< 1 Nyakati 6 >

1 Wana wa Levi walikuwa Gerishoni, Kohathi, na Merari.
filii Levi Gersom Caath Merari
2 Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
filii Caath Amram Isaar Hebron et Ozihel
3 Wana wa Amramu walikuwa Aruni, Musa, Miriamu. Wana wa Aruni walikuwa Nadabu, Abihu, Eleazari, na Ithamari.
filii Amram Aaron Moses et Maria filii Aaron Nadab et Abiu Eleazar et Ithamar
4 Eleazari akawa baba wa Finehasi, na Finehasi akawa baba wa Abishua.
Eleazar genuit Finees et Finees genuit Abisue
5 Abishua akawa baba wa Buki, na Buki akawa baba wa Uzi.
Abisue vero genuit Bocci et Bocci genuit Ozi
6 Uzi akawa baba wa Zerahia, na Zerahia akawa baba wa Meraioti.
Ozi genuit Zaraiam et Zaraias genuit Meraioth
7 Meraioti akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
porro Meraioth genuit Amariam et Amarias genuit Ahitob
8 Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Ahimazi.
Ahitob genuit Sadoc Sadoc genuit Achimaas
9 Ahimazi akawa baba wa Azaria, na Azaria akawa baba wa Yohanani.
Achimaas genuit Azariam Azarias genuit Iohanan
10 Yohanani akawa baba wa Azaria, aliye hudumu katika hekalu alilo lijenga Sulemani ndaniya Yerusalemu.
Iohanan genuit Azariam ipse est qui sacerdotio functus est in domo quam aedificavit Salomon in Hierusalem
11 Azaria akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
genuit autem Azarias Amariam et Amarias genuit Ahitob
12 Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Shalumu.
Ahitob genuit Sadoc et Sadoc genuit Sellum
13 Shalumu akawa baba wa Hilikia, na Hilikia akawa baba wa Azaria.
Sellum genuit Helciam et Helcias genuit Azariam
14 Azaria akawa baba Seraia, na Seraia akawa baba wa Yehozadaki.
Azarias genuit Saraiam et Saraias genuit Iosedec
15 Yehozadaki akaenda matekani Yahweh alipo wapeleka utumwani Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Nebukadneza.
porro Iosedec egressus est quando transtulit Dominus Iudam et Hierusalem per manus Nabuchodonosor
16 Wana wa Levi walikuwa Gerishomu, Kohathi, na Merari.
filii ergo Levi Gersom Caath et Merari
17 Wana wa Gerishomu walikuwa Libini na Shimei.
et haec nomina filiorum Gersom Lobeni et Semei
18 Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
filii Caath Amram et Isaar et Hebron et Ozihel
19 Wana wa Merari walikuwa Mahili na Mushi. Hawa walikuwa koo za Walawi kwa familia za baba zao.
filii Merari Mooli et Musi hae autem cognationes Levi secundum familias eorum
20 Uzao wa Gerishomu ulianza na mwanae Libini. Mwana wa Libini alikuwa Jahathi. Mwanae alikuwa Zima.
Gersom Lobeni filius eius Iaath filius eius Zamma filius eius
21 Mwanae alikuwa Yoa. Mwanae alikuwa alikuwa Ido. Mwanae alikuwa Zera. Mwanae alikuwa Yeatherai.
Ioaa filius eius Addo filius eius Zara filius eius Iethrai filius eius
22 Uzao wa Kohathi ulianza na mwanae Aminadabu. Mwanae alikuwa Kora. Mwanae alikuwa Asiri.
filii Caath Aminadab filius eius Core filius eius Asir filius eius
23 Mwanae alikuwa Elikana. Mwanae alikuwa Ebiasa. Mwanae alikuwa Asiri.
Helcana filius eius Abiasaph filius eius Asir filius eius
24 Mwanae alikuwa Tahathi. Mwanae alikuwa Urieli. Mwanae alikuwa uzia. Mwanae alikuwa Shauli.
Thaath filius eius Urihel filius eius Ozias filius eius Saul filius eius
25 Wana wa Elikana walikuwa Amasai, Ahimothi, na Elikana.
filii Helcana Amasai et Ahimoth
26 Mwana wa huyu Elikana wa pili alikuwa Zofai. Mwanae alikuwa Nahathi.
Helcana filii Helcana Sophai filius eius Naath filius eius
27 Mwanae alikuwa Eliabu. Mwanae alikuwa Yehoramu. Mwanae alikuwa Elikana.
Heliab filius eius Hieroam filius eius Helcana filius eius
28 Wana wa Samwali walikuwa mzaliwa wa kwanza, Yoeli, na Abija, wa pili.
filii Samuhel primogenitus Vasseni et Abia
29 Mwana wa Merari alikuwa Mahili. Mwanae alikuwa Libini.
filii autem Merari Mooli Lobeni filius eius Semei filius eius Oza filius eius
30 Mwanae alikuwa Shimei. Mwanae alikuwa Uza. Mwanae alikuwa Shimea. Mwanae alikuwa Hagia. Mwana alikuwa Asaia.
Samaa filius eius Aggia filius eius Asaia filius eius
31 Haya ndio majina ya wanaume ambao Daudi waliwaeka kusimamia muziki katika nyumba ya Yahweh, baada ya sanduku kuja hapo.
isti sunt quos constituit David super cantores domus Domini ex quo conlocata est arca
32 Walitumika kwa kuimba mbele ya hema, hema la kukutania, mpaka Sulemani alipo jenga nyumba ya Yahweh ndani ya Yerusalemu. Walikamilisha wajibu wao kwa kadiri ya maelekezo waliopewa.
et ministrabant coram tabernaculo testimonii canentes donec aedificaret Salomon domum Domini in Hierusalem stabant autem iuxta ordinem suum in ministerio
33 Hawa walitumika pamoja na wana wao. Katika makabila ya Wakohathi alitoka Hemani mwana muziki. Babu zake walikuwa hawa, kurudi nyuma ya wakati: Hemani alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Samweli.
hii vero sunt qui adsistebant cum filiis suis de filiis Caath Heman cantor filius Iohel filii Samuhel
34 Samweli alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Yerohamu. Yerohamu alikuwa mwana wa Elieli. Elieli alikuwa mwana wa Toa.
filii Helcana filii Hieroam filii Helihel filii Thou
35 Toa alikuwa mwana wa Zufi. Zufi alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Mahathi. Mahathi alikuwa mwana wa Amasai. Amasai alikuwa mwana wa Elikana.
filii Suph filii Helcana filii Maath filii Amasai
36 Elikana alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Azaria. Azaria alikuwa mwana wa Zefania.
filii Helcana filii Iohel filii Azariae filii Sophoniae
37 Zefania alikuwa mwana wa Tahathi. Tahathi alikuwa mwana wa Asiri. Asiri alikuwa mwana wa Ebiasa. Ebiasa alikuwa mwana wa Kora.
filii Thaath filii Asir filii Abiasaph filii Core
38 Kora alikuwa mwana wa Izhari. Izhari alikuwa mwana wa Kohathi. Kohathi alikuwa mwana wa Levi. Levi alikuwa mwana wa Israeli.
filii Isaar filii Caath filii Levi filii Israhel
39 Msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliye simama mkono wake wa kuume. Asafu alikuwa mwana Berekia. Berekia alikuwa mwana wa Shimea.
et fratres eius Asaph qui stabat a dextris eius Asaph filius Barachiae filii Samaa
40 Shimea alikuwa mwana Mikaeli. Mikaeli alikuwa mwana wa Baaseia. Baaseia alikuwa mwana wa Malikiya.
filii Michahel filii Basiae filii Melchiae
41 Malikiya alikuwa mwana wa Ethini. Ethini alikuwa mwana wa Zera. Zera alikuwa mwana wa Adaia.
filii Athnai filii Zara filii Adaia
42 Adaia alikuwa mwana wa Ethani. Ethani alikuwa mwana wa Zima. Zima alikuwa mwana wa Shimei.
filii Ethan filii Zamma filii Semei
43 Shimei alikuwa mwana wa Yahathi. Yahathi alikuwa mwana wa Gerishomu. Gerishomu alikuwa mwana wa Levi.
filii Ieth filii Gersom filii Levi
44 Upande wa mkono wa koshoto wa Hemani walikuwa wasaidizi wake wana wa Merari. Alikuwa Ethani mwana wa Kishi. Kishi alikuwa mwana wa Abdi. Abdi alikuwa mwana wa Maluki.
filii autem Merari fratres eorum ad sinistram Ethan filius Cusi filii Abdi filii Maloch
45 Maluki alikuwa mwana wa Hashabia. Hashabia alikuwa mwana wa Amazia. Amazia alikuwa mwana wa Hilikia.
filii Asabiae filii Amasiae filii Helciae
46 Hilikia alikuwa mwana wa Amzi. Amzi alikuwa mwana wa Bani. Bani alikuwa mwana wa Shemeri.
filii Amasai filii Bonni filii Somer
47 Shemeri alikuwa mwana wa Mahili. Mahili alikuwa mwana wa Mushi. Mushi alikuwa mwana wa Merari. Merari alikuwa mwana wa Levi.
filii Mooli filii Musi filii Merari filii Levi
48 Walawi, alipangiwa kufanya kazi zote za hema, nyumba ya Mungu.
fratres quoque eorum Levitae qui ordinati sunt in cunctum ministerium tabernaculi domus Domini
49 Aruni na wana wake walitoa sadaka katika madhabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketeza; na sadaka katika madhabahu ya uvumba kwa kazi zote katika pa patakatifu. Hizi sadaka zilifanya maombezi kwa ajili ya Waisraeli, kwa kadiri ya yote ambayo Musa mtumishi wa Mungu aliwaamuru.
Aaron vero et filii eius adolebant incensum super altare holocausti et super altare thymiamatis in omne opus sancti sanctorum et ut precarentur pro Israhel iuxta omnia quae praecepit Moses servus Dei
50 Uzao wa Aruni una kumbukwa kama ifuatavyo: Mwana wa Aruni alikuwa Eleazari. Mwana Eleazari alikuwa Finehasi. Mwana wa Finehasi alikuwa Abishua.
hii sunt autem filii Aaron Eleazar filius eius Finees filius eius Abisue filius eius
51 Mwana wa Abishua alikuwa Buki. Mwana wa Buki alikuwa Uzi. Mwana wa Buki alikuwa Zerahia.
Bocci filius eius Ozi filius eius Zaraia filius eius
52 Mwana wa Zerahia alikuwa Meraiothi. Mwana wa Meraiothi alikuwa Amaria. Mwana wa Amaria alikuwa Ahitubi.
Meraioth filius eius Amaria filius eius Ahitob filius eius
53 Mwana wa Ahitubi alikuwa Zadoki. Mwana wa Zadoki alikuwa Ahimazi.
Sadoc filius eius Achimaas filius eius
54 Hizi ni sehemu ambazo wazao wa Aruni walipangiwa kuishi, wazao wa Aruni ambao walitoka katika koo za Wakohathi (maeneo ya kwanza yalikuwa yao).
et haec habitacula eorum per vicos atque confinia filiorum scilicet Aaron iuxta cognationes Caathitarum ipsis enim sorte contigerat
55 Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda na nchi ya malisho,
dederunt igitur eis Hebron in terra Iuda et suburbana eius per circuitum
56 lakini maeneo ya mji na vijiji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
agros autem civitatis et villas Chaleb filio Iephonne
57 Kwa wazao wa Aruni waliwapa: Hebroni ( mji wa makimblio), na Libina pamoja na nchi ya malisho, Yatiri, Eshitemoa pamoja na nchi ya malisho,
porro filiis Aaron dederunt civitates ad confugiendum Hebron et Lobna et suburbana eius
58 Hileni pamoja na nchi ya malisho, na Debiri pamoja na nchi ya malisho.
Iether quoque et Esthmo cum suburbanis suis sed et Helon et Dabir cum suburbanis suis
59 Waliwapa uzao wa Aruni: Ashani pamoja na nchi ya malisho na Bethi Shemeshi pamoja na nchi ya malisho;
Asan quoque et Bethsemes et suburbana eorum
60 na kutoka katika kabila la Benjamini walipewa Geba pamoja na nchi ya malisho, Alemethi pamoja na nchi ya malisho, na Anothothi na nchi ya malisho. Jumla ya miji yao ilikuwa kumi na tatu.
de tribu autem Beniamin Gabee et suburbana eius et Almath cum suburbanis suis Anathoth quoque cum suburbanis suis omnes civitates tredecim per cognationes suas
61 Uzao mwengine wa Kohathi waliwapa kwa sehemu miji kumi kutoka kwa kabila la Manase.
filiis autem Caath residuis de cognatione sua dederunt ex dimidia tribu Manasse in possessionem urbes decem
62 Kwa uzao wa Gerishomu kwa koo zao tofauti walipewa miji kumi na tatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri, Naftali, na nusu ya kabila la Manase huko Bashani.
porro filiis Gersom per cognationes suas de tribu Isachar et de tribu Aser et de tribu Nepthali et de tribu Manasse in Basan urbes tredecim
63 Kwa uzao wa Merari walipewa miji kumi, kulingana na koo zao, kutoka kwa makabila ya Rubeni, Gadi, na Zebuluni.
filiis autem Merari per cognationes suas de tribu Ruben et de tribu Gad et de tribu Zabulon dederunt sorte civitates duodecim
64 Hivyo watu wa Israeli walitoa hii miji pamoja na nchi za malisho kwa Walawi.
dederunt quoque filii Israhel Levitis civitates et suburbana earum
65 Walitoa kwa sehemu miji iliyo tajwa awali kutoka katika kabila la Yuda, Simeoni, na Benjamini.
dederuntque per sortem ex tribu filiorum Iuda et ex tribu filiorum Symeon et ex tribu filiorum Beniamin urbes has quas vocaverunt nominibus suis
66 Kwa baadhi ya koo za Wakohathi walitoa miji kutoka kwa kabila la Efraimu.
et his qui erant ex cognatione filiorum Caath fueruntque civitates in terminis eorum de tribu Ephraim
67 Waliwapa: Shekemu ( mji wa makimbilio) pamoja na nchi ya malisho katika milima ya Efraimu, Gezeri na nchi ya malisho,
dederunt ergo eis urbes ad confugiendum Sychem cum suburbanis suis in monte Ephraim et Gazer cum suburbanis suis
68 Jokimeamu pamoja na nchi ya malisho, Bethi Horoni pamoja na nchi ya malisho,
Hicmaam quoque cum suburbanis suis et Bethoron similiter
69 Aiyaloni pamoja na nchi ya malisho, na Gathi Rimoni pamoja na nchi ya malisho.
necnon et Helon cum suburbanis suis et Gethremmon in eundem modum
70 Nusu ya kabila la Manase waliwapa Wakohathi: Aneri pamoja na nchi ya malisho na Bileamu pamoja na nchi ya malisho. Hizi zikawa mali za koo za Wakohathi.
porro ex dimidia tribu Manasse Aner et suburbana eius Balaam et suburbana eius his videlicet qui de cognatione filiorum Caath reliqui erant
71 Kwa uzao wa Gerishomu kutoka koo za nusu ya kabila la Manase, waliwapa: Golani huko Baashani na nchi ya malisho na Ashitarothi pamoja na nchi ya malisho.
filiis autem Gersom de cognatione dimidiae tribus Manasse Gaulon in Basan et suburbana eius et Astharoth cum suburbanis suis
72 Kabila la Isakari liliwapa uzao wa Gerishomu: Kedeshi pamoja na nchi ya malisho, Dabera pamoja na nchi ya malisho,
de tribu Isachar Cedes et suburbana eius et Dabereth cum suburbanis suis
73 Ramothi pamoja na nchi ya malisho, na Anemu pamoja na nchi ya malisho.
Ramoth quoque et suburbana illius et Anem cum suburbanis suis
74 Isakari alipokea kutoka kwa kabila la Asheri: Mashali pamoja na nchi ya malisho, Abdoni pamoja na nchi ya malisho,
de tribu vero Aser Masal cum suburbanis suis et Abdon similiter
75 Hukoki pamoja na nchi ya malisho, na Rehobu pamoja na nchi ya malisho.
Acac quoque et suburbana eius et Roob cum suburbanis suis
76 Walipokea kutoka kabila la Naftali: Kedeshi iliyo Galileya pamoja na nchi ya malisho, Hamoni pamoja na nchi ya malisho, na Kiriathaimu pamoja na nchi ya malisho.
porro de tribu Nepthali Cedes in Galilea et suburbana eius Amon cum suburbanis suis et Cariathaim et suburbana eius
77 Kwa Walawi wengine, uzao wa Merari, walipewa kutoka kabila la Zebuluni: Rimono pamoja na nchi ya malisho na Tabori pamoja na nchi ya malisho.
filiis autem Merari residuis de tribu Zabulon Remmono et suburbana eius et Thabor cum suburbanis suis
78 Kwa wao pia walipewa, upande wa pili wa Yordani huko Yeriko, kwa upande wa mashariki mwa mto: Bezeri katika jangwa pamoja na nchi ya malisho, Yahzahi pamoja na nchi ya malisho,
trans Iordanem quoque ex adverso Hiericho contra orientem Iordanis de tribu Ruben Bosor in solitudine cum suburbanis suis et Iasa cum suburbanis suis
79 Kedemothi pamoka na nchi ya malisho, ma Mefathi pamoja na nchi ya malisho. Hizi zilitolewa kutoka kabila la Rubeni.
Cademoth quoque et suburbana eius et Miphaath cum suburbanis suis
80 Walawi walipokea kutoka kabila la Gadi: Ramothi ya Gileadi pamoja na nchi ya malisho, Mahanaimu pamoja na nchi ya malisho,
necnon de tribu Gad Ramoth in Galaad et suburbana eius et Manaim cum suburbanis suis
81 Heshiboni pamoja na nchi ya malisho, na Yazeri pamoja na nchi ya malisho.
sed et Esbon cum suburbanis eius et Iezer cum suburbanis suis

< 1 Nyakati 6 >