.
I thank my God always about you, in respect of the grace of God given to you in Christ Jesus;
5 Amewafanya kuwa matajiri katika kila njia, katika usemi na pamoja maarifa yote.
that in everything ye have been enriched in him, in all word [of doctrine], and all knowledge,
6 Amewafanya matajiri, kama ushuhuda kuhusu Kristo ya kwamba amethibitishwa kuwa kweli miongoni mwenu.
(according as the testimony of the Christ has been confirmed in you, )
7 Kwa hiyo hampungukiwi karama za kiroho, kama mlivyo na hamu ya kusubiri ufunuo wa Bwana wetu Yesu Kristo.
so that ye come short in no gift, awaiting the revelation of our Lord Jesus Christ;
8 Atawaimarisha ninyi pia hadi mwisho, ili msilaumiwe siku ya Bwana wetu Yesu Kristo.
who shall also confirm you to [the] end, unimpeachable in the day of our Lord Jesus Christ.
9 Mungu ni mwaminifu ambaye aliwaita ninyi katika ushirika wa mwana wake, Yesu Kristo Bwana wetu.
God [is] faithful, by whom ye have been called into [the] fellowship of his Son Jesus Christ our Lord.
10 Sasa nawasihi kaka na dada zangu, kupitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba wote mkubali, na kwamba kusiwe na migawanyiko miongoni mwenu. Nawasihi kwamba muungane pamoja katika nia moja na katika kusudi moja.
Now I exhort you, brethren, by the name of our Lord Jesus Christ, that ye all say the same thing, and that there be not among you divisions; but that ye be perfectly united in the same mind and in the same opinion.
11 Kwani watu wa nyumba ya Kloe wamenitaarifu kuwa kuna mgawanyiko unaoendelea miongoni mwenu.
For it has been shewn to me concerning you, my brethren, by those of [the house of] Chloe, that there are strifes among you.
12 Nina maana hii: Kila mmoja wenu husema, “Mimi ni wa Paulo,” au “Mimi ni wa Apolo”, au “Mimi ni wa Kefa” au “Mimi ni wa Kristo”.
But I speak of this, that each of you says, I am of Paul, and I of Apollos, and I of Cephas, and I of Christ.
13 Je! Kristo amegawanyika? Je! Paulo alisulubiwa kwa ajili yenu? Je! Mlibatizwa kwa jina la Paulo?
Is the Christ divided? has Paul been crucified for you? or have ye been baptised unto the name of Paul?
14 Namshukuru Mungu kuwa sikumbatiza yeyote, isipokuwa Krispo na Gayo.
I thank God that I have baptised none of you, unless Crispus and Gaius,
15 Hii ilikuwa kwamba hakuna yeyote angesema mlibatizwa kwa jina langu.
that no one may say that I have baptised unto my own name.
16 (Pia niliwabatiza wa nyumba ya Stephania. Zaidi ya hapo, sijui kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote).
Yes, I baptised also the house of Stephanas; for the rest I know not if I have baptised any other.
17 Kwa kuwa, Kristo hakunituma kubatiza bali kuhubiri injili. Hakunituma kuhubiri kwa maneno ya hekima ya kibinadamu, ili kwamba nguvu ya msalaba wa Kristo isiondolewe.
For Christ has not sent me to baptise, but to preach glad tidings; not in wisdom of word, that the cross of the Christ may not be made vain.
18 Kwa kuwa ujumbe wa msalaba ni upuuzi kwa wale wanaokufa. Lakini kwa wale ambao Mungu anawaokoa, ni nguvu ya Mungu.
For the word of the cross is to them that perish foolishness, but to us that are saved it is God's power.
19 Kwa kuwa imeandikwa, “Nitaiharibu hekima ya wenye busara. Nitauharibu ufahamu wa wenye akili.”
For it is written, I will destroy the wisdom of the wise, and set aside the understanding of the understanding ones.
20 Yuko wapi mtu mwenye busara? Yuko wapi mwenye elimu? Yuko wapi msemaji mshawishi wa dunia hii? Je, Mungu hakuigeuza hekima ya dunia hii kuwa ujinga? (aiōn g165)
Where [is the] wise? where scribe? where disputer of this world? has not God made foolish the wisdom of the world? (aiōn g165)
21 Tangu dunia imekuwa katika hekima yake haikumjua Mungu, ilimpendeza Mungu katika ujinga wao wa kuhubiri ili kuokoa wale wanaoamini.
For since, in the wisdom of God, the world by wisdom has not known God, God has been pleased by the foolishness of the preaching to save those that believe.
22 Kwa Wayahudi huuliza ishara za miujiza na kwa Wayunani hutafuta hekima.
Since Jews indeed ask for signs, and Greeks seek wisdom;
23 Lakini tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa, aliye kikwazo kwa Wayahudi na ni ujinga kwa Wayunani.
but we preach Christ crucified, to Jews an offence, and to nations foolishness;
24 Lakini kwa wale ambao waliitwa na Mungu, Wayahudi na Wayunani, tunamhubiri Kristo kama nguvu na hekima ya Mungu.
but to those that [are] called, both Jews and Greeks, Christ God's power and God's wisdom.
25 Kwa kuwa ujinga wa Mungu una hekima kuliko ya wanadamu, na udhaifu wa Mungu una nguvu zaidi ya wanadamu.
Because the foolishness of God is wiser than men, and the weakness of God is stronger than men.
26 Angalia wito wa Mungu juu yenu, kaka na dada zangu. Si wengi wenu mlikuwa na hekima katika viwango vya kibinadamu. Si wengi wenu mlikuwa na nguvu. Si wengi wenu mlizaliwa katika ukuu.
For consider your calling, brethren, that [there are] not many wise according to flesh, not many powerful, not many high-born.
27 Lakini Mungu alichagua vitu vijinga vya dunia ili kuviaibisha vyenye hekima. Mungu alichagua kilicho dhaifu katika dunia kukiaibisha chenye nguvu.
But God has chosen the foolish things of the world, that he may put to shame the wise; and God has chosen the weak things of the world, that he may put to shame the strong things;
28 Mungu alichagua kile kilicho cha hali ya chini na kilichodharauliwa katika dunia. Alichagua hata vitu ambavyo havikuhesabiwa kuwa kitu, kwa kuvifanya si kitu vitu vilivyo na thamani.
and the ignoble things of the world, and the despised, has God chosen, [and] things that are not, that he may annul the things that are;
29 Alifanya hivi ili asiwepo yeyote aliye na sababu ya kujivuna mbele zake.
so that no flesh should boast before God.
30 Kwa sababu ya kile Mungu alichofanya, sasa mko ndani ya Kristo Yesu, ambaye amefanyika hekima kwa ajili yetu kutoka kwa Mungu. Alikuwa haki yetu, utakatifu na ukombozi.
But of him are ye in Christ Jesus, who has been made to us wisdom from God, and righteousness, and holiness, and redemption;
31 Kama matokeo, kama andiko lisemavyo, “Anayejisifu, ajisifu katika Bwana.”
that according as it is written, He that boasts, let him boast in [the] Lord.

< 1 Wakorintho 1 >