< 1 Nyakati 6 >

1 Wana wa Levi walikuwa Gerishoni, Kohathi, na Merari.
Fils de Lévi: Guerschom, Kehath et Merari.
2 Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
Fils de Kehath: Amram, Jitsehar, Hébron et Uziel.
3 Wana wa Amramu walikuwa Aruni, Musa, Miriamu. Wana wa Aruni walikuwa Nadabu, Abihu, Eleazari, na Ithamari.
Fils d’Amram: Aaron et Moïse; et Marie. Fils d’Aaron: Nadab, Abihu, Éléazar et Ithamar.
4 Eleazari akawa baba wa Finehasi, na Finehasi akawa baba wa Abishua.
Éléazar engendra Phinées; Phinées engendra Abischua;
5 Abishua akawa baba wa Buki, na Buki akawa baba wa Uzi.
Abischua engendra Bukki; Bukki engendra Uzzi;
6 Uzi akawa baba wa Zerahia, na Zerahia akawa baba wa Meraioti.
Uzzi engendra Zerachja; Zerachja engendra Merajoth;
7 Meraioti akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
Merajoth engendra Amaria; Amaria engendra Achithub;
8 Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Ahimazi.
Achithub engendra Tsadok; Tsadok engendra Achimaats;
9 Ahimazi akawa baba wa Azaria, na Azaria akawa baba wa Yohanani.
Achimaats engendra Azaria; Azaria engendra Jochanan;
10 Yohanani akawa baba wa Azaria, aliye hudumu katika hekalu alilo lijenga Sulemani ndaniya Yerusalemu.
Jochanan engendra Azaria, qui exerça le sacerdoce dans la maison que Salomon bâtit à Jérusalem;
11 Azaria akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
Azaria engendra Amaria; Amaria engendra Achithub;
12 Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Shalumu.
Achithub engendra Tsadok; Tsadok engendra Schallum;
13 Shalumu akawa baba wa Hilikia, na Hilikia akawa baba wa Azaria.
Schallum engendra Hilkija; Hilkija engendra Azaria;
14 Azaria akawa baba Seraia, na Seraia akawa baba wa Yehozadaki.
et Azaria engendra Seraja; Seraja engendra Jehotsadak,
15 Yehozadaki akaenda matekani Yahweh alipo wapeleka utumwani Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Nebukadneza.
Jehotsadak s’en alla quand l’Éternel emmena en captivité Juda et Jérusalem par Nebucadnetsar.
16 Wana wa Levi walikuwa Gerishomu, Kohathi, na Merari.
Fils de Lévi: Guerschom, Kehath et Merari.
17 Wana wa Gerishomu walikuwa Libini na Shimei.
Voici les noms des fils de Guerschom: Libni et Schimeï.
18 Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
Fils de Kehath: Amram, Jitsehar, Hébron et Uziel.
19 Wana wa Merari walikuwa Mahili na Mushi. Hawa walikuwa koo za Walawi kwa familia za baba zao.
Fils de Merari: Machli et Muschi. Ce sont là les familles de Lévi, selon leurs pères.
20 Uzao wa Gerishomu ulianza na mwanae Libini. Mwana wa Libini alikuwa Jahathi. Mwanae alikuwa Zima.
De Guerschom: Libni, son fils; Jachath, son fils; Zimma, son fils;
21 Mwanae alikuwa Yoa. Mwanae alikuwa alikuwa Ido. Mwanae alikuwa Zera. Mwanae alikuwa Yeatherai.
Joach, son fils; Iddo, son fils; Zérach, son fils; Jeathraï, son fils.
22 Uzao wa Kohathi ulianza na mwanae Aminadabu. Mwanae alikuwa Kora. Mwanae alikuwa Asiri.
Fils de Kehath: Amminadab, son fils; Koré, son fils; Assir, son fils;
23 Mwanae alikuwa Elikana. Mwanae alikuwa Ebiasa. Mwanae alikuwa Asiri.
Elkana, son fils; Ebjasaph, son fils; Assir, son fils;
24 Mwanae alikuwa Tahathi. Mwanae alikuwa Urieli. Mwanae alikuwa uzia. Mwanae alikuwa Shauli.
Thachath, son fils; Uriel, son fils; Ozias, son fils; Saül, son fils.
25 Wana wa Elikana walikuwa Amasai, Ahimothi, na Elikana.
Fils d’Elkana: Amasaï et Achimoth;
26 Mwana wa huyu Elikana wa pili alikuwa Zofai. Mwanae alikuwa Nahathi.
Elkana, son fils; Elkana Tsophaï, son fils; Nachath, son fils;
27 Mwanae alikuwa Eliabu. Mwanae alikuwa Yehoramu. Mwanae alikuwa Elikana.
Éliab, son fils; Jerocham, son fils; Elkana, son fils;
28 Wana wa Samwali walikuwa mzaliwa wa kwanza, Yoeli, na Abija, wa pili.
et les fils de Samuel, le premier-né Vaschni et Abija.
29 Mwana wa Merari alikuwa Mahili. Mwanae alikuwa Libini.
Fils de Merari: Machli; Libni, son fils; Schimeï, son fils; Uzza, son fils;
30 Mwanae alikuwa Shimei. Mwanae alikuwa Uza. Mwanae alikuwa Shimea. Mwanae alikuwa Hagia. Mwana alikuwa Asaia.
Schimea, son fils; Hagguija, son fils; Asaja, son fils.
31 Haya ndio majina ya wanaume ambao Daudi waliwaeka kusimamia muziki katika nyumba ya Yahweh, baada ya sanduku kuja hapo.
Voici ceux que David établit pour la direction du chant dans la maison de l’Éternel, depuis que l’arche eut un lieu de repos:
32 Walitumika kwa kuimba mbele ya hema, hema la kukutania, mpaka Sulemani alipo jenga nyumba ya Yahweh ndani ya Yerusalemu. Walikamilisha wajibu wao kwa kadiri ya maelekezo waliopewa.
ils remplirent les fonctions de chantres devant le tabernacle, devant la tente d’assignation, jusqu’à ce que Salomon eût bâti la maison de l’Éternel à Jérusalem, et ils faisaient leur service d’après la règle qui leur était prescrite.
33 Hawa walitumika pamoja na wana wao. Katika makabila ya Wakohathi alitoka Hemani mwana muziki. Babu zake walikuwa hawa, kurudi nyuma ya wakati: Hemani alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Samweli.
Voici ceux qui officiaient avec leurs fils. D’entre les fils des Kehathites: Héman, le chantre, fils de Joël, fils de Samuel,
34 Samweli alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Yerohamu. Yerohamu alikuwa mwana wa Elieli. Elieli alikuwa mwana wa Toa.
fils d’Elkana, fils de Jerocham, fils d’Éliel, fils de Thoach,
35 Toa alikuwa mwana wa Zufi. Zufi alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Mahathi. Mahathi alikuwa mwana wa Amasai. Amasai alikuwa mwana wa Elikana.
fils de Tsuph, fils d’Elkana, fils de Machath, fils d’Amasaï,
36 Elikana alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Azaria. Azaria alikuwa mwana wa Zefania.
fils d’Elkana, fils de Joël, fils d’Azaria, fils de Sophonie,
37 Zefania alikuwa mwana wa Tahathi. Tahathi alikuwa mwana wa Asiri. Asiri alikuwa mwana wa Ebiasa. Ebiasa alikuwa mwana wa Kora.
fils de Thachath, fils d’Assir, fils d’Ebjasaph, fils de Koré,
38 Kora alikuwa mwana wa Izhari. Izhari alikuwa mwana wa Kohathi. Kohathi alikuwa mwana wa Levi. Levi alikuwa mwana wa Israeli.
fils de Jitsehar, fils de Kehath, fils de Lévi, fils d’Israël.
39 Msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliye simama mkono wake wa kuume. Asafu alikuwa mwana Berekia. Berekia alikuwa mwana wa Shimea.
Son frère Asaph, qui se tenait à sa droite, Asaph, fils de Bérékia, fils de Schimea,
40 Shimea alikuwa mwana Mikaeli. Mikaeli alikuwa mwana wa Baaseia. Baaseia alikuwa mwana wa Malikiya.
fils de Micaël, fils de Baaséja, fils de Malkija,
41 Malikiya alikuwa mwana wa Ethini. Ethini alikuwa mwana wa Zera. Zera alikuwa mwana wa Adaia.
fils d’Éthni, fils de Zérach, fils d’Adaja,
42 Adaia alikuwa mwana wa Ethani. Ethani alikuwa mwana wa Zima. Zima alikuwa mwana wa Shimei.
fils d’Éthan, fils de Zimma, fils de Schimeï,
43 Shimei alikuwa mwana wa Yahathi. Yahathi alikuwa mwana wa Gerishomu. Gerishomu alikuwa mwana wa Levi.
fils de Jachath, fils de Guerschom, fils de Lévi.
44 Upande wa mkono wa koshoto wa Hemani walikuwa wasaidizi wake wana wa Merari. Alikuwa Ethani mwana wa Kishi. Kishi alikuwa mwana wa Abdi. Abdi alikuwa mwana wa Maluki.
Fils de Merari, leurs frères, à la gauche; Éthan, fils de Kischi, fils d’Abdi, fils de Malluc,
45 Maluki alikuwa mwana wa Hashabia. Hashabia alikuwa mwana wa Amazia. Amazia alikuwa mwana wa Hilikia.
fils de Haschabia, fils d’Amatsia, fils de Hilkija,
46 Hilikia alikuwa mwana wa Amzi. Amzi alikuwa mwana wa Bani. Bani alikuwa mwana wa Shemeri.
fils d’Amtsi, fils de Bani, fils de Schémer,
47 Shemeri alikuwa mwana wa Mahili. Mahili alikuwa mwana wa Mushi. Mushi alikuwa mwana wa Merari. Merari alikuwa mwana wa Levi.
fils de Machli, fils de Muschi, fils de Merari, fils de Lévi.
48 Walawi, alipangiwa kufanya kazi zote za hema, nyumba ya Mungu.
Leurs frères, les Lévites, étaient chargés de tout le service du tabernacle, de la maison de Dieu.
49 Aruni na wana wake walitoa sadaka katika madhabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketeza; na sadaka katika madhabahu ya uvumba kwa kazi zote katika pa patakatifu. Hizi sadaka zilifanya maombezi kwa ajili ya Waisraeli, kwa kadiri ya yote ambayo Musa mtumishi wa Mungu aliwaamuru.
Aaron et ses fils offraient les sacrifices sur l’autel des holocaustes et l’encens sur l’autel des parfums, ils remplissaient toutes les fonctions dans le lieu très saint, et faisaient l’expiation pour Israël, selon tout ce qu’avait ordonné Moïse, serviteur de Dieu.
50 Uzao wa Aruni una kumbukwa kama ifuatavyo: Mwana wa Aruni alikuwa Eleazari. Mwana Eleazari alikuwa Finehasi. Mwana wa Finehasi alikuwa Abishua.
Voici les fils d’Aaron: Éléazar, son fils; Phinées, son fils: Abischua, son fils;
51 Mwana wa Abishua alikuwa Buki. Mwana wa Buki alikuwa Uzi. Mwana wa Buki alikuwa Zerahia.
Bukki, son fils; Uzzi, son fils; Zerachja, son fils;
52 Mwana wa Zerahia alikuwa Meraiothi. Mwana wa Meraiothi alikuwa Amaria. Mwana wa Amaria alikuwa Ahitubi.
Merajoth, son fils; Amaria, son fils; Achithub, son fils;
53 Mwana wa Ahitubi alikuwa Zadoki. Mwana wa Zadoki alikuwa Ahimazi.
Tsadok, son fils; Achimaats, son fils.
54 Hizi ni sehemu ambazo wazao wa Aruni walipangiwa kuishi, wazao wa Aruni ambao walitoka katika koo za Wakohathi (maeneo ya kwanza yalikuwa yao).
Voici leurs habitations, selon leurs enclos, dans les limites qui leur furent assignées. Aux fils d’Aaron de la famille des Kehathites, indiqués les premiers par le sort,
55 Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda na nchi ya malisho,
on donna Hébron, dans le pays de Juda, et la banlieue qui l’entoure;
56 lakini maeneo ya mji na vijiji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
mais le territoire de la ville et ses villages furent accordés à Caleb, fils de Jephunné.
57 Kwa wazao wa Aruni waliwapa: Hebroni ( mji wa makimblio), na Libina pamoja na nchi ya malisho, Yatiri, Eshitemoa pamoja na nchi ya malisho,
Aux fils d’Aaron on donna la ville de refuge Hébron, Libna et sa banlieue, Jatthir, Eschthemoa et sa banlieue,
58 Hileni pamoja na nchi ya malisho, na Debiri pamoja na nchi ya malisho.
Hilen et sa banlieue, Debir et sa banlieue,
59 Waliwapa uzao wa Aruni: Ashani pamoja na nchi ya malisho na Bethi Shemeshi pamoja na nchi ya malisho;
Aschan et sa banlieue, Beth-Schémesch et sa banlieue;
60 na kutoka katika kabila la Benjamini walipewa Geba pamoja na nchi ya malisho, Alemethi pamoja na nchi ya malisho, na Anothothi na nchi ya malisho. Jumla ya miji yao ilikuwa kumi na tatu.
et de la tribu de Benjamin, Guéba et sa banlieue, Allémeth et sa banlieue, Anathoth et sa banlieue. Total de leurs villes: treize villes, d’après leurs familles.
61 Uzao mwengine wa Kohathi waliwapa kwa sehemu miji kumi kutoka kwa kabila la Manase.
Les autres fils de Kehath eurent par le sort dix villes des familles de la tribu d’Éphraïm, de la tribu de Dan et de la demi-tribu de Manassé.
62 Kwa uzao wa Gerishomu kwa koo zao tofauti walipewa miji kumi na tatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri, Naftali, na nusu ya kabila la Manase huko Bashani.
Les fils de Guerschom, d’après leurs familles, eurent treize villes de la tribu d’Issacar, de la tribu d’Aser, de la tribu de Nephthali et de la tribu de Manassé en Basan.
63 Kwa uzao wa Merari walipewa miji kumi, kulingana na koo zao, kutoka kwa makabila ya Rubeni, Gadi, na Zebuluni.
Les fils de Merari, d’après leurs familles, eurent par le sort douze villes de la tribu de Ruben, de la tribu de Gad et de la tribu de Zabulon.
64 Hivyo watu wa Israeli walitoa hii miji pamoja na nchi za malisho kwa Walawi.
Les enfants d’Israël donnèrent aux Lévites les villes et leurs banlieues.
65 Walitoa kwa sehemu miji iliyo tajwa awali kutoka katika kabila la Yuda, Simeoni, na Benjamini.
Ils donnèrent par le sort, de la tribu des fils de Juda, de la tribu des fils de Siméon et de la tribu des fils de Benjamin, ces villes qu’ils désignèrent nominativement.
66 Kwa baadhi ya koo za Wakohathi walitoa miji kutoka kwa kabila la Efraimu.
Et pour les autres familles des fils de Kehath les villes de leur territoire furent de la tribu d’Éphraïm.
67 Waliwapa: Shekemu ( mji wa makimbilio) pamoja na nchi ya malisho katika milima ya Efraimu, Gezeri na nchi ya malisho,
Ils leur donnèrent la ville de refuge Sichem et sa banlieue, dans la montagne d’Éphraïm, Guézer et sa banlieue,
68 Jokimeamu pamoja na nchi ya malisho, Bethi Horoni pamoja na nchi ya malisho,
Jokmeam et sa banlieue, Beth-Horon et sa banlieue,
69 Aiyaloni pamoja na nchi ya malisho, na Gathi Rimoni pamoja na nchi ya malisho.
Ajalon et sa banlieue, et Gath-Rimmon et sa banlieue;
70 Nusu ya kabila la Manase waliwapa Wakohathi: Aneri pamoja na nchi ya malisho na Bileamu pamoja na nchi ya malisho. Hizi zikawa mali za koo za Wakohathi.
et de la demi-tribu de Manassé, Aner et sa banlieue, et Bileam et sa banlieue, pour la famille des autres fils de Kehath.
71 Kwa uzao wa Gerishomu kutoka koo za nusu ya kabila la Manase, waliwapa: Golani huko Baashani na nchi ya malisho na Ashitarothi pamoja na nchi ya malisho.
On donna aux fils de Guerschom: de la famille de la demi-tribu de Manassé, Golan en Basan et sa banlieue, et Aschtaroth et sa banlieue;
72 Kabila la Isakari liliwapa uzao wa Gerishomu: Kedeshi pamoja na nchi ya malisho, Dabera pamoja na nchi ya malisho,
de la tribu d’Issacar, Kédesch et sa banlieue, Dobrath et sa banlieue,
73 Ramothi pamoja na nchi ya malisho, na Anemu pamoja na nchi ya malisho.
Ramoth et sa banlieue, et Anem et sa banlieue;
74 Isakari alipokea kutoka kwa kabila la Asheri: Mashali pamoja na nchi ya malisho, Abdoni pamoja na nchi ya malisho,
de la tribu d’Aser, Maschal et sa banlieue, Abdon et sa banlieue,
75 Hukoki pamoja na nchi ya malisho, na Rehobu pamoja na nchi ya malisho.
Hukok et sa banlieue, et Rehob et sa banlieue;
76 Walipokea kutoka kabila la Naftali: Kedeshi iliyo Galileya pamoja na nchi ya malisho, Hamoni pamoja na nchi ya malisho, na Kiriathaimu pamoja na nchi ya malisho.
et de la tribu de Nephthali, Kédesch en Galilée et sa banlieue, Hammon et sa banlieue, et Kirjathaïm et sa banlieue.
77 Kwa Walawi wengine, uzao wa Merari, walipewa kutoka kabila la Zebuluni: Rimono pamoja na nchi ya malisho na Tabori pamoja na nchi ya malisho.
On donna au reste des Lévites, aux fils de Merari: de la tribu de Zabulon, Rimmono et sa banlieue, et Thabor et sa banlieue;
78 Kwa wao pia walipewa, upande wa pili wa Yordani huko Yeriko, kwa upande wa mashariki mwa mto: Bezeri katika jangwa pamoja na nchi ya malisho, Yahzahi pamoja na nchi ya malisho,
et de l’autre côté du Jourdain, vis-à-vis de Jéricho, à l’orient du Jourdain: de la tribu de Ruben, Betser au désert et sa banlieue, Jahtsa et sa banlieue,
79 Kedemothi pamoka na nchi ya malisho, ma Mefathi pamoja na nchi ya malisho. Hizi zilitolewa kutoka kabila la Rubeni.
Kedémoth et sa banlieue, et Méphaath et sa banlieue;
80 Walawi walipokea kutoka kabila la Gadi: Ramothi ya Gileadi pamoja na nchi ya malisho, Mahanaimu pamoja na nchi ya malisho,
et de la tribu de Gad, Ramoth en Galaad et sa banlieue, Mahanaïm et sa banlieue,
81 Heshiboni pamoja na nchi ya malisho, na Yazeri pamoja na nchi ya malisho.
Hesbon et sa banlieue, et Jaezer et sa banlieue.

< 1 Nyakati 6 >