< 1 Wakorintho 1 >

1 Paulo, aliyeitwa na Kristo Yesu kuwa mtume kwa mapenzi ya Mungu, na Sosthene ndugu yetu,
Paul, a called apostle of Jesus Christ, by the will of God, and Sosthenes my brother,
2 kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, kwa wale ambao wamewekwa wakfu katika Yesu Kristo, ambao wameitwa kuwa watu watakatifu. Tunawaandikia pia wale wote wanaoliitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo katika mahali pote, Bwana wao na wetu.
to the church of God which is in Corinth, to the sanctified in Christ Jesus, called saints, with all that in every place call on the name of Jesus Christ our Lord, both theirs and ours:
3 Neema na amani iwe kwenu kutoka kwa Mungu baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
grace be to you, and peace from God our Father, and from the Lord Jesus Christ.
4 Siku zote namshukru Mungu wangu kwa ajili yenu, kwa sababu ya neema ya Mungu ambayo Kristo Yesu aliwapa.
I thank my God always on your account, for the grace of God which is given to you in Christ Jesus;
5 Amewafanya kuwa matajiri katika kila njia, katika usemi na pamoja maarifa yote.
that you are enriched by him in every thing, in all speech, and in all knowledge,
6 Amewafanya matajiri, kama ushuhuda kuhusu Kristo ya kwamba amethibitishwa kuwa kweli miongoni mwenu.
even as the testimony concerning the Christ was con firmed among you,
7 Kwa hiyo hampungukiwi karama za kiroho, kama mlivyo na hamu ya kusubiri ufunuo wa Bwana wetu Yesu Kristo.
so that you are deficient in no gift, while waiting for the revelation of our Lord Jesus Christ.
8 Atawaimarisha ninyi pia hadi mwisho, ili msilaumiwe siku ya Bwana wetu Yesu Kristo.
He also will establish you even to the end, and make you blameless in the day of our Lord Jesus Christ.
9 Mungu ni mwaminifu ambaye aliwaita ninyi katika ushirika wa mwana wake, Yesu Kristo Bwana wetu.
God is faithful, by whom you have been called into the fellowship of his Son Jesus Christ our Lord.
10 Sasa nawasihi kaka na dada zangu, kupitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba wote mkubali, na kwamba kusiwe na migawanyiko miongoni mwenu. Nawasihi kwamba muungane pamoja katika nia moja na katika kusudi moja.
Now, I beseech you, brethren, by the name of our Lord Jesus Christ, that you all speak the same thing, and that there be no schisms among you, but that you be perfectly united in the same mind, and in the same judgment.
11 Kwani watu wa nyumba ya Kloe wamenitaarifu kuwa kuna mgawanyiko unaoendelea miongoni mwenu.
For it has been made known to me concerning you, my brethren, by the family of Cloe, that there are contentions among you.
12 Nina maana hii: Kila mmoja wenu husema, “Mimi ni wa Paulo,” au “Mimi ni wa Apolo”, au “Mimi ni wa Kefa” au “Mimi ni wa Kristo”.
I mean this: that each one of you says, I am of Paul, and I of Apollos, and I of Cephas, and I of Christ.
13 Je! Kristo amegawanyika? Je! Paulo alisulubiwa kwa ajili yenu? Je! Mlibatizwa kwa jina la Paulo?
Is the Christ divided? Was Paul crucified for you? or were you immersed into the name of Paul?
14 Namshukuru Mungu kuwa sikumbatiza yeyote, isipokuwa Krispo na Gayo.
I thank God that I immersed none of you, but Crispus and Gaius;
15 Hii ilikuwa kwamba hakuna yeyote angesema mlibatizwa kwa jina langu.
that no one may say that I immersed into my own name.
16 (Pia niliwabatiza wa nyumba ya Stephania. Zaidi ya hapo, sijui kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote).
I did, indeed, immerse the household of Stephanus; besides, I know not whether I immersed any other.
17 Kwa kuwa, Kristo hakunituma kubatiza bali kuhubiri injili. Hakunituma kuhubiri kwa maneno ya hekima ya kibinadamu, ili kwamba nguvu ya msalaba wa Kristo isiondolewe.
For Christ sent me not to immerse, but to preach the gospel: not with wisdom of speech, lest the cross of the Christ should be deprived of its power.
18 Kwa kuwa ujumbe wa msalaba ni upuuzi kwa wale wanaokufa. Lakini kwa wale ambao Mungu anawaokoa, ni nguvu ya Mungu.
For the preaching of the cross is to those who perish, foolishness; but to us who are saved, it is the power of God.
19 Kwa kuwa imeandikwa, “Nitaiharibu hekima ya wenye busara. Nitauharibu ufahamu wa wenye akili.”
For it is written: I will destroy the wisdom of the wise; and I will set aside the understanding of the prudent.
20 Yuko wapi mtu mwenye busara? Yuko wapi mwenye elimu? Yuko wapi msemaji mshawishi wa dunia hii? Je, Mungu hakuigeuza hekima ya dunia hii kuwa ujinga? (aiōn g165)
Where is the wise man? Where is the scribe? Where is the disputer of this age? Has not God made foolish the wisdom of this world? (aiōn g165)
21 Tangu dunia imekuwa katika hekima yake haikumjua Mungu, ilimpendeza Mungu katika ujinga wao wa kuhubiri ili kuokoa wale wanaoamini.
For, since in the wisdom of God, the world, by its wisdom, knew not God, it has pleased God, through the foolishness of what is preached, to save those who believe.
22 Kwa Wayahudi huuliza ishara za miujiza na kwa Wayunani hutafuta hekima.
For the Jews ask for a sign, and the Greeks seek for wisdom;
23 Lakini tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa, aliye kikwazo kwa Wayahudi na ni ujinga kwa Wayunani.
but we preach Christ crucified; to the Jews, indeed, a stumbling-block, and to the Greeks, foolishness:
24 Lakini kwa wale ambao waliitwa na Mungu, Wayahudi na Wayunani, tunamhubiri Kristo kama nguvu na hekima ya Mungu.
but to those who are called, both Jews and Greeks, Christ, the power of God, and the wisdom of God.
25 Kwa kuwa ujinga wa Mungu una hekima kuliko ya wanadamu, na udhaifu wa Mungu una nguvu zaidi ya wanadamu.
For the foolishness of God is wiser than men; and the weakness of God is stronger than men.
26 Angalia wito wa Mungu juu yenu, kaka na dada zangu. Si wengi wenu mlikuwa na hekima katika viwango vya kibinadamu. Si wengi wenu mlikuwa na nguvu. Si wengi wenu mlizaliwa katika ukuu.
For you see your calling, brethren, that not many wise men according to the flesh, not many mighty, not many noble call you;
27 Lakini Mungu alichagua vitu vijinga vya dunia ili kuviaibisha vyenye hekima. Mungu alichagua kilicho dhaifu katika dunia kukiaibisha chenye nguvu.
but God has chosen the foolish things of the world, that he may bring to shame the wise; and the weak things of the world has God chosen, that he may put to shame the strong;
28 Mungu alichagua kile kilicho cha hali ya chini na kilichodharauliwa katika dunia. Alichagua hata vitu ambavyo havikuhesabiwa kuwa kitu, kwa kuvifanya si kitu vitu vilivyo na thamani.
and the ignoble things of the world, and the things that are despised, has God chosen, and the things that are not, that he might bring to nought things that are;
29 Alifanya hivi ili asiwepo yeyote aliye na sababu ya kujivuna mbele zake.
that no flesh should glory in his presence.
30 Kwa sababu ya kile Mungu alichofanya, sasa mko ndani ya Kristo Yesu, ambaye amefanyika hekima kwa ajili yetu kutoka kwa Mungu. Alikuwa haki yetu, utakatifu na ukombozi.
But of him are you in Christ Jesus, who has become to us, from God, wisdom and righteousness and sanctification and redemption;
31 Kama matokeo, kama andiko lisemavyo, “Anayejisifu, ajisifu katika Bwana.”
that, as it is written: He that glories, let him glory in the Lord.

< 1 Wakorintho 1 >