< 1 Nyakati 7 >

1 Isiakari alikuwa na wana wanne Tola, Pua, Yashubi, na Shimironi.
Now the sons of Issachar were Tola and Puah, Jashub and Shimron, four.
2 Wana wa Tola walikuwa Uzi, Refaia, Yerie, Yamai, Ibisami, Shemueli. Walikua vichwa katika nyumba za baba yao, toka uzao wa Tola na waliorodheshwa kama mashujaa hodari miongoni mwa kizazi chao. Katika siku za Daudi walikua na idadi ya 22, 600.
The sons of Tola: Uzzi, and Rephaiah, and Jeriel, and Jahmai, and Ibsam, and Shemuel, leaders according to the houses of their kindred. From the stock of Tola, there were numbered, in the days of David, twenty-two thousand six hundred very strong men.
3 Mwana wa Uzi alikua Izrahia. Mwana wake alikua Michaeli, Obadia, Yoeli, na Ishia, wote watano walikua viongozi wa ukoo
The sons of Uzzi: Izrahiah, from whom were born: Michael, and Obadiah, and Joel, and Isshiah; all five were leaders.
4 Pamoja nao walikua na jeshi la watu elfu thelathini na sita kwa mapambano, Kwa mujibu wa orodha zilizomilikiwa na koo za mababu zao, kwa kuwa walikuwa na wake wengi pamoja na wana.
And with them, by their families and peoples, there were thirty-six thousand very strong men, girded for battle. And they had many wives and children.
5 Kaka zao, kabila la Isakari, walikua na wanaume wa vita themanini na saba, kwa mujibu wa orodha zilizomilikiwa na koo za mababu zao.
Also, their brothers, throughout all the kindred of Issachar, were numbered as eighty-seven thousand, very fit for battle.
6 Wana watatu wa Benjamini walikuwa Bela, Beka, na Yediaeli.
The sons of Benjamin: Bela, and Becher, and Jediael, three.
7 Wana watano wa Bela walikuwa Ezibono, Uzi, Uzieli, Yerimoti, na Iri. Walikua ni wanajeshi na waanzilishi wa koo. Watu wao walikuwa na idadi ya wanaume wa vita 22, 034, kwa mujibu wa orodha zilizomilikiwa na koo za mababu zao.
The sons of Bela: Ezbon, and Uzzi, and Uzziel, and Jerimoth and Iri, five leaders of families, also very fit for battle; and their number was twenty-two thousand thirty-four.
8 Wana wa Beka walikuwa Zemira, Yoashi, Elieza, Elionai, Omri, Yeremoti, Abiya, Anatoti, na Alemeti. Wote hawa walikuwa wana wake.
Now the sons of Becher: Zemirah, and Joash, and Eliezer, and Elioenai, and Omri, and Jeremoth, and Abijah, and Anathoth, and Alemeth: all these were sons of Becher.
9 Orodha ya koo zao ilikua na idadi ya 20, 200 viongozi wa familia na wanaume wa vita.
And they were numbered according to their families, by the leaders of their kindred, very strong in warfare, twenty thousand and two hundred.
10 Mwana wa Yediaeli alikuwa Bilhani. Wana wa Bilhani walikuwa Yeushi, Benjamini, Ehudi, Kenaana, Zetani, Tarishishi, na Ahishahari.
And the sons of Jediael: Bilhan, and the sons of Bilhan: Jeush, and Benjamin, and Ehud, and Chenaanah, and Zethan, and Tarshish, and Ahishahar.
11 Wote hawa waikuwa wana wa Yediaeli. Waliorodheshwa katika ukoo orodha ilikuwa 17, 200 viongozi na wanaume wa vita imara kwa kazi ya jeshi.
All these were sons of Jediael, the leaders of their kindred, very strong men, seventeen thousand and two hundred, going forth to battle.
12 (Shupimu na Hupimu walikuwa wana wa Iri, na Hushimu alikuwa mwana wa Aheri.)
Also, Shuppim and Huppim, the sons of Ir; and Hushim, sons of Aher.
13 Wana wa Naftali walikuwa Yazieli, Guni, Yezeri, na Shalumu. Hawa walikuwa wajukuu wa Bilhahi.
Then the sons of Naphtali: Jahziel, and Guni, and Jezer, and Shallum, sons of Bilhah.
14 Manasse alikua na mtoto wa kiume aliitwa Asrieli, Ambaye suria wake wa Kiaramia alimzalia. Pia alimzaa na Makiri, baba wa Gileadi.
Also, the son of Manasseh: Asriel. And his concubine, a Syrian, bore Machir, the father of Gilead.
15 Makiri alimchukua mke wake kutoka Hupite na Shupite. Jina la dada yake lilikuwa Maaka. Mwingine wa uzao wa Manasse alikuwa Zalofehadi, ambaye alikuwa na mabinti pekee.
Now Machir took wives for his sons, Huppim and Shuppim. And he had a sister named Maacah; but the name of the second was Zelophehad, and daughters were born to Zelophehad.
16 Maaka mke wa Makiri, alimzaa mwana na alimuita Pereshi. Kaka yake aliitwa Shereshi, na wana wake walikuwa Ulamu na Rakemu.
And Maacah, the wife of Machir, bore a son, and she called his name Peresh. And the name of his brother was Sheresh. And his sons were Ulam and Rakem.
17 Mwana wa Ulami alikuwa Bedani. Hawa walikuwa uzao wa Gileadi mwana wa Makiri mwana wa Manase.
Then the son of Ulam: Bedan. These are the sons of Gilead, the son of Machir, the son of Manasseh.
18 Dada wa Gileadi Hamoleketi alimzaa Ishihodi, Abi Ezeri, na Mahila.
And his sister, Regina, bore Ishhod, and Abiezer, and Mahlah.
19 Wana wa Shemida walikuwa Ahiana, Shekemu, Liki, na Aniamu.
Now the sons of Shemida were Ahian, and Shechem, and Likhi and Aniam.
20 Uzao wa Efraimu ulikuwa kama ifuatavyo: Efraimu mwana wa Shutela. Shutela mwana wa Beredi. Beredi mwana wa Tahati.
And the sons of Ephraim: Shuthelah, Bered his son, Tahath his son, Eleadah his son, Tahath his son, whose son was Zabad,
21 Tahati mwana wa Eleada. Eleada mwana wa Shutela. (Eza na Eleadi waliuawa na wanaume wa Gati, wenyeji wa nchi, walipoenda kuiba mifugo yao.
and his son was Shuthelah, and his son was Ezer, and also Elead. But the men indigenous to Gath killed them, because they had descended to invade their possessions.
22 Efraimu baba yao aliomboleza kwa siku nyingi, na kaka zake walikuja kumfariji.
And so their father, Ephraim, mourned for many days; and his brothers arrived, so that they might console him.
23 Alilala na mkewe. Akapata mimba akamzaa mwana. Efraimu akamuita Beria, kwa sababu maafa yalishakuja nyumbani mwake.
And he entered to his wife; she conceived and bore a son. And he called his name Beriah, because he rose up during a time of evil for his house.
24 Binti yake alikuwa Sheera, ambaye alijenga miji juu na chini Beth Horon na Uzzen Sheerah.)
Now his daughter was Sheerah, who built lower and upper Beth-horon, and also Uzzen-sheerah.
25 Mwana wake alikuwa Rafa. Mwana wa Rafa alikuwa Reshefi. Mwana wa Reshafi alikuwa Tela. Mwana wa Tela alikuwa Tahani.
And Rephah was his son, and Resheph, and Telah, from whom was born Tahan,
26 Mwana wa Tahani alikuwa Ladani. Mwana wa Ladani alikuwa Amihudi. Mwana wa Amihudi alikuwa Elishama.
who conceived Ladan. And his son was Ammihud, who conceived Elishama,
27 Mwana wa Elishama alikuwa Nuni. Mwana wa Nuni alikuwa Joshua.
from whom was born Nun, who had Joshua as a son.
28 Mali zao na makazi yao yalikuwa Betheli na yalizungukwa na vijiji. Waliongeza upande wa mashariki hadi Naarani na upande wa magharibi hadi Gezeri na vijiji vyake, na Shekemu na vijiji vyake hadi Aya na vijiji vyake.
Now their possessions and habitations were: Bethel with her daughters, and toward the east, Naaran, and toward the western region, Gezer and her daughters, as well as Shechem with her daughters, as far as Ayyah with her daughters;
29 Katika mipaka pamoja na Manasse kulikuwa na Beti shani na vijiji vyake, Taanaki na vijiji vyake, Megido na vijiji vyake, na Dori na vijiji vyake. Katika huu mji waliishi uzao wa Josefu mwana wa Israeli.
also, beside the sons of Manasseh, Bethshean and her daughters, Taanach and her daughters, Megiddo and her daughters, Dor and her daughters. In these places, there lived the sons of Joseph, the son of Israel.
30 Wana wa Asha walikuwa Imna, Ishiva, Ishivi, na Beria. Sera alikuwa dada yao.
The sons of Asher: Imnah, and Ishvah, and Ishvi, and Beriah, and Serah their sister.
31 Wana wa Beria walikuwa Heberi na Malchieli, Ambaye alikuwa baba wa Birzaiti.
And the sons of Beriah: Heber, and Malchiel, the same is the father of Birzaith.
32 Wana wa Heberi walikuwa Yafeti, Shomer, na Hotamu. dada yao alikuwa Shua.
Now Heber conceived Japhlet, and Shomer, and Hotham, and their sister Shua.
33 Wana wa Yafeti walikuwa Pasach, Bimhali, na Ashivati. hawa walikuwa watoto wa yafeti.
The sons of Japhlet: Pasach, and Bimhal, and Ashvath; these are the sons of Japhlet.
34 shoma, kaka wa Yafeti alikuwa na wana hawa: Roga, Yehuba, Aram.
Then the sons of Shomer: Ahi, and Rohgah, and Jehubbah, and Aram.
35 Kaka yake Shema, Helemu, alikuwa na wana hawa: Zofa, Imna, Sheleshi na Amali.
And the sons of Helem, his brother: Zophah, and Imna, and Shelesh, and Amal.
36 Wana wa Zofa walikuwa Sua, Harinefa, Shua, Beri, IMra,
The sons of Zophah: Suah, Harnepher, and Shual, and Beri, and Imrah,
37 Beza, Hodi, Shamma, Shilsha, Ithrani, na Beera.
Bezer, and Hod, and Shamma, and Shilshah, and Ithran, and Beera.
38 Wana wa Yeta walikuwa Jefune, Pispa, na Ara.
The sons of Jether: Jephunneh, and Pispa, and Ara.
39 Wana wa Ulla walikwa Ara, Hannieli, na Rizia.
Then the sons of Ulla: Arah, and Hanniel, and Rizia.
40 Hawa wote walikuwa uzao wa Asha. Walikua mababu wa ukoo, viongozi wa familia, wananume wa kipekee, wanaume wa vita, na machifu kati ya viongozi. Kulikuwa na wanaume elfu ishirini na sita walioorodheshwa waliokuwa imara kwa kazi ya jeshi, kwa mujibu wa idadi iliyo orodheshwa.
All these were sons of Asher, the leaders of families, elect and very strong rulers among rulers. And the number of those who were of an age that was fit for warfare was twenty-six thousand.

< 1 Nyakati 7 >