< 1 Nyakati 6 >

1 Wana wa Levi walikuwa Gerishoni, Kohathi, na Merari.
Fils de Lévi: Gersom, Caath et Mérari.
2 Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
Fils de Caath: Amram, Isaar et Oziel.
3 Wana wa Amramu walikuwa Aruni, Musa, Miriamu. Wana wa Aruni walikuwa Nadabu, Abihu, Eleazari, na Ithamari.
Fils d’Amram: Aaron, Moïse et Marie. — Fils d’Aaron: Nadab, Abiu, Eléazar et Ithamar. —
4 Eleazari akawa baba wa Finehasi, na Finehasi akawa baba wa Abishua.
Eléazar engendra Phinées; Phinées engendra Abisué;
5 Abishua akawa baba wa Buki, na Buki akawa baba wa Uzi.
Abisué engendra Bocci; Bocci engendra Ozi;
6 Uzi akawa baba wa Zerahia, na Zerahia akawa baba wa Meraioti.
Ozi engendra Zaraïas; Zaraïas engendra Méraïoth;
7 Meraioti akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
Méraïoth engendra Amarias; Amarias engendra Achitob;
8 Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Ahimazi.
Achitob engendra Sadoc; Sadoc engendra Achimaas;
9 Ahimazi akawa baba wa Azaria, na Azaria akawa baba wa Yohanani.
Achimaas engendra Azarias; Azarias engendra Johanan;
10 Yohanani akawa baba wa Azaria, aliye hudumu katika hekalu alilo lijenga Sulemani ndaniya Yerusalemu.
Johanan engendra Azarias: c’est lui qui exerça le sacerdoce dans la maison que Salomon bâtit à Jérusalem;
11 Azaria akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
Azarias engendra Amarias; Amarias engendra Achitob;
12 Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Shalumu.
Achitob engendra Sadoc; Sadoc engendra Sellum;
13 Shalumu akawa baba wa Hilikia, na Hilikia akawa baba wa Azaria.
Sellum engendra Helcias; Helcias engendra Azarias;
14 Azaria akawa baba Seraia, na Seraia akawa baba wa Yehozadaki.
Azarias engendra Saraïas; Saraïas engendra Josédec.
15 Yehozadaki akaenda matekani Yahweh alipo wapeleka utumwani Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Nebukadneza.
Josédec partit pour l’exil quand Yahweh fit emmener en captivité Juda et Jérusalem par l’intermédiaire de Nabuchodonosor.
16 Wana wa Levi walikuwa Gerishomu, Kohathi, na Merari.
Fils de Lévi: Gersom, Caath et Mérari. —
17 Wana wa Gerishomu walikuwa Libini na Shimei.
Voici les noms des fils de Gersom: Lobni et Séméï. —
18 Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
Fils de Caath: Amram, Isaar, Hébron et Oziel. —
19 Wana wa Merari walikuwa Mahili na Mushi. Hawa walikuwa koo za Walawi kwa familia za baba zao.
Fils de Mérari: Moholi et Musi. Voici les familles de Lévi selon leurs pères:
20 Uzao wa Gerishomu ulianza na mwanae Libini. Mwana wa Libini alikuwa Jahathi. Mwanae alikuwa Zima.
De Gersom: Lobni, son fils; Jahath, son fils; Zamma, son fils;
21 Mwanae alikuwa Yoa. Mwanae alikuwa alikuwa Ido. Mwanae alikuwa Zera. Mwanae alikuwa Yeatherai.
Joah, son fils; Addo, son fils; Zara, son fils; Jethraï, son fils. —
22 Uzao wa Kohathi ulianza na mwanae Aminadabu. Mwanae alikuwa Kora. Mwanae alikuwa Asiri.
Fils de Caath: Aminadab, son fils; Coré, son fils; Asir, son fils;
23 Mwanae alikuwa Elikana. Mwanae alikuwa Ebiasa. Mwanae alikuwa Asiri.
Elcana, son fils; Abiasaph, son fils; Asir, son fils;
24 Mwanae alikuwa Tahathi. Mwanae alikuwa Urieli. Mwanae alikuwa uzia. Mwanae alikuwa Shauli.
Thahath, son fils; Uriel, son fils; Ozias, son fils; Saül, son fils.
25 Wana wa Elikana walikuwa Amasai, Ahimothi, na Elikana.
Fils d’Elcana: Amasaï et Achimoth;
26 Mwana wa huyu Elikana wa pili alikuwa Zofai. Mwanae alikuwa Nahathi.
Elcana, son fils; Sophaï, son fils; Nahath, son fils;
27 Mwanae alikuwa Eliabu. Mwanae alikuwa Yehoramu. Mwanae alikuwa Elikana.
Eliab, son fils; Jéroham, son fils; Elcana, son fils.
28 Wana wa Samwali walikuwa mzaliwa wa kwanza, Yoeli, na Abija, wa pili.
Fils de Samuel: le premier-né Vasséni, et Abia. —
29 Mwana wa Merari alikuwa Mahili. Mwanae alikuwa Libini.
Fils de Mérari: Moholi; Lobni, son fils; Séméï, son fils; Oza, son fils;
30 Mwanae alikuwa Shimei. Mwanae alikuwa Uza. Mwanae alikuwa Shimea. Mwanae alikuwa Hagia. Mwana alikuwa Asaia.
Sammaa, son fils; Haggia, son fils; Asaïa, son fils.
31 Haya ndio majina ya wanaume ambao Daudi waliwaeka kusimamia muziki katika nyumba ya Yahweh, baada ya sanduku kuja hapo.
Voici ceux que David établit pour diriger le chant dans la maison de Yahweh, depuis que l’arche eut un lieu de repos:
32 Walitumika kwa kuimba mbele ya hema, hema la kukutania, mpaka Sulemani alipo jenga nyumba ya Yahweh ndani ya Yerusalemu. Walikamilisha wajibu wao kwa kadiri ya maelekezo waliopewa.
ils remplirent les fonctions de chantres devant la Demeure de la tente de réunion, jusqu’à ce que Salomon eût bâti la maison de Yahweh à Jérusalem, et ils se tenaient à leur service selon leur règlement. —
33 Hawa walitumika pamoja na wana wao. Katika makabila ya Wakohathi alitoka Hemani mwana muziki. Babu zake walikuwa hawa, kurudi nyuma ya wakati: Hemani alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Samweli.
Voici ceux qui officiaient avec leurs fils: — D’entre les fils des Caathites: Héman, le chantre, fils de Joël, fils de Samuel,
34 Samweli alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Yerohamu. Yerohamu alikuwa mwana wa Elieli. Elieli alikuwa mwana wa Toa.
fils d’Elcana, fils de Jéroham, fils d’Eliel, fils de Thohu,
35 Toa alikuwa mwana wa Zufi. Zufi alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Mahathi. Mahathi alikuwa mwana wa Amasai. Amasai alikuwa mwana wa Elikana.
fils de Suph, fils d’Elcana, fils de Mahath, fils d’Amasaï,
36 Elikana alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Azaria. Azaria alikuwa mwana wa Zefania.
fils d’Elcana, fils de Joël, fils d’Azarias, fils de Sophonias,
37 Zefania alikuwa mwana wa Tahathi. Tahathi alikuwa mwana wa Asiri. Asiri alikuwa mwana wa Ebiasa. Ebiasa alikuwa mwana wa Kora.
fils de Thahath, fils d’Asir, fils d’Abiasaph, fils de Coré,
38 Kora alikuwa mwana wa Izhari. Izhari alikuwa mwana wa Kohathi. Kohathi alikuwa mwana wa Levi. Levi alikuwa mwana wa Israeli.
fils d’Isaar, fils de Caath, fils de Lévi, fils d’Israël.
39 Msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliye simama mkono wake wa kuume. Asafu alikuwa mwana Berekia. Berekia alikuwa mwana wa Shimea.
— Son frère Asaph, qui se tenait à sa droite: Asaph, fils de Barachias, fils de Samaa,
40 Shimea alikuwa mwana Mikaeli. Mikaeli alikuwa mwana wa Baaseia. Baaseia alikuwa mwana wa Malikiya.
fils de Michaël, fils de Basaïas, fils de Melchias,
41 Malikiya alikuwa mwana wa Ethini. Ethini alikuwa mwana wa Zera. Zera alikuwa mwana wa Adaia.
fils d’Athanaï, fils de Zara, fils d’Adaïa,
42 Adaia alikuwa mwana wa Ethani. Ethani alikuwa mwana wa Zima. Zima alikuwa mwana wa Shimei.
fils d’Ethan, fils de Zamma, fils de Séméï,
43 Shimei alikuwa mwana wa Yahathi. Yahathi alikuwa mwana wa Gerishomu. Gerishomu alikuwa mwana wa Levi.
fils de Jeth, fils de Gersom, fils de Lévi.
44 Upande wa mkono wa koshoto wa Hemani walikuwa wasaidizi wake wana wa Merari. Alikuwa Ethani mwana wa Kishi. Kishi alikuwa mwana wa Abdi. Abdi alikuwa mwana wa Maluki.
— Fils de Mérari, leurs frères, à la gauche: Ethan, fils de Cusi, fils d’Abdi, fils de Maloch,
45 Maluki alikuwa mwana wa Hashabia. Hashabia alikuwa mwana wa Amazia. Amazia alikuwa mwana wa Hilikia.
fils de Hasabias, fils d’Amasias, fils de Helcias,
46 Hilikia alikuwa mwana wa Amzi. Amzi alikuwa mwana wa Bani. Bani alikuwa mwana wa Shemeri.
fils d’Amasaï, fils de Boni, fils de Somer,
47 Shemeri alikuwa mwana wa Mahili. Mahili alikuwa mwana wa Mushi. Mushi alikuwa mwana wa Merari. Merari alikuwa mwana wa Levi.
fils de Moholi, fils de Musi, fils de Mérari, fils de Lévi.
48 Walawi, alipangiwa kufanya kazi zote za hema, nyumba ya Mungu.
Leurs frères, les lévites, étaient chargés de tout le service du tabernacle de la maison de Yahweh.
49 Aruni na wana wake walitoa sadaka katika madhabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketeza; na sadaka katika madhabahu ya uvumba kwa kazi zote katika pa patakatifu. Hizi sadaka zilifanya maombezi kwa ajili ya Waisraeli, kwa kadiri ya yote ambayo Musa mtumishi wa Mungu aliwaamuru.
Mais Aaron et ses fils brûlaient les victimes sur l’autel des holocaustes et l’encens sur l’autel des parfums; ils avaient à remplir tout le ministère du saint des saints, et à faire l’expiation pour Israël, selon tout ce qu’avait ordonné Moïse, serviteur de Dieu.
50 Uzao wa Aruni una kumbukwa kama ifuatavyo: Mwana wa Aruni alikuwa Eleazari. Mwana Eleazari alikuwa Finehasi. Mwana wa Finehasi alikuwa Abishua.
Voici les fils d’Aaron: Eléazar, son fils; Phinées, son fils; Abisué, son fils;
51 Mwana wa Abishua alikuwa Buki. Mwana wa Buki alikuwa Uzi. Mwana wa Buki alikuwa Zerahia.
Bocci, son fils; Ozi, son fils; Zaraïas, son fils;
52 Mwana wa Zerahia alikuwa Meraiothi. Mwana wa Meraiothi alikuwa Amaria. Mwana wa Amaria alikuwa Ahitubi.
Méraïoth, son fils; Amarias, son fils; Achitob, son fils;
53 Mwana wa Ahitubi alikuwa Zadoki. Mwana wa Zadoki alikuwa Ahimazi.
Sadoc, son fils; Achimaas, son fils.
54 Hizi ni sehemu ambazo wazao wa Aruni walipangiwa kuishi, wazao wa Aruni ambao walitoka katika koo za Wakohathi (maeneo ya kwanza yalikuwa yao).
Voici leurs habitations, selon leurs enceintes, dans leurs territoires: — Aux fils d’Aaron, de la famille des Caathites, désignés les premiers par le sort,
55 Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda na nchi ya malisho,
on donna Hébron, dans le pays de Juda, et les pâturages qui l’entourent;
56 lakini maeneo ya mji na vijiji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
mais on donna le territoire de la ville et ses villages à Caleb, fils de Jéphoné.
57 Kwa wazao wa Aruni waliwapa: Hebroni ( mji wa makimblio), na Libina pamoja na nchi ya malisho, Yatiri, Eshitemoa pamoja na nchi ya malisho,
On donna donc aux fils d’Aaron la ville de refuge Hébron, Lobna et ses pâturages,
58 Hileni pamoja na nchi ya malisho, na Debiri pamoja na nchi ya malisho.
Jéther, Esthémo et ses pâturages, Hélon et ses pâturages, Dabir et ses pâturages,
59 Waliwapa uzao wa Aruni: Ashani pamoja na nchi ya malisho na Bethi Shemeshi pamoja na nchi ya malisho;
Asan et ses pâturages, Bethsémès et ses pâturages;
60 na kutoka katika kabila la Benjamini walipewa Geba pamoja na nchi ya malisho, Alemethi pamoja na nchi ya malisho, na Anothothi na nchi ya malisho. Jumla ya miji yao ilikuwa kumi na tatu.
de la tribu de Benjamin, Gabée et ses pâturages, Almath et ses pâturages, Anathoth et ses pâturages. Total de leurs villes: treize villes, d’après leurs familles.
61 Uzao mwengine wa Kohathi waliwapa kwa sehemu miji kumi kutoka kwa kabila la Manase.
— Les autres fils de Caath eurent par le sort dix villes des familles de la tribu, de la demi-tribu de Manassé.
62 Kwa uzao wa Gerishomu kwa koo zao tofauti walipewa miji kumi na tatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri, Naftali, na nusu ya kabila la Manase huko Bashani.
Les fils de Gersom, d’après leurs familles, eurent treize villes de la tribu d’Issachar, de la tribu d’Aser, de la tribu de Nephthali et de la tribu de Manassé, en Basan.
63 Kwa uzao wa Merari walipewa miji kumi, kulingana na koo zao, kutoka kwa makabila ya Rubeni, Gadi, na Zebuluni.
Les fils de Mérari, d’après leurs familles, eurent par le sort douze villes de la tribu de Ruben, de la tribu de Gad et de la tribu de Zabulon.
64 Hivyo watu wa Israeli walitoa hii miji pamoja na nchi za malisho kwa Walawi.
Les enfants d’Israël donnèrent aux Lévites les villes et leurs pâturages.
65 Walitoa kwa sehemu miji iliyo tajwa awali kutoka katika kabila la Yuda, Simeoni, na Benjamini.
Ils donnèrent par le sort, de la tribu des enfants de Juda, de la tribu des enfants de Siméon et de la tribu des enfants de Benjamin, ces villes qu’ils désignèrent par leurs noms.
66 Kwa baadhi ya koo za Wakohathi walitoa miji kutoka kwa kabila la Efraimu.
Pour les autres familles des fils de Caath, les villes qui leur échurent furent de la tribu d’Éphraïm.
67 Waliwapa: Shekemu ( mji wa makimbilio) pamoja na nchi ya malisho katika milima ya Efraimu, Gezeri na nchi ya malisho,
On leur donna: la ville de refuge Sichem et ses pâturages, dans la montagne d’Éphraïm, Gazer et ses pâturages,
68 Jokimeamu pamoja na nchi ya malisho, Bethi Horoni pamoja na nchi ya malisho,
Jecmaam et ses pâturages, Bethoron et ses pâturages,
69 Aiyaloni pamoja na nchi ya malisho, na Gathi Rimoni pamoja na nchi ya malisho.
Hélon et ses pâturages, Geth-Remmon et ses pâturages;
70 Nusu ya kabila la Manase waliwapa Wakohathi: Aneri pamoja na nchi ya malisho na Bileamu pamoja na nchi ya malisho. Hizi zikawa mali za koo za Wakohathi.
et de la demi-tribu de Manassé, Aner et ses pâturages, Balaam et ses pâturages: pour les familles des autres fils de Caath.
71 Kwa uzao wa Gerishomu kutoka koo za nusu ya kabila la Manase, waliwapa: Golani huko Baashani na nchi ya malisho na Ashitarothi pamoja na nchi ya malisho.
On donna aux fils de Gersom: de la famille de la demi-tribu de Manassé, Gaulon en Basan et ses pâturages, Astharoth et ses pâturages;
72 Kabila la Isakari liliwapa uzao wa Gerishomu: Kedeshi pamoja na nchi ya malisho, Dabera pamoja na nchi ya malisho,
de la tribu d’Issachar, Cédès et ses pâturages, Dabéreth et ses pâturages,
73 Ramothi pamoja na nchi ya malisho, na Anemu pamoja na nchi ya malisho.
Ramoth et ses pâturages, Anem et ses pâturages;
74 Isakari alipokea kutoka kwa kabila la Asheri: Mashali pamoja na nchi ya malisho, Abdoni pamoja na nchi ya malisho,
de la tribu d’Aser, Masal et ses pâturages, Abdon et ses pâturages,
75 Hukoki pamoja na nchi ya malisho, na Rehobu pamoja na nchi ya malisho.
Hucac et ses pâturages, Rohob et ses pâturages;
76 Walipokea kutoka kabila la Naftali: Kedeshi iliyo Galileya pamoja na nchi ya malisho, Hamoni pamoja na nchi ya malisho, na Kiriathaimu pamoja na nchi ya malisho.
et de la tribu de Nephthali, Cédès en Galilée et ses pâturages, Hamon et ses pâturages, et Cariathaïm et ses pâturages.
77 Kwa Walawi wengine, uzao wa Merari, walipewa kutoka kabila la Zebuluni: Rimono pamoja na nchi ya malisho na Tabori pamoja na nchi ya malisho.
On donna au reste des Lévites, aux fils de Mérari: de la tribu de Zabulon, Remmono et ses pâturages, Thabor et ses pâturages;
78 Kwa wao pia walipewa, upande wa pili wa Yordani huko Yeriko, kwa upande wa mashariki mwa mto: Bezeri katika jangwa pamoja na nchi ya malisho, Yahzahi pamoja na nchi ya malisho,
de l’autre côté du Jourdain, vis-à-vis de Jéricho, à l’orient du Jourdain: de la tribu de Ruben, Bosor, au désert, et ses pâturages, Jassa et ses pâturages,
79 Kedemothi pamoka na nchi ya malisho, ma Mefathi pamoja na nchi ya malisho. Hizi zilitolewa kutoka kabila la Rubeni.
Cadémoth et ses pâturages, Méphaat et ses pâturages;
80 Walawi walipokea kutoka kabila la Gadi: Ramothi ya Gileadi pamoja na nchi ya malisho, Mahanaimu pamoja na nchi ya malisho,
et de la tribu de Gad, Ramoth en Galaad et ses pâturages, Manaïm, et ses pâturages,
81 Heshiboni pamoja na nchi ya malisho, na Yazeri pamoja na nchi ya malisho.
Hésebon et ses pâturages, Jézer et ses pâturages.

< 1 Nyakati 6 >