< 1 Nyakati 9 >

1 Kwa hivyo watu wote wa Israeli walinakiliwa ki uzao. Walinakiliwa katika vitabu vya kifalme vya Israeli. Yuda, walipelekwa matekani Babylon kwasababu ya dhambi zao.
So all Israel was recorded in genealogies. They were recorded in the book of the kings of Israel. As for Judah, they were carried away in exile to Babylon because of their sin.
2 Wakwanza kurudi kuishi katika miiji yao walikuwa Waisraeli, Makuhani, Walawi, na Watumishi wa hekalu.
The first to resettle in their cities were some Israelites, priests, Levites, and temple servants.
3 Baadhi ya uzao wa Yuda, Benjamin, Efraimu, na Manase waliishi Yerusalemu.
Some descendants of Judah, Benjamin, Ephraim, and Manasseh lived in Jerusalem.
4 Wahamiaji walijumusha Uthai mwana wa Ammihudi mwana wa Omri mwana wa Bani, moja ya uzao wa Perezi mwana wa Yuda.
The settlers included Uthai son of Ammihud son of Omri son of Imri son of Bani, one of the descendants of Perez son of Judah.
5 Kati ya Mashilonite kulikuwa na Asaia mtoto wa kwanza na wana wake.
Among the Shelanites were Asaiah the firstborn and his sons.
6 Kati ya uzao wa Zera alikuwa Yeuli. Uzao wao ulikuwa na namba 690.
Among the descendants of Zerah was Jeuel. Their descendants numbered 690.
7 Katika uzao Benjamini walikuwa Salu mwana wa Meshulamu mwana wa hodavia mwana wa Hssenua.
Among the descendants of Benjamin were Sallu son of Meshullam son of Hodaviah son of Hassenuah.
8 Pia walikuwa Ibneia mwana wa Yerohamu; Ela mwana wa Uzzi mwana wa Mikri; na Meshullam mwana wa Shefatia mwana waReuli mwana wa Ibnija.
There were also Ibneiah son of Jeroham; Elah son of Uzzi son of Mikri; and Meshullam son of Shephatiah son of Reuel son of Ibnijah.
9 Ndugu zao waliandika kwenye orodha ya namba 956 ya vizazi vyao. Wanaume wote hawa walikuwa viongozi wa koo za mababu zao.
Their relatives written in the genealogical lists numbered 956. All these men were heads of fathers' houses for their fathers' houses.
10 Makuhani walikuwa Yedaia, Yehoiarib, na Yokini.
The priests were Jedaiah, Jehoiarib, and Jakin.
11 Walikuwa pia Azaria mwana wa Hilkia mwana wa Meshullamu mwana wa Zadoki mwana wa Meraioti mwana wa Ahitubi, aliyekuwa na mamlaka katika nyumba ya Mungu.
There was also Azariah son of Hilkiah son of Meshullam son of Zadok son of Meraioth son of Ahitub, the one in charge of the house of God.
12 Kulikuwa na Adaia mwana wa Yerohamu mwana wa Pashuri mwana wa Malkija. Pia kulikuwa na Maasai mwanawa Adieli mwana wa Yazera mwana wa Meshulamu mwana wa Meshilemiti mwana wa Imma.
There was Adaiah son of Jeroham son of Pashhur son of Malkijah. There was also Maasai son of Adiel son of Jahzerah son of Meshullam son of Meshillemith son of Immer.
13 Ndugu zao, ambao walikuwa viongozi katika koo za mababu zao, idadi ya 1, 760. Walikuwa ni wanaume wenye uwezo sana wa kufanya kazi katika nyumba ya Mungu.
Their relatives, who were leaders for their fathers' houses, numbered 1,760. They were very capable men in the work in the house of God.
14 Kati ya Walawii, kulikuwa na Shemaia mwana wa Hashubu mwana wa Azrikam mwana wa Hashabia, kati ya uzao wa Merari.
Among the Levites, there was Shemaiah son of Hasshub son of Azrikam son of Hashabiah, among the descendants of Merari.
15 Walikuwako pia Bakbakari, Hereshi, Galali, na Mattania mwana wa Mika mwana wa Zikri mwana wa Asafu.
There were also Bakbakkar, Heresh, Galal, and Mattaniah son of Mika son of Zikri son of Asaph.
16 Walikuwako pia Obadia mwana wa Shemaia mwana wa Galali mwana wa Yedutuni; na Berekia mwana wa Asa mwana wa Elkana, aliyeishikatika vijiji vya Netophathites.
There were also Obadiah son of Shemaiah son of Galal son of Jeduthun; and Berekiah son of Asa son of Elkanah, who lived in the villages of the Netophathites.
17 Walinzi wa lango walikuwa Shalumu, Akubi, Talimoni, Ahimani, na uzao wao. Shalumu alikuwa kiongozi wao.
The doorkeepers were Shallum, Akkub, Talmon, Ahiman, and their descendants. Shallum was their leader.
18 Awali walisimama kulinda katika geti la mfalme upande wa mashariki wa kambi ya uzao wa Walawi.
Previously they stood guard at the king's gate on the east side for the camp of Levi's descendants.
19 Shalumu mwana wa Kore mwana wa Ebiasafu, ambaye kama mwana wa Kora, na ndugu zake kutoka nyumba ya baba yake, Korahite, alikuwa na mamlaka kwa kazi ya huduma, Walilinda mlango wa hema, kama mababu zao walivyolinda kambi ya Yawehi, na pia walilinda lango la kuingilia.
Shallum son of Kore son of Ebiasaph, son of Korah, and his relatives from the house of his father, the Korahites, were in charge of the work of the guard service. They guarded the door to the tent, as their ancestors had guarded the camp of Yahweh, and they also had guarded the entrance.
20 Finehasi mwana wa Eleaza aliwaongoza kipindi cha nyuma, na Yahwehi alikuwa pamoja nae.
Phinehas son of Eleazar had been in charge of them in the past, and Yahweh had been with him.
21 Zekaria mwana wa Meshelemia alikua mlinzi katika mlango wa kuingilia hekalu, “eneo la kukutania.”
Zechariah son of Meshelemiah was guard of the entrance to the temple, the “tent of meeting.”
22 Hawa wote walichaguliwa kana walinzi wa mageti ya kuingilia kwa idadi ya 212. Majina yao yaliandikwa kwenye kumbukumbu za watu katika vijiji vyao. Mtabiri aliwaweka Daudi na Samueli katika nafasi ya uaminifu.
All those who were chosen as gatekeepers at the entrances numbered 212. Their names were recorded in the people's records in their villages. David and Samuel the seer had placed them into their positions of trust.
23 Kwa hivyo wao na watotot wao walilinda mageti katika nyumba ya Yawehi, hema la kuabudia.
So they and their children guarded the gates of the house of Yahweh, the tabernacle.
24 Walinzi wa mageti waliwekwa katika pande zote nne, upande wa mashariki, magharibi, kaskazini, na kusini.
The gatekeepers were posted on all four sides, toward the east, west, north, and south.
25 Kaka zao, walioishi kwenye vijiji vyao, walikuja kuwasaidia baada ya mzunguko wa siku saba.
Their brothers, who lived in their villages, came in for seven-day rotations, in turn.
26 Lakini viongozi wanne wa walinzi, ambao walikwa walawi, walipangiwa kulinda vyumba na vyumba vya kuhifadhi katika nyumba ya Mungu.
But the four leaders of the gatekeepers, who were Levites, were assigned to guard the rooms and storerooms in the house of God.
27 Walitumia usiku wao sehemu walizowekwa kuzunguka nyumba ya Mungu, kwao ilikuwa ni wajibu wao kulinda. Na walifungua geti kila asubuhi.
They would spend the night in their posts all around the house of God, for they were responsible for guarding it. They would open it each morning.
28 Baadhi yao waliwajibika katika hekalu la vifaa; walihesabu makala zilizo ingizwa ndani na zilizo tolewa nje.
Some of them were in charge of the temple's equipment; they counted the articles when they were brought in and when they were taken out.
29 Baadhi yao pia waliwekwa kutunza vitu vitakatifu, vifaa, na vitu, kujuisha unga safi, mvinyo, mafuta, manukato, na uvumba.
Some of them also were assigned to take care of the holy things, the equipment, and the supplies, including the fine flour, the wine, the oil, the frankincense, and the spices.
30 Baadhi ya wana wa makuhani walichanganya uvumba.
Some of the priests' sons mixed the spices.
31 Matithia, mmoja wa walawi, ambaye alikuwa mtoto wa kwanza wa Shalumu wa Wakorahi, alikuwa na wajibu wa kuandaa mikate kwa ajili ya sadaka.
Mattithiah, one of the Levites, who was the firstborn of Shallum the Korahite, was in charge of preparing bread for the offerings.
32 Baadhi ya kaka zao, uzao wa kohathite, waliwajibika kwa mikate ya uwepo, kuandaa kila Sabatho.
Some of their brothers, descendants of the Kohathites, were in charge of the bread of the presence, to prepare it every Sabbath.
33 Waimbaji na viongozi wa familia ya Walawi waliishi ndani ya vyumba katika mahali takatifu walipo kuwa hawafanyi kazi, kwa sababu wapiswa kufanya kazi walio pangiwa usiku na mchana.
The singers and heads of the Levites' fathers' houses lived in rooms at the sanctuary when they were free from work, because they had to carry out their assigned tasks day and night.
34 Hawa walikuwa viongozi wa familia miongoni mwa Walawi, kama ilivyo orodheshwa katika kumbukumbu za uzao wao. Waliishi Yerusalemu.
These were leaders of fathers' houses among the Levites, as listed in their genealogical records, chief men. They lived in Jerusalem.
35 Baba wa Gibeoni, Yeiel, ambaye mkewe aliitwa Maaka, aliishi Gibeoni.
The father of Gibeon, Jeiel, whose wife's name was Maakah, lived in Gibeon.
36 Mtoto wake wa kwanza alikuwa Abdoni, alafu wana wake Zuri, Kishi, Baali, Neri, Nadabu,
His firstborn son was Abdon, then his sons Zur, Kish, Baal, Ner, Nadab,
37 Gedori, Ahio, Zekaria, na Mikloti.
Gedor, Ahio, Zechariah, and Mikloth.
38 Mikloti alikuwa baba wa Shimeamu. Pia waliishi karibu na kaka yao huko Yerusalemu.
Mikloth was the father of Shimeam. They also lived near their brothers in Jerusalem.
39 Neri alikuwa baba wa Kishi. Kishi alikuwa baba wa Sauli. sauli alikuwa baba wa Yonathani, malkishua, Abinadabu, na Ishbaali.
Ner was the father of Kish. Kish was the father of Saul. Saul was the father of Jonathan, Malki-Shua, Abinadab, and Esh-Baal.
40 Mwana wa Jonathani alikuwa Merib baali. Merib baali alikuwa baba wa Mika.
The son of Jonathan was Merib-Baal. Merib-Baal was the father of Micah.
41 Mwana wa Mika walikuwa pithoni, Meleki, Tahrea, na ahazi.
The sons of Micah were Pithon, Melek, Tahrea, and Ahaz.
42 Ahazi alikuwa baba wa Jara. Jara alikuwa baba wa Alemeti, Azmaveti, na zimri. Zimri alikuwa baba wa Moza.
Ahaz was the father of Jadah. Jadah was the father of Alemeth, Azmaveth, and Zimri. Zimri was the father of Moza.
43 Moza alikuwa baba wa Binea. Binea alikuwa baba wa Refaia. Refaia alikuwa baba wa Eleas. eleasa alikuwa baba wa Azeli.
Moza was the father of Binea. Binea was the father of Rephaiah. Rephaiah was the father of Eleasah. Eleasah was the father of Azel.
44 Wana sita wa Azeli walikuwa Azrikamu, Bochera, Ishmaeli, shearia, Obdia, na Hanani. hawa walikuwa wana wa Azeli
Azel's six sons were Azrikam, Bokeru, Ishmael, Sheariah, Obadiah, and Hanan. These were Azel's sons.

< 1 Nyakati 9 >